Anayezijua hoja za Mbowe zilizompelekea kugombea tena nafasi ya uwenyekiti wa chama aziweke hapa tuzijue

Sasa ZERO atakuwa na Hoja!!
Kazi kweli kweli
 
CCM Wana serve maslahi ya Nchi ,yeye anaserve maslahi ya Mabeberu, hawezi tumikia mabwana wawili.
Maslahi gani kwani ana mamlaka ya kuwapa vitalu vya kuwinda au vya kuchimba gesi? Haujitambui kabisa kama mama yenu
 
Hoja kubwa kwake anasema Watangulizi wake walistaafu na miaka 68
 
1: Chadema ilipomteua TAL kugombea urais 2020 walijua wazi hawezi kushinda uchaguzi huo na kua rais dhidi ya utawala uliokuwepo,,walichotazama ni nani anaweza kuipatia Chadema kura nyingi za urais ili zisaidie kupata wabunge wengi wa viti maalum.

2: Chadema inao watu wengi wasomi na wenye uwezo wa kushika uongozi wa nafasi ya mwenyekiti lakini sio wote

3:uchaguzi huru na wa haki hautegemei ni nani mwenyekiti Chadema,,, toka mfumo wa vyama vingi uanze kumeshapita viongozi wenye nguvu kuliko TAL.
 
Chadema ilipomteua TAL kugombea urais 2020 walijua wazi hawezi kushinda uchaguzi huo na kua rais dhidi ya utawala uliokuwepo,,walichotazama ni nani anaweza kuipatia Chadema kura nyingi za urais ili zisaidie kupata wabunge wengi wa viti maalum.
Ingawa unapotosha maana nachojua kura za wagombea ubunge ndio huletq viti maalum. Tanzania tunatumia D'hondt method of proportion kwa threshold ya 5% ya kura zote za ubunge ili uwe eligible kupata viti.maalum. kura za urais zinasaidia walau 30% ya ruzuku kupatikana.

Anyway tukirudi kwenye hoja, Sasa logic hii hii itumike kumuweka Lissu maana ndio mtu pekee ana ushawishi upinzani, so atasaidia tupate wabunge, viti maalum na ruzuku nyingi zaidi!! Pia ana upeo mkubwa ataendesha chadema kitaalamu sana.

2: Chadema inao watu wengi wasomi na wenye uwezo wa kushika uongozi wa nafasi ya mwenyekiti lakini sio wote
Mbona sasa ame endorse Wenje agombee uenyekiti, yaani kweli wenje ndio awe second in command? Hivi mbona ni vituko.

3:uchaguzi huru na wa haki hautegemei ni nani mwenyekiti Chadema,,, toka mfumo wa vyama vingi uanze kumeshapita viongozi wenye nguvu kuliko TAL.
Si kweli, enzi za Dr Slaa mbona CCM tuliheshimiana sana alikua mtu wa kazi sio busara busara. Tunapaswa tumpate Lissu ili awaweke CCM kwenye defensive mode muda wote naamini itarudisha morale ya nguvu ya umma kama ile 2010-2015 hata CCM wakiiba wataiba kistaarabu sio kama huu uhuni unaoendelea maana wanajua Mbowe atacheka cheka tu.

Enough is enough, wakimpa Mbowe chama ndio tumekwisha kabisa.
 
Chama hakipo salama kwenye mikono yake mwenyewe 😂 uzuri anajua kuwa yeye ndio mhusika wa kutokuwa salama
Anaropoka ropoka tu sijui konyagi ndizo zilihutubia? Ati si vema kubadilisha mwenyekiti wakati uchaguzi ni mwakani.

Hivi kwa jinsi ccm walivyomzowea kama nguo zao za ndani mwakani kutakuwa na uchaguzi kweli? Yale yale ya serikali za mitaa yatafanyika.

Jingine anasema yeye ni mfanyabiashara HABANGAIZI. Hivi kweli maneno ya nyodo kama hayo yanaweza kunenwa na mtu mwenye akili timamu?
 
Ni kweli comrade nilipotoka hapo, nilichotaka kuandika ni ruzuku,,,pengine kichwani nilikua nawaza viti maalum.

Hata Mimi ninapenda Mbowe ang'atuke ili Chadema kisiwe chama cha mtu mmoja.

Hebu jifanye wewe ndio TAL tueleze utafanya nini hadi serikali iliyopo madarakani ikuogope na hivyo ihakikishe uchaguzi unakua huru na haki?

Umetoa mfano wa Dr Slaa,, siamini kama yeye ndio sababu ya uchaguzi angalau kuonesha dalili ya kuwa uchaguzi huru na wa haki, ila ni uongozi uliokua madarakani wakati huo,,,hata mwaka 2015 Chadema ilipata wabunge wengi na kura nyingi za urais, lakini Chadema hiyohiyo ilipoteza viti vingi na sababu kuu ni utawala uliokua madarakani wakati huo.

Ili TAL alete maajabu ni kama ataweza kushawishi kundi kubwa la watu wenye nyadhfa kutoka chama tawala wahamie Chadema tofauti na hapo ataishia kupiga kelele tu.
 
Hoja yake nyingine ni kwamba:-
Ametumia fedha zake nyingi sana pale chadema
 
Hayo makubaliano ndio yamekufikisha kwenye kutekwa kudhulumiwa uchaguzi na kuumizwa kuuliwa nk. Tumia hata comon sense ulizopewa na Muumba wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…