Anayosema Kigwangalla kuhusu uaminifu wa Watanzania kuna tatizo?

Haya basi Sawa mtaalam
 
Ile kauli ya " @ Soma ule nchi" ilitengeneza wezi wengi sana katika nchi hii.

Wanasiasa walitengeneza wizi na ujanja ujanja kuwa mfumo rasmi wa maisha ya watanzania.

Aliyeko serikalini anaibia serikali, aliyeko kwa mhindi anamuibia mhindi, aliyeko kwenye biashara ya mume wake anamwibia mume wake, aliyeko kwenye biashara ya baba yake anamuibia baba yake.

Wanasiasa ndiyo walitengeneza kizazi cha namna hii kuwa utajiri unapatikana bila kufanyia kazi na ukiwa serikalini unapaswa kuishi nche ya kipato chako matokeo yake ndiyo haya.

Watanzania hawaaminiki kwa lolote bila kujali elimu zao, umri wao na nyadhifa zao, achilia mbali imani zao.

Tunatengeneza jamii ya isiyo na maadili lakini pia isiyo utashi wa kufanya kazi.

Hivi leo ni mtanzania yupi unaweza kumnyooshea kidole kuwa mfano bora kwa watu kwenye hili Tabaka la juu ?

Anachokilalamikia Kigwangala ni kitu kiko wazi tu hata kwa yeye mwenyewe uadilifu wake unatia mashaka sana. Anataka apate paka katika kizazi cha panya ? Anajidanganya panya hawezi kuzaa na kulea paka.

Kizazi hiki kisicho na maadili yoyote kilitengenezwa na siasa isiyojua kesho ya jamii yake.
 
Ukitafsiri hadith ya HK kwa lugha yeyote ile halafu ukatafuta gugu au search engine yeyote ile kwa kutumia part(sehemu yeyote ile) katika hiyo hadithi;utakutana na stori kama hiyo Duniani kote! Yaani utaweza kudhani ame kwapua na kubandika(copy and paste) vile kwa kufanana fanana na stori zingine.

Hakika yamemkuta, na ninawajua wengi kama HK. Mhindi, Mzungu, Mkenya wote have something in common, nayo ni lack of trust..hawana wakuwaamini kwa 100% kwa lugha nyingine nyepesi tu ni Uaminifu(trustworthiness) ni hulka ya binadamu. Watu wote bila kujali dini rangi nchi au jinsia yake...Hivyo basi kuwapachika Watanzania kwa ujumla kuwa hawaaminiki ni kosa kubwa sana. Tupnuguze kujishusha chini kiasi hicho na kuwaacha hawa wapotoshaji kama huyu ninayemnukuu ambaye anadai ni sababu za "Ujamaa"
Mbongo ukimpa kazi kitu cha kwanza akilini mwake ni atakuibiaje. Na kwa ujinga linaenda kwa mganga eti usifurukute!!! Ujamaa tuliopitia ndiyo umezaa hii tabia ya wizi.
....ipo siku weye huo uwakili wako utakapo kurudia... karma will devour you, hiyo tabia unayotaka kutumia kuwatukana Watanzania kila kukicha itakumaliza vilivyo. Ulaaniwe kwa jina la Mungu. Ulegee na ushindwe.
 
Mtu mwenye kampuni top management unakuta white people....ukimpa Mbongo kampuni inakufa...totally...ni ukweli mchungu na mbaya ila ni kwl
Top management ni kwa ajili ya kulinda interest, mfano crdb ,nmb,uba,etc etc, na hao top management hawatumiwi pesa ovyo kama alivyokuwa anafanya kigwa, wanakuta kuna rules za kufuata,ukikiuka unafukuzwa kazi. Suala ni misingi.
 
Kwa capital yake alitakiwa aajili external auditors, ina maana yeye mahesabu alikuwa hapeleki tra? Auditor wake hakuwa akimshauri? Risiti alikuwa anapewa kila akituma pesa?

Ndio maana nanukuu kariakoo kuna mfanyabiashara alisema ,ukimtoa mtu wa tra umpe duka na mtaji atachemka.
 
alalamike afanye atavyofanya ila aina ya maisha tunayoishi watanzania ni mfumo ulioletwa na watawala hakuna kitu kinaibuka tu from no were ila wakitaka kutulaumu vijana kwanza tuwaulize wao mali wanazomiliki zote ni za halali viongozi wetu na watendaji wetu ambao wengi ni wazazi wetu je mali zao ni za halali.??

watoto siku zote tabia wanaadopt kutoka kwa wazazi wajitazame wao na wajisahihishe then warudi kwetu watusahihishe..
tofauti na hapo ni kupigia mbuzi gitaa tu.
 
Pole mkuu ila apo kwenye MAADILI kwa nchi hii Kila sehemu tatizo labda tufe wote wazaliwe wapya tuanze 1
 
Doh! Watu wamepitia mengi
 
Ujamaa huzalisha wezi na wabinafsi. Hilo halina ubishi.
 
Alikuwa analima kwa Mpesa tu.
 
Japokuwa suala la uaminifu limekuwa ttz kubwa kwa watu wengi nchi hii lakini hili janga muheshiwa ni kama alilitengeneza mwenyewe
Haiwezekani mradi mkubwa kama huo ww uwe unatuma tu pesa kwa mtu
 
Majuto ni mjukuu ndugu mheshimiwa.

Na hapo unalia kia hujalala selo Miezi sita unaliwa na kunguni kwa Kesi ya kubambikiwa.
imagine
 
Aikael Mbowe?
 
Very motivating story,
Ila kichwa cha habari,kinataka kuonyesha kwamba vijana wa TZ,wote sio waaminifu,"a people problem"sio kweli,
Hata yeye kingwangala aliwahi kuwa kijana,mbona ni muaminifu?
Aliyopitia kwenye safari yake ya Maisha,siyo ya pekee yanaweza kutokea Duniani kote,
Kuhusu vijana kupenda kutafuta ajira,lakini hawataki kazi,lipo sana,ni matokeo ya uozo wa elimu yetu na malezi,
Sasa kijana anaona vijana wenzake,waliobahatika kupata ajira,tpa,nssf,bot,ndani ya muda mfupi,wana ukwasi wa kutisha,bila jasho,na yeye atatamani tu,
 
Ukisoma vitu anavyoandika sijui dhuruma sijui na moyo wa upendo anandika akiamini wapiga kura wake asilimia 90 wapo maporini na hawapo katika hizi social media

Yani ni hivi hakuna mtu kauzu na mdhurumati na mwenye roho mbaya ya umimi kama kigwangala anajisifu sijui nasaidia watu acheni awapige maneno mtandaoni hakuna mtu mbinafsi kama kigwangala muulizeni chuo chake cha uguzi kwanini hakina wakufunzi jamaa alipi mishahara yeye kisa waziri mbunge basi fundisha tu analipa anavyotaka ukidai sana unasikia nenda mahakamani, vistory vyake nje ya box nje ya box yeye ashukuru JK kumshika mkono akapata ubunge akapata mianya ya kupiga pesa ndio hivyo hana uhustler wowote aache wahadaa vijana kwa story za kutunga tunga tu maana anavyoandika asilimia 80 ni fiction

Alishapewa msaada wa computer na tasisi moja hivi akiwa kama mbunge aziwasilishe katika shule za jimbo lake, mwamba zile computer zote akapeleka katika chuo chake binafsi cha afya walimu wanambiwa na mfadhili waende chukua computer kapewa mbunge wao, walimu wanaenda kumuuliza anaanza watisha ooh tafunga mtu vitisho kibao, yani uyo kigwangala ni msanii kama wasanii wengine tu
 
Poa kigwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…