Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI -- 44*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Lakini kabla hajajimwaga kitandani, akaanza kupoteza uwezo wake wa kuona. Alikuwa anaona kama ukungu mbele yake na kichwa kikawa kinamzumguka, akachukua dakika mbili tu, akadondoka chini kama mzigo!

"Ms*nge wewe!" Glady akasema kwa kebehi kisha akanyanyuka toka kitandani na kumtazama Alphonce. Alikuwa anavuja damu sakafuni.

Haraka Glady akavaa na kisha akatoa chupa ya mafuta na kitambaa. Akalowanisha kitambaa mafuta kisha akapaka kwenye nyayo ya kushoto ya Alphonce na mafuta kidogo akayamiminia chini.

Alafu akaenda zake akiwa kabebelea kila kitu cha Alphonce!

ENDELEA

Saa saba mchana, Tikko Hotel ghorofa ya nne.


"Niliona hii sehemu itatufaa sana," akasema Boka akitazama huku na huko ingali akiketi. Alikuwa amevalia suti nyeusi ya kujichana ikirandana na mwili wake. Kwenye kamfuko ka koti mkewe alikuwa ameweka kijiua kidogo rangi nyekundu, kikivutia na kunogesha vazi.

Mbele yake alikuwa ameketi mwanamke mrembo Miranda. Nywele zake akiwa ameritachi na kuzimwagia kushoto. Kope za macho yake zilikuwa zimesimama dede akirembua. Lips zake zilikuwa rangi ya pink akinukia kama bustani ya kando ya mto.

"Una uhakika?" Akauliza Miranda.

"Aaaah! Unadhani nakutania?" Boka akajoki, "Hapa pametulia sana na hapana macho ya watu wengi si unajua bana siku hizi kila mtu ni mwandishi wa habari wa kujitegemea!"

Wakacheka, kabla hawajamaliza mhudumu akawa amefika. Akawauliza ni nini wanataka, wakaagiza chakula na vinywaji.

"Hivi kuna siku ulisahau kupendeza kweli? Umependeza haswa!" Boka akamsifia Miranda kisha akashushia na kinywaji.

"Ahsante, ila sijakuzidi wewe," Miranda akapokea sifa kwa sauti ya deko huku akipambana na kisu cha chakula.

Wakapiga stori kwa muda kidogo kabla hawajazama kwenye lengo la kijikao chao. Boka akasafisha koo na kusema:

"Bila shaka umeshaingia ubia na mke wangu. Nilipata kuwaona juzi mkiwa mnajinasibu mbele ya vyombo vya habari. Ni hatua nzuri."

"Ahsante, vipi ulinionaje? Nilikuwa sawa? Maana sikuwa comfortable kabisa!" Akalalama Miranda akiwa ameacha kula na kumkodolea Boka.

"You were fine! Sikuona tatizo, nilikuwa nawatazama nikiwa ofisini kwangu and felt very proud."

Miranda akashukuru akitafuna.

"Nataka kukuoa, Miranda. Nataka uwe mke wangu wa pili," Boka akasema huku anamtazama Miranda kwa jicho lisilo na utani.

"You must be joking, Boka!" (Utakuwa unatania Boka) akajibaraguza Miranda. "Mie niwe mkeo?"

"Kwani haiwezekani?"

"Haiwezekani!"

"Kwanini?" Boka akaacha kula.

"Kwasababu siwezi kugombania pakuo na mwanamke mwenzangu," akasema Miranda.

"Una maanisha nini?" Boka akauliza.

"Boka," Miranda akaita. "Mafahari wawili hawakai zizi moja. Unadhani msemo huu ulikosewa?"

"Sasa wataka nifanyaje Miranda na mie ilhali nishazama kwako. Mguu hautaki chomoka kabisa."

Miranda hakusema kitu. Akatafuna kwanza na kisha akanywa kinywaji chake rangi nyekundu ndani ya glasi yake yenye kiuno chembamba. Kisha akamtazama Boka kwa jicho la kike.

"You want to have me?" (Unataka kuwa nami?)
"Yes, I really do." (Ndio, nataka haswa.)

"But are you ready to do what it takes to have me?" (Lakini uko tayari kufanya namna ukanipata?)

"Yes, I am. But please don't tell me to abandon my wife." (Ndio, ni tayari. Lakini tafadhali usiniambie nimwache mke wangu.)

Miranda akacheka.

"Usijali, ila nikuweke wazi nashindwa kukupa jibu la moja kwa moja."

"Tena?"

"Nop! Si hivyo, I mean unajua kama nina mlezi. Nisingependa kufanya jambo hili siri. Ningependa tukamshirikisha."

Boka akaguna. Akala na kunywa kwanza kabla hajatia neno.

"It's ok! Ila huoni kama italeta matatizo na wewe hujaafiki kuwa mke kwangu?"

"Let us give it a try," akasema Miranda. "Mlezi wangu ni mzungu, huwezi jua." Akaongezea: "kama wanipenda kweli, kweli, basi nitajua kwa hatua zako."

Muda si mrefu, ujumbe ukaingia kwenye simu ya Miranda toka kwa BC. Alikuwa anataka kuonana naye hivi punde. Lakini kabla hajasema dhamira yake ya kuondoka, Boka akapigiwa simu na akamtaka waende maana yampasa afike ofisini.

"Basi twaweza tumia gari langu hamna shida," Boka akapendekeza. Wakapanda gari na kumpitisha Miranda nyumbani kwa BC.

"Ndipo hapa?" Boka akauliza.

""Ndio, karibu."

"Ningeingia na kusalimu, sema nahitajika kwa haraka ofisini."

"Sawa, usijali. Hamna shida," Miranda akasema na kisha akaaga na kujiendea zake ndani. Akamkuta BC akiwa amelisimama ghorofani akiwa anaangaza macho. Mkononi, mzungu huyo alikuwa amekamatia glasi ya mvinyo. Mwili wake akiuhifadhi kwa shati la "beach boy" alilolichomeka ndani ya suruali yake nyeusi ya kitambaa.

"Hellow, is that the man?" (Habari, yule ndiye yule jamaa?) Akauliza BC akitazama barabara.

"Yah! He is the one. Very soon he will be here talking to you." (Ndiye mwenyewe, muda si mrefu atakuwa hapa kuongea nawe.)

"That's nice! You know I called you here to talk about Eliakimu. Have you heard news about him?" (Hilo ni jema! Unajua nimekuita hapa kumuongelea Eliakimu. Umesikia habarize?)

"No! What is it?" (Hapana! Kuna nini?)

"He's passed away! Some people ambushed and killed him!" (Amefariki! Watu fulani wamemvamia na kumuua!)

Miranda akashangazwa. Akauliza zaidi kuhusu hiyo habari, BC akampatia 'full mkanda'.

"So from now on we'll be free to move on." (Kwahiyo kuanzia sasa tutakuwa huru kuendelea,) akasema Miranda akionyesha kuvutiwa.

"Yes, but I wonder who killed him. I know he had been involving in several crimes, but his killing will leave us safe?" (Ndio, lakini najiuliza nani kamuua. Najua alikuwa akijihusisha na uhalifu kadhaa, lakini kifo chake kitatuacha salama?"

Miranda hakuwa na jibu. Akaguna na kuhema akifikirisha kichwa chake. Mara akakurupuka na swali:

"About the news ... where was he killed?" (Kuhusu hiyo taarifa ... wapi ameuawa?)

"At his home!" (Nyumbani kwake!)

"All alone?" (Peke yake?)

"Yes. Heard only about him." (Ndio. Nimesikia kumhusu yeye tu.)

"Sure?" (Hakika?)

"Yes. What's wrong?" (Ndio. Nini shida?) BC akauliza akimtazama Miranda kwa macho ya kina.

"No - no nothing!" (Hamna kitu!)
"Are you sure you don't have anything to share?" (Una uhakika hauna kitu cha kushirikisha?)

"I think somebody may have the answers," (Nadhani kuna mtu anaweza kuwa na majibu,) akasema Miranda akitazama kando kwa mawazo.

"Who is it?" (Nani huyo?) BC akawahi kuuliza.

"The girl whom Eliakimu lived with," (mwanamke aliyekuwa anaishi na Eliakimu.) Kisha akaongezea:

"I think we should look for her." (Nadhani tuna haja ya kumtafuta.)

"But where? I went there, the house is empty!" (Lakini wapi? Nilienda kule, nyumba ni tupu!)

"There must be a way. We must find Nade where she is. And if we wont find her, then I will be convinced that she is the one who is responsible." (Kutakuwa na namna. Ni lazima tumtafute Nade alipo. Na kama tusipompata, basi nitaamini kwamba yeye ndiye mhusika.)

BC akanywa kinywaji chake, akatazama barabarani akiwa amekunja mdomo.


***


"Bosi, una mgeni," akasema mlinzi akimwambia mwanaume wa kichina aliyekuwa ameketi kwenye kochi akisoma gazeti.

Mwanaume huyu wa kichina kwa jina lake halisi anaitwa Foang. Ni mfanyabiashara mkubwa wa vyombo maeneo ya Kariakoo. Ana miliki maduka matatu makubwa akiwa ameajiri watu kadhaa.

Mwanaume huyu ndiye yule aliyeletewa nyaraka na wakina Mustapha kwa dhumuni la kuwasaidia tafsiri. Tangu siku ile amekuwa akisaka nyaraka hiyo pasipo mafanikio. Hivyo moyoni amekuwa na kama donda sugu ambalo lilishapewa dawa kisha ikashaisha. Sasa anaisaka kwa udi na vumba!

Anataka nyaraka hiyo kwa gharama yoyote ile. Kwani ni pesa! Pesa kubwa ambayo inazidi hata mara hamsini ya mtaji wake. Unalalaje sasa? Vipele vya baridi humtoka kila anapofikiria nyaraka hiyo.

Anafahamu ni kwa namna gani atafanya biashara safi ndani ya mji wa Hongkong. Pasi na shaka alikuwa anajiona karibu kabisa na tajiri namba moja barani Asia - Alibaba!

"Mwambie aingie!" Akasema Foang pasipo kumtazama. Macho yake yaling'ang'ania kwenye maandishi ya gazeti, ila alikwishajua ni nani mgeni wake huyo. Hakuwa na haja ya kuhangaika.

Punde, mlango unafunguliwa akaingia mwanaume aliyeshiba. Alikuwa amevalia suti rangi ya brown, koti kubwa kidogo kuvuka mwili wake. Mwendo wake ni wa hatua nzito, akaketi kwa kishindo na kusalimu.

Alikuwa ni Alphonce! Alikuwa ana bandeji kubwa kichwani kwake kwa nyuma. Uso wake ulikuwa umefuma kwa hasira na pembeni ya jicho lake la kushoto alikuwa amevimba. Macho yake yalikuwa mekundu akitengeneza ndita.

Foang akaweka gazeti lake pembeni, akamtazama Alphonce. Kwa dakika kama moja hakunena kitu. Bila shaka alishangazwa na muonekano wa Alphonce, ila hakutaka kujisumbua nao akamuuliza:

"What have you brought on the table?" (Umeleta nini mezani?)

Alphonce akasafisha koo lake kisha akazamisha mkono wake ndani ya koti na kutoa simu. Akailaza mezani. Foang akatabasamu kabla hajainyaka simu hiyo na kuikagua kwa kuigeuzageuza.

"Is this the one?" (Hii ndiyo yenyewe?) Akauliza Foang.

"Yes it is. I got it from the man who was left. I've already finished him!" (Ndio yenyewe. Nimeipata kwa yule jamaa aliyebaki. Tayari nimeshammaliza!)

Foang akatabasamu zaidi. Ila akakunja sura yake na kuuliza:

"Are you sure you've finished?" (Una uhakika umemaliza?)

"He doesn't breath anymore," (Ahemi tena) Alphonce akasema kwa uhakika.

"And about the police?" (Na kuhusu polisi?)

"Told you before. I am the only police whom you should worry about." (Nishakuambia hapo kabla. Mimi ndiye polisi pekee wa kumhofia.) Kisha akauliza:

"Where my money at?" (Pesa yangu ipo wapi?)

"Where are you rushing at?" (Unakimbilia wapi?) Foang akauliza.

"Let me inspect the phone first!" (Acha niikague simu kwanza!)

Kabla hajaifungua simu, Alphonce akamdaka mkono wake na kumwambia:

"Till I see my money first!" (Mpaka nione pesa yangu kwanza!)



****



***
 
*ANGA LA WASHENZI --- 45*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Are you sure you've finished?" (Una uhakika umemaliza?)

"He doesn't breath anymore," (Ahemi tena) Alphonce akasema kwa uhakika.

"And about the police?" (Na kuhusu polisi?)

"Told you before. I am the only police whom you should worry about." (Nishakuambia hapo kabla. Mimi ndiye polisi pekee wa kumhofia.) Kisha akauliza:

"Where my money at?" (Pesa yangu ipo wapi?)

"Where are you rushing at?" (Unakimbilia wapi?) Foang akauliza.

"Let me inspect the phone first!" (Acha niikague simu kwanza!)

Kabla hajaifungua simu, Alphonce akamdaka mkono wake na kumwambia:

"Till I see my money first!" (Mpaka nione pesa yangu kwanza!)

ENDELEA

Macho ya Alphonce yalikuwa hayana utani hata kidogo. Hakuwahi na utani kwenye pesa tangu azaliwe. Kwake pesa ndiyo kitu cha thamani maishani. Amezaliwa atafute pesa! Na kutumia pesa!

Kuhusu kiapo cha kazi ya upolisi, uzalendo na mambo ya ujamaa, hayo unaweza ukabaki nayo. Yeye mpe pesa! Kama unataka uendelee kuvuta pumzi ama kuishi kwa amani.

Foang akamtazama mwanaume huyo machoni. Akajifunza kweli hana utani. Hata akaogopa. Akatabasamu na kupandisha mabega yake:

"I still depend on you, Alphonce. I can not cheat on you." (Bado nakutegemea, Alphonce. Siwezi kukulaghai.)

Alphonce hakusema kitu, akaendelea kumtazama na macho yaliyotoa ujumbe tosha. Foang akanyanyuka na kwendaze chumbani, muda si mrefu akarejea na bahasha ya kaki aliyomkabidhi Alphonce.

Alphonce akatupia macho yake ndani ya bahasha, akatabasamu na kunyanyuka akimpatia mkono Foang.

"I think I should go." (Nadhani napaswa kwenda.)

"But I have not yet inspected the phone!" (Lakini bado sijaipekua simu!) Akalalama Foang.

"Just do it then you will inform me. You know my contacts, right?" (We fanya alafu utanitaarifu. Unajua namba zangu, sio?)

Hakungoja Foang aseme neno, akaenda zake Foang akimsindikiza kwa macho. Mchina huyo hakuwa anajua cha kufanya, akaishia kumtazama Alphonce akiyoyoma.

Alphonce akaweka bahasha yake kwenye kiti cha pembeni, akatekenya funguo na kutoka ndani ya nyumba ya Foang kwa kasi. Haikupita punde, simu yake ikaita. Ilikuwa ndani ya mfuko wa koti, akaichomoa na kuitazama kwa kuibia. Alikuwa ni kamanda.

"Ndio, mkuu ... muda si mrefu sana n'takuwa hapo ... serious? ... sijatazama na wala sijasikia kabisa! ... sawa! ... sawa."

Simu ikamuacha ameachama mdomo. Alikuwa amekunja sura, macho yake yakiwa yametambaliwa na utashi wa fikra. Habari alizozipokea zilimshangaza, na kumpatia mawazo. Zilimfanya kwa muda asahau kwamba alikuwa ameweka 'manoti' kadhaa kwenye kiti cha pembeni yake akiwa ameziingiza kwa 'kazi ndogo'.

Akashusha pumzi ndefu. Akasonya na kutikisa kichwa. Lakini ajabu, ghafla akasikia kitu cha baridi shingoni kwake! Akatazama kupitia 'sight mirror' akamwona mchina akiwa amemuwekea 'chuma', macho ameyakaza wakitazamana kiooni.

Alikiwa ni Lee!

"Habari za muda mrefu, Alphonce."

"Hivyo ndiyo namna ya kumsalimu rafiki yako ambaye hamjaonana kwa muda mrefu?"

"Si hivi, bali kwa kutoboa shingo yake na risasi! Rafiki hawi tena rafiki anapouarua mgongo wa rafiki yake aliyemkabidhi aukune."

"Una maanisha nini Lee?"

"Unajua ninachomaanisha. Peleka gari makaoni kabla sijakugeuza nyakati iliyopita ... na unafahamu vizuri kwamba sitanii."

Alphonce akamtazama Lee kiooni. Lee akamtazama Alphonce kiooni. Macho yao yalikuwa yanasema mengi zaidi ya maneno waliyoyatamka na vinywa. Macho haya yalikuwa ya janja janja! Macho ya kizandiki!

Macho ya njama!

Akilini mwa Alphonce kulikuwa kuna mafikirio, kama ilivyokuwa kwenye bongo ya Lee. Alphonce hakuwa tayari kwenda popote pale akiongozana na Lee. Mosi, kamanda anamngojea ofisini. Pili, ilikuwa ni ombwe kwake juu ya anachoenda kukutana nacho huko apelekwapo.

Akili yake ikabidi ifikirie namna ya kujinasua. Hakuwa na budi kumzidi akili Lee kisha atokomee zake! Basi akakaza mkono kwenye usukani wa gari. Akiwa katika mwendo wake wa kasi, akaanza kuhesabu kimoyomoyo, mdomo wake ukiwa unachezacheza kwa mbali.

1 ... 2 ... 3 ... 4 ...

... 5!

Akakanyaga breki kwanguvu! Lakini asifahamu kilichotokea, akajikuta hana fahamu baada ya kuhisi amegongwa kwanguvu chini ya kisogo.

Akazama kizani!

---

Robo saa mbele ...

Gazeti linatupiwa juu ya meza ya kioo, Kamanda akasonya na kunyanyuka akifuata kabati. Anatazama saa yake alafu anasonya tena. Anachukua faili rangi ya samawati, nalo analirushia mezani.

Anasimama na kufikiri jambo. Akajirejesha kwenye kiti chake na kunyakua simu yake nyeusi, SONY toleo jipya, akapiga. Simu ikaita pasipo kupokelewa. Akapiga tena, haikupokelewa!

Akaweka simu mezani na kulaza kichwa chake kwenye kiti. Akazunguka kwenda kushoto na kulia, kulia na kushoto akitazama feni yake darini.

Lile faili alilolitoa kabatini, hakuonekana kuligusa wala kuwa na mpango nalo. Mezani, kwa mbele yake, ungeweza kuliona gazeti la Habari Leo likiwa na picha ya wanaume wawili waliokuwa wamelala chini, wamejeruhiwa na kutapakazwa damu.

Kwa juu ya picha hiyo ikisomeka kichwa cha habari chenye maneno meusi:

*"WATU WAWILI WAMEUAWA KINYAMA NA MTU ASIYEJULIKANA."*

Chini ya maneno hayo, kwa mtu mwenye macho 'mepesi' angelisoma tena maneno yenye ukubwa wa saizi ya kati yaliyoandikwa kwa wino wa kijani:

"Watu hao watuhumiwa kuwa majambazi, na wameuawa kwa mkono wa siri."

Chini ya kichwa hicho, kulikuwa na habari kamili sasa ikiwa imeandikwa kwa maneno madogomadogo, ngumu kuonekana kwa macho ya wazi yaliyo mbali. Na mbele kidogo ya taarifa hiyo ikalekezwa kuendelea ukurasa wa tatu.

***

Usiku wa saa mbili ...

Baada ya sauti ya vishindo vya miguu, inafuata ya mlio wa mlango kisha Jona anaingia ndani ya makazi yake akiwa anachechemea.

Anawasha taa na kujitupia kwenye kochi kama mzigo. Akahema kwa mafundo makubwa makubwa mara tano kabla hajavua nguo yake ya juu na kubaki na kaushi ya kuzuilia risasi.

Akafungua kaushi hiyo kwa nyuma kisha akaiweka mezani. Kifuani kwake kulikuwa kuna majeraha, kwa mbali kulikuwa kuna rangi nyekundu ya kuvilia damu.

Kabla hajafanya kitu kingine chochote, akanyanyuka na kwenda chumbani akiwa anapepesuka. Alipofika mlangoni, akadondoka chini kama mzigo, akapoteza fahamu!

Baada ya kama dakika tano akiwa hapo chini, taratibu, kwa mbali akaanza kupata taswira ambazo hakuzielewa. Taswira hizi zilikuwa zinakatiza upesi kichwani kwake mithili ya mwanga wa radi!

Kulikuwa na sauti ambazo hazikueleweka. Mayowe na nderemo za kifo. Na mara sauti za watu waliomezwa na giza wakiwa wamebebelea maginga ya moto!

"Amepita wapi?" Sauti moja ya mwanaume ikauliza. Giza lilikuwa pana kiasi cha ginga la moto kutofua dafu!

"Huku! ... Amepita huku!" Akasema mwanaume mwingine upesi!

Mara tih! Tih! Tih! Vishindo vikaenda huko na kupotelea gizani.

Jona hakutikisika. Na hakuonyesha dalili ya kuamka karibuni. Masikioni hakusikia tena kitu, na machoni akawa mpofu.

***

Saa sita usiku.

"Bosi nadhani kuna mtu getini," akasema mlinzi baada ya kugonga mara mbili mlangoni, Foang akatoka akiwa amevalia taulo.

"Who is it?" (Nani?) Foang akauliza. Macho yake madogo ya kichina yalikodoa, mkono wake wa kuume ulikuwa umeshikilia taulo lake lisianguke.

"Bwana mi sielewi! Spiki kiswahili" akalalama mlinzi.

"Nani? Nani huyo?" Foang akafoka kwa lafudhi ya puani.

"Sijui nani? Hauna appointment na mtu?"

"No! No! No appointment!" Foang akatikisa kichwa, kisha akamtaka mlinzi aende, akafunga zake mlango!

Akiwa ndani ya chumba akasimamisha masikio yake apate kusikia kila jambo linalotukia huko nje. Lakini hakusikia hata lepe. Zikapita mpaka dakika nne ... tano ... sita ...

Akaulaza mwili wake kwa amani. Akazima taa, na bunduki yake ndogo ambayo alikuwa ameshaisogeza karibu akaisokomezea chini ya mto.

Kabla hajabebwa na usingizi, akasikia hodi mlangoni. Akalalama na kutusi. Aliona sasa huyu mlinzi ameshindwa kazi, na akaapa kumfunda adabu huko mlangoni aendapo.

Akajikwamua kitandani na kupiga hatua tatu ndefu. Akafungua mlango kwa hasira na kuangaza. Uso kwa uso akakutana na bomba la bunduki!

Alikuwa ni Lee!

Akamwamuru atoke na kumpatia simu aliyopewa na Alphonce. Na akitumia lugha ya kichina, akamuuliza kama amefanya lolote na ile nyaraka. Foang akatikisa kichwa chake upesi, akakana katukatu!

Kuhakiki, Lee akapekua simu ile kwa haraka. Alipomaliza, akamuaga Foang na kisha akamzamishia chuma cha risasi kichwani! Akatoka zake ndani ya jengo kwa kuchumpa ukuta.

Dakika kumi na tatumbele ...

"Ndiyo hii?" Akauliza Lee akimwonyeshea simu Alphonce aliyekuwa amefungwa kamba kitini. Walikuwa ndani ya chumba kidogo ndani ya makazi ya Lee. Kulikuwa kimya sana, kama si maongezi haya ungeliweza dhani hapana mtu.

"Ndiyo yenyewe!" Alphonce akajibu kwa kiburi. "Nifungilie basi niende!"

"Bado sijamalizana na wewe," Lee akananga akitikisa kichwa. Akaketi na kumuuliza Alphonce:

"Niambie ni nani aliyekuwa anawasiliana naye?"

"Mzee!" Alphonce akaita. "Hilo mimi silijui. Kazi yangu ilikuwa ni kutafuta hiyo simu tu!"

Kabla Lee hajaongeza kauli ujumbe ukaingia kwenye ile simu, haraka akatazama. Ilikuwa ni barua pepe toka kwa mtu aliyetunzwa kwa jina la Chen Zi. Lee akalazimika kufungua barua hiyo na kuitazama.

Akajikuta moyo unapiga fundo kubwa! Gibum! Alafu ukaanza kukimbia mbio! Mbio! Mbio!

Asiamini macho yake, aliona nyaraka ile, anayoipambania iwe siri, ikiwa imeshatumwa kwenye historia ya maongezi. Na huyu bwana Chen Zi alikuwa yupo huko Hong Kong, China!

Akahisi kuishiwa nguvu. Akapiga moyo konde na kusoma maongezi ya barua pepe ile mwanzo mpaka mwisho. Alipomaliza, akaiweka simu chini akisaga meno. Alipandwa na hasira mno. Alikunja ngumi yake kubwa akifuma ndita.

Akamtazama Alphonce kwa hasira, na mara akanyanyuka na kuchomoa bunduki yake akamuwekea kwenye paji la uso. Hakusema kitu, macho yake yalikuwa tayari mekundu. Akabinua mdomo na kufyatua kitufe cha bunduki!

Klick! Hakuna kitu. Klick! Klick! Klick! Hamna kitu, risasi zilikuwa zimeisha. Kwa hasira akaitupia bunduki mbali Alphonce akishusha pumzi ndefu ya neema.

Akatoka ndani ya chumba na kwenda kuketi sebuleni akiwa ametingwa na mawazo lukuki. Aliwaza, je kuna haja ya kumshirikisha Sheng kwenye mkasa huu?

Vipi kama Sheng akijua hizi habari, ambazo amejitahidi kuziweka chini ya kapeti akashindwa, atafanya nini na atamfanya nini?

Akajikuta akitetemeka mikono.


***
 
Back
Top Bottom