Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Nimepta tabu sana jana alipokuw akisema tunahitaji wafanya bishara na wala yeye ajaagiza wafanywe mbaya, Amasahahu ni mwaka jana tu alikuw akipiga mikwara na kusme ahata wakifunga au kuhama wahame tu hata akibaki mmoja sawa.
leo kasahahu kauli zake na anajikana.
 
Hivi ile remote control tokea msoga iliyokuwa inasemwa ina nguvu ajabu na kudaiwa kukontro tv za mnazi mmoja na maeneo jirani vipi imeishiwa betri? maana tv inajiongoza yenyewe tu mwaka wa -2 kwa mujibu wa kaunti dauni ya m.ayo
 
1. Anatutoa kwenye usafiri wa treni wa enzi za kikoloni unaotumia muda mrefu njiani anatupeleka kwenye usafiri wa treni wa kisasa unaotumia umeme na muda mchache njiani kusafirisha Watu wengi na mizigo mingi.

2. Anatutoa kwenye usafiri wa anga wa ndege uliokufa anatupeleka kwenye ufufuo wa shirika la ndege lenye ndege mpya sita.

3. Ametutoa kwenye shirika la simu lililokufa ametupeleka kwenye ufufuo wa shirika la simu linaloleta ushindani mkubwa kwenye makampuni ya simu yaliyokuwapo kutokana na ubora wa huduma na wa gharama nafuu.

4. Ametutoa kwenye uchumi uliokuwa asilimia 5.1 mwaka 2015 mpaka kutupeleka kwenye uchumi unaokuwa wa zaidi ya asilimia 7.2

5. Ametutoa kwenye mzigo wa kulipia elimu mpaka kutupeleka kwenye unafuu wa elimu bure kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari.

6. Amewatoa akina Mama Wajawazito kwenye mateso ya kujifungulia sakafuni ametupeleka kwenye faraja kwa akina Mama Wajawazito kujifungulia vitandani. Mjamzito mmoja, kitanda kimoja.

7. Ametutoa kwenye mateso ya kulanguliwa dawa na ukosefu wa dawa kwenye hospitali za Serikali ametupeleka kwenye upatikanaji wa madawa mahospitalini uliofikia kiwango cha upatikanaji cha asilimia 89, tena kwa bei nafuu.

8. Ametutoa kwenye usumbufu na mateso kwa Wamachinga na Mama Ntilie kusumbuliwa na Wagambo mpaka kutupeleka kwenye utulivu na amani ya kutosumbuliwa kwa Wamachinga na Mama Ntilie.

9. Ametutoa kwenye mfumo wa kuleana na kuchekeana dhidi ya wabadhilifu na wala rushwa na kutupeleka kwenye mfumo wa uwajibikaji wa kupelekwa mahakamani kwa wala rushwa na Mafisadi. Leo hii Tanzania imepanda kwa nafasi kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na mwaka 2017 na pia ikishika nafasi ya pili kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

10. Ametutoa kwenye mateso ya Wanafunzi kukaa chini kwa kukosa madawati na kukosa maabara. Leo hii ametupeleka kwenye hatua ya ukamilifu wa uondoshaji wa tatizo la madawati nchi nzima na maabara kwa baadhi ya shule.

11. Anatutoa kwenye uondoshaji wa tatizo la foleni jijini Dar na kutupeleka kwenye ujenzi wa barabara za juu (flyovers) za Tazara na Ubungo.

12. Amewatoa Wanazuoni wa chuo kikuu cha UDSM kwenye mateso ya kupanga na leo hii amewapeleka kwenye makazi bora ya mabweni ya kisasa wanayolipia gharama za chini kabisa.

13. Ametutoa kwenye balaa la utendaji na uwajibikaji wa hovyo kwa Watumishi wa umma na ametupeleka kwenye uimarishwaji wa kiwango cha kuridhisha cha uwajibikaji na uadilifu kwa Watumishi wa umma.

14. Ametutoa kwenye utitiri wa kodi kwenye kilimo na kutupeleka kwenye ufutwaji wa kodi mbalimbali za kilimo na kukifanya kuwa chenye tija kwa Wakulima. Leo hii bei ya korosho imepanda kutoka Tsh. 800 kwa kilo mpaka kufikia Tsh. 4000 kwa kilo.

15. Ametutoa kwenye usiri mkubwa wa mikataba na taarifa za madini na kutupeleka kwenye uwazi taarifa na mikataba ya madini. Leo hii tunajivunia mafanikio ya gawio sawia la faida za madini na Serikali ikimiliki asilimia 16 ya hisa katika makampuni ya uchimbaji wa madini.

16. Ametutoa kwenye tatizo zito na sugu la ajira na kutupeleka kwenye ongezeko la fursa za ajira kupitia kwenye viwanda zaidi ya 3000, kuwatimua wenye vyeti vyeki, miradi ya ujenzi ya bomba la mafuta, flyovers na reli ya kisasa ya standard gauge.

17. Ametutoa kwenye makusanyo ya Tsh. Bilioni 800 kwa mwezi mpaka kufikia kwenye makusanyo ya Tsh. Trilioni 1.5 kwa mwezi. Hali hiyo imeimarisha uwezo wa Serikali kibajeti.

18. Ametutoa kwenye urasimu na umangimeza kwa viongozi na kutupeleka kwenye uimarishwaji wa kiwango cha nidhamu, uwajibikaji na uadilifu kwa viongozi wa Serikali. Leo hii hakuna usumbufu kumuona kiongozi na viongozi wengi wapo site palipo shida za Wananchi wakizitatua.

19. Ametutoa kwenye mfumo wa walio nacho kujiona Mungu mtu na kuleta ukandamizi ndani ya jamii na kutupelekea kwenye uondoaji wa tabaka la uonevu kwenye masuala ya ardhi na sheria.

20. Ametutoa kwenye mkwamo wa Serikali kuhama Dar es Salaam na kutupeleka kwenye hamisho la Serikali kuhamia Dodoma. Mpaka sasa Waziri Mkuu, Wizara na idara mbalimbali zimehamia Dodoma. Tukumbuke mpango wa Serikali kuhamia Dodoma ulikuwepo na kushindikana kufanyika toka enzi za utawala wa Serikali ya awamu ya kwanza.

Hayo ni baadhi tu, sisi Wananchi wa Tabaka la chini tunaelewa Rais Magufuli alipotutoa na anapotupeleka.

*Tunasimama na Rais Magufuli*

*Na Emmanuel J. Shilatu*
 
Utu,uhuru na haki havina mbadala kwa binadamu vinginevyo Gaddafi yasingempata yaliyompata.

Usisahau pia uchumi wa nchi na uchumi wa mtu mmoja mmoja ni moja ya mambo sensitive katika nchi yoyote ile duniani.
 
1. Ametutoa kwenye usalama hadi kwenye watu kuokota fukweni ktk viroba
2. Ametutoa kwenye hospital kuwa na dawa hadi hospital kukosa dawa.
3. Ametutoa kwenye serikali kutoa ajira kila mwaka hadi kwenye serikali kutoajiri kwa miaka miwili mfululizo.
4. Ametutoa kwenye usalama wa wabunge maeneo yao ya kazi hadi kwenye wabunge kupigwa risasi 30+ hadharani.
5. Ametutoa kwenye bunge live hadi kwenye bunge gizani.
6. Ametutoa kwenye wafanyakazi kupandishwa madaraja kila mwaka hadi kutopandishwa madaraja kwa miaka miwili mfululizo.
7. Ametutoa kwenye wala rushwa kushughulikiwa hadi kwenye wala rushwa kupandishwa vyeo
8. Ametutoa kwenye ukuaji wa kilimo kwa 8% hadi kwenye ukuaji wa kilimo 0.3% kwa mwaka.
9. Ametutoa kwenye wavuvi kuendesha maisha yao kupitia uvuvi hadi kwenye kuomba omba.
10. Ametutoa kwenye deni la taifa trillion 30 hadi trillion 54.
11. Katutoa kwenye wanafunzi kuwa salama hadi kwenye wanafunzi kupigwa risasi hadharani kwenye daladala.
12. Katutoa kwenye watu wanaojulikana hadi kwenye watu wasiojulikana..

Hayo ni machache tu...

Ongezeeni...
 
Train ya umeme ndani ya udikteta aipande mwenyewe na wapiga kura wake wa Mwanza au kanda ya ziwa.

Shibe bila uhuru ni utumwa.

Watu wawe huru kuamua mambo yao almradi hawavunji sheria za nchi. Asitupangie kila kitu.
 
Asante sana Mkuu..
13. Ametutoa kwenye Watanzania kuishi kwa UMOJA hadi kwenye kuishi kwa CHUKI na VISASI.
 


1. Vyama vya Upinzani waliambiwa hakuna kufanya Siasa mpaka 2020.

2. Bunge likaambiwa hakuna kuonekana Live.

3. Wastahafu walipoongea waliambiwa waache kuwashwa washwa.

4. Wasanii walitekwa wakaambiwa wasiimbe SIASA.

5. Media(Magazeti na Tv) zilipoongewa zikafungiwa bila kupewa sababu.

6. Wanaharakati walioongea walitekwa na kupotezwa.

7.Viongozi wa Dini wakahojiwa ,wakaambiwa wasichanganye Dini Na siasa.

8. Wanafunzi wa Vyuo walipoongea walitekwa.

9. VIJANA WANAPOONGEA MITANDAONI WANAAMBIWA WANATAKA KUVURUGA AMANI.

Q. Kwa mujibu wa Katiba na Sheria za Nchi, Ni Nani Hasa anayo haki ya kuongea ili kulisemea Taifa bila kuonekana ana hatia yoyote hata ya Uchochezi?.


Tafakari..
 
Dalili zote zinaonyesha hali ya mambo iko mahututi sana mabenki yanafungwa, watumishi wameshakubali yaishe wanafanya kazi ilimradi wapo kituoni, biashara hali mbaya sana kuliko wakati wowote katika nchi hii, vifaa vya ujenzi bei imependa maradufu bati sasa ivi elfu kumi na tisa, misumari ya bati kilo ni tsh. elfu nane, mfuko wa cement ni tsh. elfu kumi na tano

Kwa kweli sijui tunaenda wapi hela inapokuwa ngumu basi mfumuko wa bei uwe unashuka cha kushangaza unapanda sana. Hali ya mambo sio shwari kabisa dereva huyu analipeleka gari korongoni.
 
Kwa mwenye akili timamu na anayeipenda nchi ya Tanzania anajua kwamba tumepelekwa shimoni ndani ya miaka 2 tu

*social life imeharibika kabisa,police wametiwa kiburi cha ajabu,leo hata kumiliki gari ni dhambi

*Kiuchumi,hali halisi inajulikana jamani haina haja ya kuongea
*Kisiasa,ndo kabisaaaaaaaa,leo wanasema maendeleo hayana vyama,kesho wanahonga watu hela waachie vyeo ili chaguzi zirudiwe

Kabla sijaendelea mbele naomba nikazie suala hilo la siasa, wanaodhani kufa kwa chadema au madiwani kuhama ndiyo mwisho wa upinzani wakapimwe akili zao.

Nyerere alinusurika kupinduliwa mara mbili na watu ambao hawakuridhika na utawala wake, hakukuwa na vyama vya upinzani ila kuna watu walikuwa na upinzani mioyoni mwao

Mtaua vyama, mtaua na kufunga wapinzani mwisho wa siku mtatengeneza waasi wasio hata na kiongozi wa kuwaambia acheni,ndo haya ya tarehe 26/04, hamjui hata mna deal na nani.

Tena hawa kina mbowe bora mngewachukulia kama marafiki badala ya maadui, kuna kundi kubwa linaloichukia ccm, limekuwepo kabla ya Mbowe na litakuwepo baada yake, hata mkigawa 10,000 kila siku kwa raia na maziwa kwa kila mtu bado kuna watu watawakataa so LEARN TO LIVE WITH IT, NDIYO MAISHA HAYO, MBONA HATA YESU NA MTUME MUHAMED KUNA WATU WALIWAPINGA, WEWE NI NANI USIYETAKA KUPINGWA?

Miaka 3 iliyopita upinzani wa ccm na cdm ulikuwa kama simba na yanga,utani wa jadi sikudhani kuna siku mtu mmoja angetufikisha kwenye hali ya chuki kama ile ya kule visiwani ya cuf na ccm, leo chadema hata kuzika hawaruhusiwi?? vikao kwenye misiba, kuna misiba isiyo na mikusanyiko ndani yake na vikao vidogovidogo? unataka wakae kama kanisani?

Utawala huu umeharibu sana ndani ya miaka 2 beyond repair,ukiona mtu ambaye anadhani kujenga madaraja na reli ndiyo furaha ya watu basi yupo out of touch kabisa,nadhani yeye ndiye angekuwa kafanikisha ile miundombinu ya Ethiopia sijui ingekuwaje????

maisha ni zaidi ya hayo ndugu yetu,open your eyes,UMEHARIBU SANA NDANI YA MIAKA 2 TU,HATUNA LA KUFANYA TUSUBIRI 2025 TUANZE UPYA KUSHONA VIRAKA NA KU REPAIR MAKOVU ULIYOYAACHA NA HAPO TUOMBE MUNGU HAYA MACHUKI UNAYOCHOCHEA YASIFIKE PABAYA
Nasema 2025 kwa sababu hiyo trailer tuliyoona kwenye chafuzi ndogo za madiwani na ule wa kinondoni ni kwamba 2020 utashinda kwa asilimia 98 kwa msaaada mkubwa wa policcm
So sad,umetuharibia, umeharibuuu mnoooooo.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…