Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Zanzibar walichakionja kikombe cha utawala wa kidikteta wa Salmin Amour kwa kipindi cha miaka 10, na sasa ni zamu ya watu wa Bara kukionja kikombe hicho. Na kuanzia hapa mchakato wa kumpata kiongozi wa nchi utakuwa ukifanywa kwa umakini mkubwa. Usiyempenda uko naye mpaka 2025, labda mabadiliko yapitie ktk mpango mbadala wa Mola mwenyewe, na wala si vinginevyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mpango wa Mungu umefaulu Mkuu,sifa na utukufu umrudie yeye daima!!..
 
Huyu mzee ametuvuruga sana watumishi wa umma! Yaani kwa sasa wengi wanaishi kwa salary advance! Maana hali ni tete. Mshahara hautoshi kiasi cha kusikitisha!

Bora hata na yeye angepumulia mtungi wa gesi hata mwezi tu kama yule msaidizi wake! ili ukaidi, ubinafsi, ukatili, uonevu dhidi ya wengine na majivuno yake yapungue kidogo.
Your prayers have been successful approved [emoji736]
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Hatimaye safari imefikia tamati
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Kesho wanafukia mgomba. Kwishaaa dictator uchwara
 
Kuna maneno mengi ambayo yakisikika masikioni tu unahisi (predict) mbeleni kuna utapeli/wizi unakuja kwa kasi ya 4G.

Kwangu mimi nikisikia maneno yafuatayo akili inakaa kitako kabisa najua ninae ongea nae/anae ongea ni mwizi na fisadi wa kutupwa.

Nitataja machache,nawe orodhesha yako pia.

1. Beberu/Mabeberu[emoji58]
2.Wanyonge[emoji16]
3.Uzalendo[emoji1751]
4.Tumechezewa sana[emoji33]
5.Uchumi wa kati[emoji24]
6.Hapa kazi tu.[emoji1787]
7.Tanzania ya Viwanda [emoji23]
8.Mtetezi wa watu maskini.[emoji849]
9.Mniombee[emoji847]
10.Nimesakirifiiz maisha yangu kwa ajili yako[emoji20]
11.Matajiri[emoji3063]

ONGEZA YAKO.

Ndugu zangu, tuendelee kujifukiza,kunywa limao na Tangawizi,na barakoa za kushona, maendeleo hanaya chama[emoji120]
20210408_230221.jpg
 
Si jambo jema kwa mtu mwenye akili timamu kupambana na marehemu.
 
Kuna maneno mengi ambayo yakisikika masikioni tu unahisi (predict) mbeleni kuna utapeli/wizi unakuja kwa kasi ya 4G.

Kwangu mimi nikisikia maneno yafuatayo akili inakaa kitako kabisa najua ninae ongea nae/anae ongea ni mwizi na fisadi wa kutupwa.

Nitataja machache,nawe orodhesha yako pia.

1. Beberu/Mabeberu[emoji58]
2.Wanyonge[emoji16]
3.Uzalendo[emoji1751]
4.Tumechezewa sana[emoji33]
5.Uchumi wa kati[emoji24]
6.Hapa kazi tu.[emoji1787]
7.Tanzania ya Viwanda [emoji23]
8.Mtetezi wa watu maskini.[emoji849]
9.Mniombee[emoji847]
10.Nimesakirifiiz maisha yangu kwa ajili yako[emoji20]
11.Matajiri[emoji3063]

ONGEZA YAKO.

Ndugu zangu, tuendelee kujifukiza,kunywa limao na Tangawizi,na barakoa za kushona, maendeleo hanaya chama[emoji120]View attachment 1747318
Tumpumzisheni sasa jamani mizigo aliyobeba ni mingi sana
 
Mmesubiri yuko kaburini,hawezi kufafanua jambo lolote,wala kujitetea kwa namna yoyote ile,mnaanza kumnanga.
Kwakweli kuna watu wanafiki sana,hadi wale unaofanya nao kazi,unakuta nao ni wanafiki,namsifu waziri mkuu,yupo kimya hadi sasa.
 
Tumechezewa sana , hiyo kauli imeniingia sana na ni ukweli . Mpaka majirani kutucheka kwa kukalia uchumi . Nasikitika aliyetuamsha hayupo ila mrithi wake ataendeleza .

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom