Anga la Ukraine Yumkini mikononi mwa NATO

Anga la Ukraine Yumkini mikononi mwa NATO

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Umeshudiwa ugeni mzito nzito Kyiv Ukraine, katika kipindi hiki cha mgogoro.

Rais wa umoja wa Ulaya amefika Kyiv. Mawaziri wakuu toka Czech, Slovenia, Poland na juzi UK nao wamefika pale wakajivinjari kwa raha zao.

Aungurumapo Simba mcheza nani?

Haitakuwa ajabu kusikia Marine Moja imetimba pale na wanaume wakivinjari mitaani Kyiv kama kwao.

Beberu hajawahi kufanya ajizi na usalama wake kama tulivyo sisi magwiji wa nyungu. Popote aendako yeye si habari mpya kumsikia akichukua jukumu lote la ulinzi likiwamo la anga ugenini.

Ilikuwa hivyo na Obama Dar es salaam. Ilikuwa nusu hivyo na Ghadafi ugenini.

IMG_20220412_162026_759.jpg


Aupate wapi utulivu wa kuhutubia mabunge duniani Zelensky, kwenye hatari ya mvua ya makombora asiyokuwa na udhibiti nayo?

Yumkini ndicho kilichomfurusha Mrusi hadi aliko sasa.

Kukiitwa, "kukiona cha mtema kuni!"
 
Mbona ziara ya Johnson haikutangazwa mapema kabla hajafika huko! Wanakwenda kwa kuvizia kama wachawi.
Gagnija ndugu yangu ukweli ni kwamba hata kwenda kwa kuvizia bado ni kujiamini kwani hizi kambi mbili i.e. Urusi vs West zinafanyiana ushushu wa kiwango wa juu sana na hata kwenda kwa kuvizia inaweza ku-leak kabla hajaenda. Unadhani Urusi hana watu wake ndani ya eg USA, UK nk? Wapo wengi tena wengine ni kwenye sehemu nyeti sana hivyo wanaweza kutoa siri kama hata ziara haikutangazwa. Unajua hivi vita Ukraine wanapewa tafu kubwa sana na nina uhakika wako mashushushu wengi wa special forces za nchi za Magharibi wako vitani wakisaidia kwa utaalam wao.
 
Umeshudiwa ugeni mzito nzito Kyiv Ukraine, katika kipindi hiki cha mgogoro.

Rais wa umoja wa Ulaya amefika Kyiv. Mawaziri wakuu toka Czech, Slovenia, Poland na juzi UK nao wamefika pale wakajivinjari kwa raha zao.

Aungurumapo Simba mcheza nani?

Haitakuwa ajabu kusikia Marine Moja imetimba pale na wanaume wakivinjari mitaani Kyiv kama kwao.

Beberu hajawahi kufanya ajizi na usalama wake kama tulivyo sisi magwiji wa nyungu. Popote aendako yeye si habari mpya kumsikia akichukua jukumu lote la ulinzi likiwamo la anga ugenini.

Ilikuwa hivyo na Obama Dar es salaam. Ilikuwa nusu hivyo na Ghadafi ugenini.

View attachment 2185031

Aupate wapi utulivu wa kuhutubia mabunge duniani Zelensky, kwenye hatari ya mvua ya makombora asiyokuwa na udhibiti nayo?

Yumkini ndicho kilichomfurusha Mrusi hadi aliko sasa.

Kukiitwa, "kukiona cha mtema kuni!"
Mbona Mrusi alishatangaza kujitoa Kyiv na kwenda Mashariki?
 
Duuhh ndio uchambuzi Huu, au umeandika kama Stori za kiniweni.

Hujiulizi kwann Ziara zao zinafanyika Kwa usiri mkubwa???


Na usichokijua, Hao Ulaya wenyewe pamoja na kutumia usiri .

Bado wanatoa taarifa Kwa urusi kupitia mpango wa Pili, ili urusi kwakutokujia, isije kufanya mashambulizi yakagharim Uhai wa viongozi hao.
 
Nato ni waoga sana, wataishia kutuma javelin na mercenaries tu ila kamwe hawatoingia kwenye direct war na Russia. Kaangalie mji wa mariupol je waingereza na warusi watakubali London na Moscow ziwe vile???? Kamwe hawatakubali... sehemu ya kupiganiwa itakua Ukraine, syria na kwingine. Lazima uzijue siasa za dunia kaka.
 
Back
Top Bottom