Kama kuna kitu kimemponza mtawala wa sasa, rais Magufuli ni papara.
Ngumu hata kujua dira/muelekeo katika mipango yake kwa kuwa hawezi kujizuia hata dk akiwa na jambo. Hii imepelekea wananchi kutomuelewa pamoja na mwanzoni walikuwa na imani naye sana. Hii ni tabia itakayom-cost dearly katika uchaguzi ujao wa 2020.
Jikumbushe matukio haya machache uelewe ninachozungumza:
- Hakuna haja ya sherehe za uhuru - nchi chafu na tutatumia siku hii kwa ajili ya usafi, mwaka mmoja baadae: sherehe ipo na jiji chafu!
- Nimeambiwa kuna watu wameficha sukari, nitawakamata, na kunyang'anya sukari na wao watakwenda ndani. mwaka sasa, hakuna sukari iliyokamatwa na kupewa wananchi, hakuna aliyefungwa na bado sukari ipo juu.
- Serikali inahamia Dodoma mara moja, safari itaanza kabla ya bajeti ijayo, miezi karibu 6 sasa hakuna hata karani aliyefika Dodoma ukiachilia mbali Waziri Mkuu ambaye maandalizi yalianza na Lowassa.
- Pesa zimefichwa majumbani, nitabadilisha pesa zote. Hadi sasa hakuna aliyekamatwa na hizo pesa zilizofichwa.
Haya ni mambo ambayo kwa kifupi naona yanam-cost sana mkuu na kama hatofanyia kazi, atali-cost taifa lake na chama chake. Yote anayoyasema mkuu inawezekana yalikuwa sawa, ya msingi na labda alipata fununu za kutosha. Shida yake ni papara, kuna saa amefanya mambo kama Katibu mwenezi wa chama cha siasa, anazungumzia kila jambo matokeo yake anatoa pre-mature conclusions, anatoa misimamo ambayo haitekelezi na inabaki kama deni ktk utendaji wake!
Ikifika 2020 watu wakarejea ahadi, kauli, mipango na utendaji lakini pia, leo hii ni muelekeo gani tunaenda hatujui! Huwa mkuu anakuja na matamko au mipango out of blue, watu wake ndio usiseme, wanaibuka na maagizo mengine hayakufuata sharia/taratibu, au mengine hayatekelezeki!
All in all kama kuna sehemu mkuu anahitaji mtu wa kumshauri ni hapa katika kitengo cha habari/usemaji ambao ni mwiba mgumu kwake kuliko eneo jingine lolote!