Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Leo Stive atatupia kimya kimya bila taarifa, Nakaa kalibu nae leo.
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 48*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Akapiga simu. Iliita. Haikupokelewa. Akaendelea kunywa zake kinywaji. Baada ya punde chache, akasikia hodi mlangoni. Akasimama upesi na kuendea mlango.

Alipofungua alikutana na sura ngeni. Zaidi akakutana na mdomo wa bunduki.

ENDELEA

Macho yakamtoka pima. Asiseme kitu akaamriwa,

“get on your seat!"

Basi akajongea kwenye kiti chake na kuketi. Uso umejawa na hofu na macho yamejawa na maulizo.

Mwanaume huyu aliyemnyooshea bunduki hakuonyesha kama ana utani. Alikuwa amekuja hapa kwa ajili ya kutenda kazi tu.

Alikuwa ni mzungu.

Alikuwa ndani ya suti.

Alikuwa ni bwana Brown!

“you can't kill me you Asian bastard!" Bwana Brown alibweka. “you are so fucking young to me. You are jus' nothing, nobody to me!" Bwana Brown aliwaka. Macho yake yalikuwa makali na mdomo wake anaupindisha.

Ila bwana huyu hakuonekana mzima. Hakuwa mzima. Upande wake wa kushoto ulikuwa unavuja damu iliyochuruzika mpaka kidevuni. Jicho lake la upande huohuo lilikuwa jekundu.

Suti yake ilikuwa chafu. Na hata shati lake jeupe lilikuwa lina mabaki ya damu ya moto kabisa. Na ungemtazama vema mkono wake wa kuume huu uliobebela bunduki, nao ulikuwa unachuruza damu. Kwa chini matone yalikuwa yanadondoka dondoka.

Na hata huu mwendo wake haukuwa wa yule bwana Brown tumjuaye.

“now who's laughing at last, you bitch!" Bwana Brown alisema aking'ata meno. “I ask you, who's laughing now??" Akapaza sauti akifoka.

Bwana Sheng alikuwa kimya akimtazama. Bila shaka bwana huyu alikuwa ana jambo analifikiri kichwani. Alitakiwa kuwa mwangalifu mno hapa maana bwana Brown alikuwa ameweka kidole chake kwenye kifyatuo cha risasi.

Akihema tu, risasi inapasua kichwa ama kifua chake na kumpeleka jehanamu mara moja!

“All over England know me!" Bwana Brown aliendelea kunguruma. Chumba kizima alikuwa anasikika yeye tu. Ungejiuliza je wale walinzi wa bwana Sheng wanaojaa eneo hilo, wako wapi muda huo!

“I am an abandoned rock. But look! Here I am still standing. I am on top of the hill and nobody can fall me down!"

Bwana Brown aliposema hayo, akafuta pua yake kwa mgongo wa kiganja cha mkono wa kushoto kisha akatoa neno lake la mwisho.

“now I am done talking. Send my wishes to hell!" Akafyatua risasi!

Click!

Click! Click! Hakuna kitu! Akaitazama bunduki ... Click!

Haraka Sheng akajitupa na kufyatua miguu yake kupiga mkono wa bwana Brown wenye bunduki na kisha katika upesi akamkita na teke la kifua lililomwangusha Bwana Brown chini!
Kisha akacheka.
“who's laughing now?" Akauliza kwa kebehi. Bwana Brown akajikusanya na kunyanyuka. Akajipanga kupambana.
Ila asingeweza. Alikuwa amechoka. Alikuwa hajiwezi. Alikuwa ana majeraha.


Alijaribu kutupa shambulio la ngumi, ila kwa Sheng akaona mchekechea. Akamlamba bwana huyo mateke mawili tu, akadondoka chini akiwa mfu!

Ni baada ya punde tu maiti ya bwana Brown ikaanza kumwaga damu kuchafua sakafu.

“send my wishes to hell," bwana Sheng alinung'una akiwa amebinua mdomo kisha akaendea jokofu lake na kutoa kinywaji. Akakiminia kwenye glasi na kuketi kitini.

Haki alikuwa ana haja ya kusherehekea kwa maana aliponea chupuchupu haswaa kutolewa roho. Alijipongeza kwa mafundo manne ya kinywaji kisha akashusha pumzi ndefu na kuegesha kichwa kitini.

Akawaza kama angelikuwa ameuawa. Hakuna mtu aliyekuja kichwani mwake isipokuwa mkewe na mtoto wake. Aliwaza sana vipi kama leo ingekuwa ndiyo mwisho wa pumzi yake?

Akaona kuna haja ya kuwasiliana na mkewe na mwanae ambao wote wapo China, Beijing. Ila asingeweza kuwapigia simu muda huo. Na ubaya ni kwamba asingeweza hata kuacha ujumbe wakapelekewa kwani familia yake hii ilikuwa ni ya siri.

Hakuna mfanyakazi wake yeyote aliyekuwa anayeijua kwani ilikuwa ni mwiko haswa! Viongozi wote wa juu wa familia hii ya Wu hawakutakiwa kuwa na familia kabisa. Na yote haya ni sababu ya kutotoa mwanya wa udhaifu.

Endapo kiongozi akiwa na familia, maadui watapata fursa ya kumkamata kwa urahisi wakitumia mke na watoto kama chambo.

Ngo! Ngo! Ngo!

“Mkuu!" Sauti ilisikika mlangoni na kumtoa Sheng kwenye kawimbi ka mawazo kalichokuwa kamemchukua. Hakuitikia, alingoja asikie tena sauti hiyo na alipohakikisha anaifahamu, akaendea mlango na kuufungua.

Alikuwa ni kijakazi wake

“Upo salama, mkuu?"

“Ulikuwa wapi mpaka maadui wanafika kwenye makazi yangu??" Sheng akafoka.

“mkuu umesahau kuwa uliniagiza?"

“vipi wenzako wamesharudi?"

“hapana, bado hawajarudi."

“umefanya nao mawasiliano yoyote?"

“hapana! Sijawatafuta tangu walipoondoka. Kwani hawajakupigia?"

“hapana. Hawajanipigia."

Sheng akaangaza macho yake huku na kule, hakuona watu. Alistaajabu akauliza walinzi wako wapi. Yule bwana aliyemjia akamwambia wengi wao wameuawa. Maiti zao zinazagaa huko mazingirani.

Ina maana Bwana Brown ndiye aliyewamaliza hao wote?

“kuna maiti mbili pia za wazungu!" Akaeleza kijakazi yule akionyeshea uelekeo. Basi akiongozana na bwana Sheng, wakaenda huko.

***

Asubuhi ya saa mbili ... Kwa mbali redio ya simu inanguruma ...

“ulifanikiwa?" Akauliza Sarah akimtazama mumewe. “maana hata hukunambia namna mambo yalivyoenda."

“yah!" Akasema Kinoo kisha akadaka kikombe cha chai na kunywa fundo moja. “nilifanikiwa. Niliwapata nikawapasha habari."

“sasa?"

“nasikilizia. Walinambia watan'tafuta wakithibitisha kama habari hizo ni za kweli."

“watathibitishaje sasa?"

“si wataenda kumkamata huko! Huoni redio ipo on hapa nataka nisikie kila kitu."

Sarah akaguna.

“vipi kama wakimkamata alafu wasikupe hiyo pesa?"

“hawawezi bana."

“unajuaje? Wakikuzunguka na kwenda zao?"

“Sarah, unaweza ukaniacha nikanywa chai basi?"

“chai gani? - Hii ya rangi? Si tujadili vya maana lakini Kinoo?"

“ningoje basi nimalize! Kwani nachukua mwaka hapa!"

Kabla Sarah hajatia neno, mara sauti ikasikika redioni kutangaza habari zilizowasili hivi punde. Wote wakajikuta wananyamaza kusikiliza kwa umakini.

“maiti sita za wanaume pamoja na bunduki nne zimekutwa kandokando ya mto Msimbazi na kusababisha taharuki kwa wakazi wa karibu na maeneo hayo. Mpaka sasa maiti hizo hazijatambulika, na uchunguzi unaendelea."

Habari ikakata. Kinoo akatazamana na Sarah.

“wanaweza wakawa wakina Miranda au?" Kinoo aliuliza kana kwamba kuna mtu mwenye majibu. Haraka akanyakua simu yake na kupiga, ikaita mara mbili na kupokelewa na sauti ya kike.

“halo Miranda! ... Vipi? Unaendeleaje? ... Safi, upo salama? ... Kabisa? ... Umesikia hiyo habari ya watu waliokutwa mtoni? ... Poa, sawa!"

Alipokata simu akanyanyuka na kuacha chai.

“wapi sasa? Umejua ni wakina nani?" Sarah aliuliza. Kinoo hakujibu, akazama chumbani na baada ya dakika moja akatoka akiwa amebadili nguo ya juu, amevalia kibodi cheusi.

“baadae!" Akamuaga mkewe. “tutaongea vizuri baadae!"

Alikuwa kwenye haraka haswa.

***

Majira ya jioni ya saa moja ...

Habari hii ya maiti mtoni ikiwa imesambaa na kukamata jiji na nchi zima, Sarah aliipata mwanya wa kuifaidi kwa kupitia mitandao ya kijamii ambayo haikuwa nyuma kabisa kwa mfululizo wa picha na vimaelezo vya hapa na pale.

Alipekua kila picha aliyoiona mtandaoni na akasoma kila neno lililoandikwa. Kila mtu akaeleza yake na kusimulia katika namna yake, ila kwa upande wa Sarah bado hakupata alichokuwa anahitaji.

Japo alipekuwa picha zile zote, hakuona sura ya Jona. Hii ikampa maswali kidogo, ina maana Jona atakuwa hajakamatwa na polisi? Na wale watu waliouawa, watakuwa wanahusika naye kwa namna yoyote ile?

Akiwa mawazoni, mlango unagongwa. Anaacha simu na kwenda anamkuta mwanaue aliyevalia helmet akiwa amebebelea mfuko mweusi.

“mzigo wako nimetumwa kukuletea."

Sarah alipoupokea, mwanaume huyo hakukaa, akaenda zake. Sarah akaketi kitini na kufungua mzigo huo.

***
 
Kwo kinoo kashachinjwa au ni dada ake sara(shasha) wameshutukiwa na hkina miranda.....!!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…