Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Kuna thread humu inaelezea ahadi za Magufuli nenda kaisome....

Halafu kuna Ilani ya CCM nenda kaisome pia.

Halafu rudi hapa uje kutuuliza ambacho hujakielewa....

HAYA ZUNGUSHAA ZUNGUSHAAA TENAA ZUNGUSHA MIKONOOO....MABADILIKOOOO!!!
Ilani zilikuwepo toka enzi ya Nyerere lakini bado Nchi inayumba, ilani zinatamka tu kama anavyotamka JPM ila hazieonyeshi dira wala speed ya tunakokwenda, yaani tutafikaje, mawaziri ndo weupe kabisa hawana hata strategic plan wapowapo tu, wanacheza Legee wakati inapigwa boringo, hawajuhi hata wanatakiwa kufanya nini kwa wakati huu....
 
Magufuli anatupeleka hapa:-
1. Nilikuwa nanunua mafuta ya gari 2,200 October 2015, sasa nanunua 1,782
2. Nilikuwa nafuatilia hati ya kiwanja changu Kigamboni toka 2011 nasumbuliwa, nimeenda January mwaka huu 2016, hati yangu imetoka March 2016.
3. Nilikuwa nikienda kwenye ofisi za uma kuhudumiwa ni kama vile naomba, sasa hivi nikiingia nahudumiwa kama mfalme.
4. Nilikuwa nafuatilia kuweka maji ya dawasco kwenye nyumba yangu toka 2014 nasumbuliwa, sasa hivi dawasco wamenifuata wenyewe waniwekee maji bure nitalipa kwa miezi 12 ijayo.
5. Nilikuwa nikishuhudia wafanyabiashara wakubwa wote wakikwepa kulipa kodi hapa bandarini, sasa hivi naona wote wakikimbilia TRA kulipa kodi wenyewe, na hakuna tena ki"memo" cha kutoa mzigo
6. Nimeshuhudia bajeti ya maendeleo ya Taifa ikiongezeka tofauti na miaka yote iliyopita, huku matumizi ya ndani tukiyagharimia kwa pesa zetu wenyewe.
7. Nilikuwa natumia masaa mawili toka sinza hadi mjini, sasa hivi MWENDO KASI natumia dakika 25.
8. Ninapotumia gari yangu Moroko hadi sayansi nilikuwa natumia saa nzima, sasa hivi nahisi natumia dakika 3-5 hivi
9. Wale waliokuwa wanafuja pesa na kusababisha vitu vinapanda bei, kwa kuwa wao hawabageni kwenye kununua, mfano kiwanja mtu anauza 20 million, wewe unajibana umbembeleze akuuzie 12 million, anatokea mfuja pesa zetu ananunua kwa 25 million, sasa hivi hakuna tena jeuri ya pesa zisizokuwa zako.
10. Ninashuhudia mengi ambayo nikimtafakari Magufuli, nahisi kuna haja ya kubadilisha katiba atawale miaka yote kama Mgabe.
Mbona mengine umetaja ya JK? Alafu sukari ulikuwa Unanunua kiasi gani na sasa?
 
Mliozoea "Mapindo Mapindo" ngoja mnyooshwe kama Rula'!
Wenye kujua tulikotoka na tulipo sasa,tunajua dhamira njema ya Rais wetu!
Anataka kila mtanzania afaidi Utajili wa nchi yake.
Kwa kuuziwa sukari kilo moja sh 4000?
 
Zinakwenda kwenye matumizi tajwa kama ilivyo ainishwa kwenye report ya kila Mwezi. Pitia utaona kipi ni kipi
Taarifa za makusanyo ya mwezi na allocations zake huwekwa wazi kwa miezi ile ambayo makusanyo yanaonekana kuwa mazuri tu?
 
Kiwanda kikubwa cha mbolea africa kitajengwa tz..., kitakamilika ifikapo2018 kama sikosei....!!

Bandari kubwa kabisa pwani ya mashariki ya africa , bagamoyo port, inaresume ujenzi wake soon.....!!!

Reli ya kati ktk standard gauge iko....!!!

Mafuta ya uganda na baadaye sudan kusini yatapita tz.....

Uranium deal na wachina na warusi ..... Wameanzq kuchimba kule nchomolo....!!

Gesimpaka ruvu ipo....., uku msimbazi hawaja fanya uchunguzi tu...., hujui kwanini n lazma kunomolewe [emoji3][emoji3][emoji3]

Kimsingi hata urlekezwe hueezi kuona kama hutaki...!!!
Kwani dhahabu, almasi na Tanzanite zimesaidia nini? Vipi kuhusu gesi ya songosongo na sasa Mtwara?
 
Kwa kuuziwa sukari kilo moja sh 4000?
Waloficha Sukari walificha,wakabana sasa wameanza kuachia sukari ilifikia 5000 hv sasa popote nchini imeshuka na inashuka na itaendekea kushuka na ktk Tz ya viwanda Magabachori na maajenti wao watamwelewa huyu anayemtegemea Mungu wake kwamba yuko kazini kutupeleka kwenye Tanzania donor country!
 
Waloficha Sukari walificha,wakabana sasa wameanza kuachia sukari ilifikia 5000 hv sasa popote nchini imeshuka na inashuka na itaendekea kushuka na ktk Tz ya viwanda Magabachori na maajenti wao watamwelewa huyu anayemtegemea Mungu wake kwamba yuko kazini kutupeleka kwenye Tanzania donor country!
Hilo neno la mwisho ebu liondoe maana linaharibu maana na ubora wa post yako
 
Mkuu ulichokianza unakijua mwenyewe.

Unapotaka kutupeleka unakujua mwenyewe.

Ila sisi tunapambana kila siku tuijue kesho yetu.

Mkuu unatuua, tuache tu tuishi kivyetu na wewe uishi na mawazo/ maono yako.
Asante.
 
yani uwe specific nini ameanza kuna mengi ukianza kutoka kwenye

1. Kuharibu biashara bandarini
2. kuongeza wizara zinazo poteza hela
3. Kuongeza kodi zinazouwa biashara
4. Kuongeza matumizi ya serikali na kupunguza uwekezaji
5. kufanya uwekezaji uwe mgumu zaidi
6. Kuweka sera za kulazimisha bei ya bidhaa, sera ambayo inapunguza upatikanaji wa bidhaa hiyo
7. kutaifisha kampuni za watu
8. kushindwa kuleta haki kwenye uchaguzi wa zanzibar
9. kutumia jeshi la polisi kama wafuasi wake ili kunyamazisha upinzani
10. Kuongeza mahitaji ya serikali kwa kufanya elemu bule wakati hata madawati hayapatikani
11. kuingilia sekta ya benki
12. kuingilia sekta ya simu

na mengine mengi yapo lakini uwe specific wewe alichokufanya mpaka ukaandika
 
Binafsi sijui unachofanya.
Sioni dalili za taifa kupiga hatua.
Naona idadi ya wanaokutetea na kukushabikia ikipungua.
Naona kama ni wakati wa kuomba kwamba, ' baba,kama ikikupendeza,kikombe hiki nisikinywe ila kama sio mapenzi yako yatimizwe'.

Ndugu yangu jipime, mtaani kila mtu analia kasoro Lizaboni,jingalao,Faiza fox,1954,mudawote,DuppyConqueror na wanao fanana na hao.
Ila mkuu, hii namba tumeshaisoma.
 
Haha Uwiii siku hiz uki Kosoa e Serikal unaambiwa eti umemtukana Rais faini million 7
Na cha ajabu zaidi hiyo milioni 7, eti hutakiwi kuchangiwa na mtu yoyote!!!

Na hoja hiyo anaitoa kila,... za, Kibajaj mle mjengoni kule Dodoma, halafu inaungwa mkono na wanasheria nguli wenye shahada za PhD, akiwemo Waziri wetu wa Sheria na Katiba na yule mdada anayekalia kigoda pale kwenye lile jumba la kutunga sheria kule Dom.

Kweli hao wasomi wetu wakubwa kabisa wameamua kuziweka 'rehani' shahada zao za PhD pale mtaani Lumumba?!
 
Nyie kaeni kulalamika humu JF Massa 24 badala kuchangamkia fulsa mnazoziona,mkijakushtuka mmeachwa.,serikali ni hii hii miaka 9 na nusu ijayo,kama hamuamini ENDELEENI kupiga debe humu,mkijakujifunika shuka kumekucha,always remember Time is Money and we always live once.
 
yani uwe specific nini ameanza kuna mengi ukianza kutoka kwenye

1. Kuharibu biashara bandarini
2. kuongeza wizara zinazo poteza hela
3. Kuongeza kodi zinazouwa biashara
4. Kuongeza matumizi ya serikali na kupunguza uwekezaji
5. kufanya uwekezaji uwe mgumu zaidi
6. Kuweka sera za kulazimisha bei ya bidhaa, sera ambayo inapunguza upatikanaji wa bidhaa hiyo
7. kutaifisha kampuni za watu
8. kushindwa kuleta haki kwenye uchaguzi wa zanzibar
9. kutumia jeshi la polisi kama wafuasi wake ili kunyamazisha upinzani
10. Kuongeza mahitaji ya serikali kwa kufanya elemu bule wakati hata madawati hayapatikani
11. kuingilia sekta ya benki
12. kuingilia sekta ya simu

na mengine mengi yapo lakini uwe specific wewe alichokufanya mpaka ukaandika
Niongezee namba 13, kuzuia vyama vya siasa vya upinzani kutofanya shughuli zozote za kisiasa hadi mwaka 2020, akielewa fika kuwa huo ni uvunjaji wa waziwazi wa Ibara ya 3 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inasema nchi yetu itakuwa na mfumo wa vyama vingi, ambayo Mheshimiwa Rais wetu aliapa kuilinda na kuitii Katiba hiyo kwa uaminifu wake wote.....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom