Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Tulimlilia Mungu atupe rais wa namna hii asiyeona haya,asiyefumba macho kwenye Mali ya umma,mkali kwa mafisadi ..Mungu akatusikia kilio chetu akatupa Magufuli.Mungu NI mkuu Sana
 
kwani kabla ya magufuli kuingia madarakani, mtoa maada ulikuwa unaelekeza wapi? direction yako ilikuwa ni nini?

na je EL angechukua nchi unajua plan yake ilikuwa wapi?

unaweza ukaelezea chadema ilipo kwa sasa ki direction ukiwa una refer context ile ile ya magufuli kwa taifa? ( rudia kusoma tena)
 
J
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Hatuwezi kupotea kwa sababu hatujui tunapoenda!
 
Ndio ana roho mbaya, tena roho mbaya kweli kweli, na msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
Amewafanya watu wasiaminiane tena, watu wanakaa kwenye vikao lakini akili ziko nje, ya kwamba humu tutoke vipi.
Watu wanaingia kwenye vikao bila ajenda. Roho mbaya iliyotukuka. Kila mmoja kapoteza dira miongoni mwa timu.
Roho mbaya ya kuwanyima ajenda wenzio. Kila kona amekaba. Wapinzani hawana tena ajenda. Mzee anatoa majibu kuntu mpaka kwenye korosho, hakuna upenyo.

Ndege zimeshindikana kuwa ajenda.

Umeme umeshindwa kuwa ajenda.

Afya imegoma kuwa ajenda.

Miundombinu imegoma kuwa ajenda.

Michezo na wasanii mzee anacheza nao fair.

Kiufupi ni roho mbaya kuwanyima wenzio ajenda ya kusemea.

NB: Labda hapa penye nyongeza ya mishahara kwa watumishi ndio wanaweza kutokea. Ukiziba na hapa 2020 kampeni chapisha vipeperushi halafu acha UVCCM wavisambaze halafu wewe nenda likizo CHATO usubiri kuapishwa.
Mdanganye
 
..Duh!!

..wakabangue korosho kwa mdomo?

..kwanini anatoa matamshi kama hayo?

..ninavyoelewa mimi maganda ya korosho yanaunguza, sasa kuna kiongozi anafikiria kuamrisha wananchi wabangue korosho kwa midomo?

.

tindo, Nguruvi3, chige
 
Wengi kumbe lazima watumie unaakili zako timamu huwezi fanya huo upuuzi
 
..Duh!!

..wakabangue korosho kwa mdomo?

..kwanini anatoa matamshi kama hayo?

..ninavyoelewa mimi maganda ya korosho yanaunguza, sasa kuna kiongozi anafikiria kuamrisha wananchi wabangue korosho kwa midomo?

.

tindo, Nguruvi3, chige
Tena yanaunguza kweli kweli! And the question is: halafu vijana wetu wa JKT wakishaenda kubangua korosho kwa mdomo kisha wanazipeleka wapi!!!
 
Huko nyuma haikuwa rahisi kudhani kwamba Tanzania ingekuwa mojawapo wa nchi ambayo ingeingia katika nyanja za nchi zinazosemwa kuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu. Haya mambo tulisikia yakisemwa juu ya nchi za wenzetu, lakini kwa nchi yetu lilikuwa jambo nadra sana.

Lakini sasa ni wazi kwamba chini ya utawala wa awamu ya tano, kadiri siku zinavyokwenda ndivyo hali ya Tanzania kusemwa na Watanzania wenyewe ndani ya nchi pamoja na mataifa mbali mbali, taasisi za kimataifa kutia ndani zinazotetea haki za wanadamu nk, kwamba ina kiuka misingi ya haki za binadamu na utawala wa sheria.

Ninachojiuliza, hivi Raisi Magufuli anadhani kwamba kelele zote hizi zinazopigwa juu ya ukosefu wa haki za binadamu na utawala wa kisheria nchini zinasemwa na watu wasio na akili ambao wameamua kuropoka bila kuona kwamba kweli Tanzania kuna tatizo? Ni ngoma ya aina gani Raisi Magufuli anataka apigiwe ili aelewe kwamba utawala wake una walakini katika suala la haki za binadamu na kwamba kuna haja ya kurekebisha kabla hali haijawa mbaya zaidi?

Au tuna tatizo la sikio la kufa kwa raisi wetu?
 
Nachukia udikteta wa hili jiwe

,hapendi kukosolewa

hapendi uhuru


hapendi upinzani


hapendi mawazo mbadala


hashauriki



wapinzani kwake ni maadui



hana diplomasia



anakurupuka



ameua uchumi



Ameua misingi ya demokrasia yote


huu ni zaidi ya udikteta

Note: Sijataja mtu anajijua mwenyewe abadilike aache udikteta na ugaidi wa kisiasa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom