Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

Mkuu ni wimbo sio nyimbo maana unazungumziwa mmoja tuu kama una bando andika jina la wimbo na la maanii kisha mp3 zitakuja link za kutoaha kisha utaupakuà ila mimi sina bando Leo ningeuweka humu
Daaah issue ipo kwenye ipo kwenye umoja na wingi ila huo wimbo niliupata baada ya kuwekwa kwenye huu uzi
 
Nmetafakari sana kuwa hivi Roma angetegemea Radio zetu ziicheze nyimbo yake sjui kama kuna kituo hata kimoja kitakacho weza icheza.

Kwa kweli tunashukuru walio leta youtube inatusaidia sana la sivyo nyimbo kama hizi tusingekuwa tunazipata kabsa

Nahisi kama Tanzania Daima au mwanahalisi au mawio wangekuwa na redio labda wangeipiga nyimbo hiyo ila kwa kuwa ni magazeti labda waiandike tu.
 
Mungu alishatatua hilo tatizo kuwa hakuna changamoto utakayopata isiwe na njia ya kutokea.
Mpaka hapo jinsi tulivyoipakua hadi viganjani ni jambo la kumshukuru Mungu.
Kilichobaki ni jinsi ya kumpatia ujira stahikI huyu #anaitwaroma#
 
Jiwe limetupwa gizani, wenye degree nne wakaanza kulalama... Hapo sasa Roma anahitaji vituo vya redio tena? Mbona wamempromote wenyewe kuliko hata " baba lenu"
 
Mkuu YouTube ilishapigwa block tayari
 
huu wimbo YouTube umeshapigwa ban
 
ROMA: KWETU BIMA YA AFYA NI BORA KULIKO IZO NDEGE.

"Yuda usimuharibie Dani ili umfurahishe Mtukufu, Sisi sote wanao kwa nini unampenda Yusuph.

Yakobo Baba Pesa Madaraka Umaarufu Ona umewapatia vijana wanakosa Hekima na Utu.

Wapunguzie Vifungo, Wafungwa wasio na hatia, Wengine walifata mkumbo kiukweli hawakuwa na Nia.

Nasikia Jimbo la Ubungo kuna mtu amelipania, Hizi tungo ni zaidi ya Waraka wa Waebrania.

Chama kilishawatimua Wanasiasa mlio wanunua, Yaani mnapiga Bomu Mochwari halafu mnajisifu mumeua !

Tuliombe Taifa tuwaombee Viongozi wetu, Nchi ina miiba sio tuwavishe viatu walioko peku.

Tusilete Uchama kwenye ishu za Kitaifa, Uongozi ni kuacha Alama Chanya na kuwajibika, Kutekana kuuana sio sifa ya Mtanganyika.

Hongera Baba kwa ukusanyaji wa Mapato Kedekede, ya kodi, Na Flyover ndo hizo kanyanga Twende, Kwetu Bima ya Afya ni Bora kuliko izo Ndege.

Atafanya yote Tumuombee yesu Nibebe, Watu wametumbuliwa kabla ya mwezi mmoja kustaafu, Walimu wamesahauliwa mapato yao, Halafu, Polisi mishahara yao hadi tuwapige tafu, boresha Mahospitalini tupunguze idadi ya Wafu."-Roma Mkatoliki.

#AnaitwaRoma..
 
Kaimba "WIMBO WA TAIFA" huu. Ila kesho asubuhi na mapema utapigwa marufuku, tena watatangaza ukikutwa nao hata kwenye simu unakula "KESI YA UHUJUMU UCHUMI" au "KESI YA UHAINI" dadeki.

Halafu lazima basata "VAR" itumike, kumwita na kumfungia "ROMA" kujihusisha na sanaa kwa muda usijojulikana. Utawasikia basata wakisema "MAUDHUI YA WIMBO" sio ya kistaarabu wasanii wote wanatakiwa waige kwa "HARMONIZE na NANDY".

#HASHtag #MWIMBOwaTAIFA
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nani ananyemelea jimbo ubungo?

Ni nani anamwambia hajui kurap, anabebwa na atamuua kwenye rap battle?
 
Mi nataka nimfahamu yule anayejifanya anajuwa kurap,make anabebwa na media siku zikimtema atakiona cha mtema kuni
Screenshot_20191116-140611.jpeg
 
Back
Top Bottom