Anayemuelewa Makonda anaeneza nini atuambie, sisi wananchi tunona kama haeleweki

Anayemuelewa Makonda anaeneza nini atuambie, sisi wananchi tunona kama haeleweki

Bush Dokta

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2023
Posts
24,831
Reaction score
45,154
Mara apande Baiskeli, mara Troli na saa nyingine unaona kama vile amelazishwa kufanya baadhi ya matukio.

Ni kweli CCM ilishakufa na hakuna namna ya kuizindua tena si Makonda wala nani.

Kwani mpaka imwshindikana wakaamua kumtafuta mtu waloyemtupa nini ilikuwa shida?

Ccm imemshinda Mjema, imamahinda Kihongosi na wengine akina Chongolo Makonda ataweza nini?

Wananchi tunaishia kucheka tu. Vituko na maigizo ya Mh Makonda.

Hatujui kaja kueneza nini? Au kaja kueneza hadaaa na sanaaa zisizo kuwa na maana kwa Wananchi.

Sisi wananchi tungemwelewa kama angeagiza Serikali yake ifanyie kazi Ripoti ya CAG iliyothibitisha wizi wa mali za umma kwa watu binafsi na familia zao.

Sisi wananchi hatumwelewi kwa sababu Msimu huu ni wa Mvua kila kona ya Nchi Alhamdullilah Mungu ameturuzuku na Mvua hivyo watu wote yatupasa tuwe mashambani tukiandaa mashamba na kupanda badala ya mtu mmoja kukusanya watu na kuwapotezea muda.

Jpm hakuwa hivyo. Alipiga marufuku siasa za majukwaani ili watu wafanya kazi.

Sasa huyu mwamba zaidi ya kuongea ongea tu maneno meengi ambayo hata hao anaowaagiza hakuna anyetekeleza.

Matamko na maagizo mengi baadhi ya watu wamedokeza kuwa hakuna anyetekeleza zaidi ya kuishia majukwaani.

Ingetosha Katibu mwenezi kufanya mikutano ya ndani kuimarisha chama kilichokosa ushawishi kwa Wananchi Huru.

Je kilichomshinda Mh Kinana, Mh Makamba, Mh Mjema, Mh Chongolo, hayati Dr Jpm, Mh Dr Samia, Dr Bashiru, Mh Polepole Mh Makonda atakiweza?

Ngoja tujipe muda
 
Mara apande Baiskeli, mara Troli na saa nyingine unaona kama vile amelazishwa kufanya baadhi ya matukio.

Ni kweli ccm ilishakufa na hakuna namna ya kuizindua tena si Makonda wala nani.

Kwani mpaka imwshindikana wakaamua kumtafuta mtu waloyemtupa nini ilikuwa shida?

Ccm imemshinda Mjema, imamahinda Kihongosi na wengine akina Chongolo Makonda ataweza nini?

Wananchi tunaishia kucheka tu. Vituko na maigizo ya Mh Makonda.

Hatujui kaja kueneza nini? Au kaja kueneza hadaaa na sanaaa zisizo kuwa na maana kwa Wananchi.

Sisi wananchi tungemwelewa kama angeagiza Serikali yake ifanyie kazi Ripoti ya CAG iliyothibitisha wizi wa mali za umma kwa watu binafsi na familia zao.

Sisi wananchi hatumwelewi kwa sababu Msimu huu ni wa Mvua kila kona ya Nchi Alhamdullilah Mungu ameturuzuku na Mvua hivyo watu wote yatupasa tuwe mashambani tukiandaa mashamba na kupanda badala ya mtu mmoja kukusanya watu na kuwapotezea muda.

Jpm hakuwa hivyo. Alipiga marufuku siasa za majukwaani ili watu wafanya kazi.

Sasa huyu mwamba zaidi ya kuongea ongea tu maneno meengi ambayo hata hao anaowaagiza hakuna anyetekeleza.

Matamko na maagizo mengi baadhi ya watu wamedokeza kuwa hakuna anyetekeleza zaidi ya kuishia majukwaani.

Ingetosha Katibu mwenezi kufanya mikutano ya ndani kuimarisha chama kilichokosa ushawishi kwa Wananchi Huru.

Je kilichomshinda Mh Kinana, Mh Makamba, Mh Mjema, Mh Chongolo, hayati Dr Jpm, Mh Dr Samia, Dr Bashiru, Mh Polepole Mh Makonda atakiweza?

Ngoja tujipe muda
Naunga mkono hoja yako
 
Wengi wao wanaokuwa kwenye hiyo mikutano live ndiyo wapiga kura,hawana smartphone Wala hawaijui JF.
 
Cameras!!! Flash!!💥⚡ Flash!!💥⚡

Nyie sasa ndiyo waenezi, mnaeneza.
Mngemkaushia kama hamumuoni vile!

Tujikumbushe madaraka ya kulevya
Madaraaaa Madaraka x2
Umenipa madaraka ya kulevya
Ooh baby
Nayumba nateleza
Umenipa madaraka ya kulevya
Oo darling
Naimba napoteza x2
Mjini nimedondoka kama chopa, chopa star...
Wananiita zee la makopa
Zee la kulia mtoto hawezi toka
Watoto wanang'oka
Zangu mimi ni kung'arisha moka
Napenda malight camera action
Na malikes nyomi attention
Nyumbani situlii na mummy
Zangu ni vijiwe na kina naniii
Napendaga makiki kama msanii
Nanii, tukipiga picha nipost
Napenda mafollowers
Napendaga makiki kama msaniii
Umenipa madaraka ya kulevya
Ooh baby
Nayumba nateleza
Umenipa madaraka ya kulevya
Oo darling
Naimba napoteza x2
Kila nikiona kibinda mi nadinda
Kila nikiona kibinda mi nawinda
Kidinda kikidinda nakitia ndinda
Wananiita mzee wa vibunda
Na mbele zikivimba nazitoa mimba
Mke wangu kila siku namtoa mapovu
Nimeshaonywa sana na baba askofu
Sijui shetani gani ameniingia
Nimeshaombewa sana na kila parokia
Na bado kila demu mkali mi narukia
Nazama next door na majala
Nakata kwa watoto na katoto nyumbani haa kajala
Mastaa Bongo muvi wananiitaga danga
Napiga mablunder
Vitumbua vinanijua bingwa la kutia mchanga
Napiga mablunder
Naishi kama kwangu na nyumba ni ya kupanga
Vitu vinaenda nganganga
Umenipa madaraka ya kulevya
Ooh baby
Nayumba nateleza
Umenipa madaraka ya kulevya
Oo darling
Naimba napoteza x2
Dereva nagonga miti
Aaacha, hiyo si sawa dereva una mkeo
Mzee nina midananda kibao
Sijui kutongoza msaada ni wao
Mdanada ukizingua mambao
Zee la mipango
Zee la majigambo
Natembelea ndoa ndoano, nawavua
Kijani naitia nyekundu, natibua
Na urithi baba alishaniahidi, nazitumbua
Ndugu wanalia nauchubua
Mke wangu yuko home nguo zangu anazifua
Mi niko guest flani zangu navua
Umenipa madaraka ya kulevya
Ooh baby
Nayumba nateleza
Umenipa madaraka ya kulevya
Oo darling
Naimba napoteza x2

View: https://youtu.be/gvP23mP9KqU?si=3Ro-BnwR2PmCq0q3
 
Daudi Albert Bashite!! Hili ndilo jina lake halisi. Ni mtu wa kujitutumua sana, aliyejaa mihemko na mpenda sifa za kijinga. Na wakiendelea kumchekea, matunda yake watayaona muda si mrefu.
 
ambatanisha picha mkuu zahayo matukio.asante.
20231112_004017.jpg
 
Back
Top Bottom