Anafanya kazi kiwandani ameshajiwekea msingi wa umasikini milele

Ndio wajinga wenyewe Sasa hao yaani unafanya kazi ya kujitolea kisa umeahidiwa kazi akili Gani hii je usipopewa hiyo kazi inamaana utakua umepoteza mda wako bure
Halafu akipata hela ananunua bajaji milioni 10 halafu anampa mtu amletee elfu 20 kwa siku 😁😁😁😁😁😁😁😁😁😁😁
 
Mkuu kama we Mungu kakujaalia shukuru, waombee nao wajaaliwe kama wewe.....hakuna mtu anapenda kuishi kwa mateso hivyo.

Kama una msaada wasaidie kama hauna usiwasimange.
Ila fikra kama hizi ni tatizo aisee. Mkuu Dunia hapa unapa unachokitafuta. Mungu hajawapangia hao kufanya hiyo kazi
 
Mkoa wa pwani miaka 10 mbele utakuwa na watoto wengi wa kichina wanaoongea kizaramo
Kasi ya dada zetu kutoa huduma ya papuchi kwa wachina wa viwandani inatisha sana..
 
Hujayajuwa maisha bro, usifikiri hawana akili, vitu vyote vimegoma, elimu huna,ajira ngumu, na familia inahitsji mahitaji, utafanya nini? Kama wewe kwa namna moja au nyingine, upo sehemu nzuri, sio kwa vile una akili Sana kuwazidi it's just life,
Wakati nasoma msingi, miaka hiyo ya 90,natembea kilomita 5 kila siku, nakalia mawe shuleni,nashinda njaa siku nzima,
Nilijiuliza kwa nini Mimi maskini?
Fast forward Leo, 2024,watoto wangu wanapelekwa shule na kufatwa na V8! Driver akichelewa, wanalalamika, siku moja wakiwa wanaenda shule, nikawauliza hawa watoto wengine wanaotembea kwa miguu na kidumu na fagio, kwa nini hawapandi basi?
Wakasema baba zao hawana uwezo!
Mtoto wangu haelewi inawezekana vipi kwenda shule kwa miguu! Kuwa humble bro!
Hao wanaopigika kwa wahindi na mchina, ni kwamba wamekosa fulsa nzuri tu,
 
We utakua unafanya kazi kiwandani s unajipa sifa ambazo huna dunia Haina huruma
 
green tea 🤣🤣
 
atizo la kwanza ni wananchi wenyewe hawajitambui, cha pili ni Serikali kushindwa kuweka Sheria rafiki kwa wafanyakazi wa Nchi yake.
Mkuu cha kwanza ungesema ni serikali kutojari raia wake.
Miaka ya nyuma,sheria za kazi zilikuwa zinatambua kiinua mgongo,
serikali ikafuta kwa kisingizio cha kuvutia uwekezaji,lakini ukichunguza ni watungasheria ama ndo wamiliki wa viwanda au wana hisa kwenye hivyo viwanda ndo maana wanatunga sheria kandamizi ili wapate faida kubwa.

2. Unakuta mtu anaitwa waziri wa wizara ya viwanda,anakuja kutembelea kiwanda,lakini hana
mpango kabisa wa kuonana na wafanyakazi ambao ni walipa kodi kupitia kiwanda hicho
anaongea na hao wachina/wahindi anapewa kilicholeta anasepa,hata kama ungekuwa wewe
utawathamini hao waajiriwa wako ambao kiongozi wao hana haja ya kuonana nao bali kushangaa machine.

3.Raia wanatekwa na kuuwawa,unasikia sauti ya mtu mmoja inasema kifo ni kifo tu
hapo nani akujali wewe,
Mi naona kama watu wanaona kupigwa viboko ni njia sahihi ya kuwawezesha kupata mlo wa siku,
waendelee tuu,mbona poliss wanawapiga na hawawalipi hati senti moja?
 
Mkuu wamuige nani aliyejiajiri?
Wazee unaona wanataka kufia kwenye ajira,kama kujiajiri ni rahisi si wangestaafu pindi wanapofikisha miaka 60
mbona wanasubiri hadi kama ni ubunge wang'olewe?
 
Mara mia uokote makopo kilo jero kaz izo ni kujitupia ktk umaskin yn huna tofaut n asie na kaz tn anakuzid maana ana uhuru
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…