Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Hiyo takwimu ya kila mtu ananalamika umeitoa wapi? Labda kama ya mtaani unakoishi ndio wanalalamika pasi kujua tatizo wanalo wao.
Ila weye ni hopeless kwelikweli! Kitu kikiwa kinanuka utamaizi muonekano wa pua na sura za waungwana kwa yanayowafika. Harufu mbaya haishikwi kwa mikono wala kuhesabiwa kama bagia. Grow up mtu!
 
"Ukiwa Raisi unatakiwa ujue hali za wananchi wako na kuzifanya ziwe bora",,raisi anapigania matatizo ya jumla kama elimu,dawa,barabara,maji,umeme na miundo mbinu kwa ujumla,tatizo nyie mnaongelea matatizo binafsi ndo maana nilikupa mifano fulani.Ok.. mfano mwingine USA tunaiita LAND OF OPPORTUNITY,ila marekani hiyo hiyo kuna wabongo kibao wanalalamika mambo magumu na kulalamikia system,tofauti kule unakufa kivyako tu,hakuna wakukusikiliza,maana yangu ni kuwa mtu mweusi ameumbwa mlalamishi sana.Tangu serikali ya Nyerere mpaka hii awamu ya tano hakuna siku watu hawajalalamikia serikali hata ingefanya nini.Pambaneni na hali zenu.
 
Mishahara kwa watumishi wa umma haijaongezwa toka 2014 , ina maana mtumishi atakaye staafu mwaka 2017 atalipwa sawa na yule wa mwaka 2014 , kwani huko si kuchezea maisha ya wa Tz huo ni mfano mmoja mingine ongezea mwenyewe.
Mkuu kama wewe ni mtumishi wa umma,kwenye mkataba wako umeandikwa mshahara utaongezeka kwa % ngapi?,na kila baada ya muda gani?
 
Kwa hiyo umekaaa, ndiyo umewasili na utetezi nyololo hivi? Mambo ya Wamarekani unataka kuyafananisha na uwanja wa fisi kwa lipi hasa? Hakupata Urais ili ajifananishe na mtu. Alisema hatawaangusha! Akatwanga na tu-pushapu twa kimtindo. Mumwambie nchi inaelea kwenye ufakiri. Abadili mbinu za kupiga pushapu.
 


Nchi iko sawa tu..Kwa mfano ukiwa nje ya nchi,ukapitia JamiiForums kwa wiki 3 au 4 mfululizo, unaweza ukafikiria Tanzania inaungua moto,labda watu hawali hata mchana kwa malalamiko ya humu, ila ukifika bongo ni picha tofauti kabisa,maisha yanaendelea kama kawaida.

Kuna mtu alianzisha uzi hapa september mwaka jana akidai hali ya uchumi ni mbaya sana hata wiki tatu hazitaisha yaweza tokea hatari yoyote uchumi usipobadilika,baadae nikagundua yawezekana ilikuwa deadline yake ya kulipa kodi asitolewe vitu nje au kitu kama hicho.Wengi wakizidiwa madeni wanakimbilia JF kulalamika.
 
Wengi wakizidiwa madeni wanakimbilia JF kulalamika.
Hahahaaa. Vijana wa Dotcom wanapenda anasa pesa hawana. Ikifikia mwenye nyumba anadai kodi ya pango lake wanalalamika pesa mtaani haipo serikali imebana.
 
Hahahaaa. Vijana wa Dotcom wanapenda anasa pesa hawana. Ikifikia mwenye nyumba anadai kodi ya pango lake wanalalamika pesa mtaani haipo serikali imebana.
Mkuu hawa vijana walizoea mtelemko,walizoea wepesi wepesi,awamu hii ni kukaza buti ili gurudumu lisonge,ila nawaambia kila siku hasira hazisaidii,ni kubadili mwenendo tu.
 
Jmc06 lazima utambue unapofanya kazi unahitaji faida kama mfanyabiashara mwingine yeyote na faida yako kama mfanyakazi huoneka kwenye kiinua mgongowmgongo .
 
tatizo lenu meweka high expectations,

na yeye ni binadamu,

mie naamini kwenye mgawanyo wa madaraka,

Nchi igawanywe katika zones,

east wawe na kiongozi wao,

west zone,wawe na wa kwao,

north and south wawe na viongozi wao,

Rais awe mtendaji mkuu wa zones zote,hii itampunguzia mzigo,sio leo makanikia kule,leo sijui vichwa vya treni,for one person its a lot take on,




 
Mfano uliotoa hauendani, ulishawai kumwona mzazi anamwachisha/mfukuza kazi mwanae? Au ulishawai kumwona mzazi anamnyima mkate mwanae ?tena hawawaji ata kukosana.
 
Hiyo takwimu ya kila mtu ananalamika umeitoa wapi? Labda kama ya mtaani unakoishi ndio wanalalamika pasi kujua tatizo wanalo wao.
Basi ni kweli wewe ni mpiga zumari wa mfalme kama hujui kinacho endelea mitaani, makazini hata vyuoni! Na kwa taarifa yako hata wale wa mabaka mabaka nao wanalalamikia hali mbaya sana hasa baada ya kufutiwa yale maduka yao yenye nafuu
 
Basi ni kweli wewe ni mpiga zumari wa mfalme kama hujui kinacho endelea mitaani, makazini hata vyuoni! Na kwa taarifa yako hata wale wa mabaka mabaka nao wanalalamikia hali mbaya sana hasa baada ya kufutiwa yale maduka yao yenye nafuu
Leta takwimu sio kuleta fununu. kama uyasemayo unayajua yabainisha hapa. Twende kwa facts.
 
Mfano uliotoa hauendani, ulishawai kumwona mzazi anamwachisha/mfukuza kazi mwanae? Au ulishawai kumwona mzazi anamnyima mkate mwanae ?tena hawawaji ata kukosana.
Kwa maana hiyo unataka watu wasifukuzwe kazi hata kama hawastahili kuwepo kazini? Ndicho hiki kutu mnacholilia?
 
Ukikua utaelewa Ila kwa Sasa una haki ya kufikiria hivyo
 
'Zip up your boots Magu and advance forward' usisikilize vilio vya WAKORA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…