Naandika haya kwa maslahi ya Taifa letu. Mambo yanayogusa taifa letu yanatuathiri kwa namna moja au nyingine hivyo kama watanzania ni haki na jukumu letu kulijadili. Hakuna mtanzania anayeichukia serikali yake ila kuna mambo mengine yanahitaji kuzungumza. Mtanzania yeyote yule anaipenda nchi yake....Kwa wale waliotembea nje ya nchi wanapenda kujitambulisha kwa ufahari kwamba "Ninatoka Tanzania" Land of Kilimanjaro, Serengeti and Zanzibar. Hiyo ni "identity" yetu wengi tupo proud na nchi yetu, wote tunaitakia mema nchi yetu....Wote tutapita lakini lakini nchi itabaki, vizazi vitakuja na vitapita. Naomba nizungumze mawazo yangu, naheshimu mawazo yenu lakini pia naomba mheshimu mawazo yangu..."it is simply my feelings" ni haki yangu kama mwananchi wa kawaida kutoa dukuduku langu....kwa wastaarabu watayasoma na ni imani yangu wataelewa.
Kuna mambo mengi sana yametokea na yanaendelea kutokea wakati mwingine ni vigumu kuamini kama kweli yanatokea kwenye nchi hii tunayoipenda, Mwezi huu au uliopita walikamatwa waandishi wa habari member wa CPJ, wakachukuliwa hotelini kwao na kupelekwa kwenye ofisi za usalama wa Taifa, hao waandishi walikuwa na vibali vya kutembelea nchi yetu...Waliteswa kisaikolojia na mmoja alipigwa vibao (sijui ni kosa lipi mgeni anapigwa kwenye host country) Kwa wale tuliotembelea nchi zingine hatukuwahi kutendewa hivyo kama nchi yetu inavyowafanyia wengine, Kufungua password ya computer ya mwandishi wa habari kwa nguvu ni kosa kubwa kisheria...HUPASWI KUFUNGUA COMPUTER YA MTU YEYOTE PASIPO RIDHAA YAKE! Mtu aliyekuwa analazimisha kufungua alikuwa akijitapa kuwa wana utaalamu wa Israel wa kufungua password lakini wakashindwa! Je hayo majitambo ya sijui Israel au wapi yanawasaidia nini? Nakumbuka Jerry Muro alipokamatwa na kesi ya kuomba rushwa ya Millioni 10 kwa nguvu alitumia neno kama hilo hilo la kusema amesomea usalama wa Taifa Israel! haya yanasaidiaje au yanatuma ujumbe gani kwa mshukiwa au anayeshikiliwa? Kwamba labda hakuna ingenuity kwenye nchi yetu zaidi ya kutumia technology ya nchi zingine? Kwa hiyo inaonyesha udhaifu wenu kuwa hamuwezi kutumia ujuzi/technolojia yenu wenyewe.
Suala la kutekwa kwa Mohamed Dewji limechukulia kirahisi sana lakini madhara yake yanaonekana.....siyo suala dogo hasa linapoandikwa kwenye media zote duniani...je waliofanya hilo walikuwa na nia gani? Serikali yetu inanyamaza, halina ubishi waliofanya ni hao hao waliozea kuteka (Ukizoea kula nyama ya binadamu huachi!) Toka awamu ya tano ianze utekaji umekuwa suala la kawaida kuanzia Roma Mkatoliki, kuvamia kituo cha TV kwa bunduki na kupotea kwa watu wanaoulizia uhalali wa serikali kufanya maamuzi ya kushangaza au kuuliza elimu ya Magufuli kama ni "valid". Nimeshtushwa na jinsi rais Magufuli anavyofuatilia mambo ya mitaandoni ya kawaida ya wananchi kutoa mawazo yao au kutoridhika na baadhi ya mambo ya serikali, nikajiuliza mbona inamuuma kiasi hicho, ina maana hajui kwamba ukiwa rais lazima ukumbane na "criticisms" hizo? Ni madikteta tu pekee ambao wanaofuatilia vitu vidogo vidogo vya kuongelewa mitaani na watu wa kawaida(common man), Rais Kagame anazo hizo tabia, niliwahi kuwa Rwanda mwenyeji wangu aliniomba tusiongelee mambo ya siasa miaka ile ya mwanzoni mwa 2000, leo nayaona haya hapa kwetu. Ni marais watatu tu duniani wapo sensitive na haya mambo ya kusemwa....Moja Kagame, mbili Magufuli na tatu Maduro wa Venezuela.....ukiacha ufalme wa Saudi Arabia! Si rahisi kuamini yanayotokea kwetu kama ni kweli, rais anajinasibu ni rais wa wanyonge........Kivipi? Ina maana wale wenye uwezo waliotumia nguvu zao kufika kwenye hali nzuri na wanaotoa ajira kwa Watanzania rais wao ni nani? Kwa wanahistoria wenzangu waliokuwepo miaka ya 1978 ( Paschal et al)tunakumbuka Idd Amin Dada alianzisha kikosi cha State Bureau....kiutendaji inafanana na TISS yetu, watu hasa wapinzani au ukishukiwa unaongea vibaya kuhusu rais au wale wa karibu naye (inner circle) unapotea, Walipokamatwa waandishi wa CPJ waliulizwa kama wanamuulizia Azory Gwanda aliyetimiza mwaka mmoja jana tangu akamatwe na wahuni (trigger happy) wa usalama wa Taifa....Swali jepesi tu, Kama mtu/mwandishi amepotea kwani waandishi wenzake au familia yake wakiulizia au wakimzungumzia kuna tatizo?? Serikali inaficha au inaogopa nini kama haihusiki na upoteaji wake?? Leo tunatengwa kwa sababu za kibabe babe tu za huyu rais, Anakataza watoto wa kike wakipata ujauzito aidha kwa kupenda wao wenyewe au kubakwa kuwa wasisome.... anataka Taifa liwe la wajinga? Je yeye ana uadilifu gani....Mbona tunajua ya Sundi Malomo na mambo yasiyo ya uadilifu ya huyu rais hasa uporaji wa nyumba za serikali na kuwapatia waliokaribu naye (Naomba nisiseme sana), Kwanini huyu rais ana chuki kubwa na watoto wa kike? (Naomba nisifukue makaburi). Kila siku kwenye hotuba zake kinachosifiwa ni kuongezwa kwa bajeti ya dawa mara 10 lakini hospitali za wilaya, mikoa na mikoa hazina dawa! Hizo dawa zipo wapi? Serikali inakosa maarifa inaona kuimarika kwa huduma za afya ni kujenga hospitali lakini madaktari bingwa, vifaa tiba, dawa na maabara za tafiti hazipo......kuna faida gani ya kuwa na majengo makubwa yaliyojengwa kwa gharama kubwa wakati hakuna Madaktari bingwa, center za tafiti za magonjwa, maabara bora, vifaa tiba,dawa n.k? Kawaida nchi zinazofanya vizuri kitiba duniani hazijenga hospitali kubwa bali zinajikita katika hayo niliyoyataja hapo juu......Majengo makubwa ni "White elephant" hayasaidia....vyumba vidogo lakini tukiwa na hayo niliyoyataja tutafanya vizuri sana kuliko kupoteza billioni 169 kwa jengo mmoja halafu hakuna vifaa tiba, hakuna madaktari bingwa, hakuna madawa, hakuna maabara bora, Mfano miezi miwili iliyopita alifanyiwa uchunguzi binti aliyeimba muziki na mwanamuziki Diamond (mimi siyo mshabiki wa muziki) aliambiwa huko Muhimbili kuwa ana matatizo ya ini.....Muhimbili hospitali yetu kubwa kabisa ya rufaa wanamtoa maji tu baada ya wiki tatu( ina maana hakuweza kusaidika zaidi ya kutolewa maji tu) Amepekwa India....Diamond Platnumz ubarikiwe sana kwa moyo wako! Kule amefanyiwa upasuaji na tatizo siyo ini bali ni moyo ukimwangalia kwa tabasamu alilonalo unajua kabisa kwamba tatizo lililomsumbua litakuwa historia...Je hospitali yetu kuu ya rufaa WAMESHINDWA KUJUA HILO? Je kutakuwa na imani kiasi gani na wanaotibiwa hapo kama kuna element za MISDIAGNOSIS kama zinazofanyika sasa? Ruge amepelekwa South Africa na rais ametoa million 50 kusaidia matibabu yake, ina maana bado rais anafahamu kuwa kuna tatizo kubwa katika sekta yetu ya Afya.......KAMA ANAFAHAMU HILO KUNA KITU GANI KIMESHINDIKANA KULETA HUDUMA BORA ZAIDI KIASI KWAMBA HAKUNA MAGONJWA YANAYOTIBIKA HAPA NCHINI KWETU???JE NI WATANZANIA WANGAPI WANA TATIZO KAMA LA RUGE LINALOTIBIKA NCHINI AFRIKA KUSINI?.....NI WAZI NI WENGI MNO.....JE RAIS ATAWEZA KUWALIPIA MILLIONI 50 KILA MMOJA (UKIZINGATIA MILLIONI 50 KWA KILA KIJIJI IMEKUWA NGUMU!)
Kulikuwa na umuhimu wa kuimarisha huduma za afya kwenye kila kipengele hasa Kuwasomesha madaktari bora zaidi, Kuongeza vifaa tiba, Vituo bora vya tafiti, Maabara bora, Ethics bora na Professionalism kama CUBA wameweza sisi tutashindwaje?
Yanayotokea yanasikitisha, hatuoni impact kwa sasa lakini kutakuwa na ripple effects muda si mrefu....Haya ya kutumia Wanajeshi kuingia Bureau De Change ni upuuzi usio na maana na unaendelea kuharibu kuliko kujenga.....Kwa nini viongozi wetu wanakosa hekima kwa kufanya vitu vya kijinga? Namheshimu sana Luoga alikuwa Vice Chancellor wakati nikiwa chuo lakini usomi huo kwa kukosa maarifa unamweka katika kundi la wasio na hekima wala busara.....Hotuba yake ni pathetic iliyojaa uongo kuanzia mwanzo hadi mwisho, KUDANGANYA KUNAPUNGUZA HESHIMA NA INASHUSHA THAMANI YA ELIMU YAKO. Huyu Gavana wa Bank Kuu anasema tuna akiba kubwa ya fedha kuliko nchi yoyote Africa Mashariki....anachekesha!!! Bank of Tanzania ina akiba ya fedha za kigeni kiasi cha US$ 5.6 Billion inatosha kununua huduma na bidhaa (Import) kwa muda wa miezi mitano (5 months), Central Bank of Kenya (CBK) inayo akiba ya US$ 8.3 Billion ambayo inatosha ku-service import kwa miezi 6 na nusu (6.5 months) hizo figures ni za jana ......SASA NANI ANA AKIBA KUBWA KATI YA Bil 5 na Bil 8? Hesabu za darasa la kwana zinakuwa ngumu kwa wanasiasa wetu. Waziri Kabudi anadanganya waziwazi kwenye kila analosema kiasi kwamba anavuka mipaka kuwadanganya Wamarekani kwenye nchi yao!!!!! Haoni aibu anatoa macho kama mjusi aliyekabwa na chakula!
Kwa mauji haya yanayofanywa, upigwaji risasi wa wanasiasa, utekwaji na upoteaji wa watu wa kawaida na waandishi wa habari wanaotoa mawazo tofauti au wanaohoji mambo ya haki nchi yetu itaendelea kutengwa tutabaki kama kisiwa kwa sababu ya utashi wa watu wachache......wawili au mmoja anayeogopwa kama Mungu na itatugharimu sana. Ndiyo hatusapoti ndoa za jinsia moja kama zilivyo nchi nyingi duniani lakini kufuatilia mambo ya watu binafsi mmoja na kuwadhalilisha hilo si sawa....Binafsi sitaki kusikia ndoa za jinsia moja lakini kuwatafuta watu wenye matatizo yao binafsi kuwafunga, kuwadhalilisha na kuwapiga siyo sahihi hata kidogo, Wenye matatizo hayo walikuwepo kabla ya uhuru, wakati wa uhuru, wakati wa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa, na wakati wa Kikwete.Mbona kipindi hiki iwe hivyo. Kiongozi wetu Papa Francis alisema hao wagonjwa waombewe kwa sababu ni watoto wa Mungu....NI BINADAMU KAMA SISI!!!
Naona tunakwenda kule walikoanzia Zimbabwe... Kiongozi wetu anapenda kuandikwa na kusemwa kwenye media sidhani kama ni jambo zuri sana.