Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Alishasema kazi ya kuendesha ngumu na ameshachoka,unadhan destination tutafika kwa wakat?
 
Ha ha haaaaa

Nashukuru kwa kuninoti kuwa mimi nimeshikilia msimamo wa kutetea hao wasio na tatizo lolote.

Uhuru na uamuzi ni wangu ndugu, na mimi naadika yanayojiri sifati mkumbo wa wanaovutwa na wachache.

Makonda oyeeeeeee

N.b. mimi sina chama
Wewe huenda ni yule mdada aliyetanjwatajwa sana ambaye Bash...e ametajwa kumlinda kwenye biashara hiyo haramu!
 
Wewe huenda ni yule mdada aliyetanjwatajwa sana ambaye Bash...e ametajwa kumlinda kwenye biashara hiyo haramu!


Fikiria lolote, ila kwani shida ipo wapi mimi kufurahia juu ya Mh. Makonda? wenzako humu waliyaandika hayo pia kabla.



Makonda oyeeeeeee
 
Yeye mwenyewe hajui anapoenda atajua sasa anapotupeleka
 
Reactions: SDG
Tulishahama kwenye msitari siku nyingi,kinachoendelea kwa sasa ni MUNGU anasaidia.Nimeamini ukishakuwa mtu wa wivu,ujuaji na visasi hakuna chochote utakachofanikiwa.
[HASHTAG]#TUNDULISSUFOR2020[/HASHTAG]
 
Watu wengi makini wamekuwa kimya juu ya mwenendo wa utawala wa JPM, Viongozi wengi wameamua kufunga mdomo. Serikali yake imekuwa ikitumia nguvu sana katika kukandamiza hoja kinzani. Kwanza walianza kwa kukata matangazo ya bunge live kwa kibwagizo cha hapakazi tu, baadae wakaanzisha kamatakamata katika mitandao kwa kutumia cybercrime act, sheria ambayo mpaka sasa imekamata wapinzani tu, baadae wakapiga marufuku mikutano ya kisiasa na maandamano mpaka 2020 kwa kigezo kwamba hapakazi tu, wakapeleka muswada bungeni kubana vyombo vya habari, alipomaliza nje akarudi ndani ya chama chake, akajijenga zaidi,akautishi mhimili wa bunge, mara kadhaa ameelekeza mhimili wa mahakama kutenda anavyotaka. Haya yote yamefanyika kwa nia njema? Je mtu mwenye nia njema anaweza kufanya haya?
1. Kuamua matumizi ya fedha bila kufuata utaratibu wa kisheria, na bajeti iliyopitishwa na bunge?
2. Kuagiza ujenzi wa Airport chato huku nchi inakabiliwa na changamoto lukuki zinazogusa maslai ya umma?
3. Kununua ndege kwa cash bila kufuata taratibu za manunuzi?
4. Kufungia akaunti za manji, kumhusisha na madawa,kumnyanganya mali zake, kudai sio raia wa tanzania?
5. Kufumbia macho ufojaji wa vyeti kwa RC.
6. Kufumbia macho tuhuma za RC kumiliki mali za watuhumiwa wa madawa ya kulevya, baadhi kuziuza na nyingine kuzitumia.
7. Kufumbia macho uvamizi wa ofisi ya kituo cha redio ili kulazimisha tukio kurushwa hewani.
8. Kufumbia macho matumizi ya anasa ya sherehe ya RC aliyorushwa live katika tv huku akidai anabana matumizi.
9. Mkuu wa Mkoa kuhongwa gari na GSM na kubadili plate namba na kuweka ya RC
Binafsi nadhani JPM na Albert wanashirikiana katika dili za upigaji, wameamua kujinufaisha kwa kivuli cha uzalendo. Kwa hali hii bado wanaoweza kumwamini ?
 
Fanya kazi, jitume utajua mwelekeo
 
Inapofika wakati ambapo anapaswa kuonyesha ukweli Wa kile anachokisema a.k.a vita shidi ya mafisadi Magufuli huwa anaziba maskio had I upepo upite ndo huyafungua tena.

Hivi kama Magufuli sio fisadi anayejifichia kwenye vita dhidi ya mafisadi, anashindwaje kutoa amri Makonda achunguzwe Mali alizonazo na tuhumua za kugushi vyeti?

Kama Magufuli sio fisadi, aliwezaje kumteua Mwakyembe kuwa waziri Wa katiba nasheria?

Ujue kwanini anashindwa kumgusa Makonda, ni kwasababu inawezekana kuna siri za huyu MTU Makonda anazifahamu, kama ilivyokuwa kwa Mwakyembe.

Mi nasema, Magufuli ni fisadi, wewe unasemaje?
 
Leo katolewa hadi result slip ya mtoto pendwa, akishindwa kutoa uamuzi tuu, beyond reasonable doubt.........
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…