Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI --- 20*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Mbele ya macho yake, Bigo akalegeza kichwa, akakata pumzi.

Muda mfupi mbele, bado Jona akiwa ameduwaa, ulimi ukatoka mdomoni mwa Bigo na kudondokea chini!

Bigo alikuwa ameunyofoa ulimi wake kwa kutumia meno!

ENDELEA

“Shit!” Jona akaalaani. Alishika kiuno akitafakari. Hakutaka kumuua Bigo ila bado tu msala ulimwangukia. Sasa hakuwa na namna nyingine zaidi ya kwenda kumzika, tena wakati huo huo wa usiku isije ikaleta nongwa.

Aliubeba mwili wa Bigo mpaka uani kisha akachimba shimo na kuuzika. Zoezi hilo lilimchukua nusu saa kulimaliza. Alikuwa ametepeta jasho, akaenda kuoga kabla hajatulia sebuleni kutafakari.

Bigo ameshaenda sasa nini anafanya? Akapata wazo la kufuatilia yale maneno ya kichina ‘pumzi ya mwisho’. Alihisi pengine inaweza kuwa ishara ikamsaidia kugundua vitu vingine muhimu na vikubwa.

Akaunganisha tarakilishi yake na mtandao toka kwenye simu kisha akaanza kuwandawanda mtandaoni. Aliandika maneno yale ya kichina na maana yake kwa kiingereza alafu akaanza kusaka majibu.

Baada ya punde majibu kadhaa yakaja. Akaanza kuyapitia moja baada ya moja.

Taarifa zilikuwa finyu. Na taarifa nyingi katika hizo finyu hazikuwa zile anazozitaka. Lakini asitoke mtupu akakutana na taarifa moja, tena iliyojifichaficha huko mwishoni mwishoni.

Taarifa hii ilikuja kabla ya kidogo hajaghairi. Ilikuwa inawahusu watu wawili huko Shanghai – China waliouawa na polisi.

Jona akapitia taarifa ya tukio hilo ambalo lilitukia mnamo mwaka 2002. Akaja kugundua watu hao wawili walikuwa wametumwa kummaliza mfanyabiashara mmoja wa vipuri ambaye kwa bahati yake alitoa taarifa mapema kwa polisi.

Mfanyabiashara huyo aliwaambia polisi alitumiwa ujumbe mfupi kwenye simu yake: ‘Pumzi ya mwisho’ siku moja kabla hajavamiwa. Hakuuelewa ujumbe huo ila kwa usalama wake maana ana maadui wengi kibiashara akatoa taarifa polisi.

Hapo sasa Jona akajua kumbe ‘Pumzi ya mwisho’ ni kitu ambacho kipo ulimwenguni na si tu Tanzania pekee, ni mtandao mpana, lakini pia ni kitu cha muda mrefu. Na tageti yake kwa kiasi kikubwa ikiwa ni watu wakubwa, haswa wafanyabiashara.

Wauaji hao wa ‘pumzi ya mwisho’ waliuawa na polisi kwenye majibizano ya risasi hivyo haikupatikana taarifa yoyote toka kwao. Haikujulikana nani aliyewatuma na ni kwa malengo gani.

Jona aliamua kutafuta jina la mfanyabiashara huyo aliyenusurika kifo, akapata taarifa aliuawa baada ya juma moja tu tangu aliposalimika. Aliuawa kwa risasi na watu wasiojulikana waliotumia gari lililokuwa kwenye mwendokasi.

Kumbe alikuja kutafutwa na kuuawa! Jona akatahamaki. Alitafuta na kutafuta lakini hakupata kingine zaidi ya hicho.

Hili likamaanisha kwa Jona kwamba wauaji hawa wa ‘Pumzi ya mwisho’ walifanikiwa kutekeleza mauaji yao mengine pasipo kujulikana. Ishu ya mfanyabiashara huyu wa vipuri ilikuwa ndiyo pekee ambayo iliwaweka uchi, angalau ikaacha nyayo juu ya mchanga.

Lakini wapo nyuma ya nani? Nani anawatuma na kwa ajili ya malengo gani? Hayo bado yalimsumbua.

Aliona njia pekee ya kupata majibu ni kwa kutumia udadisi wake kwenye hili jambo la Fakiri. Huo ndiyo moshi pekee ambao unaweza kumwonyesha moto upo wapi.

Akadhamiria kukutana na mjane wa Fakiri, na kama akifanikiwa basi atapata ngazi ya kumpeleka hatua nyingine.

Akazima tarakilishi yake na kwenda kuchomoa chupa ya kileo toka kwenye jokofu. Akaenda nayo mpaka kitandani alipoketi na kunywa taratibu kilevi hicho huku akitafakari na huku akingoja kileo kimkate fikira alale.

Baada ya kama robo saa, chupa ikawa kando wakati yeye akiwa tayari ameshajigeuzia upande mwingine.


***


Majira ya saa kumi na moja na dakika kumi na nane asubuhi, Afrikana: Mbezi beach, Dar es salaam.


“Chai ipo tayari,” alisema mwanamke mmoja mnene mweusi aliyekuwa amevalia gauni la kulalia. Makadirio ya umri wake miaka thelathini na mapema hivi. Alikuwa anamwambia mwanaume mwenye umbo la saizi ya kati, maji ya kunde, akiwa anatengenezea suruali yake akijitazama kwenye kioo.

Kwa makadirio pia, umri wake haukuwa mbali sana na wa mwanamke, ambaye kwa wazi alikuwa mkewe.

“Ahsante, umeshawaamsha watoto?” mwanaume akauliza.

“Yah! Wanajiandaa saa hizi, si unajua shool bus lao linavyowahi.” mwanamke akajibu kisha akaenda kitandani alipoketi na kuendelea kumtazama mwanaume ambaye hakukaa muda mrefu sana kabla hajatoka ndani ya chumba kwenda sebuleni kupata kifungua kinywa.

Zoezi hilo likamchukua dakika nane tu, akarejea tena chumbani kuchukua mkoba wake na kumuaga mkewe.

“Usisahau kuja na kile kitu, sawa?” mwanamke alisema akimtazama mume machoni. Mume akatabasamu.

“Nitaomba unikumbushe kwa ujumbe majira ya jioni.”

“Sawa,” mwanamke akaitikia kisha akambusu mumewe kumuaga. Mwanaume akatoka ndani mpaka kwenye gari, Suzuki – vitara nyeupe, akatupia begi lake viti vya nyuma na kuwasha gari.

Ila kabla hajasogeza chombo kwenda popote pale, ghafla akajikuta akibanwa pumzi na kitambaa. Alipapatika kwa muda mchache mno kabla hajalegea akilaza kichwa chake akiachama mdomo wazi.

Anatoka mwanamke ndani ya gari akiwa amevalia suti nyeusi, suruali ya kitambaa na koti, mkono wake wa kuume umeshikilia pochi nyeusi. Alikuwa amevalia wigi kubwa jeusi lililokuwa linaficha uso wake.

Alifuata uzio akaukwea na kujimwagia nje ya nyumba. Alipitia pale ambapo nyaya ya umeme zilikuwa zimekatwa.

Haikujulikana aliingiaje kwenye gari na kufanikisha zoezi lake, hiyo kazi sasa wakaachiwa polisi wahangaike nayo.

Mwanamke huyo aliposonga mbali na nyumba aliyofanya tukio, akatoa simu ndani ya pochi na kutuma ujumbe:

‘Tayari kazi imeisha.’

Alipoona taarifa kwamba ujumbe umefika, akarejesha simu ndani ya pochi. Akapotea akiacha msiba nyuma.


***


Majira ya saa kumi na nusu jioni, ndani ya nyumba ya mheshimiwa Eliakimu.


“Naona umekuja on time!” alisema Eliakimu kwa tabasamu akipeana mkono na Miranda.

“Si unajua ukiitwa na mheshimiwa lazima uzingatie muda,” alisema Miranda akirudisha tabasamu kwa Eliakimu.

“Nyie ndo’ waheshimiwa wenyewe bwana, sio sisi! – karibu sana.”

“Ahsante, nimeshakaribia.”

Alikuja mfanyakazi wa ndani akapewa oda ya kuleta vinywaji laini. Maongezi yakaendelea baina ya Miranda na Mheshimiwa.

“Nimekuita hapa kwa ajili ya ule mpango wetu, nataka nikupatie mrejesho wa hatua ambayo imefikia sasa.”

“Ndio, Mheshimiwa.”

“Kila kitu kipo sawa, mambo yameenda kama ambavyo nilitaka yaende japo kuna kamushkeli kadogo kalijiri ila nimeshakasuluhisha. Nimeshaongea na kuwapanga wahusika. Sasa kinachohitajika ili tumalize hii hatua yetu ni pesa.”

Mfanyakazi akakatisha kidogo maongezi yao kwa ujio wake wa kuleta vinywaji – sharubati ya embe. Kila mtu akateka glasi yake moja toka kwenye trei, mfanyakazi akaenda zake, maongezi yakaendelea:

“Hii pesa ambayo inahitajika hapa si yangu, la hasha. Ni ya kufanikisha tukio kwa kuwapatia mgao hawa vibaraka wadogowadogo angalau ili wafunge midomo yao. Kama unavyojua sisi ni waelekezaji na wasimamiaji ila utendaji upo mikononi mwao.”

“Ndio, mheshimiwa.”

“Sasa nawasikiliza ninyi. Hili jambo la malipo yao mtalikamilisha muda gani?”

Miranda akanywa kwanza kinywaji fundo moja, kisha akauliza:

“Ni kiasi gani, Mheshimiwa?”

“Aaaah mama, kwani haufahamu? Kiasi ni kile kile cha siku zote. Kwani tulishawahi kubadili?”

“Sawa, Mheshimiwa. Lakini siwezi kukupa majibu ya moja kwa moja pasipo kuonana na mkuu wangu kwanza. Inabidi nimfikishie hizi taarifa.”

“Unajua kabla sijakutafuta wewe, nilimtafuta kwanza yeye maana najua yeye ndiye mhusika wa mambo ya fedha. Na nilifanya hivyo kwa siku mbili kabla sijakutafuta wewe. Hakuwa anapokea simu zangu wala kujibu meseji zangu. Sijajua nini shida.”

“Pengine anakuwa ametingwa tu.”

“Kiasi cha kutoweza hata kurejesha ujumbe mfupi? Na ilhali anajua kabisa kuna jambo nyeti lipo mbele yetu?”

Miranda akakosa cha kusema.

“Au mna mpango mwingine wa ziada?” Mheshimiwa akauliza akimtazama Miranda machoni. Miranda akahisi msisimko fulani mwilini.

Swali hili lilifanya sharubati aliyokunywa igome kupita kooni. Alijitahidi kukaza macho yake yasizalishe shaka, akatikisa kichwa.

“Hapana, Mheshimiwa, usiwe na mawazo hayo. Hatuna mpango wowote ule. Hili jambo la mawasiliano si kwako tu, hata kwangu pia. Kwa muda kidogo sijawasiliana na mkuu. Hapatikani kwenye simu yake … ndiyo maana nikasema pengine amebanwa na kazi.”

“Sasa anabanwa na kazi gani kama hizi zake hazifanyi? … Anyway, hili jambo ni la haraka. Kumbukeni huu ni mpango haramu hautakiwi kuvuta muda otherwise utabumburuka.”

“Nimekuelewa mheshimiwa. Nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu kufanikisha hili.”

“Kama kuna tatizo mnaweza mkanishirikisha. It’s ok.”

“Sawa.”

Miranda alishindwa hata kumaliza sharubati yake. Akaweka glasi chini na kuaga.

“Mbona mapema hivyo?”

“Kuna mahali natakiwa kupitia, Mheshimiwa.”

Hakutaka kubakia zaidi hapo. Aliona kadiri anavyokaa hapo basi muda si mwingi anaweza akashtukiwa.

Alipopanda gari na kutoka ndani ya jengo la Mheshimiwa akampigia simu BC na kumpasha habari aliyokumbana nayo. BC akamtaka waonane kesho yake kwani amebanwa na kazi kwa muda huo.


***


Baadae kwenye vyombo vya habari na mitandaoni taarifa ya mauaji ya afisa wa serikali ajulikanaye kwa jina Maxwell Ndoja ikasambaa na kutawala.

Picha za afisa huyo akiwa kwenye gari lake ambalo bado lilikuwa linachemsha injini, ndizo zikawa mjadala huku na huko watu wakishangazwa kwa namna tukio hilo lilivyofanyika kwa ustadi.

Msemaji wa jeshi la polisi alisema tukio hilo lilifanyika majira ya asubuhi ya mapema ambapo mlinzi aliziraishwa na muuaji kabla hajafanikiwa kumnusisha sumu afisa huyo.

Mke wa marehemu ndiye aliyetoa taarifa polisi ya kumkuta mumewe amekufa ndani ya gari baada ya kwenda kumtazama kutokana na kupata mashaka kuliona gari kwenye majira ya saa moja ilhali mumewe aliaga kuondoka muda mrefu nyuma.

Hakuna uharibifu wowote uliotokea zaidi ya ukataji wa nyaya za umeme na hakuna mtuhumiwa yoyote aliyekamatwa. Upelelezi unaendelea.

***


Usikose sehemu ijayo.


*Simulizi za series*
 
*ANGA LA WASHENZI --- 21*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Mke wa marehemu ndiye aliyetoa taarifa polisi ya kumkuta mumewe amekufa ndani ya gari baada ya kwenda kumtazama kutokana na kupata mashaka kuliona gari kwenye majira ya saa moja ilhali mumewe aliaga kuondoka muda mrefu nyuma.

Hakuna uharibifu wowote uliotokea zaidi ya ukataji wa nyaya za umeme na hakuna mtuhumiwa yoyote aliyekamatwa. Upelelezi unaendelea.

ENDELEA

Nade na bwana Eliakimu wakatazama habari hiyo kwa tabasamu. Kazi si kwamba ilikuwa imeisha bali pia ilikuwa imetendwa vema.

Lengo la kutazama habari hiyo ilikuwa ni kuthibitisha kama tendo limefanikiwa, yani Max amekufa, na hakuna ushahidi wowote ulioachwa nyuma.

Hivyo vyote kwa pamoja vilikuwa vimepatikana. Bwana Eliakimu akampongeza Nade kwa kazi nzuri.

"Hujawahi kuniangusha, Nade. Inabidi nikupe zawadi nzuri, kubwa!" Alisema kwa tabasamu.

"Nimefanya tu kazi yangu, wala usijali mkuu," Nade akasema akitabasamu kwa haya.

"Ndio ni kazi yako, ila umeitenda vema. Anayetenda mema siku zote hupongezwa."

"Ahsante mkuu. "

"Unataka zawadi gani nikupatie?"

"Yoyote tu mkuu unayoona nastahili."

Eliakimu akajikuna kidevu akitabasamu.

"Sawa, najua nitakupatia zawadi gani. Nipe muda kidogo wa kuitafakari."

Nade akatikisa kichwa kuafiki. Eliakimu akaendeleza maongezi:

"Vipi alikupatia mushkeli kwenye tendo?"

"Hapana. Hakuweza kufurukuta hata kidogo."

"Kabisa?"

"Ndio. Alipovuta hewa mara moja tu basi habari yake ikaishia hapo hapo."

"Aisee! Hizi dawa zina nguvu eenh?"

"Sana! Zinaonekana ni kali mno. Ile glovu niliyovaa kwa ajili ya tukio nimeitazama hivi punde nimeikuta imekatikakatika na kulainika kama bubble gum!"

"Serious?"

"Ndio, mkuu."

"Unajua haya ndiyo madawa yanayosafirishwa kuingizwa nchini na wakina Miranda?"

"Yah ulinambia."

"Nilifanya tu kuchomoa chupa moja kwa ajili ya kaudadisi changu, nikagundua ni sumu ila sikuwa makini kwenye kuchambua madhara yake.

Kama ni makubwa hivi, hili jambo linatisha, ni hatari. Itabidi tufuatilie kwa karibu namna mwili wa Max utakavyokuwa baada ya kuingiza sumu hii mwilini."

"Kwenda hospitali?"

"Hapana, mbona kuhangaika hivyo? Nitaenda tu msibani kutoa pole. Bila shaka mke wake ataeleza yote nayotaka kuyafahamu."

Nade akatikisa kichwa kuafiki.

"Huenda tukaja tumia pia sumu hizi kummaliza yule mtu wetu baada ya kumaliza kazi," Mheshimiwa akapendekeza na kuongezea:

"Siku tutakayokata mzizi huo wa fitna, nitafurahi sana na roho yangu itakaa kwa amani. Hilo ndilo jambo pekee lililobakia likininyima usingizi."

"Usijali, mkuu. Nalo litaisha," Nade akasema kwa kujiamini.

"Siku litakapoisha, nitahakikisha, kwa uwezo wangu wote, nakutafutia zawadi ambayo hautaisahau maishani mwako daima! Umesikia?"

"Nimesikia, mkuu."

"Haya nenda kapumzike sasa kesho uendelee na kazi."


**


Saa mbili asubuhi maeneo ya Masaki, Dar es salaam.

"Karibu!" Sauti ya kiume ilifoka tokea ndani ya uzio, punde geti likafunguliwa na kichwa kikachomoza kutazama nje.

Alikuwa mwanaume mweusi mwenye nywele ndogo pilipili. Amevalia koti kubwa rangi ya bluu na suruali ya kitambaa miguuni akiwa peku.

Alivyotazama nje akakutana na Jona aliyekuwa amevalia shati jeupe la drafti, suruali ya kitambaa na mokasi nyeusi.

"Naweza nikakusaidia?"

"Ndio, bila shaka hapa ni kwa marehemu Fakiri."


Mwanaume getini akatikisa kichwa kukubali.

"Mimi ni afisa polisi," Jona akaonyeshea kitambulisho chake bandia. "Nimekuja hapa kuonana na mwenye nyumba."


"Kuna tatizo gani afande?" Mwanaume getini akauliza upesi. Macho yake yalibeba hofu.

"Hamna tatizo," Jona akamshusha presha.
"Ni kwamba nahitaji tu kufanya naye maongezi."

"Kuhusu marehemu au kuna jipya?"

Jona hakujibu, akamkazia macho mwanaume huyo.

"Karibu, unaweza ukaingia tu."

Jona akazama ndani mpaka sebuleni. Mke wa marehemu Fakiri akaitwa kuja kuungana naye.

Alikuwa mwanamke mnene mfupi maji ya kunde. Alivalia dera la njano lenye maua mekundu mekundu.

Macho yake yalikuwa madogo, mashavu makubwa na kidevu kisichoonekana.

Alimkarimu Jona kwa sauti nyembamba ya chini.

"Unatumia kinywaji gani?"

"Hapana, mama, nashukuru wala usijichoshe. Nipo sawa."

"Hata chai?"

"Hapana,mama. Basi naomba unipatie maji ya kunywa kama hutojali."

Mama akamwita mwanaume yule aliyempokea Jona, Sabi kwa jina, akamwagiza alete maji ya kunywa.

Jona akajitambulisha na kueleza dhamira yake. Alikuwa hapo kwa lengo la kufufua kesi ya bwana Fakiri iliyopotelea hewani.

"Kuna taarifa chache nazihitaji toka kwako," akasema Jona. "Naomba ushirikiano wako kamilifu."

"Usijali, lakini sina taarifa yoyote mpya. Zote nilishatoa kwenu polisi."


"Utaniambia tu hizo hizo ambazo ulizitoa. Kama nilivyosema hapo awali, tunaifufua hii kesi."

"Karibu."

Mama huyu hakuonekana mtu mwenye matumaini. Si bure alichoshwa na mahojiano ya aina hiyo, hakuona jipya ama la maana.

Alikuwa anatimiza tu wajibu.

"Kuna adui yoyote wa kibiashara unayemhisi pengine anahusika na mauaji ya mumeo?"

"Hapana."

"Hamna yeyote?"

"Ndio."

"Wewe unahisi kwanini mumeo aliuawa?"

"Sijui. Siku zote ukiwa na mafanikio, maadui hawakosekani."

"Mama, nipo hapa kwa ajili ya kusaidia. Najua umechoshwa na mahojiano ya aina hii na pengine waona yanakupotezea muda.

Tafadhali, naomba unipe ushirikiano wako. Nakuahidi utaona matunda ya hichi utakachokifanya," Jona alisema kwa kujiamini akimtazama Mama machoni.

Muda mfupi macho ya mama yakawa mekundu.

"Nimeongea na kuongea sana, nimelia na kusaga meno lakini hakuna aliyejali. Alipotokea mtu wa kujali, naye hakuishi wakammaliza!"

Mama akajipangusa machozi kwa vidole vyake.

"Pole mama, najua inaumiza. Nitafanya kadiri ya uwezo wangu kuwaleta wahusika wote mbele ya haki."

Mama akawa kimya kwa muda kidogo. Ni kama vile alikuwa anavuta kumbukumbu, ila iliyokuwa inamchoma, uso wake ulijieleza kwa ndita za majonzi.

"Nakumbuka kabla mume wangu hajafa, alikuwa ananiambia kila usiku maisha yake yapo mashakani. Nilimuuliza kwanini haendi polisi, akawa ananijibu haitosaidia.

Sikumwelewa anamaanisha nini mpaka pale alipokuja kufariki. Ile kauli yake ya haitosaidia kweli nikaanza kuishuhudia."

"Alikuwa anakwambia nini kinaweka maisha yake rehani?"

"Ndio. Unajua alikamatwa kwa kosa la kutokulipa kodi. Bishara yake ikayumba sana kwa maana ilikuwa ni kiasi kikubwa sana alichotakiwa kulipa, mbali na msongo wa mawazo.

Akahangaika huku na huko kutafuta pesa hiyo lakini hakuipata kwa wakati.

Alipokuja kupata haikuwa kamili, bali nusu ya ile anayotakiwa kulipa. Alinambia amepewa na mshirika mmoja wa kibiashara anayeitwa Sheng.

Lakini pesa hiyo alipewa kwa masharti ambayo alishindwa kuyatimiza na hatimaye kuuawa."

"Naomba uniweke wazi kila kitu mama. Masharti gani hayo? Na huyo Sheng wamjua?"

Mama akafuta kwanza machozi kabla hajasema:

"Hakuniweka wazi, alinambia kifupi tu kuwa ameambiwa asafirishe vitu fulani ndani ya mzigo wake wa samaki kwenda Rwanda na Burundi."

"Na huyo Sheng?"

"Simjui. Yeye mwenyewe mume wangu hakuwa anamjua. Sheng ni mtu wa kutuma watu tu. Walikuwa wanakuja hapa wawakilishi wake kuteta na mume wangu."

"Kwahiyo ina maana mumeo aligoma kusafirisha mzigo huo?"

"Ndio. Hivyo Sheng hakumalizia kumpatia nusu ya pesa anayodaiwa mpaka kiasi fulani cha mzigo kitakaposafirishwa.

Sasa mume wangu baada ya kupata nusu ile toka kwa Sheng, akaamua kutafuta nusu nyingine ambayo kwakuwa kiasi kilikuwa kishapunguzwa, akaipata kwa urahisi.

Kabla hajalipa, wakamuua."

Mama akamalizia kwa kulia. Ikabidi Jona apoteze kama dakika nne kumbembeleza kurudia kwenye hali ya kuongea.

"Na kumhusu mwanao? Kifo chake kinahusiana na haya?"

"Ndio. Salim alikuwa anataka kutafuta haki ya baba yake. Unajua Salim alikuwa anashirikiana sana na baba yake kwenye mambo ya biashara. Alikuwa anajua mengi huko kuliko mimi.

Shida yake ilikuwa ni kutafuta haki ya baba yake, ila matokeo yake akapata kifo."

Jona alinakili yale yote aliyopata kwa mama huyo. Alipomaliza akamuaga na kumpa moyo. Alimwambia:

"Haki itapatikana, hata kama yakawia."


***


Saa nne usiku: Lorenzo Night club.

Baada ya kugongesha glasi zilizojazwa mvinyo, Lee akanywa fundo moja kubwa kisha akauliza wenzake watatu waliokuwa pamoja naye mezani.

"Bado kimya?"

Wakatazamana kwanza. Wengine hao watatu walikuwa ni Nigaa, Devi na Mombo; kampani yake ya kazi.

Wote walikuwa wamevalia jeans za bluu zilizokuwa zinatofautia kukoza. Juu wakivalia matisheti, isipokuwa Lee peke yake ambaye alivalia jaketi dogo jeusi mtindo wa kizibao.

"Naona bado kimya," akajibu Mombo na sauti yake nzito baada ya wenzake kuwa kimya kujibu swali.

"Usikute Bigo kamalizwa na sisi tupo hapa tunabung'aa?" Akasema Devi. Sauti yake muda wote ilikuwa inakwaruza kama bati linalosuguliwa na msumari.

"Home kwake hayupo, wala maskani zake. Muda sasa hajatutafuta. Si kawaida!" Nigaa naye akatia neno kisha kukawa kimya.

"Kwa namna bosi anavyomtafuta, akimpata anaweza akamtafuna mbichi," Devi akasema akitikisa kichwa chake kama mtu anayesikitika.

"Ila mimi nina mashaka," akasema Lee. "Bigo atakuwa yupo matatizoni. Akili yangu inagoma kabisa kuamini kama yu buheri wa afya."

"Sasa tutafanyaje?" Akauliza Mombo. Na hilo ndilo lilikuwa la msingi, watafanyaje kama wanatilia mashaka juu ya Bigo?

"Nina wazo," akasema Nigaa. "Kwanini tusiende kumuuliza mkuu juu ya yule mshkaji ambaye alitakiwa kuuawa na Bigo?"

"Ili?" Devi akauliza.

"Ili tumfuatilie mshkaji wetu. Kama jamaa huyo aliyetakiwa kuuawa bado yupo hai, maana yake Bigo ndiyo atakuwa ameuawa."

Kukawa kimya kidogo watu wakimeza wazo hilo.

"Naunga mkono hoja," Lee akasema akitikisa kichwa. "Kama kweli tunataka kujua hatma ya Bigo, hiyo ndiyo njia pekee."

Basi wakakubaliana wote kufanya vivyo.


JE WATAGUNDUA BIGO AMEUAWA? NINI WATAMFANYIA JONA?

WAPI JONA ANAELEKEA NA UDADISI WAKE?

BWANA ELIAKIMU NA WAKINA MIRANDA?


Usikose sehemu ijayo.


*Simulizi za series*
 
*JOANA ANAONA KITU USIKU --18*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Usiku kwake ukawa mtihani mkubwa. Alikuwa anakurupuka mara kwa mara na kuangaza. Akawa anaona vitu vinacheza. Sauti za watu zinateta zikiyoyoma. Mlango na madirisha yakiwa wazi.

Siku nyingine alikuwa anasikia sauti za vishindo vya miguu na watu hawaoni. Ama anakuta ujumbe mezani!

ENDELEA

Akakosa kabisa furaha. Kwani watu hao aliokuwa anawaona kila usiku, hawakuishia tu kumsumbua yeye bali na wengineo aliokuwa nao karibu.

Mara kadhaa mama yake alikuwa anakurupuka na kusema anaona kitu. Anaona watu wakizunguka ama kutembea huku na huko.

Hata baba yake aliporejea nyumbani, alisadiki kusumbuliwa na watu fulani fulani usiku.

Siku moja usiku, baba yake Joana alikurupuka baada ya kusikia sauti ya kugonga mlangoni. Ilikuwa ni majira ya saa tisa hivi usiku.

Baba akanyanyuka na kwenda kutazama akiwa kabebelea bunduki yake ndogo kwa ajili ya ulinzi. Hakukuta mtu. Akageuza uso wake huku na huko, hakuona kitu.

Basi akageuka atizame ndani anapoenda. Lah! Si ndiyo akakutana na mtu mrefu mweusi mwenye uso mweupe!

Kabla hajafanya jambo, akala kofi zito mpaka chini.

Kutazama, hamna mtu!

Akapaza sauti kumwita mlinzi ambaye alikuja upesi na kumtazama bosi wake akiwa chini. Akamuuliza mlinzi kama ameona mtu, mlinzi akatahamaki kwani alikuwa peke yake nje.

Siku nyingine, wakiwa wamelala wakasikia tena mtu akipita dirishani. Ulikuwa ni usiku mzito. Mama akamwamsha baba na kumwambia kuna mtu anapita dirishani.

Punde tu wakasikia sauti ya Joana ikilia kwanguvu! Haraka baba akanyakua bunduki yake na kukimbilia huko chumbani, nyuma akiwa na mama.

Walifika wakamkuta Joana amefumba macho, ameziba masikio anapiga makelele kuomba asiuawe.

Walipomkurupusha akasema alikuwa usingizini na kuna mtu alikuwa anamkimbiza akitaka kumuua.

"Alikuwa ameshikilia shoka kubwa. Nguo yake ilikuwa imetepeta damu na kuchafuka."

Sasa ikalazimu familia ikae kujadili hili swala maana limekuwa zito sasa na halibebeki. Ilibidi sasa watafute namna ya kujikomboa na swahibu hili ili kurejea kwenye maisha yao ya awali.

Mama akashauri wamuite mtu mwenye wadhfa kanisani aje kuwaombea na kuwatakia kheri.

Baba yake Joana ni mtu asiyeamini katika Mungu, yaani Atheists, hakuafiki hilo jambo. Hata mwanzoni alikuwa mgumu sana kuamini yale Joana alikuwa anasema mpaka pale alipoyashuhudia mwenyewe kwa macho.

Badala ya kumleta mtu toka kanisani, yeye akaonelea awalete wataalamu wa haya mambo. Yani wa haya mambo ya kiimani zaidi.

Kesho yake mapema baba yake Joana akapiga simu kuwaita wataalamu, basi kwakuwa walikuwa na miadi na watu wengine, wataalamu wakasema watafika hapo kesho kutwa.

Kwahiyo wakina Joana wakawa na siku mbili, yani usiku mmoja na wa pili, zaidi wa kuhangaika nao kabla ya kuonana na wataalamu.

Usiku wa siku hiyo vibweka vikaendelea kama kawaida. Usiku huo ni sauti za wanyama ndizo zilizokuwa zinasumbua nyumba, kila mnyama akisikika huku na huko.

Picha za watu waliokufa zilirandaranda na kudai uhai.

Siku hiyo ndiyo baba yake Joana akauawa kwa kuchomwa kisu.

Alikuwa anasikia sauti ya kitu kikivutwa kwa kuburuzwa maeneo ya koridoni. Alipotoka kwenda kutazama akakutana na taswira ya mtu aliyekuwa anatisha kwa macho ya bundi, mikono mirefu na kucha ndefu kama dubu.

Mtu huyo akamrarua rarua. Na kama haitoshi akamsindika kisu chote kifuani.

Akiwa anakata roho mtu yule akamwambia neno moja tu:

"Usithubutu."

Mama alipokuja kutazama, akamwona mtu huyo akipotea kama upepo. Akaachwa akilia kwa uchungu akimwita mumewe aliyeanza kuwa baridi kwa ufu.

Basi kutokana na shuruti za msiba, hata wale wataalamu waliotakiwa kuja wakapangiwa tena kalenda kupisha msiba ambao ulikuwa mkubwa kwa kuhudhuriwa na watu wakubwa na wazito.

Mpaka walipokuja kutengemaa ilikuwa ni karibia juma zima. Wakawatafuta tena wale wataalamu mara hii mama akiwa ndiye aliyewapigia simu.

Watalamu hawa walikuwa wanatokea Ureno. Hivyo kuja kwao haikuwa rahisi sana. Ukiachia mbali na taratibu zingine za usafiri kama unazozijua toka nchi moja kwenda nyingine.

Wakatoa miadi ya kuja kesho yake tu, wakiwa wamejitahidi sana kutafuta upenyo.

Hivyo mama na Joana wakatakiwa kusubiri masaa kadhaa tu kabla ya kuonana na wataalamu hao.

Usiku ulipowadia, Joana akiwa yupo chumbani kwake hajalala, yupo macho amejikunyata, akasikia sauti ya pupa iliyomshtua moyo!

Ilikuwa ni yowe kali ya sauti ya mama yake. Kabla hajanyanyuka, mlango wake ukafunguliwa na jirani akaingia ndani.

Jirani huyu alikuwa analala na mama yake Joana akimpa kampani kutokana na hofu ya kulala peke yake.

Alimtazama Joana kwa macho yaliyojaa hofu nzito na taharuki, akaropoka:

"Mama amekufa!"

Haraka Joana akakimbilia huko .... kweli mama alikuwa amekufa. Alikuwa amelala chini, sakafuni, akichuruza damu puani na mdomoni.

Hata jirani hakuwa anajua nini kimemuua zaidi ya kusikia kishindo na kuhamaki akamwona mama amelala chini, hajitambui na hana uhai!

Hapo sasa mzunguko wa Joana ukawa umekamilika kamili. Hakubakiziwa sasa hata nguzo moja ya kuegamia.

Watu wake wote wa karibu, aliowapenda na kuwategemea wakawa wameenda ... wamekufa ... wamepotea!

Na haya ndiyo maisha Joana anayoishi mpaka sasa. Hana ndugu, rafiki wala jamaa. Amekuwa mtu wa kujitenga, mtu aliyekondeana, mtu aliyejikatia tamaa ya maisha.

Hakutaka kuishi wala kuwa karibu na yeyote yule kwa kuhofia kupoteza maisha yake na hatimaye wakaanza kumfuata nyakati za usiku. Kwani hata mama na baba yake nao wameungana, wote humtokea usiku na kumkosesha amani.

Nyuso zao zimekengeuka. Miili yao imemomonyoka. Wana macho ya kuogofya na mwendo wa wafu.

Joana amejaribu mara kadhaa kujiua lakini inashindikana. Kila anapojaribu zoezi hufeli, hushindikana.

Alijaribu kunywa sumu, kujinyonga na kujichoma kisu akaishia kupata jeraha tu akiwahishwa hospitali.

Hajui afanye nini. Amekuwa akiishi mwenyewe ndani ya jengo ambalo limeanza nalo kuwa ghofu kwa kutokupata matunzo.

Siku moja akiwa sebuleni, alishangaa akitembelewa na inspekta Westgate. Alikuwa amevalia suti yake ya kahawia na kofia ambatano.

Inspekta alimwonea huruma Joana kwa namna alivyokuwa. Ila akafurahi kumkuta hai.

"Pole sana, Joana. Najua umepitia mengi sana. Nipo tayari kukusaidia."

Joana hakujua ni namna gani inspekta anaweza kumsaidia. Alivyomwona tu, akili yake ilianza kuwaza kesi.

Ila ikawa ndivyo sivyo.


NINI INSPEKTA ANATAKA KUMWAMBIA JOANA?
 
*JOANA ANAONA KITU USIKU --- 19*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Joana akaelezea. Phillip akamwambia watu hao aliowaona huko ndipo yalipo makazi yao. Huku duniani ni vivuli tu.

Sasa watafanyaje?

Safari ya kwenda Brazil ikabidi ianze kuandaliwa. Kule ambapo agano lilipoanzia, ndipo pa kulikatia

ENDELEA

Baada ya maandalizi ya siku mbili, Joana pamoja na Phillips, Teddy na Inspekta Westgate wakawa tayari kwa ajili ya safari.

Wakachukua ndege mpaka Brazili, wakaweka makazi yao kwenye hoteli fulani ndogo malipo yakisimamiwa na Inspekta.

Wakapanga kwenda nyumbani kwa wakina Moa kwa ajili ya kutazama mambo fulani fulani ambayo Phillips na Teddy waliona ni muhimu kwenye harakati zao.

Basi ilipofika majira ya saa mbili usiku, kwa maelekezo ya Joana, wakaelekea kwa wakina Moa. Phillips na Teddy wakakagua eneo hilo kwa macho na kushuhudia watu ambao Joana aliwaona akiwa ulimwengu mwingine.

Katika mazingira hayo hayo, Joana akamwona Moa pia. Hawakuchukua muda sana, wakaondoka zao.

Lakini haya yanayoendelea, Mama Moa alikuwa ameshayafahamu. Akiwa kule ulimwengu mwingine, alimwona Joana. Na basi kwa namna moja ama nyingine akajiandaa kwa ajili ya vita.

Alijua fika Joana hakuwa peke yake. Kuna watu wapo nyuma yake.

Hata pale walipokuja nyumbani kwake kumpekua, basi alikuwa amewaona vile vile. Na kuzidi kuthibitisha kuwa kuna mipango juu yake.

Akaazimia kujipanga vema kwa ajili ya vita.

Ilipofika majira ya saa saba kuelekea usiku, Joana akiwa na kijikundi chake huko hotelini wakazima taa ndani ya chumba chao, mazingira yakaanza kuandaliwa kwa ajili ya kumsafirisha Joana kwenda ulimwengu wa pili.

Mishumaa miwili ikawashwa, na kisha Phillips na Teddy wakapulizia marashi fulani ndani ya chumba. Alafu wakawasha redio yao ndogo iliyokuwa inaimba wimbo fulani usioeleweka.

Wimbo huu ulikuwa ni wa kutetema. Mwimbaji akiwa mwanamke mwenye sauti nyembamba. Na baadae akisaidiwa kuimba na mwanaume mwenye sauti nzito.

Vyombo vilivyokuwa vinatumika ndani ya wimbo vilimezwa na sauti ya gitaa kali iliyokuwa inapuliza na kuacha.

Wimbo ulikuwa unatisha. Unasisimua ukijumlisha na mazingira yaliyokuwa yametengenezwa.

Joana akawekwa kwenye kiti, kabla hajafunga macho yake Phillips akamwambia:

"Inabidi ushinde. Inabidi urudi na roho yako duniani. Haijalishi utakachokutana nacho. Hili ni jambo la kifo na uhai. Pambana. Okoa nafsi yako na za wengine."

Kisha Joana akafunga macho. Sauti ya wimbo ikaongezwa akiachwa kwenye kiti mwenyewe.

Phillips, Teddy na Westgate wakakaa kando wakimtazama Joana kwa umakini.

Zikapita dakika nane, wimbo ule uliowekwa redioni ukabeba fikra na roho ya Joana na kuipeleka ulimwengu mwingine.

Joana akajikuta yupo nje ya mwili wake. Sauti ya wimbo redioni ikiwa imefifia, na kusikika kwa mbali.

Akawaona Teddy, Phillips na Westgate wakiwa wamekaa kitini kumtazama. Kabla hajaondoka eneo hilo, Teddy akapaza sauti yake kusema:

"Nenda nyumbani kwa kina Moa, Joana."

Joana akasikia kauli hiyo kwa mbali ikitetema masikioni mwake, basi akafuata mlango na kuufungua, akatoka zake nje.

Nje huko ambapo palikuwa giza. Taa zilizokuwa zinawaka katika ulimwengu huo, hazikuwa zinang'aa kabisa. Huu ulikuwa ni ulimwengu wa giza!

Upepo ulikuwa unavuma na kusababisha baridi. Joana akajikumbatia kujilinda.

Katika hali isiyo ya kawaida, akatembea kuelekea kwa wakina Moa, upesi akafika huko tofauti na majira yale walipoenda na usafiri.

Nyumba ya wakina Moa ilikuwa kimya na giza. Hakukuwa na taa hata moja iliyokuwa inawaka. Joana aliitazama vema na pembeni yake akaliona lile banda aliloliona kipindi kile, lile banda kubwa ambalo mama Moa alikuwa anataka kulifungua kabla hajaghairi.

Taratibu akalifuata lile banda kwa hatua zake ndogo ndogo. Kabla hajalifikia, akasikia sauti za vishindo vya miguu nyuma yake.

Kutazama, akamwona baba yake Moa. Alikuwa amevalia suti nyeusi akiwa amebebelea mnyororo mkubwa mkono wake wa kuume.

Akasikia tena sauti ya vishindo mbele yake. Na mara akamwona kaka zake Moa, wawili! Punde Moa naye akatokea kabla mama hajamalizia kwa kuibukia upande wa kushoto.

Alikuwa amevalia gauni jeusi lililokaba koo. Kofia nyeusi kichwani. Na mikono iliyofunikwa glovu za nyavu.

Kofia hii ilikuwa imefunika jicho lake moja, moja likiwa wazi. Macho yake yalikuwa yanang'aa kama kito cha dhahabu.

Mdomo wake ulikuwa mwekundu.

"Karibu, Joana," mama akasema akishika kiuno chake. "Leo itakuwa mwisho wako. Leo yote yatakoma."

Joana akaogopa sana. Kwa namna gani ataweza kupambana na watu watano? Tena wanaotisha vile?

Watu hawa hawakuwa wa kawaida. Macho yao yalikuwa ya simba. Rangi zao zilikuwa za tai, ziking'aa. Walikuwa wanamtazama kwa uchu wa kummaliza, na hata kumla nyama.

"Tukikuua katika ulimwengu huu, hutarudi tena katika ulimwengu wa walio hai. Nitaiteka roho yako na utakuwa mtumwa wangu milele!" Akasema mama Moa.

Basi kuokoa uhai wake Joana akachoropoka mbio! Mama Moa na watu wake wakasimama kumtazama katika macho ya furaha. Walimtazama kana kwamba katoto ka swala kanachojifunza mbio mbele ya umati wa simba.

Joana akakimbia sana. Usipite muda mrefu, akamwona mama yake Moa mbele yake! Mama huyo akamkandika kofi zito Joana. Akadondoka chini.

Haikujulikana wapi alitoa kisu, akamdondokea Joana, na kutaka kumchoma kisu.

Joana akaudaka mkono huo na kupambana kwa muda akizuia kisu kisimchome. Lakini mama Moa alikuwa na nguvu kumshinda, taratibu ncha ya kisu ikawa inasonga kifuani mwake.

Akaona muda si punde, atauawa. Basi akamtemea mate mama Moa machoni. Mama akapoteza mazingatio, Joana akamsukumia kando. Ila mara hii hakukimbia, akapambana kukamata kisu.

Akiwa anafanya hivyo, mara Moa, baba na kaka zake wakatokea. Wakamkamata Joana na kumpeleka nyumbani kwao. Wakamfungia mnyororo kitini.

Kisha sahani ikasogezwa mezani, sahani nyeupe iiliyokuwa imebebelea kila aina ya nyenzo. Kama haitoshi, ikaletwa na bakuli nyeusi, pamoja na kitabu kimoja kikuukuu.

Kitabu hichi kilikuwa kina jarada gumu lililoandikwa kwa maneno ya lugha ya kirumi: *MWANZO na MWISHO.*

Wakati wanaume wakiwa wamesimama, mama Moa akaketi kitabu kikiwa karibu. Bakuli akalisogezea kwa Joana aliyefungwa na minyororo.

"Joana," mama akaita. "Sasa ni wakati wa kumaliza kila kitu. Kuziba mashimo yote na kutia viraka. Ni wakati wa kuufanya mwanzo uwe mwisho."

Mara mama aliponyamaza, wanaume wakadakia kwa kuimba wakinguruma.

Japokuwa Joana hakujua kilichomo ndani ya kitabu, ila alifahamu si jambo jema. Si jambo lenye kheri kwake. Na endapo likifanyika, basi atakumbwa!

Lakini atafanyaje wakati yupo ndani ya minyororo?

Kitabu kikafunguliwa. Mama Moa akatia kidole ndani ya bakuli na kisha akapakaa damu kitabuni kwenye sehemu ile aliyokuwa anataka kusoma.

Kisha akaanza kusoma. Wakati huo sauti za mngurumo za wanaume zikiendelea kuita.

Basi kadiri mama anavyosoma, Joana akaanza kupapatika. Hata ule mwili wake aliouacha kule hotelini ulikuwa unahangaika. Teddy na Phillips wakijaribu kuutuliza.

Kama dakika tatu zikapita, ikawa imebakia aya moja tu ambayo mama Moa alikuwa anamalizia kusoma.

Kila alipokuwa anamaliza aya moja, ifuatayo akawa anaipakaza damu kwa kuchovya kidole bakulini.

Basi ni Mungu, ghafla wakasikia sauti ya mtu akiita Joana huko nje. Mama Moa akaacha kusoma.



***

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
*JOANA ANAONA KITU USIKU --- MWISHO*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Kama dakika tatu zikapita, ikawa imebakia aya moja tu ambayo mama Moa alikuwa anamalizia kusoma.

Kila alipokuwa anamaliza aya moja, ifuatayo akawa anaipakaza damu kwa kuchovya kidole bakulini.

Basi ni Mungu, ghafla wakasikia sauti ya mtu akiita Joana huko nje. Mama Moa akaacha kusoma.

ENDELEA

Akawatazama wanaume wale waliokuwepo hapo wakimzingira. Akawatikisia kichwa kuwapa agizo, wanaume hao wakaenda huko nje. Ila sasa ibada ikiwa imeharibika. Kwani ili itimie ilibidi hao wanaume wawepo.

Hao wanaume wakaenda huko nje na kuangaza kutafuta. Hawakuona kitu. Wakakasirika sana. Wakatazamana na kujigawa kwenda kila upande.

Huko wakazamia gizani kusaka.

Lakini sasa wakatafuta kweli pasipo kuona jambo. Ikabidi warudi kule nyumbani kurejesha taarifa kwamba hawajaona mtu. Lakini wakafika na hawakumkuta mtu. Mama hakuwepo, ila Joana bado alikuwa ndani ya minyororo!

Lakini ajabu zaidi, watu hao hawakuwa wanaweza kuongea. Isipokuwa kuonyesheana tu ishara. Basi wakapeana ishara wakatazame ndani. Huko napo wakaenda, lakini mmoja wao, ambaye ni Moa, kuna kitu akawa amegundua.

Walipofika kule chumbani akaona kuna haja ya kurejea sebuleni. Haraka akafanya hivyo na kukiendea kile kitabu. Akakipekuapekua. Muda huo Joana akiwa anamuita na kumkubusha kwamba yeye ni mpenzi wake wa enzi.

Lakini Moa hakuonekana kujali wala kusikia. Akaendelea na kazi yake ya kupekua kitabu. Na kweli, akaona kuna karatasi fulani ilikuwa imechanwa!

Akamtazama Joana na kumuuliza kwa ishara akionyeshea karatasi ile iliyochanwa. Nani kachana na yupo wapi?

Ila akiwa anahangaika na Joana ampatie majibu, akasikia sauti kubwa huko nje. Mara akatoka na kwenda huko. Akawakuta wenzake wakiwa wamemzingira Mama akiwa amelala chini. Hakuonekana kama mtu mwenye fahamu.

Walimtikisa tikisa lakini haikusaidia. Kumbe karatasi ile iliyokuwa imechanwa kwenye kile kitabu cha kilozi ndicho kilichokuwa kinampatia mamlaka na uwezo mama huyo kupata kuwepo duniani na kule walipo wafu kwa wakati mmoja.

Sasa walikuwa wamemwondoa na kumrejesha duniani kwa kuchana mkataba wake kitabuni.

Wakina Moa wakiwa hapo wamemzingira huyo mama, Phillip na Teddy wakazama ndani ya nyumba isijulikane walitokea wapi. Teddy akafuata kitabu, wakati Phillip akimfuata Joana kumfungua dhidi ya minyororo.

Teddy akafungua akipepesa huku na kule mpaka alipofikia karatasi fulani mbili ambazo zilikuwa karibia na katikati. Karatasi hizo zilikuwa zina picha ya binadamu mmoja akigawika mara mbili.

Teddy akasoma maelezo upesi, akajiridhisha. Basi akachana karatasi hizo kwa wakati mmoja na kuzigawa kwenye vipande vipande. Wakati huo wakina Moa walikuwa wameshafika mlangoni wakitaka kuingia ndani.

Ila karatasi hizo zilipochanwa, wakaanguka chini na kuwa kimya. Teddy, Phillips pamoja na Moa wakatoka ndani. Ndani ya jalada gumu la kitabu, Teddy akatoa funguo kubwa na kumkabidhi Joana.

“Twende tukafungue lile banda.”

Wakaenda huko upesi na kulifungua banda. Lakini ndani hakukuwa na mtu! Banda lilikuwa tupu likitikwa na giza.

“Joana, wale watu wote uliokuwa unawaua, walikuwa wanafungiwa humu,” Teddy akasema.

“Sasa mbona hawamo?” Joana akauliza.

“Hii ina maana kwamba agano lako lilivunjika. Siku ulipopata ajali, mkufu wako utakuwa ulikatika hivyo basi nafsi zote zilizokuwa zimeshikiliwa na roho yako iliyokuwepo huku, zikatoka kifungoni,” akasema Phillips. Na mara Teddy akaongezea.

“Ila sasa nafsi hizo zilizotoka kifungoni, zimekuwa zikikurudia kukufuata na kukudai. Na yote hayo yamewezekana kwasababu nafsi hizo zimeshikishwa kwako na damu. Damu ile uliyoimwaga kwenye ajali.”

“Sasa tunafanyaje ziache kunisumbua?” Joana akauliza kwa hofu.

“Ni lazima watu hao waitwe, na wafungiwe humu ndani maana wapo huko nje wanazurura kisha mlango ufungwe.”

Basi wakarejea ndani na kutafuta chanzo kizuri cha mwanga, kisha wakarejea karibu na banda ambalo lilikuwa limeachwa wazi. Teddy akafungua kitabu kutafuta karatasi anazotakiwa kuzisoma.

Akamwambia Joana.

“Kazi hii itakuwa ngumu. Inahitaji uvumilivu mkubwa na mazingatio. Nafsi hizo zinaweza kuja hapa na kusumbua, ila haitakiwi kusumbuka nazo. Fuata kile nitakachokuambia ufanye.”

Baada ya muda kidogo, Teddy akawa amepata mahali pa kusoma. Ila bado hakuwa na uhakika asilimia mia moja kama mahali hapo ndipo sahihi. Hivyo akamtahadharisha Joana.

“Kuna sehemu tatu na mojawapo kati ya hizo ni sahihi, kwahiyo itabidi tujaribu zote. Tuwe tayari kukabiliana na lolote litakalotokea. Tulia na usifumbue macho yako.”

Baada ya hapo Teddy akaanza kusoma sehemu ya kwanza. Wakati anaendelea kusoma, mlango wa banda ukaanza kuchezacheza kwenda mbele na nyuma. Kadiri ambavyo Teddy alikuwa anasoma, na mlango ule ukawa unacheza zaidi na zaidi!

Ikafikia mahala ukawa unajibamiza kujifunga na kujifungua. Mpaka Teddy anamaliza kusoma hakuna kitu kilichotokea.

Ikabidi wahamie sehemu ya pili. Teddy akaanza kusoma. Akamaliza sehemu yote hiyo pasipo lolote kutokea! Sasa ikawa imebakia sehemu moja tu. Sehemu ambayo Teddy akaamini ndiyo ambayo walikuwa wanaitaka.

Akaanza kusoma. Na kweli muda si mwingi, wakaanza kusikia sauti za watu toka mbali. Sauti hizo zikajongea karibu na karibu. Na mara wakajikuta wamezingira na nafsi za watu zikiwazunguka kama upepo.

Sura za watu hao ungepata kuziona kwa mbali zikikatika kama pepo. Zimeachama midomo.

Zikawajeruhi wakina Joana. Kwa kuwang’ata na kuwachana chana. Ila Teddy hakukoma kuendelea kusoma. Na pia Joana hakufumbua macho.

Lakini mpaka Teddy anamaliza kusoma. Hakuna kilichotokea. Zile nafsi zikapotea! Wakaachwa na majeraha mwilini na mafadhaiko.

“Inabidi Joana ndiyo asome,” Phillips akashauri.

“Lakini hajui hii lugha,” Teddy naye akasema.

“Hakuna namna, inabidi ajue kusoma. La sivyo hatutafanikisha hili,” Phillips akakazia uzi.

Basi ikabidi Teddy amwelekeze Joana herufi za lugha ile. Moja baada ya moja. Kwa muda wa kama dakika kumi na tano, Joana akaanza kujikongoja kusoma.

“Jitahidi. Huu mtihani inabidi uumalize wewe!” Phillips alimsisitizia.

Taratibu akaanza kusoma. Kadiri alivyokuwa anasonga mbele, akagundua lugha ile ilikuwa ni Kilatini kilichogeuzwa kushoto kwenda kulia. Sasa basi akatumia ufahamu wake kwenye lugha hiyo kusoma vema.

Ndani ya muda mfupi, zile nafsi zikaja. Zikawazunguka na kuwasumbua zaidi ya mara ya kwanza! Ziliwachanja na kuwang’ata. Zilipiga kila aina ya makelele. Ila Joana akapiga moyo konde. Akaendelea kusoma.

Mpaka anamaliza, nafsi zote zikawa zimeingia ndani ya banda. Na mlango ukajifunga wenyewe. Joana akaenda kumalizia kwa kuufunga na funguo. Kisha wakachimba shimo na kuzika kitabu kile na funguo yake kabla hawajarejea duniani.

Huo ukawa ndiyo mwisho wa Joana kuteseka daima!

.
.
.
***

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Kazi nzur sana y joana....endelea kutupa burudani
 
Back
Top Bottom