Anayetuhumiwa kumlawiti mtoto katika Vyoo vya Kanisa - Sinza, asema “Sina lolote, naiachia Mahakama”

Anayetuhumiwa kumlawiti mtoto katika Vyoo vya Kanisa - Sinza, asema “Sina lolote, naiachia Mahakama”

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Baada ya mshtakiwa katika kesi Namba Cc.5866 /2024, Baraka Benedicto anayedaiwa kumlawiti mtoto kushindwa kutoa utetezi wake siku ya Februari 26, 2025 akitoa sababu mbele ya Mahakama kuwa anaumwa, jana Machi 3, 2024 shauri hilo limetajwa, ambapo alipopewa nafasi ya utetezi amesema hana lolote la kueleza, hivyo anaiachia Mahakama.

Kufuatia mshtakiwa kueleza hayo, Mahakama kupitia Hakimu Nabwike Mbaba imeahirisha shauri hilo mpaka Machi 7, 2025.

Ikumbukwe Baraka Benedicto alipandishwa mahakamani baada mdau wa JamiiForums kudai kwamba kulikuwepo na mazingira ya danadana ya kutomfikisha Mahakamani mtuhumiwa (Baraka) ambaye inadaiwa akiwa anatekeleza majukumu ya ulinzi katika Parokia ya Bikira Maria Mama Mwokozi-Sinza ambapo ilidaiwa alimfanyia ukatili wa kumlawiti mtoto wa kiume kwenye vyoo Parokia hiyo.

Kesi hiyo inayosikilizwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni awali ilianza kutajwa mbele ya Hakimu Ramadhani Rugemalira lakini baadae ilihamishiwa kwa Hakimu Nabwike Mbaba ambaye anaiendesha hadi sasa.

Ikumbukwe, kesi hiyo ilifikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza Machi 2024 siku chache baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuomba Mamlaka kuchukua hatua kumsaidia mtoto husika.

Vilevile itakumbukwa mshtakiwa Baraka Benedicto alikana shtaka la ulawiti alilosomewa alipofikishwa mbele ya Mahakama.
Gwajima (1).png

Kulawiti (1).jpg


Pia soma

~ Mlinzi wa Kanisa (Sinza, Dar) aliyeshtakiwa kwa kumlawiti mtoto kwenye vyoo vya Kanisa, atupwa jela Miaka 30

~
Anayetuhumiwa kulawiti Mtoto kwenye Vyoo vya Kanisa ashindwa kutoa Ushahidi, adai anaumwa, kesi yaahirishwa hadi Machi 3, 2025

~ Serikali imsaidie Mtoto huyu anayedaiwa kulawitiwa na Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza

~ Dar: Mlinzi wa Kanisa anayetuhumiwa kumlawiti Mtoto Muimba kwaya kwenye vyoo vya Parokia apandishwa kizimbani

~ Tukio la Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza kudaiwa kumlawiti Mwanafunzi, Padri asimulia kilichotokea

~ Madai ya Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza kumlawiti Mwanafunzi, mama wa Mtoto aomba Serikali imsaidie
 
Kama ni kweli basi ahukumiwe, ila kuna tabia ipo mitaani unaweza kutengenezewa tatizo ambalo hata kujitetea unashindwa
 
Mambo mengine bwana!

Hivi na Ulaya kuna issues kama hizi kwenye mainstreams zao au hili jua la utosi Africa medulla zimebabuka?
 
Mambo mengine bwana!

Hivi na Ulaya kuna issues kama hizi kwenye mainstreams zao au hili jua la utosi Africa medulla zimebabuka?
Child abuse ipo aise, UK juzi juzi waliunda tume kuchunguza, watoto wananyanyasika sana
 
Mtu kama huyu analindwa ili aendelee kubokoa watoto... ajabu sana.
 
Hapa watuhawatataja dini, atasemwa shetani. Ila angekua ni muislam kwenye vyoo vya msikiti pasingetosga, wagaratia mnamatatizo sana
 
Kama ni kweli basi ahukumiwe, ila kuna tabia ipo mitaani unaweza kutengenezewa tatizo ambalo hata kujitetea unashindwa
Kesi hazina uhalisia hizo , hakuna ukweli hata unazosikia kwenye media ni uongo kabisa ...Ukikutwa kwenye mazingira watu wakakuhisi vibaya basi umekwisha .

Kuna jamaa alimchukua mtoto mdogo akampeleka chooni kukojoa , sasa alikuwa anamfungua zipu ili akojoe maana ni dogo wa miaka kama mitano , kwa vile wako chooni na alifunga mlango ..Watu wakaanza kusema anataka kumlawiti na dogo kweli alikuwa anataka kukojoa ila jamaa alipigwa vibao mpaka watu walipokuja kugundua .
 
Kesi hazina uhalisia hizo , hakuna ukweli hata unazosikia kwenye media ni uongo kabisa ...Ukikutwa kwenye mazingira watu wakakuhisi vibaya basi umekwisha .

Kuna jamaa alimchukua mtoto mdogo akampeleka chooni kukojoa , sasa alikuwa anamfungua zipu ili akojoe maana ni dogo wa miaka kama mitano , kwa vile wako chooni na alifunga mlango ..Watu wakaanza kusema anataka kumlawiti na dogo kweli alikuwa anataka kukojoa ila jamaa alipigwa vibao mpaka watu walipokuja kugundua .
Ndio maana mazoea na watoto sitaki labda mtoto watoto wangu tu
 
Mambo mengine bwana!

Hivi na Ulaya kuna issues kama hizi kwenye mainstreams zao au hili jua la utosi Africa medulla zimebabuka?

Ulaya ndo zaidi ya hayo mauchafu.. washa VPN kisha ingia hapa theync.com
 
Kesi hazina uhalisia hizo , hakuna ukweli hata unazosikia kwenye media ni uongo kabisa ...Ukikutwa kwenye mazingira watu wakakuhisi vibaya basi umekwisha .

Kuna jamaa alimchukua mtoto mdogo akampeleka chooni kukojoa , sasa alikuwa anamfungua zipu ili akojoe maana ni dogo wa miaka kama mitano , kwa vile wako chooni na alifunga mlango ..Watu wakaanza kusema anataka kumlawiti na dogo kweli alikuwa anataka kukojoa ila jamaa alipigwa vibao mpaka watu walipokuja kugundua .
Bro miaka mi 5 anakojoleshwaje na mtu bak tena chooni serious
 
Back
Top Bottom