*ANGA LA WASHENZI II -- 57*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Glady akashtuka. Akapatwa na maulizo kichwani. Sasa akapata picha juu ya nini yule bwana wa kichina alikuwa anaongea na wale wajamaa. Akaguna. Akapiga moyo konde na kutoka bafuni. Akaketi kitandani.
Bado bwana yule wa kichina alikuwa anaongea na simu.
ENDELEA
Alikuwa anatoa maelekezo na huku akisisitiza kuwa mlengwa lazima amalizwe kwa namna ya siri isije zua utata. Basi baada ya muda, akanyamaza na kisha kumgeukia bibie Glady. Ila macho yake yalieleza namna gani alivyokuwa yupo nje ya ‘mood’.
“Umekwishaoga?”
“Ndio, kama unavyoniona,” akajibu Glady ila naye akiwa na sura ya woga na maulizo.
“Kuna shida yoyote?”
“Mmh mmh hamna.”
“Mbona unaonekana haupo comfortable?”
“Wala, niko ok tu.”
Kukawa kimya kidogo. Bwana yule wa kichina akatazama chini kisha akashusha pumzi ndefu puani na kuuliza,
“Haujaja na nguo nyingine mbali na zile?” huku akitazama nguo za Glady zilizopo kwenye kiti.
“Hapana, sijaja na zingine. Kwani vipi?”
“Nothing. Nilidhani umekuja na zile nguo za kusisimua, zile zaaa … you know? Anyway, usijali. Nipe muda kidogo. Sawa?”
“Kwani tulikubaliana nilale huku?”
“Kulala itakuwa shilingi ngapi?”
“Utaongezea mara mbili ya ile tuliyokubaliana.”
“Haina shida.”
Bwana yule wa kichina akakwapua simu yake na kusimama, “Ningojee hapa.”
Akaenda zake sebuleni. Glady akatulia pale kitandani kwa muda kidogo kisha akasimama na kwenda mlangoni kutega sikio. Kulikuwa kimya. Ila baada ya muda kidogo akasikia sauti ikianza kuteta na simu.
Kuna wazo likamjia kichwani. Haraka akaendea simu yake na kutafuta jina la Lee. Akajaribu kubipu. Alipoona haiiti, akazama upande wa ujumbe, ila akatoka tena na kwenda kwenye mtandao wa whatsapp, huko akamsaka Lee na kumtumia ujumbe.
**
“Kuna ulinzi, ila tutafanikisha,” alisema bwana mmoja mshirika na yule bwana wetu wa kichina. Aliposema hayo akaweka simu mfukoni kisha akatazama kando, kulikuwa na jamaa yake mwingine. Walikuwa wameazimia kufanya kazi hii watu wawili tu kuepusha msongamano ambao ungelipeleka kushtukiwa.
Akampatia ishara ya kichwa, na huyo mwenzake, kwa haraka, akaenda nyuma ya jengo. Jengo hili ni lile ambalo amelazwa bwana Sheng kwa matibabu zaidi. Na halipo pweke, bali limezingirwa na walinzi kadhaa.
Basi huyu bwana baada ya kutia simu yake mfukoni, akaanza kujongea, punde akamfikia mlinzi na kusalimiana naye, akaumulizia hali ya mgonjwa.
“Anaendelea vema,” akajibu mlinzi, na kisha kama mtu asiye na habari au shaka, akatazama zake kando kuendelea na kazhi yake.
“Naweza kumwona?” bwana yule akanena. Mlinzi akamtazama kwa kukunja ndita.
“Saa hii?”
“Kwani kuna shida?”
“Huoni kama kuna shida? Mgonjwa anatazamwaje saa hii. Daktari amesema anahitaji ma …” upesi akadakwa shingo, kak! Akavunjwa. Akadondoka chini kama mzigo.
Basi bwana yule haraka akasonga ndani asionekane na mlinzi mwingine yeyote. Akadaka korido na kusonga kwa hatua kadhaa kubwa kabla hajakutana na nesi.
“Nikusaidie nini, mlinzi?”
Alikuwa ni nesi wa kichina. Mfupi na mdogo kwa umbo. Sura yake ilikuwa thabiti na macho yenye mkazo. Basi bwana huyu akatabasamu na kusema, “Samahani, ni usiku mkubwa. Nimekuja kumtazama mkuu, kuna machache ya kusema naye.”
“Siwezi nikakuruhusu kwa sasa. Njoo kesho asubuhi.”
“It’s urgent, please. In fact nimeagizwa na mkuu. Hatonielewa kama nikimwambia sijafanikiwa.”
Nesi akashusha pumzi na kuminya lips zake nyembamba. “Ok, ni muda mfupi nakupa.”
Hakujua amempatia kibali muuaji. Bwana yule akatabasamu na kwenda zake upesi akakamilishe kazi. Ila bahati isiwe kwake, hakuwa anajua wapi alipolazwa mlengwa wake. Hivyo ikamlazimu kupoteza kama dakika mbili kabla hajawa mbele ya mtu anayetakiwa kumuua.
Kabla hajafanya hilo, simu yake ikanguruma mfukoni. Akaitoa na kutazama, alikuwa ni mtu aliyemuagiza akafanye tukio. Akapokea na kumwambia kwa kunong’oneza, “I am in, wait.” kisha akakata simu.
Sasa ikawa imebakia kumaliza tu kazi, bwana Sheng akawe historia ya kale inayotisha.
Alikuwa amelala kitandani hajielewi hata linaloendelea. Dripu ilikuwa ipo kwa juu ikidondosha matone, na usoni alikuwa ana ‘nyago’ ya kumpatia hewa ya oksijeni. Mwili wake wote ulikuwa umefunikwa n shuka isipokuwa shemu yake ya kichwa na mikono tu.
Kando kando yake kulikulikuwa na vifaa kadhaa vinavyobeba uhai wake kwa ncha ya kidole. Na pia kulikuwa na kifaa kioo kionyesha maendelea ya mapigo yake ya moyo. Ama kwa hakika yalikuwa hafifu.
Bwana yule akaweka mikono yake shingoni mwa Sheng. Hajaminya, mara akasikia kipyenga cha ‘hafla, Prrrrriiiiiii!!!! prrrrrrrriiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii! Prrrrriiiiiiiiiii! Akatoa macho. Huko nje akasikia vishindo vya watu vikitesa ardhi!
Kwa muda kidogo akawa ametekwa na buwazo. Akimbie? Au amalize kazi yake? Alihisi kutetemeka. Kama angeendelea kumnyonga bwana Sheng, wazi ingelimchukua muda kidogo na yeye huo muda hakuwa nao. Basi afanye nini cha haraka kunusuru roho yake na huku atimize wajibu?
Akanyofoa waya za mashine zimsaidiazo mgonjwa, kisha upesi akatoka nje akikimbia. Kufika nje, akakutana na watu taribani kumi kwa idadi ya haraka. Wote wakiwa wamemnyooshea bunduki, akaamriwa anyanyue kwapa. Akatii.
Kule ndani nesi akawahi chumba cha mgonjwa. Huko akakuta ‘alarm’ zalia kwa fujo na mgonjwa akiishilia uhai. Haraka akarejesha mashine katika hali ya kawaida, na akaokoa maisha ya mkuu wake kwa ncha ya sindano. Mashine ya mapigo ya moyo ikaanza kusoma upya. Akatip! … akatip! … akatip! … akatip!
Mgonjwa akihema kwanguvu ndani ya kinyago.
***
Ngo! Ngo! Ngo! Bwana wa kichina alisikia hodi hiyo, ila akasita kwanza. Macho yalikuwa yamemtoka. Jasho jembamba lilikuwa lamchuruza. Na moyo wake ulikuwa unakita kwanguvu kubisha hodi mbavu.
Hodi ikarudiwa tena. Na hakuwa na namna ya ziada sasa zaidi ya kwenda kuiitikia. Akiwa na kibukta chake, na mwili unamtetemia, akajonga na kutengua kitasa. Nje akawaona wanaume wawili anaowatambua wakiwa wamepigishwa magoti, na wanaume wengine takribani kumi wakiwa wamewasimamia na bunduki.
“Walitaka kumuua mkuu Sheng!” shtaka likatolewa kwa sauti kuu. “Wamevamia hospitali na kuua walinzi wanne katika jaribio hilo!”
“Inawezekanaje jambo kama hilo?” akashangaa bwana huyu wa kichina, kisha akawatazama walengwa na kuwauliza kwa sauti ya ukali kidogo,
“Ni kweli yanayozungumzwa?”
Wale watu wawili wakamtazama. Na kwa soni, akaepusha macho yake kutazama kando.
“Mkuu, wanastahili kuuawa mara moja!” akasema mmoja wa wale mabwana waliowaleta wale mateka. Akaungwa mkono na wenzake wote. Ndio! Wanastahili kuuawa. Na hiyo ndiyo ilikuwa sheria. Hamna anayebakiziwa uhai akidiriki kufanya jaribio la kummaliza mkuu. Na adhabu yake yafanyika mbele ya umati.
Hata bwana huyu hakuweza kulikataa hili kwani litazua mjadala mkubwa na hata kumweka rehani. Basi akakbidhiwa bunduki kutimiza agizo. Bunduki ilikuwa na risasi kumi na nane.
Wakati hayo yote yanaendelea, Glady alikuwa anashuhudia kwa kupitia dirisha. Mambo haya yalikuwa yanamtisha mno. Ametoa macho na kinywa chake kipo wazi.
Risasi zikavuma mara mbili! Wale watu wakadondoka wafu. Wakabebwa na kwenda kuzika kana kwamba mizoga, na huku nyuma wakimwacha bwana yule wa kichina majuto na maumivu makubwa sana kifuani.
Aliingia ndani akamtaka Glady aondoke zake upesi. Na baada ya punde akakutana na jamaa wake mmoja mpangoni aliyebaki. Akiwa amekabwa na donge la uchungu kooni, akasema, “Mpango wetu ulikuwa wa kipumbavu na wenye papara. Sasa tumeshawapoteza wawili.”
Yule bwana akamuuliza, “Una mpango mwingine?”
“Pengine ninao,” akasema bwana huyu wa kichina. “Na sasa nitaufanikisha mwenyesha jua likiwa linawaka.”
Basi hawakuongea sana, jamaa yule akaendaze. Watakutana baadae.
***
Saa tatu asubuhi …
“Do we need to hold on more?” aliuliza Wales akimtazama Denmark. Wote walikuwa wameketi sebuleni, vichwani wa earphones zilizokuwa zinawaletea taarifa toka kwenye kifaa maalum kidogo walichomfungia Sheng. Na mpaka sasa kifaa hicho kiilikuwa kimeshawatanabahisha makazi aliyopo Sheng na hata sauti ya yale yanayozungumwa ndani ya duara la robo kilomita toka kila pande ya dunia ya mahali alipo Sheng. Tena kwa usikivu mzuri.
“No,” akajibu Denmark. “Perhaps we should wait a bit. It seems the are more and more to discover.”
***