Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Sababu ya laana ya ben na azory Hakuna zao lolote litakalo ota shambani.
 
Wanja jamaa atuue kwa maisha magumu ili akili zisogeleane.Tumeendekeza uoga sana.Mtu gani anatia njaa taifa kwa kuendesha nchi kwa kibuli na mabavu watu wanapaza sauti maisha magumu yeye anasema wote waliao ni wapiga deal
Well said! Ila edit kidogo hapo mwanzo. Nadhani ulimaanisha “wacha jamaa atuue kwa maisha magumu...”
 
Ujue ukweli ujinga ni wetu, yaani tunaona Mambo ya hovyo yanatendeka lkn bado tunakubali kuwa Kama mazobe. Wabunge wetu ni waoga kuliko hata raia wenyewe. Yani sijui Nani mwl wetu
Inachotakiwa haya maisha yazidi kuwa magumu ili tukichoka tuchoke wote na majibu yatapatikana siku hiyo.Mtu mwenye hasira na njaa huwa vigumu sana kumtawala labda awe zezeta.
 
Sisi tuliowekeza vimilioni vyetu kwenye korosho presha na matumbo moto
 
Anaeweza kujibu kwa ufasaha ni katiba mpya maana walio sain mikataba hewa wote wanaweza kulipa na kufia ndani ila kwa kawaid tu bado tunapiga marktime
 
Mkuu bado pia kuna machungu zaidi kwenye mifuko ya jamii, Mimi mwenyewe ni mhanga mmoja wapo nilifanya kazi kwa nguvu zangu katika mashirika yasio ya kiserikali kodo nikawa nakatwa kubwa kwa mwezi ya laki 2 na kitu, nimefanya kazi kwa muda miaka miwili baadae kazi ikaisha, eti Leo kila ukienda kwenye kutafuta haki yako majibu yanayotoka yanatia hasira na uchungu sana, jasho la mtu alive teseka akitumikishwa Leo ni virio miongoni mwetu, mtu kazi ilishaisha yuko na familia kashatafuta kazi sana bila mafanikio eti ata kinua mgongo chake kinawekewa pingamizi kwa sheria mpya tena ata elewaka ,, INAUMA SAAAAANA but time will tell
Inachotakiwa haya maisha yazidi kuwa magumu ili tukichoka tuchoke wote na majibu yatapatikana siku hiyo.Mtu mwenye hasira na njaa huwa vigumu sana kumtawala labda awe zezeta.
 
Kwanini rais alale na mafaili kitandani?
Kwanini rais awe overloaded na clerical works?
Ikulu yetu haina utaratibu wa kumbreef rais?
Why does he have to be the one digging the small details?
Ikulu amekosekana mtu mwenye attention to details?
Ukiona unafanya kazi ambayo walipaswa unaowasimamia waifanye basi ni dhahiri umeshindwa kuwasimamia.

Uchumi wetu kwa sasa sio siri unatembelea ulimi. Hamna siri tena maana kila mtu anaumia.
☆Mfanyakazi hajapandishwa mshahara.
☆Wastaafu wanaibiwa na serikali mchana kweupe.
☆Wafanyabiashara wanaumizwa na kodi na mdororo wa soko.
☆Wakulima ndio usiseme. Waliposikia serikali inanunua korosho kidogo wakapata matumaini. Wakaanza kuiita serikali kwenye mazao mengine kama kahawa,mahindi, mbaazi,n.k mara ghafla boomerang -serikali inataifisha korosho. Wakulima wakakaa kimya kama vile ile shida ya bei kwenye mazao mengine imekwisha.

Kuna tatizo Kongo kwa majeshi yetu, tukubali au tukatae. They are being targeted, for what reason? Hatujui.
Aliyepaswa kuwapa moyo na kutupa maelezo hana habari.

Mahusiano yetu ya kidiplomasia kwa marafiki wa karibu na wa mbali yamedorora vibaya. Mwana diplomasia namba moja ndio mhusika mkuu katika huu mdororo au kwa kauli au kwa matendo yake.

Mabadiliko katika baraza na sekta mbalimbali yameshafanyika vya kutosha lakini hali inazidi kuwa mbaya zaidi.

Nenda vituo vya polisi, vijana wamejaa, wavulana kwa wasichana for petty crimes.
Asilimia 90 ya makosa yao yanahusisha kujitafutia kipato. Tena haifai kuitwa hata kipato ila mlo wa kila leo.

Taifa linaumia ila rais anatimiza ndoto zake za kununua ndege, kujenga reli na flyovers!

Rais alipaswa kuwa mwakilishi wa ndoto na matamaanio yetu sio ndoto na matamaanio yake.
Rais alipaswa kuhakikisha kila kundi/tabaka katika jamii linatimiza ndoto zake na sio kuumiza na kuharibu matabaka yote na kuwageuza wote tabaka moja la wanyonge ili awaongoze.

Mheshimiwa rais ni dhahiri umajaribu na umeshindwa, hongera kwa kujaribu!
2020 utuhurumie, umuachie mwingine naye ajaribu!
 
2020 kazi na bata
 
Note: nchi huwa haijaribiwi kwa kuongoza never ever.....na kusema apumzike 2020 ni sawa na "kumpigia mbuzi gitaa"
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…