SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #461
*ANGA LA WASHENZI --- 20*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mbele ya macho yake, Bigo akalegeza kichwa, akakata pumzi.
Muda mfupi mbele, bado Jona akiwa ameduwaa, ulimi ukatoka mdomoni mwa Bigo na kudondokea chini!
Bigo alikuwa ameunyofoa ulimi wake kwa kutumia meno!
ENDELEA
“Shit!” Jona akaalaani. Alishika kiuno akitafakari. Hakutaka kumuua Bigo ila bado tu msala ulimwangukia. Sasa hakuwa na namna nyingine zaidi ya kwenda kumzika, tena wakati huo huo wa usiku isije ikaleta nongwa.
Aliubeba mwili wa Bigo mpaka uani kisha akachimba shimo na kuuzika. Zoezi hilo lilimchukua nusu saa kulimaliza. Alikuwa ametepeta jasho, akaenda kuoga kabla hajatulia sebuleni kutafakari.
Bigo ameshaenda sasa nini anafanya? Akapata wazo la kufuatilia yale maneno ya kichina ‘pumzi ya mwisho’. Alihisi pengine inaweza kuwa ishara ikamsaidia kugundua vitu vingine muhimu na vikubwa.
Akaunganisha tarakilishi yake na mtandao toka kwenye simu kisha akaanza kuwandawanda mtandaoni. Aliandika maneno yale ya kichina na maana yake kwa kiingereza alafu akaanza kusaka majibu.
Baada ya punde majibu kadhaa yakaja. Akaanza kuyapitia moja baada ya moja.
Taarifa zilikuwa finyu. Na taarifa nyingi katika hizo finyu hazikuwa zile anazozitaka. Lakini asitoke mtupu akakutana na taarifa moja, tena iliyojifichaficha huko mwishoni mwishoni.
Taarifa hii ilikuja kabla ya kidogo hajaghairi. Ilikuwa inawahusu watu wawili huko Shanghai – China waliouawa na polisi.
Jona akapitia taarifa ya tukio hilo ambalo lilitukia mnamo mwaka 2002. Akaja kugundua watu hao wawili walikuwa wametumwa kummaliza mfanyabiashara mmoja wa vipuri ambaye kwa bahati yake alitoa taarifa mapema kwa polisi.
Mfanyabiashara huyo aliwaambia polisi alitumiwa ujumbe mfupi kwenye simu yake: ‘Pumzi ya mwisho’ siku moja kabla hajavamiwa. Hakuuelewa ujumbe huo ila kwa usalama wake maana ana maadui wengi kibiashara akatoa taarifa polisi.
Hapo sasa Jona akajua kumbe ‘Pumzi ya mwisho’ ni kitu ambacho kipo ulimwenguni na si tu Tanzania pekee, ni mtandao mpana, lakini pia ni kitu cha muda mrefu. Na tageti yake kwa kiasi kikubwa ikiwa ni watu wakubwa, haswa wafanyabiashara.
Wauaji hao wa ‘pumzi ya mwisho’ waliuawa na polisi kwenye majibizano ya risasi hivyo haikupatikana taarifa yoyote toka kwao. Haikujulikana nani aliyewatuma na ni kwa malengo gani.
Jona aliamua kutafuta jina la mfanyabiashara huyo aliyenusurika kifo, akapata taarifa aliuawa baada ya juma moja tu tangu aliposalimika. Aliuawa kwa risasi na watu wasiojulikana waliotumia gari lililokuwa kwenye mwendokasi.
Kumbe alikuja kutafutwa na kuuawa! Jona akatahamaki. Alitafuta na kutafuta lakini hakupata kingine zaidi ya hicho.
Hili likamaanisha kwa Jona kwamba wauaji hawa wa ‘Pumzi ya mwisho’ walifanikiwa kutekeleza mauaji yao mengine pasipo kujulikana. Ishu ya mfanyabiashara huyu wa vipuri ilikuwa ndiyo pekee ambayo iliwaweka uchi, angalau ikaacha nyayo juu ya mchanga.
Lakini wapo nyuma ya nani? Nani anawatuma na kwa ajili ya malengo gani? Hayo bado yalimsumbua.
Aliona njia pekee ya kupata majibu ni kwa kutumia udadisi wake kwenye hili jambo la Fakiri. Huo ndiyo moshi pekee ambao unaweza kumwonyesha moto upo wapi.
Akadhamiria kukutana na mjane wa Fakiri, na kama akifanikiwa basi atapata ngazi ya kumpeleka hatua nyingine.
Akazima tarakilishi yake na kwenda kuchomoa chupa ya kileo toka kwenye jokofu. Akaenda nayo mpaka kitandani alipoketi na kunywa taratibu kilevi hicho huku akitafakari na huku akingoja kileo kimkate fikira alale.
Baada ya kama robo saa, chupa ikawa kando wakati yeye akiwa tayari ameshajigeuzia upande mwingine.
***
Majira ya saa kumi na moja na dakika kumi na nane asubuhi, Afrikana: Mbezi beach, Dar es salaam.
“Chai ipo tayari,” alisema mwanamke mmoja mnene mweusi aliyekuwa amevalia gauni la kulalia. Makadirio ya umri wake miaka thelathini na mapema hivi. Alikuwa anamwambia mwanaume mwenye umbo la saizi ya kati, maji ya kunde, akiwa anatengenezea suruali yake akijitazama kwenye kioo.
Kwa makadirio pia, umri wake haukuwa mbali sana na wa mwanamke, ambaye kwa wazi alikuwa mkewe.
“Ahsante, umeshawaamsha watoto?” mwanaume akauliza.
“Yah! Wanajiandaa saa hizi, si unajua shool bus lao linavyowahi.” mwanamke akajibu kisha akaenda kitandani alipoketi na kuendelea kumtazama mwanaume ambaye hakukaa muda mrefu sana kabla hajatoka ndani ya chumba kwenda sebuleni kupata kifungua kinywa.
Zoezi hilo likamchukua dakika nane tu, akarejea tena chumbani kuchukua mkoba wake na kumuaga mkewe.
“Usisahau kuja na kile kitu, sawa?” mwanamke alisema akimtazama mume machoni. Mume akatabasamu.
“Nitaomba unikumbushe kwa ujumbe majira ya jioni.”
“Sawa,” mwanamke akaitikia kisha akambusu mumewe kumuaga. Mwanaume akatoka ndani mpaka kwenye gari, Suzuki – vitara nyeupe, akatupia begi lake viti vya nyuma na kuwasha gari.
Ila kabla hajasogeza chombo kwenda popote pale, ghafla akajikuta akibanwa pumzi na kitambaa. Alipapatika kwa muda mchache mno kabla hajalegea akilaza kichwa chake akiachama mdomo wazi.
Anatoka mwanamke ndani ya gari akiwa amevalia suti nyeusi, suruali ya kitambaa na koti, mkono wake wa kuume umeshikilia pochi nyeusi. Alikuwa amevalia wigi kubwa jeusi lililokuwa linaficha uso wake.
Alifuata uzio akaukwea na kujimwagia nje ya nyumba. Alipitia pale ambapo nyaya ya umeme zilikuwa zimekatwa.
Haikujulikana aliingiaje kwenye gari na kufanikisha zoezi lake, hiyo kazi sasa wakaachiwa polisi wahangaike nayo.
Mwanamke huyo aliposonga mbali na nyumba aliyofanya tukio, akatoa simu ndani ya pochi na kutuma ujumbe:
‘Tayari kazi imeisha.’
Alipoona taarifa kwamba ujumbe umefika, akarejesha simu ndani ya pochi. Akapotea akiacha msiba nyuma.
***
Majira ya saa kumi na nusu jioni, ndani ya nyumba ya mheshimiwa Eliakimu.
“Naona umekuja on time!” alisema Eliakimu kwa tabasamu akipeana mkono na Miranda.
“Si unajua ukiitwa na mheshimiwa lazima uzingatie muda,” alisema Miranda akirudisha tabasamu kwa Eliakimu.
“Nyie ndo’ waheshimiwa wenyewe bwana, sio sisi! – karibu sana.”
“Ahsante, nimeshakaribia.”
Alikuja mfanyakazi wa ndani akapewa oda ya kuleta vinywaji laini. Maongezi yakaendelea baina ya Miranda na Mheshimiwa.
“Nimekuita hapa kwa ajili ya ule mpango wetu, nataka nikupatie mrejesho wa hatua ambayo imefikia sasa.”
“Ndio, Mheshimiwa.”
“Kila kitu kipo sawa, mambo yameenda kama ambavyo nilitaka yaende japo kuna kamushkeli kadogo kalijiri ila nimeshakasuluhisha. Nimeshaongea na kuwapanga wahusika. Sasa kinachohitajika ili tumalize hii hatua yetu ni pesa.”
Mfanyakazi akakatisha kidogo maongezi yao kwa ujio wake wa kuleta vinywaji – sharubati ya embe. Kila mtu akateka glasi yake moja toka kwenye trei, mfanyakazi akaenda zake, maongezi yakaendelea:
“Hii pesa ambayo inahitajika hapa si yangu, la hasha. Ni ya kufanikisha tukio kwa kuwapatia mgao hawa vibaraka wadogowadogo angalau ili wafunge midomo yao. Kama unavyojua sisi ni waelekezaji na wasimamiaji ila utendaji upo mikononi mwao.”
“Ndio, mheshimiwa.”
“Sasa nawasikiliza ninyi. Hili jambo la malipo yao mtalikamilisha muda gani?”
Miranda akanywa kwanza kinywaji fundo moja, kisha akauliza:
“Ni kiasi gani, Mheshimiwa?”
“Aaaah mama, kwani haufahamu? Kiasi ni kile kile cha siku zote. Kwani tulishawahi kubadili?”
“Sawa, Mheshimiwa. Lakini siwezi kukupa majibu ya moja kwa moja pasipo kuonana na mkuu wangu kwanza. Inabidi nimfikishie hizi taarifa.”
“Unajua kabla sijakutafuta wewe, nilimtafuta kwanza yeye maana najua yeye ndiye mhusika wa mambo ya fedha. Na nilifanya hivyo kwa siku mbili kabla sijakutafuta wewe. Hakuwa anapokea simu zangu wala kujibu meseji zangu. Sijajua nini shida.”
“Pengine anakuwa ametingwa tu.”
“Kiasi cha kutoweza hata kurejesha ujumbe mfupi? Na ilhali anajua kabisa kuna jambo nyeti lipo mbele yetu?”
Miranda akakosa cha kusema.
“Au mna mpango mwingine wa ziada?” Mheshimiwa akauliza akimtazama Miranda machoni. Miranda akahisi msisimko fulani mwilini.
Swali hili lilifanya sharubati aliyokunywa igome kupita kooni. Alijitahidi kukaza macho yake yasizalishe shaka, akatikisa kichwa.
“Hapana, Mheshimiwa, usiwe na mawazo hayo. Hatuna mpango wowote ule. Hili jambo la mawasiliano si kwako tu, hata kwangu pia. Kwa muda kidogo sijawasiliana na mkuu. Hapatikani kwenye simu yake … ndiyo maana nikasema pengine amebanwa na kazi.”
“Sasa anabanwa na kazi gani kama hizi zake hazifanyi? … Anyway, hili jambo ni la haraka. Kumbukeni huu ni mpango haramu hautakiwi kuvuta muda otherwise utabumburuka.”
“Nimekuelewa mheshimiwa. Nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu kufanikisha hili.”
“Kama kuna tatizo mnaweza mkanishirikisha. It’s ok.”
“Sawa.”
Miranda alishindwa hata kumaliza sharubati yake. Akaweka glasi chini na kuaga.
“Mbona mapema hivyo?”
“Kuna mahali natakiwa kupitia, Mheshimiwa.”
Hakutaka kubakia zaidi hapo. Aliona kadiri anavyokaa hapo basi muda si mwingi anaweza akashtukiwa.
Alipopanda gari na kutoka ndani ya jengo la Mheshimiwa akampigia simu BC na kumpasha habari aliyokumbana nayo. BC akamtaka waonane kesho yake kwani amebanwa na kazi kwa muda huo.
***
Baadae kwenye vyombo vya habari na mitandaoni taarifa ya mauaji ya afisa wa serikali ajulikanaye kwa jina Maxwell Ndoja ikasambaa na kutawala.
Picha za afisa huyo akiwa kwenye gari lake ambalo bado lilikuwa linachemsha injini, ndizo zikawa mjadala huku na huko watu wakishangazwa kwa namna tukio hilo lilivyofanyika kwa ustadi.
Msemaji wa jeshi la polisi alisema tukio hilo lilifanyika majira ya asubuhi ya mapema ambapo mlinzi aliziraishwa na muuaji kabla hajafanikiwa kumnusisha sumu afisa huyo.
Mke wa marehemu ndiye aliyetoa taarifa polisi ya kumkuta mumewe amekufa ndani ya gari baada ya kwenda kumtazama kutokana na kupata mashaka kuliona gari kwenye majira ya saa moja ilhali mumewe aliaga kuondoka muda mrefu nyuma.
Hakuna uharibifu wowote uliotokea zaidi ya ukataji wa nyaya za umeme na hakuna mtuhumiwa yoyote aliyekamatwa. Upelelezi unaendelea.
***
Usikose sehemu ijayo.
*Simulizi za series*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mbele ya macho yake, Bigo akalegeza kichwa, akakata pumzi.
Muda mfupi mbele, bado Jona akiwa ameduwaa, ulimi ukatoka mdomoni mwa Bigo na kudondokea chini!
Bigo alikuwa ameunyofoa ulimi wake kwa kutumia meno!
ENDELEA
“Shit!” Jona akaalaani. Alishika kiuno akitafakari. Hakutaka kumuua Bigo ila bado tu msala ulimwangukia. Sasa hakuwa na namna nyingine zaidi ya kwenda kumzika, tena wakati huo huo wa usiku isije ikaleta nongwa.
Aliubeba mwili wa Bigo mpaka uani kisha akachimba shimo na kuuzika. Zoezi hilo lilimchukua nusu saa kulimaliza. Alikuwa ametepeta jasho, akaenda kuoga kabla hajatulia sebuleni kutafakari.
Bigo ameshaenda sasa nini anafanya? Akapata wazo la kufuatilia yale maneno ya kichina ‘pumzi ya mwisho’. Alihisi pengine inaweza kuwa ishara ikamsaidia kugundua vitu vingine muhimu na vikubwa.
Akaunganisha tarakilishi yake na mtandao toka kwenye simu kisha akaanza kuwandawanda mtandaoni. Aliandika maneno yale ya kichina na maana yake kwa kiingereza alafu akaanza kusaka majibu.
Baada ya punde majibu kadhaa yakaja. Akaanza kuyapitia moja baada ya moja.
Taarifa zilikuwa finyu. Na taarifa nyingi katika hizo finyu hazikuwa zile anazozitaka. Lakini asitoke mtupu akakutana na taarifa moja, tena iliyojifichaficha huko mwishoni mwishoni.
Taarifa hii ilikuja kabla ya kidogo hajaghairi. Ilikuwa inawahusu watu wawili huko Shanghai – China waliouawa na polisi.
Jona akapitia taarifa ya tukio hilo ambalo lilitukia mnamo mwaka 2002. Akaja kugundua watu hao wawili walikuwa wametumwa kummaliza mfanyabiashara mmoja wa vipuri ambaye kwa bahati yake alitoa taarifa mapema kwa polisi.
Mfanyabiashara huyo aliwaambia polisi alitumiwa ujumbe mfupi kwenye simu yake: ‘Pumzi ya mwisho’ siku moja kabla hajavamiwa. Hakuuelewa ujumbe huo ila kwa usalama wake maana ana maadui wengi kibiashara akatoa taarifa polisi.
Hapo sasa Jona akajua kumbe ‘Pumzi ya mwisho’ ni kitu ambacho kipo ulimwenguni na si tu Tanzania pekee, ni mtandao mpana, lakini pia ni kitu cha muda mrefu. Na tageti yake kwa kiasi kikubwa ikiwa ni watu wakubwa, haswa wafanyabiashara.
Wauaji hao wa ‘pumzi ya mwisho’ waliuawa na polisi kwenye majibizano ya risasi hivyo haikupatikana taarifa yoyote toka kwao. Haikujulikana nani aliyewatuma na ni kwa malengo gani.
Jona aliamua kutafuta jina la mfanyabiashara huyo aliyenusurika kifo, akapata taarifa aliuawa baada ya juma moja tu tangu aliposalimika. Aliuawa kwa risasi na watu wasiojulikana waliotumia gari lililokuwa kwenye mwendokasi.
Kumbe alikuja kutafutwa na kuuawa! Jona akatahamaki. Alitafuta na kutafuta lakini hakupata kingine zaidi ya hicho.
Hili likamaanisha kwa Jona kwamba wauaji hawa wa ‘Pumzi ya mwisho’ walifanikiwa kutekeleza mauaji yao mengine pasipo kujulikana. Ishu ya mfanyabiashara huyu wa vipuri ilikuwa ndiyo pekee ambayo iliwaweka uchi, angalau ikaacha nyayo juu ya mchanga.
Lakini wapo nyuma ya nani? Nani anawatuma na kwa ajili ya malengo gani? Hayo bado yalimsumbua.
Aliona njia pekee ya kupata majibu ni kwa kutumia udadisi wake kwenye hili jambo la Fakiri. Huo ndiyo moshi pekee ambao unaweza kumwonyesha moto upo wapi.
Akadhamiria kukutana na mjane wa Fakiri, na kama akifanikiwa basi atapata ngazi ya kumpeleka hatua nyingine.
Akazima tarakilishi yake na kwenda kuchomoa chupa ya kileo toka kwenye jokofu. Akaenda nayo mpaka kitandani alipoketi na kunywa taratibu kilevi hicho huku akitafakari na huku akingoja kileo kimkate fikira alale.
Baada ya kama robo saa, chupa ikawa kando wakati yeye akiwa tayari ameshajigeuzia upande mwingine.
***
Majira ya saa kumi na moja na dakika kumi na nane asubuhi, Afrikana: Mbezi beach, Dar es salaam.
“Chai ipo tayari,” alisema mwanamke mmoja mnene mweusi aliyekuwa amevalia gauni la kulalia. Makadirio ya umri wake miaka thelathini na mapema hivi. Alikuwa anamwambia mwanaume mwenye umbo la saizi ya kati, maji ya kunde, akiwa anatengenezea suruali yake akijitazama kwenye kioo.
Kwa makadirio pia, umri wake haukuwa mbali sana na wa mwanamke, ambaye kwa wazi alikuwa mkewe.
“Ahsante, umeshawaamsha watoto?” mwanaume akauliza.
“Yah! Wanajiandaa saa hizi, si unajua shool bus lao linavyowahi.” mwanamke akajibu kisha akaenda kitandani alipoketi na kuendelea kumtazama mwanaume ambaye hakukaa muda mrefu sana kabla hajatoka ndani ya chumba kwenda sebuleni kupata kifungua kinywa.
Zoezi hilo likamchukua dakika nane tu, akarejea tena chumbani kuchukua mkoba wake na kumuaga mkewe.
“Usisahau kuja na kile kitu, sawa?” mwanamke alisema akimtazama mume machoni. Mume akatabasamu.
“Nitaomba unikumbushe kwa ujumbe majira ya jioni.”
“Sawa,” mwanamke akaitikia kisha akambusu mumewe kumuaga. Mwanaume akatoka ndani mpaka kwenye gari, Suzuki – vitara nyeupe, akatupia begi lake viti vya nyuma na kuwasha gari.
Ila kabla hajasogeza chombo kwenda popote pale, ghafla akajikuta akibanwa pumzi na kitambaa. Alipapatika kwa muda mchache mno kabla hajalegea akilaza kichwa chake akiachama mdomo wazi.
Anatoka mwanamke ndani ya gari akiwa amevalia suti nyeusi, suruali ya kitambaa na koti, mkono wake wa kuume umeshikilia pochi nyeusi. Alikuwa amevalia wigi kubwa jeusi lililokuwa linaficha uso wake.
Alifuata uzio akaukwea na kujimwagia nje ya nyumba. Alipitia pale ambapo nyaya ya umeme zilikuwa zimekatwa.
Haikujulikana aliingiaje kwenye gari na kufanikisha zoezi lake, hiyo kazi sasa wakaachiwa polisi wahangaike nayo.
Mwanamke huyo aliposonga mbali na nyumba aliyofanya tukio, akatoa simu ndani ya pochi na kutuma ujumbe:
‘Tayari kazi imeisha.’
Alipoona taarifa kwamba ujumbe umefika, akarejesha simu ndani ya pochi. Akapotea akiacha msiba nyuma.
***
Majira ya saa kumi na nusu jioni, ndani ya nyumba ya mheshimiwa Eliakimu.
“Naona umekuja on time!” alisema Eliakimu kwa tabasamu akipeana mkono na Miranda.
“Si unajua ukiitwa na mheshimiwa lazima uzingatie muda,” alisema Miranda akirudisha tabasamu kwa Eliakimu.
“Nyie ndo’ waheshimiwa wenyewe bwana, sio sisi! – karibu sana.”
“Ahsante, nimeshakaribia.”
Alikuja mfanyakazi wa ndani akapewa oda ya kuleta vinywaji laini. Maongezi yakaendelea baina ya Miranda na Mheshimiwa.
“Nimekuita hapa kwa ajili ya ule mpango wetu, nataka nikupatie mrejesho wa hatua ambayo imefikia sasa.”
“Ndio, Mheshimiwa.”
“Kila kitu kipo sawa, mambo yameenda kama ambavyo nilitaka yaende japo kuna kamushkeli kadogo kalijiri ila nimeshakasuluhisha. Nimeshaongea na kuwapanga wahusika. Sasa kinachohitajika ili tumalize hii hatua yetu ni pesa.”
Mfanyakazi akakatisha kidogo maongezi yao kwa ujio wake wa kuleta vinywaji – sharubati ya embe. Kila mtu akateka glasi yake moja toka kwenye trei, mfanyakazi akaenda zake, maongezi yakaendelea:
“Hii pesa ambayo inahitajika hapa si yangu, la hasha. Ni ya kufanikisha tukio kwa kuwapatia mgao hawa vibaraka wadogowadogo angalau ili wafunge midomo yao. Kama unavyojua sisi ni waelekezaji na wasimamiaji ila utendaji upo mikononi mwao.”
“Ndio, mheshimiwa.”
“Sasa nawasikiliza ninyi. Hili jambo la malipo yao mtalikamilisha muda gani?”
Miranda akanywa kwanza kinywaji fundo moja, kisha akauliza:
“Ni kiasi gani, Mheshimiwa?”
“Aaaah mama, kwani haufahamu? Kiasi ni kile kile cha siku zote. Kwani tulishawahi kubadili?”
“Sawa, Mheshimiwa. Lakini siwezi kukupa majibu ya moja kwa moja pasipo kuonana na mkuu wangu kwanza. Inabidi nimfikishie hizi taarifa.”
“Unajua kabla sijakutafuta wewe, nilimtafuta kwanza yeye maana najua yeye ndiye mhusika wa mambo ya fedha. Na nilifanya hivyo kwa siku mbili kabla sijakutafuta wewe. Hakuwa anapokea simu zangu wala kujibu meseji zangu. Sijajua nini shida.”
“Pengine anakuwa ametingwa tu.”
“Kiasi cha kutoweza hata kurejesha ujumbe mfupi? Na ilhali anajua kabisa kuna jambo nyeti lipo mbele yetu?”
Miranda akakosa cha kusema.
“Au mna mpango mwingine wa ziada?” Mheshimiwa akauliza akimtazama Miranda machoni. Miranda akahisi msisimko fulani mwilini.
Swali hili lilifanya sharubati aliyokunywa igome kupita kooni. Alijitahidi kukaza macho yake yasizalishe shaka, akatikisa kichwa.
“Hapana, Mheshimiwa, usiwe na mawazo hayo. Hatuna mpango wowote ule. Hili jambo la mawasiliano si kwako tu, hata kwangu pia. Kwa muda kidogo sijawasiliana na mkuu. Hapatikani kwenye simu yake … ndiyo maana nikasema pengine amebanwa na kazi.”
“Sasa anabanwa na kazi gani kama hizi zake hazifanyi? … Anyway, hili jambo ni la haraka. Kumbukeni huu ni mpango haramu hautakiwi kuvuta muda otherwise utabumburuka.”
“Nimekuelewa mheshimiwa. Nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu kufanikisha hili.”
“Kama kuna tatizo mnaweza mkanishirikisha. It’s ok.”
“Sawa.”
Miranda alishindwa hata kumaliza sharubati yake. Akaweka glasi chini na kuaga.
“Mbona mapema hivyo?”
“Kuna mahali natakiwa kupitia, Mheshimiwa.”
Hakutaka kubakia zaidi hapo. Aliona kadiri anavyokaa hapo basi muda si mwingi anaweza akashtukiwa.
Alipopanda gari na kutoka ndani ya jengo la Mheshimiwa akampigia simu BC na kumpasha habari aliyokumbana nayo. BC akamtaka waonane kesho yake kwani amebanwa na kazi kwa muda huo.
***
Baadae kwenye vyombo vya habari na mitandaoni taarifa ya mauaji ya afisa wa serikali ajulikanaye kwa jina Maxwell Ndoja ikasambaa na kutawala.
Picha za afisa huyo akiwa kwenye gari lake ambalo bado lilikuwa linachemsha injini, ndizo zikawa mjadala huku na huko watu wakishangazwa kwa namna tukio hilo lilivyofanyika kwa ustadi.
Msemaji wa jeshi la polisi alisema tukio hilo lilifanyika majira ya asubuhi ya mapema ambapo mlinzi aliziraishwa na muuaji kabla hajafanikiwa kumnusisha sumu afisa huyo.
Mke wa marehemu ndiye aliyetoa taarifa polisi ya kumkuta mumewe amekufa ndani ya gari baada ya kwenda kumtazama kutokana na kupata mashaka kuliona gari kwenye majira ya saa moja ilhali mumewe aliaga kuondoka muda mrefu nyuma.
Hakuna uharibifu wowote uliotokea zaidi ya ukataji wa nyaya za umeme na hakuna mtuhumiwa yoyote aliyekamatwa. Upelelezi unaendelea.
***
Usikose sehemu ijayo.
*Simulizi za series*