Anayehitaji msaada wa mambo ya kodi

Malyenge

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
6,658
Reaction score
3,659
Je unatatizo la kodi. Lete suala lako hapa na utasaidiwa.
 
naomba kujua mchanganuo wa kiwango cha mshahara na asilimia yake ktk kodi ya "pay as you earn" (PAYE)
 
naomba kujua mchanganuo wa kiwango cha mshahara na asilimia yake ktk kodi ya "pay as you earn" (PAYE)
Soma jedwali hili.
[TABLE="align: left"]
[TR]
[TD]MSHAHARA KWA MWEZI[/TD]
[TD]KIWANGO CHA KODI[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Shilingi 0 –Mpaka shilingi 170,000[/TD]
[TD]HAKUNA yaani mshahara huo umesamehewa kodi[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Shilingi 170,000 –Mpaka shilingi 360,000[/TD]
[TD]Kodi ni 12% ya ziada ya shs 170,0000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Shilingi 360,000 –Mpaka shilingi 540,000[/TD]
[TD]Kodi ni sh 22,800 kujumlisha 20% ya ziada ya 360,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Shilingi 540,000 –Mpaka shilingi 720,000[/TD]
[TD]Kodi ni sh 58,800 kujumlisha25% ya ziada ya 540,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Shilingi 720,000 –Na zaidi[/TD]
[TD]Kodi ni sh 103,800 kujumlisha 30% ya ziada ya 720,000[/TD]
[/TR]
[/TABLE]









Mfano:
Mshahara ni shilingi 509,888.89 KODI ITAKUWA KIASI GANI?
JIBU
Mshahara wa shilingi 509,888.89 utasamehewa 10% ya NSSF ikiwa mwajiriwa ni mwanachama wa NSSF na mshahara wake unakatwa hiyo NSSF ambayo ni 10%. Hivyo hivyo kwa wanachama wote wa mifuko ya hifadhi ya jamii inayotambulika na srikali.
Kwa hiyo shilingi 509,888.89 ukitoa 10% yake unapata NSSF ni shs 50,988.89.
Unachukua shs 509,888.89 tos shilling 50,988.89 unapata sh 458,900. Hizi shilingi 458,900 ndo zitatozwa kodi ya PAYE. Kutokana na jedwali hapo juu kodi yake itaangukia kwenye band three hapo juu.
Shilingi 458,900 ipo kati ya shilingi 360,000 mpaka 540,000
Yaani shs 458,900 ni ziada ya 360,000
Unachukua shs 458,900 unatoa na shs 360,000 unapata shs 98,900 ndio hiyo ziada ya 360,000!!!
Kwa hiyo shs 98,900 unaitoza asilimia 20 itakuwa (20%xshs 98,900)= sh19,780
Kwa hiyo jumla ya kodi ni ile kodi fixed iliyopo kwenye jedwali shs 22,800+shs19,780 ambayo jumla ya kodi ya mshahara wa Shs 509,888.89 ni SHS 42,580
 
nami naomba msaada nina ndugu yangu amepanga nyumba ya mama mmoja mjini Arusha, baada ya kukosa uwezo wa kulipa kodi ya nyumba ilipita miezi mitatu bila kulipa mama wa nyumba kafunga nyumba na kusema alipe kwanza ndo aendelee kuishi,wiki mbili zilizopita ndo amepata kazi hivyo mwezi April ndo anaweza kulipa deni je alichotendewa ni sahihi?
 
maana hata vyombo vyake vimefungiwa. yaani anaishi maisha ya taabu. kisheria nini utaratibu wa kuadhibu mpangaji aliyeshindwa kulipa kod? isitoshe huyu jamaa hakuwa na mkataba wowote wa upangaji nyumba.
 
mkuu Malyenge kwa gratuity inayorange kwenye 2.5m kwa sisi tulio na mkataba wa mwaka mmoja mmoja ktk ajira zetu inakuaje?manake inatakiwa nipokee 2.5m lakini natakiwa nikalipe tra kodi inayofikia 666800,hapa inakuaje mkuu?pesa kidogo kodi kubwa kiasi hicho?msaada wako tafadhali
 
Last edited by a moderator:
Hii kodi ya wafanyabiashara wa huduma za kipesa uko vipi? Nazungumzia watu wa Tigopesa, M-pesa, Airtel money n.k. Hawa wanakatwa kodi za kamisheni zao kila mwisho wa mwezi wa kupokea mishahara/kamisheni zao. Inakuwaje bado mtu huyu anatakiwa kwenda kulipa tena TRA wakati kodu yake ishakatwa kwenye simu?
 


[TABLE="class: cms_table, align: left"]
[TR]
[TD]Gratuity ya Shilingi 2.5 milioni inaangukia katika wigo wa kodi wa kati ya shilingi 720,000 –Na zaidi ambao kodi ni sh 103,800 jumliosha 30% ya ziada ya sh 720,000
Kwa hiyo ukikokotoa kwa kutumia kanuni hapo juu utapata jumla ya kodi. Suala la kodi kuwa kubwa kwenye kipato kikubwa ni suala la kisera. Uzuri muundo wa serikali ya Tanzania ni mzuri kuanzia ngazi ya chini kabisa. Muone diwani wako aliwasilishe ngazi ya wilaya mpaka ngazi ya taifa litafika. Inawezekana kabisa kwa kulizungumzia ngazi husika sera inaweza kubadilishwa na kodi ikawa nafuu kwa wanaopokea mishahara na marupurupu.[/TD]
[TD]


[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 

Mkuu hapoa twazungumzia kodi ya mapato na si kodi za kupanga nyumba. Waone wanasheria waliosomea civil case watakushauri vizuri.
 

Mkuu hiyo kodi ya kamisheni anayelipa ni kampuni inayotoa huduma ya simu yaani vodacom, Airtel, Tigo nk. Kwa hiyo wakala anapolipwa pesa yake anakuwa amepata kipato kipya yaani anaangukia kwenye kifungu cha 4 cha sheria ya kodi ya mapato kinachosema mtu atalipa kodi ikiwa anakipato.......
Kwa hiyo huyu wakala akishapokea pesa zake anakuwa amepata kipato sasa. kabla ya hapo pesa hiyo ilikuwa bado mikononi mwa kampuni ya simu.
Kama hujanielewa niulize tena.
 
Habari yako kiongozi, na swali na income tax act ya Tanzania. Suala la deferred tax kwenye nchi yetu likoje ?? TRA wana deal vipi na hii ishu kwenye assessment za income taxes ?
 
Habari yako kiongozi, na swali na income tax act ya Tanzania. Suala la deferred tax kwenye nchi yetu likoje ?? TRA wana deal vipi na hii ishu kwenye assessment za income taxes ?

Ili kuwa vizuri katika masuala ya sheria inakupasa uijue sheria yenyewe inasemaje. Umeniuliza TRA wana deal nayo vipi suala la Deferred taxation ni vizuri nikujibu kwa mujibu wa sheria inavyosema na si TRA wana deal nayo vip maana wanaweza kuwa wanakosea. Subiri nitakujibu muda si mrefu sheria yasema nini kuhusu deferred tax.
 
Mkuu Malyenge, kwa mshahara wa 1.2 kukatwa kodi ya 200000+ ni sawa?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu BIGURUBE hilo swali watawala wanalo jibu sahihi. Mimi ni mtaalamu wa kodi kuitafsiri na kukokotoa kwa mujibu wa sheria inavyosema tu basi. Swali hilo akiulizwa mbunge ama diwani anaweza kuwa na jibu. hata kama hawatakuwa na jibu lakini wao ndio wenye jukumu la kupeleka malalamiko ya kodi kuwa kubwa kwenye mshahara na wakaweza kuyafikisha malalamiko hayo sehemu husika. Kuhusu sheria kuwa mabaya hilo liko nje ya uwezo wangu ingawa ninaweza kuwa na maoni yangu binafsi kama nikitafutwa na serikali kuchangia hoja ya tax reforms.
Nadhani nimekujibu vema mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…