Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI --- 28*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Kwahiyo mpaka lini mpenzi?"

"Nitakutaarifu."

Baada ya hapo wakateta kidogo juu ya mkewe Boka, Boka akimtaarifu Miranda kwamba mkewe anaweza kumtafuta muda si mrefu kwani alikuwaanamwongelea hivi karibuni.

Hawakukaa tena sana, wakaagana na kila mtu akaenda zake. Miranda akampigia simu BC na kumtaarifu vile mpango ulivyokwenda.

Yote yalikuwa mema!

ENDELEA

***

Simu iliita kwanguvu! Ilikuwa ni alarm ambayo ilimkurupusha Lee toka kitandani akaangaza. Lah! Ilikuwa ni saa kumi na mbili jioni. Akanyanyuka upesi na kwenda kujiandaa pasipo kuoga.

Akajipaki kwenye gari lake na moja kwa moja akanyookea mpaka nyumbani kwa yule mwanamke ambaye alimuahidi kumtafutia nyaraka yake toka kwa yule mwanaume aliyelala naye.

Uzuri akafika na kumkuta akiwa ndani nay u maandalizini akikaribia kuruka viwanja. Mwanamke huyu ni kama popo kwani hulala mchana na usiku kwake ni kazini.

Alikuwa pamoja na marafiki zake watatu ambao walijikuta wanamwonea wivu mwenzao baada ya kumwona akiitwa na mchina. Hawakujua alikuwa matatizoni.

“Vipi ile ishu?” Lee akauliza. Alikuwa ameegemea ukuta akimtazama mwanamke kama vile maelekezo ya mtihani.

“Bado hajanipatia,” Mwanamke akajibu. Lee akajikuta akipandwa na hasira! Akauliza shida ni nini, mwanamke akamwambia wale wanaume wamesema wana hizo nyaraka lakini wanataka pesa kwanza.

Kama kweli ni za muhimu basi na wao wanataka angalau ‘kamgao’. Lee akastaajabu. Yani kamgao na nyaraka ni zangu! Akamkwida mwanamke shingo na kumkazia macho.

“Nipeleke kwa hao mabazazi!”

Mwanamke akamwambia si kwa sasa kwani ana mtoko. Lee akacheka na kumwambia hakutakuwa na mtoko wowote ule mpaka pale atakapohakikisha amepata karatasi zake.

“Twende ama nikuvunje taya saa hii!”

Basi kwanguvu Lee akampaki mwanamke ndani ya gari na kwenda mpaka kule kwenye yale makazi ya yule mwanaume. Wakagonga lakini hakukuwa na majibu. Wakauliza pia hata kwa majirani pasipo mafanikio.

“Sijaona mtu leo hii,” alisema jirani mmoja, mmama mnene mweusi aliyekuwa amevalia khanga aliyoifungia kifuani. Mdomo wake mwekundu akiupindua.

Siku hiyo ndiyo Lee akatambua jina la mwanamke yule anayesumbuka naye kutafuta vilivyo vyake. Alikuwa anaitwa Glady! Akamtaka ampeleke kwenye viwanja anavyoenda huyo mwanaume akamkute huko. Hapo akiwa anajilaumu kwanini ile jana aliimwacha salama.

“Nadhani alikuwa anahitaji funzo, na mbaya sikumpatia.”

Kwahiyo Glady na Lee wakaongozana mpaka viwanja. Lakini Glady alikuwa anasisitizia kwamba ule muda sio. Hawawezi kumkuta huyo mlengwa wao huko labda mpaka baadae, usiku ukiwa umevunja ungo.

Lakini kwa hamu aliyokuwa nayo Lee, hakuelewa! Bado alitaka kwenda akashuhudie na macho. Kweli wakafika kiwanja cha kwanza, hawakupata kitu. Cha pili vilevile hakukuwa na kitu. Mpaka cha tatu!

Glady akamwambia:

“Unaona? Hapa inawezekana bado akawa kwenye mihangaiko yake.”

Lee akauliza: “Na yule mwanamke tuliyemwona jana kule nyumbani?”

Glady akaangua kwanza kicheko. Akamjibu kuwa yule alikuwa ni malaya tu kama yeye. Mwanaume yule huwa anabadili wanawake, kwahiyo itakuwa hajaleta malaya siku hiyo.

Lee akachoka. Kichwa kikagoma kuzalisha mawazo kwa muda. Asikae muda, akasikia simu yake inaita. Haraka akaichoropoa mfukoni na kutazama. Alikuwa mkuu! Alimtunza kwa jina la ‘The Big.”

Akasita kupokea simu akifikiria. Ila mwishowe akapokea na kuongea kwa sauti ya chini.

Maongezi yakadumu sekunde tatu tu! Akakata simu. Sura yake ilikuwa imenyong’onyea. Na macho yake yalifumbwa kwa mawazo.

Ujumbe ukaingia kwenye simu yake. Akautazama. Ulikuwa unatoka kwa Nigaa akimuuliza yupo wapi. Hakujibu akairudisha simu mfukoni na kulalia usukani.

Glady akamuuliza nini kimejiri. Baada ya muda kidogo akamtazama tena Glady na kumuuliza:

“Ina maana hamna namna nyingine tunayoweza kumpata?”

Glady akabinua mdomo na kutikisa kichwa. Lee akawasha gari na kutimka! Akamrejesha Glady nyumbani kwake akimuahidi anaweza kuja baadae, alafu akanyookea mpaka yalipo makao yao kwenda kuonana na mkuu.

“Vipi, ulikuwa wapi?” Nigaa akamuuliza. Lee, kwa sauti ya unyong’onyevu, akamwambia alipotoka.

“Mkuu alikuwa anakuulizia kweli. Bado hujapata ile ishu?”

Lee akamwambia namna mambo yalivyo. Nigaa akafunika mdomo kwa kiganja.

“Sasa utamwambiaje mkuu?” Akauliza.

“Nitajua huko huko,” Lee akajibu akaminya lips.

Nigaa akapendekeza waende wote, ila Lee akakataa. Ule ulikuwa ni wito wake na ilibidi autimize. Kwahiyo akaenda zake, lakini Nigaa akabaki na moyo mzito, basi akasonga karibu na mlango apate kusikia.

Maongezi yakachukua kama dakika nane. Mara Nigaa akasikia sauti ya risasi! Pah – pah! Kukawa kimya.

Lee ameuawa? Nigaa akatoa macho.


***


“Katika siku ambazo umefanya kazi za kiume, basi ndiyo hii!” alisema mheshimiwa Eliakimu alafu akaangua cheko pana. Macho yake yalikuwa mekundu. Mkononi alikuwa amebebelea chupa kubwa ya mvinyo akiipeleka mdomoni kupiga tarumbeta.

Alikuwa amevalia bukta kaki ya ‘timberland’. Kifua chake kilikuwa wazi na miguuni peku. Pembeni yake tu hapo, alikuwa amesimama Nade akiwa amevalia ‘vest’ ya bluu na suruali ya jeans. Mkononi alikuwa amebebelea bunduki.

Ndani ya chumba hichohicho, alikuwapo pia Miriam. Yeye peke yake ndiyo alikuwa amekaa. Kiti kilikuwa kimoja tu chumba kizima, Miriam alikuwa amefungiwa hapo na kamba ya katani rangi ya manjano.

“Unastahili zawadi, tena nono!” alisema Mheshimiwa akimtazama Nade. “Na nitakupatia zawadi hiyo kwa kuniletea kichwa huyu mbwa koko hapa ngomeni.”

Akanyooshea kidole kwa Miriam aliyekuwa amekaa akimtazama kwa uso wa ghadhabu kali.

Akamwambia Nade kwamba hakuamini pale alipopokea taarifa ya kukamatwa kwa mkewe. Alimfanya asifanye kazi kabisa na kutazamani kutoka ofisini papo hapo. Amekimbiza sana gari mpaka kufika hapo. Hakutaka hata dereva aangaike.

Alipomaliza kusema hayo, akamtazama Miriam na kumuuliza alikuwapo wapi siku zote hizo. Na huko alikuwa anafanya nini. Miriam akacheka kwanza. Akimtazama mumewe, akasema:

“Bwana, nilikuwa kwetu. sikutaka kabisa kuwa na wewe, si uligoma kunipa talaka?”

Mheshimiwa akabana pua na kurudia maneno ya mkewe. Akamzaba kofi kali na kufoka:

“Unadhani mimi ni mjinga, sio?”

Eliakimu alikuwa anaamini kuwa mwanamke huyo alikuwepo mahali na anafanya jambo. anahofia siri zake anaweza akawa ameziweka wazi. Hivyo akamlazimisha sana Miriam aongee kwa kutumia mabavu.

Miriam akachakaa kwa kipigo asiseme kitu. Alitema meno matatu nje lakini bado akisema alikuwa kwa ndugu ambao Eliakimu alishawauliza na wakasema mwanamke huyo hakuwako.

“Utasema tu … utajua namna gani nilivyo mafia!”

Wakiendelea na zoezi hilo, mara simu ya Miriam ikanguruma. Ilikuwa ndani ya mfuko wa bukta ya mheshimiwa Eliakimu. Kabla mheshimiwa hajapokea, akamtazama kwa Nade. Alafu akatoa simu hiyo na kutazama.

‘My heart’ Pale’ alikuwa anapiga.

Eliakimu akasonya. Bila shaka huyo ndiye anayemchukulia na kumzuzua mkewe, akasema. Akamtazama Nade na kumkabizi simu apokee ajifanye Miriam.

Miriam akatamani kupiga kelele, lakini mdomo ulikuwa hautamaniki. Ulikuwa umevuja damu na kupasukapasuka. Ajabu hata Eliakimu alikuwa anangojea mwanamke huyo aongee. Kwa namna gani sasa!

“Hallow!” akasema Nade kwa sauti ya utulivu.

“Vipi, mbona sauti imekuwa hivyo?” sauti nzito ya kiume ikauliza.

“Mafua mafua tu yananisumbua.”

“Upo wapi?” mwanaume akauliza. Nade akamtazama Eliakimu akifikiria jibu.

“Nipo kwa shangazi,” ndilo jibu lililokuja kichwani.

“Unafanya nini huko? Ina maana hujui kwamba huko ni hatari kwa usalama wako?!” Sauti ikafoka.

“Nitatoka muda si mrefu,” akajibu Nade na kisha akauliza: “Kwani wewe upo wapi saa hii?”

Sauti ikaelekeza makazi. Alikuwa hoteli ipi na chumba namba ngapi, kisha simu ikakata. Eliakimu akafurahi sana kwani aliona sasa anaenda kumpata na huyo mwanaume amalize kazi.

Wakaachana na Miriam kwa muda wapange namna ya kumtia nguvuni ‘mwanahizaya’ huyo. Nade akasema yeye mwenyewe atosha kufanya hiyo kazi, ahitaji msaada. Eliakimu akahofia kidogo kutokana na jeraha alilo nalo mwanamke huyo begani.

“Ukiona inashindikana kumpata hai, mmalize kabisa!”

“Sawa, mkuu.”

“Na usisahau na yule mshenzi pia. Hatuwezi jua amepata nini toka kwa huyu malaya. Hakikisha naye unammaliza haraka iwezekanavyo,” Eliakimu aliagiza. Nade akahepa zake.

Kama isingelikuwa Jona alikuwa hotelini, mahali ambapo kuna watu wengi na ulinzi pia, mwanamke huyu angemdungua risasi Jona. Na Jona alilifahamu hilo hapo kabla na ndiyo maana hakutaka kukutana na Miriam mahali pa kimya zaidi.

Na pia alifahamu Eliakimu na Nade wataenda kubwabwaja maneno lukuki mbele ya Miriam, ndiyo maana akaishurutisha simu ya Miriam kumletea mrejesho wa sauti zote zilizokuwa zinasikika karibu kwa kupitia ‘application’ aliyokuwa ameipakua.

Hawakujua Jona alikuwa ‘amewapelekea’ Miriam, ila wampelekee taarifa pasipo jasho. Na alikuwa anafanikiwa hilo!

Akiwa ametulia chumbani kwake, alikuwa anasikiliza yatukiayo kwa njia ya ‘earphone’. Akajiuliza, je na yeye azuke eneo ambalo Nade ataenda kukutana na mwanaume yule anayedaiwa ndiye kipenzi cha Miriam kwa sasa?

Hakupata jibu haraka.


**


Ujumbe ukaingia kwenye simu ya Kinoo - kweng! kweng! – kweng! kweng!

Mwanaume huyo alikuwa amejilaza kitandani akiwa amevaa nguo ya ndani tu. kwa mujibu wa saa yake ya mkononi ambayo alikuwa ameiweka juu ya meza, ilikuwa inasema ni saa nne na robo.

Na ama kwa hakika, hii ilikuwa ni mojawapo ya siku nadra sana kumwona Kinoo hajavalia kibodi chake cheusi. Kifua chake kilikuwa kipo nje kinahema akiwa amelowea usingizi.

Hakusikia sauti ya mlio wa ujumbe. Ila ujumbe huo ukajirudia mara mbili, na baada ya muda kidogo simu ikaanza kuita. Kinoo akamka na kutazama. Namba ngeni! Akajivuta kupokea akijiuliza ni nani huyo amsumbuaye.

“Hallow!”

“Hallo, Sarah hapa. Unanikumbuka?” sauti ya kike iliuliza kwa pupa. Kinoo akaguna akijaribu kuvuta kumbukumbu. Sarah? … Saraaah…

“Yule mfanyakazi wa marehemu Bite!” Sarah akamkubusha. Sasa Kinoo akamkumbuka. Alikuwa ni mmoja wa wale mapacha wawili aliwaona kwenye kikao cha siku ile.

Amepata wapi namba yake na alikuwa anataka kumwambia nini? Akajiuliza upesi akijtengenezea kitako. Sarah akamwambia juu ya mauaji ya Mudy. Kinoo akashtuka sana! Sarah akamwambia na mpaka kuzikwa alishazikwa. Kilichomfanya akampigia ni kutomuona msibani.

Kisha simu ikakata!


***
 
Washa motoooooo [emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Back
Top Bottom