Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Binafsi nahisi tunakimbilia kituo cha polisi na kuuaminisha umma na kama sio dunia kuwa Tanzania ni nchi pekee dunia ya ajabu isiyojua umhimu wa kutumia rasiliamali vizuri. Hasa rasiliamali vitu(natural resource) na rasiliamali watu(human resources) na pia naona nchi haiwezi kuongozwa na mwanasayansi na ndo maana ukiangalia marais wengi walisoma arts na wanamudu kazi. Ila hawa wazee wa PCM ambao hawatambui uwepo wa kuumbwa kwa mwanadamu ni shidaaaaaa.

Nimalizie kwa kusema tutaona mengi maana tunakoelekea nadhani watu wachache tu tanzania ndo wanaona kuna uhalali wa kuendelea kuishi na the rest watajiua ili kukimbia masumbuko na taabu za kuishi tz ya viwanda bila umeme wa uhakika
 
Kwani tulikuwa tuna mwelekeo wa kwenda kokote? maana mm naona tuko vile vile na tuko pale pale na tz kamwe haitakuja badlka kwa sera na siasa za fitina na chuki
 
Huelewi nini sasa wakati alisema huu ni wakati wa watanzania kuishi kama mashetani. japo ushetani wenyewe una exemption(refer to kolo boy)
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa?

Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Htl
 
Km tuna viongozi Leo anasema hiki,kesho kasahau anakula matapishi yake hapo tambua tumepoteza.

kiongoz badala ya kuweka mipango kazi yake ni kumlaumu mtangulizi then tambua hapo hamna kitu.

Leo anazungumzia Tanzania ya namna Fulani halaf ukimuuliza strategy zikowapi anasema nisiulizwe wala kushauriwa chochote mm ndio najua ntafanyeje.

wananchi Tuamke tuache kulala fofofo.
 
Wengi tunaumizwa na serikali hii ya awamu ya tano. Tunakatishwa tamaa na serikali hii ya awamu ya tano. Tunapuuzwa. Tunaonewa. Tunadhalilishwa. Tunadhihakiwa. Ndugu zetu wanapotea. Ndugu zetu wanaumizwa. Ndugu zetu wananyanyaswa. Ndugu zetu wanatishwa. Hakuna wa kuwatetea. Hakuna anayejali.

Tupeanae faraja. Tujengane kisaikolojia. Tuungane kwa maumivu yetu. Tutafute majibu kwa pamoja. Tutafute adhabu inayostahili kwa serikali ya awamu ya tano.

Wafanyabiashara. Mama ntilie. Wafanyakaz/watumishi. Wakulima. Wafugaji. Wavuvi. Madereva. Wakandarasi. Vijana. Akina mama. Wazee. Wasomi. Wanaolala njaa. Tuungane, tuiadhibu CCM na serikali yake.

Hatuwezi kukombolewa na vyama vya upinzani. Hatuwezi kukombolewa na wazungu. Hatuwezi kukombolewa na Mbowe ,Maalim ,Lipumba wala Zitto. Hatuwezi kukombolewa na CHADEMA, CCM, CUF. Hatuwezi kukombolewa na Rais Magufuli.

Njia pekee ya kujikomboa ni kuungana. Ni kupambana na kila fikra hasi bila kujali imetolewa na nani. Njia pekee ni kuamua leo ni namna gani tuendeshwe sio wao watuamulie namna gani watuendeshe. Muda ni sasa. Tuchukue hatua. Tujikomboe.

Kila kundi tuna wajibu wa kujikomboa kwa kuweka tofauti zetu pembeni na kuungana.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu ibariki Africa.
 
Mnatumia nguvu kulalamika badala ya kuwaelimisha ndugu zenu vijijini,mana wao ndo mtaji wa chama chakavu
Kweli kabisa. Wa mjini wanaopewa ma T shirt Ndio wanaotuharibia maisha kila siku,wanachagua watu hovyo kabisa
 
Kwa kweli kuna umuhimu wa kuungana na yeyote yule aliye madhubuti na tayari kuwaondoa huyu mkoloni mweusi Tanzania.
Tukutane 2020 tukinia mamoja.
Together we can.
 
Wananchi hawajaanza kuumizwa na serikali awamu ya tano pekee,huu ni unyanyapaa,vipi wale walioumizwa na awamu zilizopita nao wakalalamike wapi?

Uzi wako ni wa kutafuta kiki,fanya kazi kijana vinyongo na visasi havitakusaidia kamwe
 
Kwa kweli kuna umuhimu wa kuungana na yeyote yule aliye madhubuti na tayari kuwaondoa huyu mkoloni mweusi Tanzania.
Tukutane 2020 tukinia mamoja.
Together we can.
[emoji106] [emoji106] [emoji106]
 
Nakweli tena kwa kuanzia sasa hivi ndugu ,baba .mama unawakatia misaada .mpaka walalamike .wakiuliza kulikoni unawaambia mmechagua ccm .[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Wanunulieni ndugu zenu smartphone ziko mpaka za alfu 60,wawe wanaingia mitandaoni kutoa tongotongo
 
Wengi tunaumizwa na serikali hii ya awamu ya tano. Tunakatishwa tamaa na serikali hii ya awamu ya tano. Tunapuuzwa. Tunaonewa. Tunadhalilishwa. Tunadhihakiwa. Ndugu zetu wanapotea. Ndugu zetu wanaumizwa. Ndugu zetu wananyanyaswa. Ndugu zetu wanatishwa. Hakuna wa kuwatetea. Hakuna anayejali.

Tupeanae faraja. Tujengane kisaikolojia. Tuungane kwa maumivu yetu. Tutafute majibu kwa pamoja. Tutafute adhabu inayostahili kwa serikali ya awamu ya tano.

Wafanyabiashara. Mama ntilie. Wafanyakaz/watumishi. Wakulima. Wafugaji. Wavuvi. Madereva. Wakandarasi. Vijana. Akina mama. Wazee. Wasomi. Wanaolala njaa. Tuungane, tuiadhibu CCM na serikali yake.

Hatuwezi kukombolewa na vyama vya upinzani. Hatuwezi kukombolewa na wazungu. Hatuwezi kukombolewa na Mbowe ,Maalim ,Lipumba wala Zitto. Hatuwezi kukombolewa na CHADEMA, CCM, CUF. Hatuwezi kukombolewa na Rais Magufuli.

Njia pekee ya kujikomboa ni kuungana. Ni kupambana na kila fikra hasi bila kujali imetolewa na nani. Njia pekee ni kuamua leo ni namna gani tuendeshwe sio wao watuamulie namna gani watuendeshe. Muda ni sasa. Tuchukue hatua. Tujikomboe.

Kila kundi tuna wajibu wa kujikomboa kwa kuweka tofauti zetu pembeni na kuungana.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu ibariki Africa.
Kwa akili yako ndogo unadhani ccm haina watu?Huwezi kuitoa ccm madarakani kwa kukutana jamii forums
 
Tumeingia. Tufanye nini sasa. Au tuingie barabarani mkuu. Unaonaje. Kushinda humu mtandaoni tunapiga kelele wamesha tufananisha na chura anayepiga kelele lakini hamzuii tembo kunywa maji.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom