Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Leo nimepanda daladala,robo tau ya abiria walikuwa wanapiga miayo mpaka konda akalalamika,
Basi zima hakuna aliyetoa noti ya elfu kumi,elfu tano,au elfu mbili,ni hamsini hàmsini,miamia zilizochakaa.
Wengi walikuwa wamezifunga kwa nguvu kwenye pindo za nguo zao
 
Bandiko hili laweza kuwa ni dhihaka kwa "mtakatifu" na linapaswa kupewa kesi ya uchochezi. Mtu mwenye daraja la utakatifu au umalaika huwa hakosei na wala hashauriwi. Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kumshauri "mungu wetu" yeye ni alfa na omega.

Kumshauri mtakatifu mwenye heri kunaweza kuchukuliwa kuwa ni kumjaribu, kumjaribu ni kiashiria cha fyokofyoko kinachoweza kukufanya "upotee" ndani ya dk.5. Hizi ni zama za kushughulikiwa ndani ya dk. 5 hivyo ni vema kabla hujaleta jukwaani hoja yenye viashiria vya kuhoji "utukufu" wa baba mtakatifu uandike wosia ili ukipotea ndani ya dk5 familia yako isiparaganyike kwa kugombea mali ulizoziacha.
Tayari nimeshaandika wosia.
 
Style yake ya uongozi ni kama ya Mugabe. Wananchi wa hali ya chini ndio tutaumia, yeye na familia yake watabaki salama kama ilivyo ada ya watawala wengi wa Afrika.
 
2020 inachelewa sana, jibu ndio litapatinaka aisee.
 
Ndio vilio vimeanza,mkuu analeta ubishi kwenye mambo ya kiuchumi. Pesa kwenye mzunguuko imepungua,Bandarini mizigo imepungua,biashara zinafungwa na wengine wanaziuza.Ni katika kipindi hiki ndio viwanja na majumba mengi yanauzwa na pesa za kununulia hakuna,waliokopa miezi kadhaa nyuma wameshindwa kulipa mikopo wanaishiwa kufilisiwa na bado baadhi ya mali hazinunuliki hali inayopelekea wakopeshaji nao kupata pesa iliyo chini ya malengo.

Nini mh rais hafanye kuinusuru hali hii ............maana mambo ya kiuchumi yanatugusa wote,sio wanasiasa tu.
Mh rais anasema pesa zimefichwa,inawezekana hii ni kweli, hebu tumpeni ushauri mh rais nini kifanyike na ni wapi alipokosea.
Ndio mjifunze kufanya saving, na maisha yenye utaratibu ndivyo kulivyo huko duniani kote....
 
Ndio vilio vimeanza,mkuu analeta ubishi kwenye mambo ya kiuchumi. Pesa kwenye mzunguuko imepungua,Bandarini mizigo imepungua,biashara zinafungwa na wengine wanaziuza.Ni katika kipindi hiki ndio viwanja na majumba mengi yanauzwa na pesa za kununulia hakuna,waliokopa miezi kadhaa nyuma wameshindwa kulipa mikopo wanaishiwa kufilisiwa na bado baadhi ya mali hazinunuliki hali inayopelekea wakopeshaji nao kupata pesa iliyo chini ya malengo.

Nini mh rais hafanye kuinusuru hali hii ............maana mambo ya kiuchumi yanatugusa wote,sio wanasiasa tu.
Mh rais anasema pesa zimefichwa,inawezekana hii ni kweli, hebu tumpeni ushauri mh rais nini kifanyike na ni wapi alipokosea.
Wanaokosea hupewa adhabu full stop
 
Kulikuwa na habari kuwa bank hamna hela za kukopesha mzunguko wa hela umekua mgumu, it was mentioned Kimei kasema, baadaye crdb wakakanusha kuwa hakusema na hela ziko kibao za kukopesha! Then bandarini watu wakasema hamna mizigo! Akaja jamaa wa bandari (sijui msemaji sijui mkurugenzi!) Akasema mizigo iko tele wala hakuna shida ya mizigo! Jana wamethibitisha mizigo hakuna na waende wakamshauri kama atapokea ushauri sijui
 
Mh. Rais ni vema abane uchumi mara 3 ya hapa. Ili watu wafanye kazi za kuzalisha. Vijana waondoke mjini wakajiajiri kwenye kilimo. Na kubana matumizi serikali itapata pesa ya kuwapelekea pembejeo, elimu ya kilimo cha kisasa na huduma za jamii. Mjini tuheshimiane.
 
Bandiko hili laweza kuwa ni dhihaka kwa "mtakatifu" na linapaswa kupewa kesi ya uchochezi. Mtu mwenye daraja la utakatifu au umalaika huwa hakosei na wala hashauriwi. Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kumshauri "mungu wetu" yeye ni alfa na omega.

Kumshauri mtakatifu mwenye heri kunaweza kuchukuliwa kuwa ni kumjaribu, kumjaribu ni kiashiria cha fyokofyoko kinachoweza kukufanya "upotee" ndani ya dk.5. Hizi ni zama za kushughulikiwa ndani ya dk. 5 hivyo ni vema kabla hujaleta jukwaani hoja yenye viashiria vya kuhoji "utukufu" wa baba mtakatifu uandike wosia ili ukipotea ndani ya dk5 familia yako isiparaganyike kwa kugombea mali ulizoziacha.
Hanna hats hati ya mashitaka,mashahidi,hukumu? Atahukumu yeye hapohapo au?
 
Unafikiri kuongoza nchi ni vitisho na mikwara, nani awezae kupambana na wafanya biashara? Mlidhani mtawakomoa mlipokua mnawachukulia sukari yao nanyi mkishangilia? Ndo kwanza safari imeanza
 
Kulikuwa na habari kuwa bank hamna hela za kukopesha mzunguko wa hela umekua mgumu, it was mentioned Kimei kasema, baadaye crdb wakakanusha kuwa hakusema na hela ziko kibao za kukopesha! Then bandarini watu wakasema hamna mizigo! Akaja jamaa wa bandari (sijui msemaji sijui mkurugenzi!) Akasema mizigo iko tele wala hakuna shida ya mizigo! Jana wamethibitisha mizigo hakuna na waende wakamshauri kama atapokea ushauri sijui
Mkuu inabidi tuite fundi umeme....hii gari ina shoti na tunakoenda hatutafika,tutaungua humu ndani
 
Aache kutegemea mawazo ya PhD holders kutoka vyuo vikuu wao wana majibu ya kinadhalia ya Google. Wafanyabiashara, wakulima, wafugaji, wavuvi, meneja wa biashara na wafanyakazi kwenye makampuni makubwa ndo wana majibu kutoka field. Hao PhD holders kama hawajawahi kufanya biashara ategemee majibu ya kupika kama wanavyo cook data za research.
 
Kipindi changu hakutakuwa na pesa za bure bure - JPM. Sasa tulielie au tutafute shughuli za kipato tuendelee na maisha yetu.
 
Nchi imemshinda hi..kuna sehemu za kuleta ubabe siyo kwenye biashara za watu..
 
Na kweli tunakaa sawa,kama una pesa zako kipindi hiki ni cha kujizolea majumba/viwanja. maana hali ni mbaya kitaani.
Hata hao wanazo wanazikumbatia..Kwani wao hawaoni uchumi uporomoka mdogo mdogo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom