Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Kuamini maendeleo yataletwa na chama fulani ni zaidi ya uwendawazimu

Mfumo wetu wa kuongoza nchi ni kwa kupitia vyama vya Siasa . . , Sera za maendeleo , uchumi, afya, elimu, na kila kitu chetu tunachofanya hapa nchini vinabuniwa na wanasiasa wa ccm . .
Sasa unasemaje maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa . . ???!!
 
Wapinzani wa Tanzania ni wanaharakati. Hakuna serikali yeyote duniani inayoweza kuwavumilia. Wanamlaumu Magufuli kwa nchi kukosa amani lakini wanatakiwa waangalie kioo. Wajipime wanayoyafanya ni DEMOKRASIA AU DOMOKULASIE.

Hakuna serikali yeyote duniani inayochukua ushauri kwa chama cha upinzani.

Hawa jamaa wakisharopoka wakipuuzwa wanasema Magufuli hashauriki.

Kimsingi wanataka washiriki kuongoza nchi. News flash!!! Hawako madarakani. Waache walio madarakani watekeleze sera zao zilizowapa ushindi kwenye uchaguzi.

Ni upuzi kupambana na serikali eti wanaikosoa. Unaikosoa kwanini. Ukiikosoa itarekebisha makosa yake na itashinda uchaguzi ujao. Iache iharibu halafu tumia makosa ya serikali kufanyia kampeni uchaguzi ujao.

Sasa hivi chama cha Democrat cha Marekani kinajiaanda na uchaguzi ujao.

Hakijiandai kwa kupambana au kumtukana Trump. Kinajiandaa kwa kufikisha ujumbe wao kwa wananchi.

Wamegundua sababu kubwa iliyofanya Trump ashinde ni udhaifu wa mgombea wao kisiasa na kukosa ujumbe au ahadi za maana kwa wananchi.

Na hawajiandai kwa mikutano na maandamano ya chama. Maandamano ya Marekani hasa kwa kipindi hiki ni fujo tu na yanaishia polisi.

Wanajiandaa kwa kutumia vyombo vya habari na mitandao.

Wanajiandaa kwa kukusanya pesa za kampeni.

Wanajiandaa kwa kukwamisha maazimio ya Trump bungeni.

Hawapambani na serikali wanapambana na wapiga kura.
 
Kabisa ni km kuota pilau msimu wa njaa
 
Nashangaa sana kuona baadhi ya watu(watanzania) wenye MAWAZO MGANDO na UJINGA uliopita kiwango wakiendelea kushabikia mambo anayofanya the so called president katika nchi yetu, kwa hakika ameifanya tanzania kuwa si sehemu salama kiuchumi, kisiasa na wala kimaendeleo kwa ujumla ukizingatia ni miaka miwili sasa anasema ananyoosha nchi, swali je ilikuwa imepinda? Anaendesha nchi Kimihemko na kishamba kabisa!
 
Naomba unijibu haya maswali,
Kule mnako tembeza Bakuli kimya kimya hakuna wanasiasa?
Na je kama kuna wanasiasa wao wamepataje maendeleo mpaka mnaenda kutembeza mibakuli?.
Mbona magufuli alikua anasema kua Tanzania tutakuja kuwapa watu misaada je unaamini hilo?
Na kama unaamini hilo mtarudisha mikopo yao lini mpaka muanze kuwapa misaada nchi zingine?!
 
nakucorect kidogo msomi international space unayoiona juu mrussia ndio yake bt wana special agreement na marekani,china,japan pamja urope countries..
Sasa hapo nimekosea nini ? Mimi nimeitaja marekani na nchi zingine washirika na sijataja marekani kama ndo mmiliki pekee ya ISS
 
Kutoelewa hoja nako ni magonjwa kama magonjwa mengine.

Wewe unataka mimi nikishabikie chama kwa kukionea huruma??
Kisa eti nikicuanga, nikikabidhi nchi kwa majaribio??

Nengependa ukatambua kabisa nchi sio maabara pa kufanyia majaribio ya vyama, tunataka chama kitakachosimamia maslahi ya taifa
 

Tatizo lenu nyinyi wasomi mnataka mpige pesa za dili au za rushwa kwani Pombe kavuruga uchumi wa wananchi wake kivipi? ukiwa kama msomi lazima ufafanue hoja yako vizuri/Ukitegemea pesa za dili utapoteza muda wako bure,pia mnapenda kuishi maisha yasiyo na uhalisia na vipato vyenu,Serikali iliyobora kiongozi inatengeneza mfumo uliobora kwa wananchi wake na wala hawagawi pesa .
 
Wanasiasa wapo.
Lakini siasa zetu sio kama hizi zibazofanyika tz,
Kutembeza bakuli hilo ndio nalisikia kwako, sijapata taarifa rasmi.

Kuhusu maendeleo wao wameweza kutofautisha muda wa siasa na muda wa majukumu

Kuhusu kutoa misaada ni suala la muda, udhibiti wa mali asili umeanza, masharti maoya ya uwekezaji umeanza ili uwe na tija kwetu.

Tutaanza kunufaika na maoato yatokanayo na mali asili zetu
 

Kwa lugha yako to ulipoanza na kumaliza Kama umesoma basi chooni. Ungekuwa na point na nia njema tungekomment kukusaidia. Ila bahati mbaya hakuna mwanadamu asiyetenda jema. Na kama sikosei Dr hajafikisha hata 2 years. Hata wewe na pumba zako at least umeandika kwa kusomeka.
 
Kuhusu Lugha usiongee ,Magufuli anatumia Lugha chafu kuliko mtu yeyote duniani.
Na ndio tumerithi kwa muda mchache huu aliotuongoza.
Tofauti unayoona ni kua huyu kaandika tu, na Magufuli yeye anayatamka hadharani.Rejea clip zake zote hakuna Lugha nzuri hata moja.
 
Mtu aliyeshindwa kuendesha familia yake, unategemea aongoze watu millions kadhaa .
 
Nikupe mifano miwili hai:

MFANO wa 1.
Marekani na nchi za magharibi waliwadharau sana Urusi walipoanzisha kituo chao cha utafiti angani kilichoitwa MIR. Warusi walitumia teknologia rahisi sana ya kupeleka/kurejesha watu na vifaa kwenye MIR yao. Walijifunza mengi kuhusu athari za binadamu kukaa angani kwa muda mrefu.

Wakati wote huu Marekani ilitimbwirika kupeleka mtu mwezini na kumrudisha hai, waliunda space shuttle kupeleka vyombo angani. Mwisho wa siku Wamarekani wakakubali kuwa mission na system za Kirusi ni bora kuliko zao na ndipo wakaomba waungane kujenga hiyo ISS na kutumia system rahisi kama ya Kirusi ya kupeleka na kurudisha wanaanga kwenye ISS.

Mrusi walimdharau mwanzoni lakini mwisho wa siku wakakubali kuwa system za Kirusi ni bora na bei ya chini kuliko zao.

MFANO wa 2.
Kwa kipindi kirefu sana Marekani na Ulaya waliona kuwa mfumo wao wa kibepari (capitalist system) ni bora zaidi na kuwadharau China kuwa mfumo wao wa kijamaa ni duni. Wachina waligangamala na mfumo wao, wengi wakiuita ni wa kidikteta (reminds you of anyone?). Leo hii China imeikaribia marekani kiuchumi na ndio wanaowakopesha Marekani. Marekani inadaiwa mpaka kwenye kope na Wachina.

Imekuaje nchi ya mfumo wa kikomunisti iwapite wenye mfumo wa kibepari? Swali zuri sana.

HITIMISHO:
Usizidharau juhudi za Magufuli katika kuleta maendeleo TZ. Hii nchi ilikuwa haiendelei kwa sababu kila mtu alikuwa anachota toka serikalini tani yake. Sio viongozi wa juu, makampuni ya nje, mpaka mtumishi wa chini kabisa (mesenja) alikuwa amategemea kuchota kutoka hii serikali. Hatua ya kwanza ya kuleta maendeleo ni kuhakikisha hii mianya ya uchotaji rasilmali zetu inazibwa. Magufuli amejaribu kwa kiasi kikubwa kuiziba na ndio maana wale waliokuwa wanategea ule mfumo wa zamani wanapiga kelele kuwa maisha magumu.

Kama Marekani ilivyowakejeli Urusi na Uchina hapo nyuma na sasa wanafuata nyayo zao, vile vile hata watu wanaomkebehi Magufuli kwa sasa watakuja msifia na kufuata nyayo zake hapo baadae.
 
Mkuu, inabidi uelewe kitu kimoja kwa sasa hapa bongoland. Ni kwamba mtu anakuwa na frustrations zake halafu hapa jamii forum ndio sehemu ya kutafuta kuziondoa.

Maybe kagombana na mkewe, kafukuzwa kazi, au kaharibu tu maishani kwa namna moja au nyingine, kwa hiyo ili aondoe stress, anakuja kuandika uzi ambao kadri anavyopata wachangiaji ambao ni wa aina yake ndivyo kichwa chake kinakuwa chepesi.

Uhuru wa kuongea na kuandika, unageuka sehemu ya tiba za maumivu mbalimbali ya vichwa vya baadhi yetu watanzania.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…