Ancestral Curse: Ujerumani iliwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6, lakini ndio nchi yenye nguvu zaidi Ulaya. Je, hii dhana ya laana ya asili ipo sahihi?

Ancestral Curse: Ujerumani iliwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6, lakini ndio nchi yenye nguvu zaidi Ulaya. Je, hii dhana ya laana ya asili ipo sahihi?

Hitler aliteketeza roho za watu achana na suala la Uyahudi kwanza. Kwanini hawa jamaa hawatafunwi na laana badala yake wanazidi kuneemeka?...
Kama hoja yako haitokani na porojo za ukiifanyia ubaya Israel unalaaniwa, suala lako la kwamba kuua roho za watu kunaleta laana umelitoa wapi?!

Kama hoja yako haitokani na porojo za Israel ni Taifa Teule, kwanini hukumtaja Stalin ambae anaaminika kuwa ndie ameua rohho nyingi zaidi pengine kuliko hata huyo Hitler?! Kwanini isiwe Wajapan ambao na wenyewe waliua mamilioni ya roho?! Kwanini wasiwe Wachina, hususani kipindi cha Mao ambao waliua mamilioni ya Wachina wenzao?
 
Pili, kwamba wayahudi ni binadanu bora zaidi au mungu aliwapendelea hiyo ni kulingana na nyakati za kipindi hicho na namna jinsi mungu alivyokuwa anashughulika na matatizo ya binadamu more (direct) kuliko sasa hivi.
Mkuu, ni wapi nimezungumzia kuwa Wayahudi ni bora zaidi ya wanadamu wengine?...
 
Mkuu, ni wapi nimezungumzia kuwa Wayahudi ni bora zaidi ya wanadamu wengine?...
Mkuu umetoa hoja kwa kutumia wayahudi na mimi nimejibu hoja kutumia wayahudi kama mfano.( sababu tayari kuna utaratibu wa kuwachukulia wayahudi kama wateule wa mungu nadhani ndio sababu hata wewe ukaja nahoja kama hii ukiwatumia wayahudi kama mfano)
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Ndugu zangu watanzania;

Kwanini Ujerumani ndio nchi yenye nguvu zaidi Ulaya (European Powerhouse) licha ya ukweli kwamba iliwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6? Je, hii dhana ya laana ya vizazi (Ancestral/Generational Curse) ipo sahihi kweli? Kama ipo sahihi, kwanini iwepo Afrika tu na sio Ulaya?

Laana ya Asili kama inavyofafanulia na Mtumishi Joel Osteen (American Preacher & Televangelist)
=============
Laana ya vizazi inaaminika kutithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa sababu ya uasi dhidi ya Mungu. Ikiwa ukoo wako umepewa laana ya talaka, uchumba, umaskini, hasira au mifumo mingine isiyo ya kimungu, unaweza kuwa chini ya laana ya ukoo.

Familia zetu zina ushawishi mkubwa juu ya maendeleo yetu, pamoja na ukuzaji wa mifumo yetu ya dhambi. Watu wengine wanadai kwamba laana za kifamilia au kizazi hupitishwa kwa njia ya kizazi.

Imani hii inatokana na vifungu vya Agano la Kale ambavyo vinasema kwamba Mungu "huwaadhibu watoto na watoto wao kwa dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne" (Kutoka 34: 7).

Ikiwa familia zinarithi laana za kiroho au la, ni dhahiri kwamba mifumo ya dhambi hupitishwa kupitia familia. Kila mtu hutenda dhambi; lakini kama vile utamaduni, kabila, na jinsia zinavyoongoza mwelekeo wetu wa dhambi katika mwelekeo fulani, ndivyo pia familia zetu.

Tunarithi tabia nyingi na mapenzi ya kitu fulani kutoka kwa wazazi wetu ambao sio ushawishi mzuri kwetu au kwa wengine. Tunapopata tabia ya imani au imani ambayo inaathiri vibaya maisha yetu au wale wanaotuzunguka, hii inajulikana kama laana ya kizazi. Ni upande uliojificha wa tabia uliopitishwa kupitia vizazi.

HISTORIA NDOGO YA MAUAJI YA WAYAHUDI BARANI ULAYA (HOLOCAUST)
==========
Holocaust, yalikuwa ni mauaji ya halaiki ya Vita vya pili vya dunia kwa Wayahudi wa Ulaya. Kati ya mwaka 1941 na mwaka 1945, Ulaya nzima ambayo ilikuwa inakaliwa na Wajerumani, Ujerumani ya wa Nazi na washirika wake waliwaua Wayahudi wapatao milioni sita, karibu theluthi mbili ya idadi ya Wayahudi wote wa ulaya kwa wakati ule.

Mauaji hayo yalifanywa kwa watu wengi kwa njia za upigaji wa risasi kwa halaiki ya watu;sera ya mauaji ya kutokomeza watu kupitia kazi katika kambi za mateso; na katika vyumba vya gesi na gari za gesi katika kambi za kuangamiza za Wajerumani, haswa Auschwitz, Belzec, Chelmno, Majdanek, Sobibór, na Treblinka katika Poland iliyokaliwa na Wajerumani.

UCHUMI WA UJERUMANI KWA UFUPI
=============
Pamoja na Pato la Taifa la zaidi ya Euro trilioni 3.4, uchumi wa Ujerumani ulikuwa mkubwa zaidi barani Ulaya mnamo mwaka 2019. Chumi zenye ukubwa sawa za Uingereza na Ufaransa zilikuwa chumi za pili na wa tatu kwa ukubwa barani Ulaya wakati wa mwaka jana, ikifuatiwa na Italia na Uhispania.

Uchumi mdogo kabisa katika takwimu hii ni ule wa taifa dogo la Balkan la Montenegro, ambalo lilikuwa na Pato la Taifa la Euro bilioni 4.66 tu, karibu mara 74 ndogo kuliko uchumi wa Ujerumani.

Uchumi wa Ujerumani umekuwa ndio uchumi mkubwa zaidi barani Ulaya tangu mmwaka 1980, hata kabla ya kuungana tena kwa Ujerumani Magharibi na Mashariki. Uingereza, kwa kulinganisha, imekuwa na bahati wakati huo huo na ilikuwa na uchumi mdogo kuliko Italia mwishoni mwa miaka ya 1980.

Uingereza pia ilipata mapigo makubwa zaidi ya chumi zingine kubwa wakati wa anguko la uchumi wa mwishoni mwa miaka ya 2000, ikimaanisha uchumi wa Ufaransa ulikuwa wa pili kwa ukubwa barani kwa muda baadaye. Uchumi wa Uhispania ulikuwa wa tano kwa ukubwa Ulaya katika kipindi hiki cha miaka 38, na kutoka 2004 kuendelea umekuwa na thamani ya zaidi ya Euro trilioni moja.

Tazama takwimu kutoka chanzo sahihi hapo chini.

View attachment 1559175

Kwanini Ujerumani haijawahi kutafunwa na laana hii ya asili licha ya kuwaua Wayahudi zaidi ya Milioni 6 badala yake inazidi kuneemeka kiuchumi na kisiasa?

Kwanini wahandisi wazuri sana duniani (Magari, Mitambo) wanapatikana nchini Ujerumani? Siri yao ni ipi hasa?

Je, dhana hii ya laana ya asili ipo sahihi kweli?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Majority ya wazungu Ulaya hawaamini ktk dini. Hivyo hizo dhana za taifa teule na stori za laana kwa atakayeliadhibu hilo taifa hawazizingatii...tuendelee kuamini hivyo sisi waafrika.

Hujatenda haki kutumia data za GDP ulizoziweka za nchi mbalimbali ktk kujenga hoja ya nguvu kati ya nchi mbali mbali ulizoelezea. Hii ni kwa kuwa umelinganisha GDP za nchi zenye watu lukuki (mfano Germany ina watu zaidi ya 83 milioni) na nchi nyingine ambazo zina watu kiduchu (mfano Norway ina watu takriban 5 milioni) . GDP per capita ndiyo itaakisi zaidi uchumi wa nchi hizo na kuzi-rank nchi hizo pasi na uonevu wowote. Kwa Data hizi, Germany ni ya 12.
SmartSelect_20200905-121335_Gallery.jpg
 
Majority ya wazungu Ulaya hawaamini ktk dini. Hivyo hizo dhana za taifa teule na stori za laana kwa atakayeliadhibu hilo taifa hawazizingatii...tuendelee kuamini hivyo sisi waafrika.
Mkuu, siwazungumzii Wayahudi kama taifa teule la Mungu bali ninazungumzia roho za binadamu wa asili ya Uyahudi. I am taking humanity and not ethnicity...
 
Mkuu umetoa hoja kwa kutumia wayahudi na mimi nimejibu hoja kutumia wayahudi
Mkuu, suala ni humanity na sio ethnicity. Hata kama wangekuwa ni wajaluo, wahaya ama wamakonde waliuawa na Hitler huko Ulaya, bado ningehoji juu ya suala la Ujerumani kutokutafunwa na hii inayoitwa laana ya asili...
 
Hii ni kwa kuwa umelinganisha GDP za nchi zenye watu lukuki (mfano Germany ina watu zaidi ya 83 milioni) na nchi nyingine ambazo zina watu kiduchu (mfano Norway ina watu takriban 5 milioni) .
Mkuu, hiyo Norway ina ushawishi gani katika siasa za Ulaya na Dunia? Norway iliwahi kutawala nchi ngapi hapa duniani ukilinganisha na Ujerumani?...
 
Kuna baadhi ya watu na nchi nyingine duniani humu wanasema holocaust is a hoax. Kwamba hakuna Wayahudi milioni 6 waliouliwa. Hizo figure ni siasa zenye makusudio maalum na dunia inaaminishwa hivyo kwa sababu za kifisadi
 
Achana na hizo mambo mkuu....Hakuna kitu inaitwa Karma...bt survival of the fittest do exist...ndo mana unajiuliza hayo maswali.
 
Hitler aliteketeza roho za watu achana na suala la Uyahudi kwanza. Kwanini hawa jamaa hawatafunwi na laana badala yake wanazidi kuneemeka?...
Huchukua muda kidogo kwa mfano dola ya kirumi ilikuwa ndio yenye nguvu ikitawala dunia lakini baada ya askari wake wa kirumi kumuua Yesu dola ya kirumi ilisambaratika na sasa Italia ni kiinchi kidogi tu cha hovyo

Pili kuna mjerumani mtu wa Mungu Martini Luther aliyeanzisha imani ya kiprotestanti duniani kazi yake yaweza kuwa sababu ya ujerumani kutopigwa na laana hadi sasa
Ulutheri imo pote duniani
 
Back
Top Bottom