Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Pasco. Good governancy ni kuwa mnafki kama una taarifa ya ulicho kifanya kwanini una shindwa kuelezea. Au mlizoea mfumo wa kuundiwa tume kila kajambo kadogo kanako tokea. Na ripoti zina somwa kimya kimya ishu inaishia jukwa juu.
 
Hii nchi tulipofika Pasco tusichekeane. Kucheka cheka na mkeo nyumbani.
Ukiwa CEO unatakiwa kuwa na data at your fingertips. Kama hauwezi kaa pembeni.
Wanyooshwe tu. Hakuna namna nyingine

Hivi unadhani Bade alikuwa hajui kuwa makontena yalikuwa yanatolewa bila kulipiwa kodi? Hata kama hakushiriki kwa mfano. Huyo wa TRL hakujua hela ya mkopo imelipia salary?

Good governance?

Huyu pasco huwa ananishangaza sana kwa kweli...sijui definition yake ya good governance ni nini hasa! Yani CEO au Manager anaulizwa swali na waziri, ANADANGANYA mbele ya kamdamnasi, eti mfumo uko perfect kabisa, alafu eti pasco anasema waziri amlinde huyo mtu mbele ya kadamnasi, eti aende akamuulize hayo maswali kwenye kakichumba! khaa!!
Mie nilimsikia yule manager sijui ni wa bandari, alivyoonyeshwa zile data, akaanza kuweweseka eti ohooo muheshimiwa ningekuja kukupa hizo information baadaye lakini sio hapa! Loh!
Yani ni kwamba hawa watu wamezoea kudiscuss haya MAUONGO yao na UBABAISHAJI wao huko ndani ya vijumba na yanaishia humo humo ambako hakuna mtu anajua nini kinaendelea au nini kimeamuliwa...
Mie naaminni kuwa kama hao ma-CEO wasingedanganya mbele ya kadamnasi, wakatoa majibu ya ukweli kama ilivyo, then wasingedhalilika.
 
S niliweka uzi kuuliza bandari imesafishwa nini na kina Mwakyembe na Sitta?
mkanijibu bandari iko safi tatizo liko TRA?
Tatizo lao huwa wamepotshwa na ushabiki hadi mantiki huwa hawazioni. kwenye lilee bandiko walidai Bandari ni safi tatizo ni TRA. Ilipokuja hoja kwamba kama tatizo ni TRA geti namba 5 lipo TRA? Wao wakang'ang'ania kuwa tatizo ni TRA, leo tena wanasema tatizo ni Bandari, wala hawajielewi!!
 
Kwa hiyo mnataka kusema kwa kuwa kuna mtu mtaani kweni kakutwa anabaka katoto kadogo, na nyie suluhisho ni kupiga mpaka afe?
 
Wabongo bwana ! Magufuli hakuna kupunguza spidi ! Majitu mALAFI ETI NINI WACHEKEWE ????
 
Mkuu mie nakushauri tazama maswali wanayo ulizwa viongozi wa kiserikali na kamati za mabunge ya marekani ( congress and senate) katika uteuzi kuwa waandamizi wa serikali au inapotokea scandal naserikali inatakiwa itoe maelezo.

nikupe mfano Hillary Clinton juzijuzi tu hapa aliitwa kujieleza kama waziri wa mambo ya nje aeleze uwajibikaji wake wa kifo cha wamarekani kadhaa Bengazi akiwemo balozi wa marekani nchini libya, hebu tazama yale maswali kwa masaa 12 kawekwa kiti moto, namengine mengi tu. alafu linganisha na hiyo nusu saa wanazopewa maofisa wa serikali Tanzania utupe mrejesho

[video]http://nyti.ms/1GXXSfv[/video]
 
What i do believe good governance inaendana na transparence.kwa hio anachokifanya waziri mkuu ni sawa kabisa.
 
Umwite aliyesababisha makontena yapotee mkajadili, kisa utawala bora, let them go to hell, we will employ others. nchi inanuka rushwa, ufisadi wa kutupa. matajiri wanatamba kwa pesa za wizi.....
 
Sijashawishika kabisa na hoja mfu za Pasco,
Kwa hapa tulipofika kama nchi, tunataka mtu wa jamii ya Magufuli na Majaliwa. Kufanya kazi kwa mazoea kuishe na kuondoke kabisa na awamu ya nne. Sisi tulio kwenye sekta binafsi tunajua maana ya kuwajibika, kila wakati tuko alert, kwa sababu hatujui saa wala dakika ambapo kinaweza kunuka. Serikalini mmezoa mdebwedo.
Pole sana brother.
 
Last edited by a moderator:
Pasco kwa mfano hao wanaoshtukizwa wangesema ukweli hio karatasi aliokuja nayo ingewadhalilisha?? Wamesema uongo ndio maana anatoa data ili kuthibitisha uongo wao.
Like siioni ila ujumbe wako mujarabu kwa huyu Pasco.Watu wanafanya kazi kwa mazoea tu wizi wizi tu,uongo uongo,Pasco unaangalia upande mmoja wa shilingi huoni mara ya kwanza huyo menaja wa bandari aliongopa na alipoonyeshwa ile nondo akaanza kujikanyaga wewe unaona hiyo ni sawa??acha wanyooshwe tu maana hakuna namna nyingine.Mimi naona hiyo ni cha mtoto ila tulipofikia ilibidi tumpate dicteta kwa miaka mitano watu wangekaa sawa.
 
Halafu, hao wote si walikuwa kwenye serikali iliyopita?

Manake wanachofanya sasa ni kama kuivua nguo hiyo serikali.

Ina maana walikuwa wanatumikia serikali iliyokuwa imefeli?


Chochote kile ukitaka kwenda mbele Zaidi kutaka kudadavua, lazima uje na tafsiri au maswali mengi!

Mmoja anaweza akahoji, kulikuwa kuna haja gani ya Mungu kuuweka mti wa katkati katika ile busatani?

------------------------
As long kuwa wamehusika na upotevu, wanatakiwa kujibu shauri lao, ila ukienda mbele Zaidi ndio unaweza ukaja na swala kuwa serikali iliopita inavuliwa nguo, au serikali iliopita imefeli! Inategemea anayehoji anataka kuliangalia hilo swala kwa mtazamo upi.

Cha msingi Zaidi ni kuwa, kama yanayo fanyika yana tija kwa jamii!
 
Hizi hela wangekuwa wakiiba wanazitumia kwa kuvizia hapo ningeungana na mtoa hoja, mijitu inatuibia halafu inatumia kwa mashauzi kuonekana kama wao wanaishi juu ya dunia lazima waumbuliwe hakuna namna malipo ni hapahapa
 
Mbona hueleweki wakinyamaza ooh wanakumbatia mafisadi wameona wanakemea oooh udhalilishaji umeshazoea kuisoma namba wewe
 
Mkuu Pasco Labda tungeanzia hapa "What is Good Governance?"
 
Last edited by a moderator:
Vyombo vya usalama kamata huyu mtu hana maana . Mwizi haitaji heshim yoyote .
 
Wanabodi,

Kwanza naomba kukiri, kuwa ninaunga mkono kwa asilimia 100% juhudi za serikali awamu ya 5 kupambana na rushwa, ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi, ili mtindo unaotumiwa na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kassim Majaliwa, sio!.

Baada ya kukisikia kisanga cha TRA kilichomng'oa Kamishna Mkuu na maofisa kadhaa kufuatia sakata la makontena, leo amerudi tena bandarini na nimekishuhudia kitu anachokifanya, japo anashangiliwa na umati wa watu, lakini anachokifanya ni kuviziana, kutishana, kudhalilishana na kunakwenda kinyume cha utawala bora, yaani good governance!.

Waziri Mkuu anafanya ziara za kushtukiza mahali, huku akiwa na karatasi lenye tuhuma specific, lakini amelificha!, anakwenda kumuuliza mhusika wa pale kuhusu utendaji wa mfumo fulani, anaelezwa kuwa mfumo uko perfect, kisha analiibua hilo karatasi lenye tuhuma na kuanza kumsomea mhusika mbele ya kadamnasi ya watu, abcd!, mhusika anashindwa kujibu, atasimamishwa kazi, na kama yuko juu ya mamlaka yake, atamchongea kwa Rais!.

Hata TRA siku hiyo alikwenda na nondo za makontena, alipomuuliza Bade, akamjibu details ziko kwa maofisa wangu, ndipo akaibua nondo lake na kumsomea kwenye kadamnasi ili aonekane mjinga!, huku ni kuaibishana, kudhalilishana na kinyume cha good governance!.

Baada ya kutoka bandaini, akaenda TRL na kumuuliza mkurugenzi mkuu, mlikopa bilioni 3 TIB za kufanyia nini?!, kwa nini hamkufanya kile mlichokopea?, akaambiwa tumelipia mishahara, nani aliwapa idhini ya kukopa?!, Mkurugenzi hana jibu na naamini kesho atatangazwa hana kazi!.

Top management angekaa nao ofisini na kuulizana kistaarabu ndio good governance!. Mimi hata home, wife alikuwa na tabia ya kuwafokea ma tx home, mbele ya watoto, nikamkataza!, nikamsisitiza if things are not right, muite pembeni ndipo umseme, sio kumdhalilisha mbele ya watoto!.

Anachofanya Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa ni kuviziana, kudhalilishana na kuabishana bila sababu za msingi!, hili la kuitana na kuanza kuhojiana mbele ya waandishi ili watu wamuone alivyo mkali, ni tabia za ma populist leaders!, Leo nimemuona Magufuli akiongea na wafanyabiashara yuko very humble even cracking some jokes!.

Kama kuna watu wako karibu na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, wamwambie anavyofanya sio vizuri, Sio Sawa, Sio Haki, Sio Good Governance!, Ni Udhalilishaji na Kuaibishana tuu!. Akumbushwe kuna kitu kinatwa 'karma' kisije kumshukia!.
Au wewe unaonaje?!, toa maoni yako ni sawa au sio sawa!.

Pasco

waacha waumbuliwa nchi hii ilishaoza kila mkurutez hufqnya mambo yake...me cna cha jushaur hapo
 
Barbarosa Pasco hajalazimisha maoni yake ndiyo yawe ya watanzania wote, kama wewe unaona maoni yako hayafanani na ya kwake siyo mbaya ukayapinga kwani ndiyo demokrasia. Kwa bahati mbaya sana Afrika kuna fikra mufulisi kwamba mtu akiwa madarakani apingwi kwani busara za kuongoza huzitoa kwa mungu!!

Maoni ya Pasco yanaungwa mkono na watanzania wenzako ambao wanaona Majaaliwa kama waziri Mkuu wetu anadhalilisha utu wa wale anaowahoji kwa lengo la kuujua ukweli wa ukwepwaji kodi. Hakuna anayepinga wanaokwepa kodi kufuatiliwa, lakini kama njia zinazotumika zinadhalilisha utu wa wengine ni lazima zipingwe!

Unaongeleaje kwa serikali kama ya China ambayo ingeenda mbele Zaidi ya hapo kwa kuwauwa?

Ni wakinamama wangapi wamedhalilishwa utu wao kwa kujifungilia chini, au kufariki dunia kwakuosa huduma stahiki kwa kukosekana kwa fedha ya vifaa tiba nk?
 
Back
Top Bottom