Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Hao wameanza na nauli tu ya kwenda Mkuranga ?
Inawezekana wakawa wamejiunga group wakafika hapo walipofika na nadhani ni wahitimu wa Udsm lakini wametoka kimaisha wengine kwa kulima tu bustani za mbogamboga wamenunua magari,

Sitaki kujua wameanza na pesa kiasi gani lakini utayari walikua nao na wamefanikisha pakubwa hawakubweteka
 
Kwahiyo ndugu yangu unakaa kijiweni kusubiria mbowe au seif waje kukujengea uchumi wako na ndugu zako? umepotea njia
 
Hayo mashamba yamerudishwa sababu ya kutokuendelezwa zaidi ya miaka 20 ni mapori, wakati kuna wananchi wanakosa ardhi ya kulima na kufuga wakulima na wafugaji wanauana sababu ya kugombea ardhi kidogo wakati watu wamekalia tu ardhi ya serikali bila kuiendeleza lazima wapewe wananchi wenye uhitaji nayo.
 

Nielewe ndugu, simtetei Sumaye kwani hanisaidii lolote, pakia basi nenda mpaka kigoma, sehemu kubwa ni mapori tena mazito. Sio kwamba watu hawayaoni, bali uwezo wa kuyageuza kuwa mashamba ndio ngoma. Ndio maana nikasema kama kweli serekali ina ni njema ya kuwapa wananchi mashamba ni lazima watenge fungu la kufanya hivyo. Watoe madozzer kwenda kusafisha hayo mapori, wachimbe maji kwenye maeneo hayo, watoe pembejeo uone kama watu hawajaenda wenyewe. Hii kusema unawapa watu mashamba ambayo ni mapori nao watabaki wanayamiliki yakiwa mapori hivyohivyo bila tija.
 
Sasa shamba upewe bure, unataka tena wakulimie na kukuchimbia maji? Dah wewe tafuta shughuli nyingine tu ya kufanya.
 
Sasa shamba upewe bure, unataka tena wakulimie na kukuchimbia maji? Dah wewe tafuta shughuli nyingine tu ya kufanya.

Hakuna mwenye akili timamu anayetaka shamba la bure, tena ni rahisi hayo mashamba yakatolewa kama mkopo kama wanavyofanya nyumba za NHC, baada ya hayo mashamba kusafishwa na hiyo miundo mbinu kama drip systems, kuchimba visima au malambo kuwekwa. Kinyume na hapo kwenda kumpa mtu pori mwenye fyekeo, panga na jembe la mkono ni kumfungisha ndoa ya kudumu na umasikini. Ndio ile unakutana na mtu anamiliki zaidi ya heka 5 za pori lakini anaendesha bodaboda mjini, mpiga debeb ubungo nk
 
Ukisoma ilani ya chama chako ndo utajua ya kuwa alipania kuitoa nchi kuipeleka sehemu....
Leo mnaruka ahadi zenu
 
Acacia wanadai Trilioni 5

Ile meli ya samaki za Magufuli,wenyewe wameamka wanadai Trilioni 1.2

Jumla trilioni 6.2, hii no hasara tuliyopata kutokana na wewe kuvunja mikataba na taifa litatakiwa kulipa,

Hizi trilioni ni sawa na makusanyo ya kodi ya miezi sita

Bado bilioni 87 za wale jamaa waliokamata bombadia

Ile sheli ya MWARABU uliyovunja mwanza tulilipa mamia ya mabilioni

Wizara ya ujenzi inaongoza kwa kushtakiwa na wananchi na kudaiwa matrilioni

Sasa Mimi nakuuliza,tangu tupate Uhuru,ni maamuzi ya waziri gani/kiongozi yaliyolitia hasara taifa zaidi ya trilioni 6? Na huyo ni waziri mmoja/kiongozi

Tumesikia mawaziri wanaofata sheria na taratibu wakiitwa wapumbavu kwa kuchelewa kuamua,je wafanye maamuzi kama yako yatakayoitia serikali hasara ya matrilioni? Kufata sheria na taratibu imekuwa upumbavu siku hizi?

Sasa kila waziri akikurupuka na mwishowe akaishia kuleta madeni ya trilioni 6,na nchi INA mawaziri zaidi ya 30,si nchi itakuwa inadaiwa trilioni 180?

Sisi tunataka utuambie wewe mwenyewe,wewe binafsi,bila kutumia kodi zetu,umejipangaje kuwalipa hizo trilioni 6

Binafsi naamini madeni yote ya kuvunja mikataba kutokana na maamuzi yako yanaweza kufika trilioni kumi,zikikusanywa kesi zote za pale wizara ya ujenzi na sasa ukiwa mkuu,

Hii no hasara iliyoletwa na mtu mmoja tu!

Nadhani wale waliokuwa wanahoji mbona DENI la TAIFA NI KUBWA LAKINI HAKUNA MAENDELEO wamepata jibu,madeni yenyewe ndio haya
 

Bado kimara had I kiluvya mtalipa trillions,ukichaa utatuponza
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…