Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Bado tuuuuuu? [emoji850][emoji850][emoji850][emoji124][emoji124]
 
*ANGA LA WASHENZI --- 38*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Sikuwa na kwengine pa kwenda, Glady. Naomba unisaidie hifadhi," alisema Mustapha kwa huruma. Haraka Glady akaenda dirishani na kutazama huko nje.

Akateta na wenzake wakiwa katika hali ya taharuki.

"Mustapha, utakuwa umefanya nini saa hii?"

"Sijafanya kitu, ila nahisi atakuwa ni yule mchina tuliyempelekea ile nyaraka atutafsrie. Anatuzunguka, anataka kuichukua!" Alisema Mustapha. Jasho lilikuwa linamtiririka.

Akamweleza Glady kinaga ubaga walivyoenda kuomba msaada kwa yule mchina ambaye aliwapa lifti kuwarejesha nyumbani.

Wakiwa taharukini, wanasikia mlango unagongwa! Glady anamtazama Mustapha, kisha anawatazama wenzake waliokuwa kitandani.

ENDELEA

Kila mtu akajawa na hofu. Habari zile za Mustapha ziliwatisha na sasa wakadhani mambo yameanza kutiwa chumvi kunoga. Roho ya mtu imeshafuatwa.

Basi kwa tahadhari, Glady akachungulia dirishani kutazama aliyemlangoni. Akamwona mwanaume fulani mrefu mweusi akiwa amevalia suruali ya kijani na tisheti nyeupe.
Mwanaume huyu alikuwa amepachika hereni kwenye sikio lake la kushoto akitafuna jojo kwa mapozi.

Glady akaguna na kisha akamweleza Mustapha juu ya mwonekano wa mwanaume huyo ili ajue kama ndiye yeye anayemtafuta. Kwa kuhakikisha, Mustapha naye akachungulia na akaona si yule ambaye anamuwinda. Ila bado akawa na hofu.

“Embu msikilize anataka nini,” akamwambia Glady. Glady akatoka na kwenda kukutana na mwanaume huyo. Alisimama mlangoni mkono wake wa kushoto ukiwa umeshikilia mlango ambao hakuwa ameufunga ili lolote litakapotokea, ajue namna ya kujikomboa.

“Habari, dada,” akasema mwanaume huyo akimtazama Glady kuanzia juu mpaka chini. Glady akaitikia salamu na kisha akamtaka aeleze shida yake ni nini. Mwanaume akalamba lips zake, akashika kidevu na kumwambia anataka kuonana na Rose.

Angalau hapo Glady akashusha pumzi ya hofu na kuona mambo yapo sawa. Rose ni rafiki yake na yupo ndani. Basi aklichofanya ni kumuita Rose akutane na mgeni wake, alafu yeye akaenda kuteta na Mustapha.

“Najuta kwanini nimejiingiza kwenye janga hili,” akasema Mustapha. “Naona kuna haja ya kuonana na yule mchina na kumweleza yote haya, pengine anaweza kunisaidia.”
Glady hakuafiki, wakazoza kwa muda kidogo pasipo kufikia makubaliano.


***


Saa tatu usiku, Mbezi beach: Afrikana ya chini. Ndani ya nyumba kubwa rangi ya kijani yenye uzio mweupe.

Kamanda akasafisha koo lake, akauliza:

“Kwahiyo mpaka sasa umejua yupo na move gani?”

Akiwa ameketi kibarazani kwenye kiti kikubwa kilichofumwa na kambakamba za mbao na kujazwa sponji. Kando yake akiwa ameketi yule mwanaume muuaji wa Jumanne, akiwa amevalia suti rangi nyeusi, ila nayo ikiwa imemzidi umbo. Mbele yao kukiwa kumeketi stuli ndogo nyeusi inayong’aa kama kioo.

Juu ya stuli hiyo kulikuwa kuna chupa kubwa ya maji ya Kilimanjaro na glasi mbili pembeni.

“Bado yupo msibani, ni ngumu kujua amepanga kufanya nini, lakini kwasababu msiba utaisha leo, nitapata kujua,” akasema muuaji. Jina lake ni Alphonce Ndebali – afisa wa polisi, mwanaume huyu akihusika na kitengo nyeti cha mateso.

Kamanda akamhusia:

“Kuwa makini, hakikisha kila jambo linaenda kama lilivyopangwa. Unamjua vema Jona.”

“Usijali, mkuu. Sijawahi kukuangusha na wala haitakuja kutokea,” akasema Alphonce. Hii haikuwa kazi yake ya kwanza kwa Jona kwani alishafanikisha kumuua mke na mtoto wake kwa kuchoma nyumba.

Alishafanikisha pia kufuatilia na kuharibu mipango ya biashara ya Jona. Kwa ujumla, alifanikisha mengi kumfanya Jona aishi maisha ya tabu na dhiki. Na kama haitoshi alikuwa anawinda zaidi na zaidi.

Kazi yake ilikuwa ni kumfanya Jona arejee jeshini kama sehemu yake ya mwisho ya kupata msaada. Akose mkono wa kumsaidia wala mlango wa kutokea. Na alipewa kazi hii kwakuwa anaiweza na kuimudu ipasavyo.

Alphonce Ndebali ama Jabali kama wamuitavyo wenzake hakuwa mtu wa mchezo hata kidogo. Alikuwa ni mtu asiye na chembe ya huruma. Anamuua mtu huku akimtazama machoni na kutabasamu! Anapata raha kila anapomwaga damu na kukatisha pumzi ya mtu.

Hana roho ya binadamu, mishipa yake ya utu ilishakatika muda mrefu sana huko nyuma!

Na japokuwa ni afisa wa polisi, amekuwa akijihusisha na ‘michongo’ mbalimbali ya biashara haramu. Ni muuza madawa ya kulevya, lakini pia amekuwa akikodishwa na watu mbalimbali kufanya mauaji ama kutishia uhai watu kwasababu binafsi.

Huo ulikuwa ni upande wake ambao jeshi haufahamu. Huo ulikuwa ni upande wake ambao unamwingizia kipato kikubwa kuliko kile anachopewa kila mwisho wa mwezi na jeshi la polisi.

“Unajua kuna kitu nawaza,” Kamanda alisema akikuna kidevu chake. Alphonce akamwazima macho na masikio yake. Kamanda akamwambia kama ikishindikana kumrejesha Jona kwa haya yote watakayoyafanya, basi wammalize. Hakuna haja ya kumwacha awe hai kwani itakuwa dharau na ishara ya kufeli.

Alphonce akatabasamu na kuuliza: hilo tu mkuu? Huo ni mfupa mdomoni mwa fisi.


***


Saa sita mchana, Koko bar …


Mezani kuna Smirnoff moja pweke, na Jona ameketi akiwa amelaza kichwa chake juu ya tama. Anawaza mambo kadhaa na hana furaha. Jumanne ameshazikwa na kaenda zake, ila kamwachia maswali mengi sana. Anahisi kichwa chake kimevurugika.

Anachomoa simu yake mfukoni na kutazama, anapiga na kuiweka sikioni. Anaongea na mtu anayemuelekeza mahali alipo na isichukue muda mrefu, mtu huyo anafika. Alikuwa ni Panky akiwa amebebelea begi jeusi, amevalia shati jeupe na suruali ya jeans.

Baada ya kusalimiana na kujuliana hali, Panky anafungua begi lake na kutoa tarakilishi mpakato, anaiwasha na kuchomeka flash disk. Punde inasoma, anamwonyesha Jona kile ambacho alikipata toka kwa Marwa.

Kwenye kioo cha tarakilishi kulikuwa kuna mahesabu kadhaa na drafti ya kwanza ya mchoro. Kupata maana vema, Jona aliona kuna haja ya kuwa na mchoro ule pale pale kwa ajili ya kulinganisha. Hivyo basi akanywa kinywaji chake kwa mkupuo alafu wakaenda nyumbani kwake.

Hapakuwa kule pa zamani, la hasha, bali nyumba nyingine ndogo tu isiyo na uzio. Ina vyumba vitatu na sebule. Humo Jona akatoa picha ile chumbani na kuanza kuirejelea na yale mahesabu ya Marwa na drafti yake ya kwanza.

Wakaja kugundua kumbe kila kilichochorwa mule kilikuwa kimepangwa kisanii na kimahesabu. Vipimo umbali na upana vilikuwa vinafanana. Kuanzia umbali wa kila ndege aliyekuwa anaruka angani, visiwa pichani, na hata mawimbi baharini.

Lakini maana yake nini? Walishindwa kuipata. Lakini hata hivyo, akili ya Jona bado haikuwa imetulia. Hakuwa anawaza vema. Akamwomba Panky amwachie picha hiyo, ataifanyia kazi akitulia na kufanya mambo taratibu.

Panky akaridhia na haikuchukua muda mrefu akaenda zake akimwacha Jona peke yake. Jona akaongeza kinywaji cha pili kisha akalala kwa muda kidogo. Aliikuja kukurupuka akatazama simu yake, saa kumi jioni! Akaoga na kisha kuketi sebuleni.

Akaendelea kupekua pekua picha ile kwa macho yake mekundu. Lakini hakupata kitu. Akaghafirika. Aliona anapoteza muda na kichwa kinazidi kumuuma. Akaifunga picha ile na kwenda kuificha kabatini.

Mara simu yake ikaita, alikuwa ni Mheshimiwa Eliakimu. Akapokea na kuiweka sikioni. Mheshimiwa alikuwa anamuulizia lile jambo la kumuokoa Nade. Wale wanaume watekaji wamempigia simu na wamempatia masaa matano tu awe amatekeleza, la sivyo wasitafutane!

“Yakipita masaa hayo, wamesema watammaliza Nade na sitosikia lolote toka kwao milele!” Akasema mheshimiwa.

“Hamna haja ya kuhofia,” Jona akamhusia. “Hakuna lolote watakaolifanya kwa Nade kwasababu nao pia wanamhitaji Miriam kwa hali na mali. Ni vitisho tu!”

“Umejuaje? Na unafahamu wanamhitaji kwasababu gani?”

“Nitafahamu karibuni, pamoja na wewe kwanini hutaki wampate Miriam.”

Baada ya kusema hivyo, Jona akamwambia Mheshimiwa kwamba ataifanya kazi yake usiku. Na kabla ya kupambazuka, Nade atakuwa kwenye mikono salama. Kisha akakata simu na kuanza kujipanga kwa ajili ya kazi hiyo.


---


‘Ukithubutu kuleta ujanja wowote, utajuta!’ Ulisomeka ujumbe ndani ya simu ya Mheshimiwa Eliakimu, ujumbe huo ukitokea kwa watekaji, na ukiingia punde tu Mheshimiwa alipotoka kuongea na Jona.

Mheshimiwa akaagiza kwanza maji ya kunywa. Aliogopa kwa kudhani huenda watekaji hao wamejua janja yake ya kumwokoa Nade. Ila hapana! Akatikisa kichwa. Watakuwa wanahisi tu, akawaza. Hakuwa na budi kumwamini Jona. Hakuwa na mlango mwingine wa kutokea.

Mambo yalikuwa tafrani.


***


Saa mbili jioni…


‘Napitia hapo, basi nikukute,’ Boka akatuma ujumbe kwenda kwa Miranda. Mwanamke huyo akaupokea kwa tabasamu kabla hajarudisha majibu:

‘Sawa, utanikuta nakungoja.’

Boka akatabasamu mwenyewe nyuma ya gari kama mwehu. Akampatia maelekezo dereva wake apitie nyumbani kwa Miranda, maeneo ya Kawe.

Miranda naye akaweka mazingira yake safi kwa ajili ya kumpokea mgeni. Aliandaa mvinyo na glasi zake, pamoja na chakula kitamu cha kumfanya mgeni ajilambe na kwenda kusimulia.

Alafu akajivesha nguo maridadi na kufanya hali ya hewa inukie. Akaketi kumngoja mgeni wake kwa hamu.

Dakika chache kupita, akasikia sauti ya honi huko getini. Akatabasamu na kujitengenezea vema gauni lake jekundu. Akamwita mlinzi na kumuagiza afungue geti upesi kwani kuna mgeni wake wa maana.

Geti likafunguliwa, na akastaajabu kuona gari aina ya Murrano nyeupe ikiingia ndani. Kutazama, akamwona mke wa Boka akishuka toka kwenye gari hilo, akamtazama kwa tabasamu akimpungia mkono.

Kichwani akajiuliza mwanamke huyu ametokea wapi? Kwa namna moja akahisi pengine ndiye aliyekuwa anatumia simu ya mumewe, Boka, kumtumia ujumbe. Basi akawa na hofu.

Lakini wakati mama huyo anamjongea akiwa anatabasamu, simu yake ikaingia ujumbe. Akatazama upesi. Ulikuwa unatoka kwa Boka.

‘Nakaribia kufika.’

Moyo wa Miranda ukapasuka pah!










****
 
*ANGA LA WASHENZI --- 39*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Geti likafunguliwa, na akastaajabu kuona gari aina ya Murrano nyeupe ikiingia ndani. Kutazama, akamwona mke wa Boka akishuka toka kwenye gari hilo, akamtazama kwa tabasamu akimpungia mkono.

Kichwani akajiuliza mwanamke huyu ametokea wapi? Kwa namna moja akahisi pengine ndiye aliyekuwa anatumia simu ya mumewe, Boka, kumtumia ujumbe. Basi akawa na hofu.

Lakini wakati mama huyo anamjongea akiwa anatabasamu, simu yake ikaingia ujumbe. Akatazama upesi. Ulikuwa unatoka kwa Boka.

‘Nakaribia kufika.’

Moyo wa Miranda ukapasuka pah!

ENDELEA

Kwahiyo Boka na mkewe hawakuwa wanajua kama wanakutana sehemu moja! Miranda akajua hilo. Sasa afanyaje? Japokuwa alimpokea mke wa Boka na kumkarimu kwa tabasamu matata, akili yake haikuwa pale kabisa.

Haraka alitumikisha vidole vyake kuandika ujumbe na kuutuma. Akimtaarifu Boka juu ya ujio wa mumewe eneo hilo. Kama haitoshi, pengine kwa kuhofia Boka anaweza akawa hajaupata ujumbe huo, akaibipu simu yake kumtaarifu.

Boka akatazama simu yake akikunja uso. Kiooni akaona ujumbe toka kwa Miranda. Ila kabla hajaufungua ujumbe huo, dereva akawa tayari ameshapiga honi mara tatu getini! Na kwakuwa mlinzi alikuwa na taarifa juu ya ujio huo, haraka akafungua geti.

“Simama!” Boka akampiga dereva begani. “Rudi haraka, tuondoke hapa!” Dereva hakuelewa kinachoendelea. Alipigwa na butwaa, ila kutii amri ya bosi akarudisha gari nyuma upesi, na kuligeuza. Alidhani pengine itakuwa ni kuhusu mambo ya usalama. Wakayoyoma.

Lakini mama Boka akahisi jambo. Akauliza:

“Nimeona kama gari ya mume wangu,” alisema akitazama nje kupitia dirishani. Miranda akaigiza kushtukiza. Mama akanyanyuka na kwenda nje. Akaangaza pasipo mafanikio kwani geti lilikuwa limefungwa.

“Hamna kitu, mama! Utakuwa umeona vibaya,” akasema Miranda akitabasamu kiuongo.

“Hapana, sidhani. Nimefikia uzee huo!”

Basi Miranda kumaliza zogo akamwita mlinzi aliyemkonyeza tayari kwa ishara. Akamuuliza eti ni nani yule aliyekuja na kuondoka, kwanini ameondoka, na alikuwa anataka nini?

“Aaah Madam, ni Kinoo yule!” Mlinzi akasema akijichekesha. “Amesema kuna kitu alikuwa anakuletea ila sasa bahati mbaya amekisahau?”

“Kwahiyo ndo’ ameenda kukichukua?”

“Eeeenh! Ndo maana nikaona hamna hata haja ya kuja kukwambia huku … anaweza akarudi muda si mrefu.”

Angalau Mama Boka akawa ametuliza kifua. Wakarejea ndani na kueleza lile lililonyanyua mguu wake kumleta hapo.

“Samahani sana, najua nimekuja kwa kukushtukiza. Nilikuwa njiani kuelekea City mall, nikaona kuna haja kama nikikatiza hapa maana nina habari za kupasua kifua.”

Akaweka kituo akimeza mate.

“Kuna kampuni kubwa sana ya usambazaji ya huko nchini Kenya, wamevutiwa na kazi zetu na hivyo basi wanataka tuwe na ubia. Maana yake ni kwamba, bidhaa zetu sasa zitavuka mipaka na kwenda Kenya kwa uhakika!”

“Habari nzuri sana hizo!” Miranda akatahamaki. Ila kinafki. Hakuna wazo lake lolote lililokuwa pale. Alikuwa anamuwaza Boka. Namna alivyomkosa. Akijipa moyo ni kukuwe na hana haja ya kumshikia manati.

Ila alikuwa anataka kumaliza kazi. Huyu kuku atakaa nje ya banda kwa muda gani? Basi mawazo hayo yakapeleka mbali kichwa chake, yale aliyokuwa anayaongea Mama Boka kwake yakawa kama kelele za chura. Alichokuja kusikia mwishoni ni kile cha kuambiwa lazima interview yake ifanyike kesho kutwa.

“… Tutakapofanya hicho kitu, hapo ndo’ tutaeleza pia umma kwamba kampuni yetu imetanuka na sasa imefika Kenya.”

Akaitikia: “Sawa.”

Na hata hivyo vingine vyote vilivyofuatia, akamkubalia pasipo shida. Alikuwa anataka mama huyo aondoke amwache huru, haikupita muda akaaga na kwenda. Kitu cha kwanza ambacho Miranda alifanya ni kuchukua simu yake na kumtumia ujumbe Boka.

‘Ameondoka.’

Boka akamjibu baada ya muda mfupi:

‘Tutaonana siku nyingine mpenzi. Usijali.’


***

Saa tano usiku …


“Sasa Mustapha? – nataka kuondoka,” akasema Glady. Alikuwa amevalia bukta fupi rangi ya pinki na kaushi nyeupe nyepesi. Hakuwa amevalia sidiria, na hivyo basi chuchu zake zilikuwa zinaonekana vema zikitoboa kaushi. Miguuni alikuwa amevalia raba nyeupe – converse, mkononi akibebelea mkoba mkubwa mweusi.

“Sawa, we nenda tu,” Mustapha akajibu. Alikuwa ameketi kitandani nyayo zake zikigusa sakafu. Glady akacheka.

“Unajua unachekesha we Mustapha. Niende wapi na wewe umetuama humu? Au mpaka nikuambie amka uende mie nataka kufunga chumba?”

Mustapha akawa kimya kwanza. Sijui akitafakari nini, akamtazama Glady kwa huruma akisema:

“Unajua mikasa yangu ndugu yangu, unadhani n’taenda wapi? Huko nje si salama kwangu,”

“Leo nimekuwa ndugu yako, Mustapha?” Glady akapiga kofi akiangua kicheko. “Kweli shida kirusi. Sasa na mimi chumba changu hakipo salama nikikuacha humu. Umesikia? Mie n’takufuga humu mpaka lini labda?”

“Naomba unihifadhi kwa leo tu,” Mustapha akanyenyekea. “Kesho n’tajua mie pa kuelekea.”

“Sasa Mustaphaa …” Glady akakaa kitandani na kumtazama Mustapha. “Mie nikienda nikapata danga langu huko, n’talipeleka wapi? Mfano halina chumba, au anataka tufanyie kwangu? Ntafanyaje?”

“Kwa leo tu, Glady.”

“Mustapha mie n’takula nini?”

Mustapha akazamisha mkono wake mfukoni, “Basi lala na mimi leo.” Akatoa shilingi alfu kumi na kumwonyeshea Glady. Glady akaangua kicheko kikali. Akakohoa mara kadhaa kabla hajatulia na kumtazama Mustapha kwa macho yake mekundu.

“Mustapha, yani ulale na mimi kwa shing’ efu kumi!”

“Ntakupatia zingine bana, Glady. Mbona unakuwa kama hunijui? Unajua kabisa tukipiga ile hela na wewe utapata mgao au umesahau?”

“Mustapha, mie sio mtoto, sawa?” alisema Glady akiweka pesa yake kwenye mkoba. “Kwanza sasa hivi hakuna cha dili wala nini, ona unavyohangaika hangaika hapa kama digidigi. Pili, hii … hii pesa hii … haiwezi kun’tosha kabisaa! Hii ni pesa niliyolipwa kwa busu tu, upo? … cha kukusaidia, ntakuacha ulale humu, ila haiwezi kun’fanya nikabakia nyumbani.”

Hata hivyo Mustapha akashukuru, Glady akahepa. Alichukua bodaboda mpaka maeneo ya klabu ya usiku, Maasai, akaanza kufanya doria huko akichangamana na wenzake.


Baada ya robo saa …


“Shosti, yule siyo mchina wako uliyeenda naye siku ile?” alisema mwanamke mmoja kandokando ya Glady. Mwanamke huyu alikuwa amevalia topu na sketi fupi. Ilikuwa ngumu kujua rangi ya nguo hizo kwasababu ya ufinyu wa mwanga wa wingi wa taa za rangi rangi zilizokuwa zinakatiza zikienda huku na huko kwa kukimbizana.

Glady alitazama kule alipoelekezwa, kaunta, akamwona Lee! Mwanga uliokuwepo maeneo hayo ya kaunta uliwawezesha kuona vema.

“Au nimekosea?”

“Wala! Ndiye yeye. Acha niende,” akasema Glady akichukua hatua kwa mwendo wake wa madaha.

Lee alikuwa ameketi na marafiki zake, wakina Nigaa, wakipata kinywaji. Kila mtu alikuwa ameshikilia glasi ama chupa yenye kileo. Walikuwa wanasindikizia vinywaji vyao na soga za hapa na pale pamoja na cheko.

Mara Lee akasikia mkono begani, kutazama akamwona mwanamke ambaye kwa haraka alimtambua kama malaya. Akampuuzia akimshukuru na kumwambia ahitaji huduma.

“Ni mimi, unanikumbuka?” Glady alisema kwa sauti ya kubana pua. Hapo ndiyo Lee akatazama na kumgundua sasa Glady. Akamuuliza anataka nini?

“Naweza nikaongea na wewe kidogo?” Glady alisema kwa unyenyekevu.

“Glady, sihitaji usumbufu, sawa?”

“Ni jambo la muhimu, naomba unisikilize.”

Lee akageuka na kumtazama.

“Enhe, nini unataka kunambia?”

Glady akamwambia kumhusu Mustapha na matatizo yake. Yote yakisababishwa na ile nyaraka. Namna Mustapha alivyotaka kuitumia kupata pesa lakini mwisho wa siku ikamdumbukiza matatizoni, anawindwa anyofolewe roho!

Habari hizo zikamshtua Lee. Hakutegemea kama saga hili la nyaraka lilikuwa linaendelea katika ulimwengu huo ambao alidhani ameuacha. Lakini akajiuliza ni mchina gani huyo aliyepokea nyaraka hiyo na kuanza kumsaka?

Akamuuliza Glady:

“Unamjua mchina huyo? Unajua anakaa wapi?”

“Hapana, sijui lolote lile kumhusu.”

Lee akamtaka Glady waongozane mpaka kwa Mustapha. Lakini Glady akamuuliza:
“Sasa ukinitoa hapa, maana yake sitaingiza pesa yoyote. Vipi, utan’lipa?”

Lee akaukwapua mkono wa mwanamke huyo na kumswaga baada ya kuwatonya wenzake kwa ufupi ya kwamba anatoka.

“Taratibu basi jamaniii!” alisikika Glady akilalamika.


***

Saa saba kasoro usiku …

Kuna makelele makali ya muziki. Wanaume kadhaa pamoja na wanawake wapo ndani ya mahali hapa ambapo unaweza ukapaita klabu ya usiku, lakini ilikuwa ndani ya nyumba ya mtu! Ndani ya eneo hilo kulikuwa kuna kaunta, na eneo kubwa tu la watu kujimwaya kucheza muziki uliokuwa unapigwa.

Vinywaji vilikuwa vingi na vya kumwaga. Kila mtu aliyekuwa eneo hili alikuwa amebebelea kinywaji chake, haswa mvinyo ama whisky, katika mtindo wa chupa ama glasi. Na kila mtu alionekana akiwa na mtu wake.

Mwanga ulikuwa hafifu. Taa zilikuwa mbili tu, nyekundu na ya kijani. Wakati taa moja ikiwa inamulika kushoto, nyingine ilikuwa inamulika kulia. Kwahiyo ilikuwa ngumu kujua watu waliokuwemo humo kwa uso. Labda kwa maumbo.

Kulikuwa kuna milango miwili maeneo hayo, milango yote hii ikiwa ni ya kioo. Ukutani kulikuwa kumechorwa picha kadhaa za wanawake, maua na silaha.

Muziki ukiwa unaendelea kukonga nyoyo za watu, kama si vichwa, mlango mmoja ukafunguliwa na mwanaume fulani aliyekuwa amejaza mwili. Mwanaume huyu alitembea kwa kasi kuelekea meza fulani ukutani. Hapo akamnong’oneza mwenziwe sikioni.

Ghafla huyo aliyenong’onezwa akanyanyuka. Aliangaza kule kaunta akatoa ishara ya mkono, mara muziki ukakata! Akapaza sauti kusema wamevamiwa!


***
 
Back
Top Bottom