Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Jpm hela utazitoa Wapi kila dhehebu likidai barabara utaleta shida kidogo
Najiuliza tu,
Ikatokea wenzetu wanalalamika msikiti wao upo madongo kuinama
Hivyo waumini wanafika kwa taabu.

Je atawajengea barabaraa, wangapi sasa watademand hiyo?
 
Sasa unatetea watu wanaokiuka kanuni za BUNGE walizo zitunga wenyewe????.....sasa unataka hizo kanuni zimuadhibu nani?....Hapa unalalamika kisa zimewaadhibu wabunge wa CDM si sawa acha kanuni zifanye kazi tulizoea kuishi kwa mazoea sana
tumia akili acha ushabiki wa kisiasa, unataka kunambia wabunge wa ccm huwa hawafanyi makosa? aliewaita wabunge wa kke wa ukawa n mababy, alichukuliwa hatua gan? jitutumue lakn ujue kila jambo linamwisho.
 
Najiuliza tu,
Ikatokea wenzetu wanalalamika msikiti wao upo madongo kuinama
Hivyo waumini wanafika kwa taabu.

Je atawajengea barabaraa, wangapi sasa watademand hiyo?
Nakumbuka kiongozi mmoja mstaafu hapa nchini aliomba fedha kwa rafiki yake nje ajenge nyumba ya ibada kwa dini mmoja kijijini mwake. Alipofariki ndipo tukajua kwa maelezo ya mnufaika mkuu aliyekuwa kiongozi wa dini hiyo pale kijijini. Dini hiyo haikuwa ya Kikristo na mfadhili wa ndani alikuwa Mkristo.
 
Nasikia mfalme Mbowe hakosolewi .

Ngoja niwashawishi nyumbu wamkosoe nione kitatokea nini
 
"... Eti Tindu lisu na Bulaya kuliona bunge ni 2017. Hivi ni hiyo kamati iliyowapeleka bungeni au?"

Ndo hapa ninapoiona CHADEMA ya sasa ni minyumbu tu!!! Mlipokomaa kumvua Zitto ubunge mliyajua hayo!? Mlijua kuwa nyie genge la chadema hamkumchagua wala kumpeleka bungeni bali wananchi wa kigoma!!! Leo bila aibu, nyumbu anakuja mbele kulialia wale wahuni wanaodhani bungeni ni sehem ya kunywea viroba eti waachwe watambe!!! Wakalime hata magimbi ili wakirudi wawe na nidhamu.
 
Kweli mfumo kristo hauwezi kuisha nchi hii

Rais anasemaje eti alimsikia mzee wa upaka analalamika kuwa barabara inayopita kwake mbovu kwa hio kaenda kujionea mwenyewe...
Na katoa ahadi ya kujengwa
Hii NDIYO raha ya kuwa Rais. Mwenye wivu ajinyonge!!?
Jpm hela utazitoa Wapi kila dhehebu likidai barabara utaleta shida kidogo
 
Kweli mfumo kristo hauwezi kuisha nchi hii

Rais anasemaje eti alimsikia mzee wa upaka analalamika kuwa barabara inayopita kwake mbovu kwa hio kaenda kujionea mwenyewe...
Na katoa ahadi ya kujengwa

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu tumuombee Rais wetu!
 
Lengo lake kubwa ni kuimarisha kanisa kwa kuhakikisha anaondoa uswahili (waislam) wachache walokuwa maofisini , ndo maana kwa haraka sana tumeweka ubalozi wa israel hapa, na kazi ya kuwaondoa waswahili inaendelea vzr, wiki ijayo ni zamu ya IDRISSA KIKULA , WIKI ILOPITA TUMEMWONDOA YUNUS, NA KABLA TULIMTOA DR DAU etc , NDALICHAKO ANAONEKANA KUIMUDU SANA KAZI HII YA KUWAONDOA WASWAHILI KAMA RECORD YAKE ILIVYO
Nimeanza kukuelewa mkuu Leo tumeanza kwenda kanisani na kutoa ahadi za kujenga barabara ili tusipate shida ya kwenda kwenye ibada
 
Wewe utakuwa mkenya, watanzania hawana uwezo wa kuhitaji kufikiria hayo wanasubiri 2020 wapige kura za style ya wabunge wao bungeni...tehteh ndiyoooooooooo....siyooooooooooo hata kama hawajui...
 
Hutumia neno kuwahurumia ''watanzania maskini'' lakini kwa ndani hakuna kitu zaidi ya ukandamizaji, sababu mpaka leo sijaona ata hatua 1 aliyopiga ikaonekana inamsaidia mtanzania mmoja mmoja. fedha zinazookolewa bado zimo mifukoni ni stori za kwenye magazeti na vyombo vya habari tu. bei za vyakula ni pale pale au kuzidi kuwa gali, ajira imekuwa ndoto na hao walio makazini ni timua timua tu ata wakifukuzwa wafanyakazi hawaingizwi wengine mtaani shida inaongezeka ni dalili mbaya sana kwa anakoelekea.
 
Uyu mzee ana nia nzuri sana na hili taifa ila ana kauli zinazoumiza sana,nafikiri kuna mda akiangalia marudio ya speech zake huwa anajikosoa moyoni.
 
Kuna thread humu inaelezea ahadi za Magufuli nenda kaisome....

Halafu kuna Ilani ya CCM nenda kaisome pia.

Halafu rudi hapa uje kutuuliza ambacho hujakielewa....

HAYA ZUNGUSHAA ZUNGUSHAAA TENAA ZUNGUSHA MIKONOOO....MABADILIKOOOO!!!
Piga push up kisha ingia Kwa Lugumi ukanywe chai mchana kashinde kwenye mabehewa ya Mwakyembe utapata wa kukupa Dili la sukari upige magendo ili kesho wakikukamata iawasaidie kuwasahaulisha watu UDOM na skendo nyinginezo kibao .
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida. Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.
Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa? Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi. Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!

Ni mimi pekee ndio ninajua Magufuli atupeleka wapi.

Kifupi tunamfuata Lenin, huku tukienda kuinyume nyume. Tunakwenda ktk UKOMUNIST.
 
Hofu yangu juu ya yanayoendelea nchini

Ni dhahiri sasa bila kumung'unya maneno nchi hii inaelekea katika ombwe la Demokrasia.

(1) Tulianza kwa kuona nyumba za wananchi mabondeni zikibomolewa bila huruma, tushukuru mahakama ilipifa stop lile zoezi la sivyo hali ingekuwa mbaya zaidi.

(2)Tumeona Bunge likiminywa, lisionekane Live

(3) Tumeona watu wakisimamishwa kazi hadharani kwenye majukwaa ya kisiasa

(4)Tumeona watoto UDOM, waliodahiliwa na serikali ileile ya CCM wakifukuzwa kwa notisi ya masaa machache tu

(5) Tumeona wafanyabiashara wakitaitiwa, wakipelekewa vyombo vya dola eti wameficha sukari.

(6)Sasa tunashuhudia Vyama vya upinzani vikizuiwa kufanya siasa

HOFU YANGU.
(1) Mitandao ya Kijamii yenye Sauti kama JF kuanza kusumbuliwa

(2) Kubambikiana Kesi, ili kuwanyamazisha watu wenye kuukosoa utawala huu

(3) Kufukuza watu Kazi kisiasa, kuwapelekea wafanyabiashara bili za kodi kubwa

(4) Watu kupotezwa

TUNAFANYAJE?

(1) Tuwaunge mkono Wabunge wote wenye kuweka mbele maslahi ya Umma badala ya vyama vyao

(2) Ni lazima Vyombo vya habari viwe jasiri kuliita Sepetu, Sepetu

(3) Ni lazima tuendelee kuzungumza, kupiga kelele na kuusimamia ukweli

(4) Kila mmoja kwa nafasi yake hana budi kuwaelimisha wananchi madhara ya Ubanaji huu wa Demokrasia unaotamalaki kwa kasi nchini, vijiwe vya kahawa, vijiwe vya magazeti, kwenye magulio huko vijijini, misibani, kwenye vikao vya kifamilia, sherehe n.k

(5) Wasomi wetu, tunawahitaji kuliko wakati wowote ule tangu mfumo wa vyama vingi uanze, ni lazima wasimame bila woga

(6) Ni muhimu sana kuitumia mahakama kwa ajili ya kudai haki

Nchi hii tulipigania uhuru siyo kwa ajili ya barabara, maji na umeme peke yake, Tulitaka uhuru wa Kuendesha nchi yetu kidemokrasia, Tulitaka heshima ya kujitawala kwa maana uongozi unaoheshimu raia, unaolinda haki za binadamu, unaoheshimu uhuru wa watu wake, unaoheshimu utu na uongozi wa sheria.

Katika vitu ambavyo Watanzania hawatokubali na ninawatahadharisha viongozi wote wa leo na Kesho ni kwamba kwa mujibu wa misingi iliyowekwa na waasisi wanchi hii, Kamwe Watanzania hawatakubali Kuburuzwa Kiimla. ile hasira ya Umma waliyokutana nayo mwaka 2015, inaweza ikageuka mara kumi yake!, Ni hatari, naogopa sana! . Ni vizuri wakajifunza na kulijua hili.
 
Kwa serikali hii ilivyo ya kibabe uwepo wa JF hewani uko mashakani sana.

Soon tutaminywa tu, subiri uone.
kuna tetesi kwamba kule facebook wameanza kuzishughulikia account za baadhi ya watu wanaomkosoa JPM.

labda wamebaini mapungufu kwenye ile sheria yao ya mtandao.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom