Anayosema Kigwangalla kuhusu uaminifu wa Watanzania kuna tatizo?

Anayosema Kigwangalla kuhusu uaminifu wa Watanzania kuna tatizo?

Tatizo linaanzia ngaz ya familia. Karibu watanzania wote huwa tunaandaliwa kuwa wapigaji kwa hoja kwamba tufanye kazi sehemu zenye marupurupu. Hata kama mtoto kazaliwa na hana roho ya upigaji atalazimishwa kuingia kwenye upigaji... sehemu kama BOT, TRA, Hazina hasa miaka ya nyuma zimekuwa zikilaumiwa mno kuingiza vilaza ambao ni ndugu au watu wa karibu wa vigogo ili tu kuendeleza upigaji. Mimi wakati namaliza chuo nilipenda sana kuwa mjasiriamali na baadae mfanyabiashara mkubwa ila vita na wazazi ilikuwa kubwa sana kutaka niingie kwenye ajira ya serikali kwa hoja kwamba ukiingia kwenye mfumo utazikuta hela humohumo. Bahati nzuri nilisimamia msimamo wangu.
Walimu wengi hasa wa Primary Schools wamekwenda kusoma masuala ya ugavi, uhasibu, mipango, biashara, and the like, na, wamekimbia ualimu wako huko; Ni "wapigaji" hao! Wanapiga pesa na mali za umma kama vile kesho watarudishwa tena kufundisha shuleni!
 
Sasa hao wasomi ndo watakunyoosha vizuri. Hao watakupa justifications zote za kutetea upigaji wao na hutawafanya kitu. Na hao wasomi ni wachache sana ambao wanaweza apply walichosomea darasani. Na unadhani kwa usomi wa Kigwangala alikuwa hajui kuwa kuna wasomi? Vijana wengi wasomi ni wapumbavu sana.. akiwa anaomba kazi kitu cha kwanza ni kuniuliza utanilipa Tsh ngapi bila kueleza ataifanyia nini kampuni....
Uko sahihi.
 
Nashukuru tupo katika mawazo sawa na wewe.
Katika maelezo yake kamtaja jamaa mmoja mfanyabiashara anaitwa la kairo, huyu bwana mdogo la kairo anamiliki kiwanda cha pipi na hotel. Anasema alijitolea range rover akampa dogo kulitumia baada ya harusi kwa miaka mitatu. Nafikiri angekaa chini afundishwe na la kairo biashara inavyoenda sio kwa sababu anajiona anapokea milioni 10 kwa mwezi za ubunge basi anaweza fanya biashara yoyote. Huyo anayemsema la kairo hatumi pesa zake ktk mpesa ili mtu amfanyie ni bega kwa bega
Yeah, uko sahihi.
 
Kigwa kama Kigwa alikosea sana kuleta Zogo na Tajiri angetulia zake kimya haya yote tusingeyasikia na alikua anaenda vizuri huko Utalii...
Kigwangala na wanasiasa wengine natamani sana tena sana niwafundishe namna ya kuongoza biashara na kuzisimamia, natamani sana wangejua namna ya kuwekeza mimi ni professor hilo eneo ila kwa sababu nipo mbali basi inasikitisha sana tena sana. Naamini kidogo kidogo watajifunza
 
Imani za dini zinatupumbaza mno watanzania. Mno. Wewe mtu anakutendea uovu huo, unamwacha. Ni dhambi kwa sababu unapomwacha hujamsaidia. Mhalifu ni mhalifu tuu, peleka kwenye vyombo vya sheria aadhibiwe, akirudi mpokee. Atakuwa GM mzuri kabisa maana amefundishwa huko maana ya kufanyakazi na uadilifu. Watanzania wengi wanadhani kumfunga mtu jela ni dhambi. Hamna. Gereza ni vyombo vya Mungu pia kuifanya dunia mahala pa amani. Ona sasa, mtu anafikia hatua ya kutaka kuteketeza mali za mamia ya mamilioni! Kweli? Huyo anakuua pia, tena mchana kweupee!
Nina mtoto alijifanya ameshindikana; Peleka shule, tena hizi za gharama, wapi! Geuza na kugeuza, wapi! Wananchi wakanishauri kuwa nisimlazimishe hataki shule, kwani wote lazima wasomee? Nikawaelewa. Nikampeleka kusomea udereva, nikampatia motokaa, akashirikiana na mafundi anaiba vipuri, gari mwisho wa siku likakaa juu ya mawe. Navumilia ila moyo unaniuma kwelikweli. Akakwiba kwa mtu akafungwa, Nikamtoa. Si unajua Bongo ukiwa na "kitu kidogo" hakuna jambo gumu. Nikamweka dukani, akapora. Aah, akili zikanirudi. Utu wangu ukanirudia. Utu wa ndani kabisa. Nikahisi kuwa na hatia kwa kuendelea kumdekeza wakati Serikali imeajiri vyombo vyenye vijana wasomi waliosomeshwa hadi shahada juu ya kurekebisha tabia za watu. Nikampeleka gerezani. Mapolisi, mahakimu, maafisa magereza walinipongeza sana, walisema, Bongo tungekuwa na wazazi kama wewe tungetengeneza kizazi cha vijana kilicho bora bora kabisa. Kijana alifundishwa adabu kule. Watu wamesomea mambo haya bwana. Tena alikaa miezi mitatu tu. Aliporudi sikuamini. Jambo la kwanza alitubu kwa machozi mengi Nimsamehe. Nilimsamehe. Ni mtoto, kama mzazi sikuwa namwadhibu ili ateseke bali a-reform. Baada ya hapo Akaokoka. Aliomba shamba, nikampatia na vitendeakazi vyote. To cut story short, sasa hivi ni kijana mzuri, mzuri mno na ndiyo tegemeo langu.
Mhe: Kigwangala, ulikosea kijana huyo ulitakiwa kumpeleka jela. Ange-reform na kuwa chombo chenye kufaa. Kwa kumwacha ataendeleza ujinga wake. Polisi, mahakama, na gereza, vipo kwa ajili ya watu kama hao, ukimwacha atakufa ktk dhambi zake na akifa anakwenda Jehanamu. Damu yake mwenyezi Mungu ataitaka mikononi mwako mhe. Kigwangala.
Over.
Nimesoma nikakuelewa sanaa sana mnooo
 
Ndio ukweli huo halisi nakuambia. Either uufuate ufanikiwe ama ubaki kulalamika.
Eg: crdb,nmb,tbl,tcc,nk kampuni hizo wanaofanya kazi ni vijana wazungu ama wajapani? No ni watanzania, ishu ni system hakuwa nayo. Kwa capital yake hakutakiwa kuwa mchuuzi. 100% blaming ni juu yake
Swali inakuwaje viongozi na kigwangwala sio wakwanza wanalalamikia utendaji wetu watanzania? Iweje mtandao umejaa malalamishi Kuhusu walimu, watendaji wa afya nk

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Swali inakuwaje viongozi na kigwangwala sio wakwanza wanalalamikia utendaji wetu watanzania? Iweje mtandao umejaa malalamishi Kuhusu walimu, watendaji wa afya nk

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Kwa hiyo mtu akiwa kiongozi mwanasiasa ndio msafi? Mbona bandari watu wameuza hiyo nayo ni usafi? Ni suala la muda tu kila kitu kitakuwa wazi kuhusu bandari
 
kusema imeuzwa nayo sio sahihi, kitu kilichouzwa kinaondoka na hakirudi, hii inamuelekeo wa kukodishwa kinacholalamikiwa masharti gandamizi
 
Sasa kwa mikataba hiyo unafikiri huyo kwenye ujasiriamali atatusua?
Amezoea rushwa,favour,kuogopwa. Muondolee hivyo vitu mpe mtaji wa milioni 100 ,nakuhakikishia baada ya mwaka ukija utamkuta anamlalamikia mwingine aliyemsababishia umasikini na hana huo mtaji umepotea
 
Ukiona mfanyabiashara ana kiwanda hiki, ana biashara ile, usifikiri na wewe ambae unaanza utaweza, kashatengeneza system ya biashara. Huyo jamaa muulize kwa nini alipoenda kukopa pikipiki 50 kwa mo akamkatalia. Pikipiki 50 ni sawa na milioni 100, kwa mo anaweza ingiza hata hiyo faida kwa siku kadhaa kwa nini hakumkopesha? Anajua principle ya biashara. Na ili ujue ana system kwa nini Kigwangala asingeongea na muuzaji ama msimamizi wa mo amkopeshe? Hawezi sababu tayari kuna system imewekwa kuendesha biashara
 
Kigwangala na wanasiasa wengine natamani sana tena sana niwafundishe namna ya kuongoza biashara na kuzisimamia, natamani sana wangejua namna ya kuwekeza mimi ni professor hilo eneo ila kwa sababu nipo mbali basi inasikitisha sana tena sana. Naamini kidogo kidogo watajifunza
Mkuu kama unataka watu watoke kwenye Umasikini na wewe ni mtaalamu wa Investment weka madini hapa yawasaidie wote kuwa mbali sio kigezo cha kukosa Elimu yako...
 
tunaposikia na kuona CAG anaainisha utepetevu, tunapolalamikia walimu, watendaji serikalini, huduma za afya na kote huko walioko ni watanzania , hatuoni kwamba uzawa sio uzalendo. Na kwa maana hiyo kuendelea kuaminishishwa kwamba kuweka watanzania kwenye nafasi zote kisa ni watanzania nacho ni sehemu ka kuendeleza uozo. Tumia mfano wa mitandao ya simu. Vodacom Tanzania ilianza kabla ya Safaricom ya Kenya. Iweje Safaricom faid yake inazidi ya vodaom mara mbili au zaidi. Ni swala la utendaji uliotukuka. Leo nna wiki 2 nimepeleka email voda na Tigo hamna jibu
 
Back
Top Bottom