Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
¶ Viwanda vyetu mlibinafsisha.
¶ Mashirika yetu mliyaua ninyi.
¶ Nyumba za serikali mliuza wenyewe.
¶ Migodi yetu mmewapa makaburu.
¶ Mafisadi mnawapa hadi uenyekiti wa bunge.

Leo mnakuja na wimbo wa "UZALENDO". Siwaelewi, kama sigara ya nyota. Mbele unavuta, nyuma unavuta.
Kwani Vilibinafsishwa na Upinzani.. si na Hao hao kidumu chama Cha Mapinduzi
 
Kwanza nafahamu kuwa kuna mijitu mioga itafuta huu uzi h

Napenda kuwatangazia umma wa watanzania wote kuwa kinachofanyika nchini sio matukio yanayotokea sio kwa bahati mbaya. Katika jicho la tatu ni wazi Magu anataka kubadilisha katiba kutawala milele. Magufuli

1.Mauaji ya kutisha.

Ni wazi na wengi wetu mmeona matukio ya mauaji ya kutisha yanayotokea toka uhuru wa nchi hii. Tunaanza na Kibiti,watu kupotea,viongozi wa upinzani kupigwa risasi na kuuwawa na hata kuminya demokrasia. Magufuli anachotaka kufanya watu wasiongee na wala wasiwe na maoni juu ya nchi yao na yeye kufanya kile anachotaka kufanya nacho ni kutawala maisha.

2.Utawala wa Mabavu (Police State).

Sasa hivi kama mnavyoona,jinsi gani polisi wameshika nguvu na kutumia mabavu juu ya wananchi. Wanatumia nguvu nyingi kushindana na raia ambao hawana silaha.
Kwa mfano tukio lililosababisha kufa kwa mwananfunzi kwenye basi ni tukio liliopangwa.Haiwezekani katika mtu kwenye basi akapatwa na risasi (point black) kama hakuna aliyedhamiria na kufanya target kuua raia. Huyu mwanafunzi aliuwawa kwa makusudi kabisa.

3. Singularity and popularity.
Magufuli anachotaka kufanya ni kutawala milele na kufuta kabisa kwa kila namna yoyotw ukosoaji wa serikali yake na upinzani.
Anachotaka ni kubadilisha katiba na wabunge wa CCM hawtakuwa na kipingamizi bali kusema ndio. Hapo ndio itakuwa mwisho wa Tanzania.Raisi magufuli pia anatafuta matukio kwa hali yoyote kwa kutunga au uwongo kujaribu kuwa relative na kuonyesha anapendwa.

Nilichokiandika hapa ni mawazo yangu mwenywe na maon yangu.
 
aisee ww uliandika muda mrefu uliopita lakn ukisoma sahiz ni kama umeandika jana. hongera sana. kiujumla tushapotea mazima
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Mkuu mbele ni giza giza giza. Hakuna nuru kabisa.
 
Kuna thread humu inaelezea ahadi za Magufuli nenda kaisome....

Halafu kuna Ilani ya CCM nenda kaisome pia.

Halafu rudi hapa uje kutuuliza ambacho hujakielewa..
Ahadi ahadi ahadi. Zitatekelezwa lini?
 
Anachokitaka hakieleweki katika nyanja hizi:-
  • Uchumi.
  • Siasa.
  • Jamii (ustawi na utangamano wake).
Kiuchumi. Taifa liko ktk mserereko hasi (deceleration) awamu hii. Ni muda muafaka wa kumkatalia na kumkataza anakotupeleka.

Kwenye siasa. Tunachagua kiongozi kusimamia tulichokubaliana kifanyike (katiba) na siyo kutuamlia nini kifanyike. Tusikubali kugawanywa na kujengeana chuki.

Kijamii. Asibadilishe mila na desturi za watanzania bali avisimamie.
 
Kiuchumi anataka yeye ndio awe tajiri mkuu nchini ili akitoa msaada wa milioni kumi aonekane mungu.
Kijamii anataka kutugawa ili atutawale vizuri - divide and rule
Kisiasa hataki habari ya kupingana kwa hoja iwe ndani au nje ya ccm, ni 'ndiyo mzee'
 
Ukiwa hujifunzi na kutangamana na wenzio hata vitu vya kawaida unaweza kufikiri ni vipya sana kwako..wini wini situesheni ni ya kawaida sana kwenye maisha ya kila siku !
 
Huyu mtu ni simply mshamba,kule Uganda kina Kenyatta walikuwa wanamcheka kwa kebehi kwa kila utumbo alokuwa anamwaga
 
Huwa na mawazo mkurupuko ambayo anashindwa kuyaweka kwenye mkakati sahihi.
Kifupi ni mwenye ndoto na matamanio isipokuwa anaamini yeye anajua kila kitu na haamini wasaidizi wake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom