TANZIA Anayesadikiwa kuwa MwanaJF afariki dunia

TANZIA Anayesadikiwa kuwa MwanaJF afariki dunia

macho_mdiliko

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2008
Posts
25,191
Reaction score
48,765
Memba mwenzetu ametangulia mbele ya haki. Pengine nisingejisumbua kuripoti huu msiba lakini mazingira ya kifo chake ni ya kuhuzunisha na yenye mafunzo. Sijui username yake ya JF kwani tulikutana ''casually'' kwenye kilevi mwezi wa tatu mwaka huu tena siku moja tu. Katika maongezi alinijulisha kuwa yeye ni ''active member'' wa JF na anapenda sana kuchangia. Baada ya kilevi (maeneo ya Boko) tulipokuwa tunaondoka akanionyesha nyumbani kwake na mimi nikaondoka kurudi kwetu Msasani ninakoishi.

Fast forward, wiki kama mbili zilizopita nilirudi tena maeneo tuliyokutana kwenye mishe zangu. Nikaona msiba kwenye boma aliloniambia ni nyumba yake. Kuulizia kulikoni nikaambiwa ni yeye, mwenye nyumba amefariki. ''Eti'' alitoka kwenye kilevi usiku, akagonga geti, mke akagoma katukatu kumfungulia. Akachukua uamuzi wa kuruka ukuta. Kwa bahati mbaya akachomwa na moja ya nondo zilizoko kwenye geti la nyumba (nadhani wengi mnafahamu nondo zinazochongwa kama mkuki na kuwekwa juu ya kuta au geti ili kuzuia vibaka). Kwa bahati mbaya akavuja damu nyingi mpaka akapoteza maisha. RIP member.
 
Jaman wale mnaopenda kulewa au kuchelewa kurudi majumbani mwenu kwa sababu za starehe kama hizi muwe mnakuwa na funguo za ziada ili ukirudi unajifungulia mwenyewe kuepusha vifo visivyo vya lazima.

Inachosha sana kuamshwa na mtu aliyetoka kwenye starehe zake ukatishe usingizi wako ili umfungulie
 
Jaman wale mnaopenda kulewa au kuchelewa kurudi majumbani mwenu kwa sababu za starehe kama hizi muwe mnakuwa na funguo za ziada ili ukirudi unajifungulia mwenyewe kuepusha vifo visivyo vya lazima .
Inachosha sana kuamshwa na mtu aliyetoka kwenye starehe zake ukatishe usingizi wako ili umfungulie
Kwanza poleni wanajamii forams kwakuondokewa na mwenzetu.

Kuhusu ushauli wako huu ,ebu wambie wifi zako mama zako wadogo, waache adhabu zakikatiri. Unaanzaje Kugoma kumfungulia mwezio? Ona Sasa amekua mjane .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza poleni wanajamii forams kwakuondokewa na mwenzetu.

Kuhusu ushauli wako huu ,ebu wambie wifi zako mama zako wadogo, waache adhabu zakikatiri. Unaanzaje Kugoma kumfungulia mwezio? Ona Sasa amekua mjane .

Sent using Jamii Forums mobile app
Yeye alipokataa kufungua wala hakuwaza hayo. Lakini pia huwezi jua ndoa yao ilikuwaje...ukute marehemu alikuwa aina ya wanaume ambao hawajali hisia za mke bali kujifurahisha yeye mwenyewe kwenye hizo pombe zake jambo ambalo mkewe alikuwa halimfurahishi
 
Pole kwa wafiwa..

Mi nilikuwa na mazoea hayo ya kulewa na kurudi usiku naruka hizo nondo asubuhi najikuta nimekwaruzika mwili mzima kisa cha kuacha mchezo huo sitasahau.

Nilirudi siku hiyo kilevi kimezidi kuliko kawaida nikapiga simu na kugonga sikufunguliwa nikachukua maamuzi ya kuruka. Niliacha kila kitu juu ya nondo surwali shati hadi boksa. Nikaingia ndani nikalala na viatu tuu. Asubuhi kidogo mama angu afe kwa presha akajua nimeuliwa nikatupwa juu ya nondo kumbe nguo. Akaingia ndani nimelala uchi akanikagua mzima zaidi ya michubuko tuu. Sitasahau
 
Kuhusu ushauli wako huu ,ebu wambie wifi zako mama zako wadogo, waache adhabu zakikatiri. Unaanzaje Kugoma kumfungulia mwezio? Ona Sasa amekua mjane .
Ametoa ushauri muwe na funguo zenu, hujaona? Umeona tu roho mbaya ya huyo alogoma kufungua mlango?

Yan mtu umejizoelea kulala saa 4, mumeo mlevi anakaa bar mpaka saa7/8/9, kuamshwa kila wakati hivyo inaboa sana.
 
Back
Top Bottom