Anayosema Kigwangalla kuhusu uaminifu wa Watanzania kuna tatizo?

Kila siku nawaambia,hii ni athari endelevu za ujamaa na hulka ya ubinafsi uliopitiliza wa Watanzania akiwemo yeye..

Jinsi ya kuondoa hii ni kuanzisha soma la maadili na liwe compulsory Hadi Chuo Kikuu..

Mtanzania ukikemea Uovu hadharani watu wanakushangaa na kukuchora na mwisho unaonekana ni mbaya.
 
Kigwangala ni bingwa wa fix

Juzi tu hapa kamtolea mtu mguu wa kuku kisa funguo za godown

Huyu si ndio alirusha vichura watu wazima?
 
Kigwa kama Kigwa alikosea sana kuleta Zogo na Tajiri angetulia zake kimya haya yote tusingeyasikia na alikua anaenda vizuri huko Utalii...
Ushuhuda huu wa Kigwa umenikumbusha fate yangu shambani huko.Ni kama unataka kufanana...baadaye nikawaza huu ni ujinga.Na invest hivi na kutengeneza ajira za watu ambao hawajitambui! Uza kila kitu hela weka kuliko secured zaidi..sasa hivi wamekaa vijiweni eti wanalalamika maisha magumu.Unawaangalia tu halafu unasema...hiii!ish!
Jamii tunayoishi kuna tatizo la uaminifu kwa walio wengi,hii tabia ikemewe kwa nguvu zote ni li kansa fulani halizungumzwi.
 
It is pathetic! Nakuelewa mno!! Try real estates labda
 

Dogo fala sana, kwa namna alivyoaminiwa na jamaa angekuwa tajiri mkubwa sana leo. Akaleta ukengeufu.

Ila nae kigwa alifeli sana kufanya recruitment ya mtu kumsaidia kusimamia shughuli za shamba. Uzoefu wake kama kiongozi haukuwa na tija kabisa.

Ila afahamu kuvunjika kwa mpini sio mwisho kulima. Mashamba yapo arejee tuendeleze kilimo.
 
Sindicate ovu la uliowaajiri likiwepo ni hatari.Umeona hapo kwa kigwa vitabu viko fresh,figure za store zina tally lkn mwisho kuficha uongo wanakuambia...tufanye mpango godown liungue..!!
 
Uko sahihi. Ni Mfumo wa siasa za "Nnji hii" ndio uliotutengeneza tukawa hivi tulivyo. Hali ni mbaya.
 
Tatizo linaanzia ngaz ya familia. Karibu watanzania wote huwa tunaandaliwa kuwa wapigaji kwa hoja kwamba tufanye kazi sehemu zenye marupurupu. Hata kama mtoto kazaliwa na hana roho ya upigaji atalazimishwa kuingia kwenye upigaji... sehemu kama BOT, TRA, Hazina hasa miaka ya nyuma zimekuwa zikilaumiwa mno kuingiza vilaza ambao ni ndugu au watu wa karibu wa vigogo ili tu kuendeleza upigaji. Mimi wakati namaliza chuo nilipenda sana kuwa mjasiriamali na baadae mfanyabiashara mkubwa ila vita na wazazi ilikuwa kubwa sana kutaka niingie kwenye ajira ya serikali kwa hoja kwamba ukiingia kwenye mfumo utazikuta hela humohumo. Bahati nzuri nilisimamia msimamo wangu.
 
Wabongo pia tunaponzwa na kufanya biashara "kienyeji" sana. Kigwangala inaonesha alikuwa ame-invest mamia ya mamilioni ya pesa, alitakiwa kuwa na mgt sahihi ya watu waliosomea Agroeconomics and marketing. Unamwajiri mtaalam kwa mkataba mzuri unaoeleweka (siyo kama huu wa pale "ferry).
Wabongo tunapenda vya rahisi; rahisi ni aghali ndugu. Unamweka mdogo wako au ndugu au rafiki yako bila mkataba hivyo anajua yeye yuko ktk kazi hiyo kwa "mkataba wa undugu"; sasa ndugu aki-misbehave Si anajua ni mali yake. Wabongo tubadilike. Tuache "ukabani".
 
Sasa hao wasomi ndo watakunyoosha vizuri. Hao watakupa justifications zote za kutetea upigaji wao na hutawafanya kitu. Na hao wasomi ni wachache sana ambao wanaweza apply walichosomea darasani. Na unadhani kwa usomi wa Kigwangala alikuwa hajui kuwa kuna wasomi? Vijana wengi wasomi ni wapumbavu sana.. akiwa anaomba kazi kitu cha kwanza ni kuniuliza utanilipa Tsh ngapi bila kueleza ataifanyia nini kampuni....
 
Kumbe ndivyo alivyo, ... Apigwe tuu!
 
Yeah, Bongo ukiwa Mtumishi Serikalini halafu ukajifanya mwadilifu, watu wanakudhihaki sana. Ukiwa "mpigaji" wa pesa na mali za umma unasifiwa kuwa mtu mwerevu sana.
 
Nashukuru tupo katika mawazo sawa na wewe.
Katika maelezo yake kamtaja jamaa mmoja mfanyabiashara anaitwa la kairo, huyu bwana mdogo la kairo anamiliki kiwanda cha pipi na hotel. Anasema alijitolea range rover akampa dogo kulitumia baada ya harusi kwa miaka mitatu. Nafikiri angekaa chini afundishwe na la kairo biashara inavyoenda sio kwa sababu anajiona anapokea milioni 10 kwa mwezi za ubunge basi anaweza fanya biashara yoyote. Huyo anayemsema la kairo hatumi pesa zake ktk mpesa ili mtu amfanyie ni bega kwa bega
 
Wewe ni maskini sana wa akili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…