Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Tulipigania uhuru wa nchi za kusini mwa Afrika kwa hali, mali na DAMU, tukasahau kupigania uhuru wetu. MACHOZI YANANITOKA, pole Tanzania, pole sanaaaaa. Tulikua tunawalaani makaburu, sasa sisi wenyewe tunawafanyia watanzania wenzetu ukaburu.
 
Rais wa Tanzania amezidi kupoteza kuungwa mkono na walio wengi katika jamii. Watu kutoka chama chake pia wameanza kumpinga.

Hakujawahi kuwa na siku ya furaha katika Ikulu ya Tanzania toka Magufuli awe rais. Kama umemuona kiongozi yeyote akitabasamu akiwa karibu na rais basi ujue ni kwaajili ya kulinda kitumbua chake na si vinginevyo.

Katika muda mfupi alioongoza ambao unaonekana kama miaka elfu tayari, kumekuwa na amri za ajabu ajabu na kujiuzulu kwa viongozi wakubwa katika serikali bila majibu ya kutosha.
Ila rais mwenyewe anasema hakuna 'tatizo' katika utawala wake japo kinachoongelewa na wananchi mitaani ni stori tofauti kabisa.
Baadhi ya viongozi kutoka CCM wanaielezea Ikulu kama meli inayozama.

Magufuli amezidi kutengwa au kujitenga katika jamii. Wafanyabiashara wakubwa na viongozi makini wakimuona kama 'ugonjwa wa kansa' kwenye uchumi wa nchi.
Kusudio lake la kuua demokrasia nchini limemjengea chuki na zaidi ya nusu ya watanzania.

Wengi tumeanza kujiuliza kama Magufuli atamudu siku ngapi zaidi mbele kama rais???
 
Jamaa yangu mmoja akaniuliza kwa hali hii maisha daily yanazidi kuwa magumu. Je tutafika?

Ukweli ni kuwa watanzania ni wavumilivu sana. Tutafika na tutaanza tena safari nyingine kwa kipindi kingine. Tutafika ingawa wengi watakuwa wamejeruhiwa sana. Wengi watafika wakiwa na ulemavu.

Safari ni ngumu kuna ambao watafia njiani hapo tuwaombee tu huko waliko waenende kwa amani. Kuna ambao tayari roho zao ni kama wamezitoa rehani hawa wameshasaini mkataba wa kufa au kupona. Wanaweza wakafika mwisho wa safari lakini kwa mateso makubwa sana. Hawa watabebeshwa mizigo ya wengine.

Kuna ambao hawa watatakiwa kuwabeba wengine ili hawa wengine wasafiri kwa raha.wapo. na wapo ambao watalazimika kuwabeba walemavu,maskin na wazee kwa upendo wao...watafika wakiwa hoi sana.

Kuna ambao watauawa njian...hawa wataonekana wanazorotesha safari.ni mzigo... Hivyo watakatishwa safari zao.

Mwisho wa yote. Tutafika.... Ila asilimia kubwa watakuwa na majeraha au vidonda vikubwa sana. Wengi watakuwa na ulemavu.wamepoteza macho au jicho, hawataona tena yanayoendelea. Wengine ndimi zao zitakuwa zimegandamana na vinywa vyao hawataweza kunena tena. Kuna ambao watakuwa wakichechemea kutokana na kukatwa mguu au wakitambaa kwa kukatwa miguu yote miwili. Lakini tutafika tu.

Iwe mchana au usiku, iwe mvua au kiangazi, iwe majira ya joto au baridi tutafika.
 
shall we make it?-makwaia
patamu hapooooo,parudie tena(in makwaia's voice)
 
To be honest, uungawaji wa mkono kwa jamaa ni kwa watanzania wachache sana hasa wanachama wake. Watu wamechoka hawaoni faida yeyote itokanayo na maamuzi yao ya 2015 zaidi ya maisha magumu kila kukicha. Wafanyabiashara hawana hamu kabisa mambo hayaendi mbele kila mtu analia na hali ngumu, watu wanashindwa kurudisha watoto shule walizokua wakiwasomesha watoto wao baada ya kukosa karo.

Pamoja na mambo mazuri yanayosemwa kua kayatimiza, kulikua na haja gani system nzima ya mifumo ya kibiashara kwenda mrama? Sasa kua na kiongozi flani ndio kuwe na maisha magumu jamani? Is it necessary to live within a worsened situation while it my come back to knock for its existence again?

2020 bado na hali hii hii na hata kama unapata mlo mmoja kwa siku utasema naenda kumchagua jamaa tena aboreshe maisha yangu walao nipate milo miwili kwa siku? Yaani amefanya ule mlo mmoja, bado utarudi kumpa kura akupatie milo miwili, how come?


Mbona wakati wa jamaa wa Msoga usalama ulikuwepo, majengo kule UDOM na kwingine yalikua yakiporomoshwa tuu? Mbona Life lilikua safi tuu? Kwani life kua gumu ni kwa sababu ya kuziba mianya ya rushwa au ni namna ya kuchagua kupanga jamani? Mbona hapo Rwanda Life ni tamu sana na pesa ipo ya kutosha watu wanafurahia maisha?
 
HAMNA.

WAMEJIFUNZA SASA KUWA KUTOKA CHUNGU KILE KILE HAKUNA JIPYA.
 
Nilikuwa nawaza ka nitamchagua tena lakini kwa anavyo wanyoosheni, nadhani nitapiga kura 3 za ndiyo. Baki Magu, Baki umwage tena maji moto miaka ingine 5, viuno vyetu vitanyooka tu. Hekooo Maguuu.
 
Hakuna kwa sababu hata serika yake haina hata mvuto. Niliongea namzee ambae ulikuwa ukimchanja anatoka damu ya ccm lakini nimempigia simu juzi anavyowatuka serkali huwezi kuamini.
 
Mkuu u are very correct..

Huyu jamaa amefeli completely..

Kuna sababu nyingi zilizopelekea hali kuwa hivi. Pamoja na namna alivyovuruga mifumo mingi hasa ya uchumi na biashara,hakuna kosa KUBWA alilofanya kama la kuvuruga DEMOKRASIA hii Nchi ambayo ilikuwa imefikia.

Hivi sasa Tanzania isn't a DEMOCRATIC Country.

Nchi hii ili iende mbele inahitaji investors hasa Foreign Investors. Hawa ndio watakuja kuwekeza, ajira zitapatikana,kodi itapatikana na uchumi kufunguka.

Hakuna foreign investor anayeweza kuja Tanzania hivi sasa.

Kitu cha kwanza muwekezaji kabla hajaamua kwenda kuwekeza kwenye Nchi yoyote anatizama hali ya DEMOKRASIA kwenye Nchi husika. Nani atakuja kuwekeza mahali ambapo hujui kesho yako??

Hakuna foreign investors hakuna uchumi utakaokuwa kwa Hizi zetu za Africa.

Ndio maana Kenya a lot of investors are running into that Country. Wana problem ya Ethnicity,wana problem za hapa na pale za insecurity lakini Kenya is a Democratic Country. Hiyo tu ni uhakika mkubwa kwa investors.
 
Hata kama wewe ni muwekezaji,ukisikia mambo ya wadai mpaka wanashika ndege nje ya nchi ili tuwalipe,utawekeza?Labda kama pesa uliokota!
 

Anatupeleka motoni
 
"Memori fullu!"
Ukigeuka hivi, huyu kacharazwa na Dc, ukitaka kujikuna, huyu kanyimwa dhamana, ukisema uanze kusali, huyu kasepa na rambirambi! Ukitaka kwenda kuoga, huyu anazuia sabuni hadi ulipe deni la ugoro... Ukitaka kuketi kula, huyu ashaagiza uhame mji bila ndala!

Ukitaka kujipumzisha baada ya stress za mchana, buldoza linachungulia dirishani! Ukisema ushike mswaki upunguze wadudu mdomoni, mkemia anataka mkojo apime wadudu wa mdomoni...

Ukitaka kula makande, huyu ashazuia mahindi anasema yasagwe! Ukiinama ufunge kamba za viatu, noah ishafunga breki miguuni... Ukisema ufanye kazi kwa bidii, huyu anataka ukrem jina lake... Ukitaka kulia kwa ghadhabu, unawekwa korokoroni kwa kupigia watu kelele isiyowahusu....

Ukitaka kuandika shairi lako, washakudaka na sheria ya mitandao... Ukitaka kupanda bajaji, washakulazimisha upande pangaboi... Ukimdai bosi mshahara wako, ashakutupia jembe ukalime... Ukikodisha shamba ukalima, jua lishaizidi mvua na hakuna msaada....

Ukitaka kumpeleka mwanao chuo, washakuitia mkopo kwenye ofisi za chama... Ukitaka kwenda Zimbabwe, usharudishwa na ushuzi wa babalao.... Ukitaka kuwa karibu na mema ya nchi, ushaulizwa kama wewe ni "sibling".'.. Ukitaka haki yako, washakulazimisha usimamishe msafara wake....

Ukitaka "kupupu," ushadakwa uoneshe risiti ulikula wapi.... Ukitaka jshshsjsosks, jshdjejsie????(peni imegoma ngoja nijaribishe tena...) nsnsjshdeueuhdisisksks! (Naenda dukani kusaka nyingine)

Ila nikirudi, Hasira zote nazimaliza kwa marafiki wanaopost picha kuanzia januari hadi disemba...... No, sio hao... Ngoja.... Nimekumbuka... Wale wanaohamisha posti za wenzao hawataki kushea, wanazikopi na kuzifanya zao.... Nawablokuuuuuuuuuuuuu hadi vidole viume....

Memorifufjfjdirirrirkkkmmldjdjdieiss!'&#&#$&÷&#
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…