Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Na cha ajabu zaidi hiyo milioni 7, eti hutakiwi kuchangiwa na mtu yoyote!!!

Na hoja hiyo anaitoa kila,... za, Kibajaj mie mjengoni kule Dodoma, halafu inaungwa mkono na wanasheria nguli wenye shahada za PhD, akiwemo Waziri wetu wa Sheria na Katiba na yule mdada anayekalia kigoda pale kwenye lile jumba la kutunga sheria kule Dom.

Kweli hao wasomi wetu wakubwa kabisa wameamua kuziweka 'rehani' shahada zao za PhD pale mtaani Lumumba...
Mkuu wanaongoza kwa ujinga hapa Tz ni hao PhD holder na maprof.
 
Paul Alex
Tatizo nchi zetu za kiafrika tushazowea misaada kujitegemea wenyewe hatuwezi ndio maana mzee wa push up kaja na usanii wa kutumbua majipu, kuzuia sukari, kuongeza kodi, kufunga midomo wapinzani na mengine bado yanakuja zaidi. Hapa ndio kwanza ameanza tu lakini ukweli nchi ipo taabani haina kitu. Nchi imekuwa kama mgonjwa wa sukari inadhoofika kiafya tunasubiri mauti yake tu.
 
Hakukuwa na Lazima kukataa safari za nje, hata zile zinazolipiwa na wafadhili au zile zenyekuhitaji taaluma fulani.

Hakukuwa na lazima ya kuruhusu polisi waue majambazi hadharani.

Hakukuwa na lazima ya wewe kushikilia mhimili wa bunge.

Hakukuwa na lazima ya wewe kutoa katazo ya sukari kutoka nje.

Nini kilifanya uwatusi wanafunzi wa udom hata baada ya kuwatesa.

Nini kinafanya uongee hovyohovyo bila kusoma hotuba.

Mkuu, unakataje kodi direct kutoka kwenye account ya kampuni?

Mkuu haueleweki, tusamehe mkuu. Tuachie nchi yetu.
 
Paul Alex
Tatizo nchi zetu za kiafrika tushazowea misaada kujitegemea wenyewe hatuwezi ndio maana mzee wa push up kaja na usanii wa kutumbua majipu, kuzuia sukari, kuongeza kodi, kufunga midomo wapinzani na mengine bado yanakuja zaidi. Hapa ndio kwanza ameanza tu lakini ukweli nchi ipo taabani haina kitu. Nchi imekuwa kama mgonjwa wa sukari inadhoofika kiafya tunasubiri mauti yake tu.
Kikwete Rudi Maana hali mbaya
 
Hakukuwa na Lazima kukataa safari za nje, hata zile zinazolipiwa na wafadhili au zile zenyekuhitaji taaluma fulani.
Hakukuwa na lazima ya kuruhusu polisi waue majambazi hadharani.
Hakukuwa na lazima ya wewe kushikilia mhimili wa bunge.
Hakukuwa na lazima ya wewe kutoa katazo ya sukari kutoka nje.
Nini kilifanya uwatusi wanafunzi wa udom hata baada ya kuwatesa.
Nini kinafanya uongee hovyohovyo bila kusoma hotuba.
Mkuu, unakataje kodi direct kutoka kwenye account ya kampuni?
Mkuu haueleweki, tusamehe mkuu. Tuachie nchi yetu.
Na anataka kuendesha nchi kwa kile kitu kinaitwa one man show......

Na mteule wake yeyote anayepingangana na mawazo yake anang'olewa kwa staili ya kutumbuliwa jipu...

Hali inayofanya watendaji wengi serikalini kufanya kazi kwa hofu tupu kumfurahisha Mfalme, badala ya kutumia ujuzi na utaalam wao!
 
Jmc06, Magufuli akishinda 2020 najisaidia mafungu mafungu kutoka Mwanza hadi Dar.
Wewe ongelea hii mitano kama atatoboa!
Naona mzee anavyozidi kukaribia kuchukua kiti cha mwenyekiti mafisadi matumbo yanazidi kuwakata..mnakosa usingizi
 
Na mbaya zaidi anafanya madudu yote hayo kwa kiburi cha kuamini kuwa yeye ndiye 'anayemiliki' vifaru vya kijeshi na magari ya washawasha.

Inapotokea wananchi wakatoa maoni yao, ambapo wanaruhusiwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu Ibara ya 18.

Lakini kwake yeye kila anayetoa maoni yake yeye anamuona analeta fyoko fyoko na anaviamrisha vifaru 'vyake' na magari ya washawasha, viwashughulikie hao anaowaita waleta fyoko fyoko!
 
Naona mzee anavyozidi kukaribia kuchukua kiti cha mwenyekiti mafisadi matumbo yanazidi kuwakata..mnakosa usingizi
Let us be realistic.

Usitake kuidivert mada kama ilivyo kawaida yenu nyinyi buku 7 Lumumba sports Club.

Hapa suala ni Rais wa nchi anavunja Katiba ya nchi waziwazi kwa kuzuia shughuli zozote za kisiasa kwa vyama vya upinzani hadi mwaka 2020, wakati chama chake cha majipu kikiendelea kufanya shughuli za kisiasa bila kubughudhiwa na vyombo vya dola.

Hiyo ndiyo double standard ya hali ya juu inayofanywa na Jeshi letu la Polisi.
 
Magufuli baba yangu mzazi alimpigia kura Edward Lowassa kama ilivyo mimi, na alinipa sana moyo kwenye kusimamia kura.
Ila alikuunga mkono ulipoanza mbwembwe zako, alifurahi sana siku za mwanzo alipokuona kwenye taarifa za habari ukitumbua.
Tulitofautiana sana kwasababu mimi ni mtu mwenye misimamo isiyohama.
Magufuli leo mzee hakuelewi. Hajui unafanya nini tena.
Anasema mambo ambayo sitaki kusema.
 
Jmc06, Magufuli akishinda 2020 najisaidia mafungu mafungu kutoka Mwanza hadi Dar.
Wewe ongelea hii mitano kama atatoboa!

Mlisema hivyo mwaka Jana October mpaka leo sijaona Hata mmoja wenu aliyekunya,wengi wenu mnaolalamikia utawala huu ni vijana mliozunguka mjini,asilimia 75 ya watanzania wanaishi vijijini,na wengi ni wakulima pamoja na watoto wao,Kwa wakulima wa kahawa,korosho,pamba,nyanya,Michele,miwa,matunda nk,wanapenda serikali hii kuliko serikali yoyote,maana wamepunguziwa kodi kibao na Maisha kwao yameboreshwa kuanzia ada mashuleni na madawati kila kona ya nchi na u serious kwa manesi wakienda hospitalini,unaviona ni vitu kidogo,ila Kwa makini ni Mwanga umulikao kilometa nyingi sana.,

CCM ilipata wabunge 186 na UKAWA ni 35 (bila wale wa kuteuliwa),wengi wa hawa wa CCM walitoka vijijini,CCM ina matawi kila IATA na kijiji nchi nzima,na ndo nguvu kubwa ya wapiga kura walipo,.

Mianya mingi ya uvujaji wa pesa imezibwa na madili mliyozoea hakuna tena,ndo kisa cha kushinda mnalalamika humu JF,ila kundi lenu ni dogo sanaaa,kwa mchapakazi na mkulima wa kipato halali wa miaka yote Mimi nikiwemo, hii serikali ni nzuri sanaaa,na ninaomba JPM akaze Uzi zaidi,Kwa waliozoea michongo ndo mnaendeleza kampeni 24/7 mkipeana moto kwenye mitandao mkidhani wa TZ wengi wanawasapoti kumbe ni wachache kuliko unavyodhani.

Mwisho mgombea wenu wa UKAWA mwaka Jana September aliwahi kusema upinzani usipochukua dola 2015,itawachukua miaka 50 kuchukua dola sababu alimjua mtu anayekuja JPM akishinda atarudisha nidhamu iliyopotea miaka mingi nchini,kama Lile kundi nililokwambia mwanzo wakulima nk wanasonga vizuri kuliko miaka yote ya nyuma hizi kelele za upinzani Mara dikteta haina maana kwao sanasana ni kupoteza muda tu.

Ushauri wangu vijana changamkieni fulsa,nendeni wizara ya viwanda na biashara Kuna michongo mingi sana,malalamishi humu yatawapotezea muda sanaa,mkijakushtuka too late,hayo mnaowaita mashujaa wa upinzani wapo kazi ni wanapewa ruzuku Hata wakilala rumande wanalipwa, ni hayo tu.
 
Mheshimiwa mimi niko kwako nyumbani.
Wakwako hawaelewi kwanini unataka uwanja wa ndege Chato.
Hawana shida ya kuruka kwa ndege,
wako sawa na usafiri wa basi!
Mkuu,ukisogea kidogo katolo na Geita, Busanda ya Mawazo napo hawajui umepatwa na Lipi!
Uliwaambia utawapa Buckreef wafanye kazi, kwamba utawapa Magwangara ya GGM.
Kiongozi upo Kimya, upo karibu na Kagame.
Watu wako hatujui, au mkuu tujiandae kwa safari ya Rwanda?
 
Nyie kaeni kulalamika humu JF Massa 24 badala kuchangamkia fulsa mnazoziona,mkijakushtuka mmeachwa.,serikali ni hii hii miaka 9 na nusu ijayo,kama hamuamini ENDELEENI kupiga debe humu,mkijakujifunika shuka kumekucha,always remember Time is Money and we always live once.
Subutu eti 9 yrs kwani unadhani kila mtu kiziwi kwa ccm huu ndo mwisho wa ccm especially walivompa magufuli nnchi he is done in the next four
 
Jmc06, Magufuli akishinda 2020 najisaidia mafungu mafungu kutoka Mwanza hadi Dar.
Wewe ongelea hii mitano kama atatoboa!

Tukumbushane mkuu. Alishinda lini kweli?

Mtu ukiwa na nguvu, na ukawa sahihi, woga wa nini?
 
Paul Alex
Tatizo nchi zetu za kiafrika tushazowea misaada kujitegemea wenyewe hatuwezi ndio maana mzee wa push up kaja na usanii wa kutumbua majipu, kuzuia sukari, kuongeza kodi, kufunga midomo wapinzani na mengine bado yanakuja zaidi. Hapa ndio kwanza ameanza tu lakini ukweli nchi ipo taabani haina kitu. Nchi imekuwa kama mgonjwa wa sukari inadhoofika kiafya tunasubiri mauti yake tu.

Endelea kusubiri mauti yake ila kaa ukijua Tanzania itakufa na kufufuka siku ya tatu kama ilivyotamkwa,tanzania mpya inakuja
 
Magufuli baba yangu mzazi alimpigia kura Edward Lowassa kama ilivyo mimi, na alinipa sana moyo kwenye kusimamia kura.
Ila alikuunga mkono ulipoanza mbwembwe zako, alifurahi sana siku za mwanzo alipokuona kwenye taarifa za habari ukitumbua.
Tulitofautiana sana kwasababu mimi ni mtu mwenye misimamo isiyohama.
Magufuli leo mzee hakuelewi. Hajui unafanya nini tena.
Anasema mambo ambayo sitaki kusema.
Magufuli, Mzee wangu ana tatizo la presha.
Na umri wake kidogo umesogea.
Mkuu nampenda baba yangu, naomba utuachie nchi yetu!
Hivi magufuli anajua kitaa watu hawamtaki am supa serious kitaa kwetu neno maguli kilaa baada ya dakika kadhaaa he is gaining not only haters but anakua society reject au anajipanga kuhamia rwanda bcoz hata apae hewani hashindi next 5
 
K
Nyie kaeni kulalamika humu JF Massa 24 badala kuchangamkia fulsa mnazoziona,mkijakushtuka mmeachwa.,serikali ni hii hii miaka 9 na nusu ijayo,kama hamuamini ENDELEENI kupiga debe humu,mkijakujifunika shuka kumekucha,always remember Time is Money and we always live once.
Kumbe wewe ndio unaanza kutafuta fursa Leo? Wenzako tayari tuna maisha yetu tena matamu kama mcharo! Ndio maana mnajitoa ufahamu kukumbatia hats ujinga.
 
Magufuli mwanao nimesoma uchumi kidogo, tena hapahapa wala sijaenda nje kama Tulia. Mimi ni mzalendo kuliko Ally Kessy na Lusinde kibajaji angalau kwa hoja.
Sitaki sanamu ya Diamond posta ila natamaani kujua sera yako kiuchumi iliwahi kujaribiwa nchi gani ikaleta manufaa?
Kagame asikudanganye, Kagame ni mwizi anaiba Kongo.
Anatumia udhaifu wa Kongo na Ukabila wa Rwanda kurefusha makucha.
Mkuu hatuna pakuiba!
Zanzibar tumeipa ukilema na ndio kwanza inataka tuibebe.
Kiongozi unatupeleka Chaka.
 
Hivi magufuli anajua kitaa watu hawamtaki am supa serious kitaa kwetu neno maguli kilaa baada ya dakika kadhaaa he is gaining not only haters but anakua society reject au anajipanga kuhamia rwanda bcoz hata apae hewani hashindi next 5
Unaelewa maana ya "ushindi wa kishindo"?
Kama huelewi soma jina la Chama chake. M inamaanisha nini?
Nyinyi nendeni na kapigeni kura, wenyewe wanae kivuitu. Kivuitu never lies, neither does he dissappoint anybody.

Angalia video na sikiliza dakika ya 4 - 4:40 utaelewa.

 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom