Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II -- 57*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA


Glady akashtuka. Akapatwa na maulizo kichwani. Sasa akapata picha juu ya nini yule bwana wa kichina alikuwa anaongea na wale wajamaa. Akaguna. Akapiga moyo konde na kutoka bafuni. Akaketi kitandani.

Bado bwana yule wa kichina alikuwa anaongea na simu.

ENDELEA

Alikuwa anatoa maelekezo na huku akisisitiza kuwa mlengwa lazima amalizwe kwa namna ya siri isije zua utata. Basi baada ya muda, akanyamaza na kisha kumgeukia bibie Glady. Ila macho yake yalieleza namna gani alivyokuwa yupo nje ya ‘mood’.

“Umekwishaoga?”

“Ndio, kama unavyoniona,” akajibu Glady ila naye akiwa na sura ya woga na maulizo.

“Kuna shida yoyote?”

“Mmh mmh hamna.”

“Mbona unaonekana haupo comfortable?”

“Wala, niko ok tu.”

Kukawa kimya kidogo. Bwana yule wa kichina akatazama chini kisha akashusha pumzi ndefu puani na kuuliza,
“Haujaja na nguo nyingine mbali na zile?” huku akitazama nguo za Glady zilizopo kwenye kiti.

“Hapana, sijaja na zingine. Kwani vipi?”

“Nothing. Nilidhani umekuja na zile nguo za kusisimua, zile zaaa … you know? Anyway, usijali. Nipe muda kidogo. Sawa?”

“Kwani tulikubaliana nilale huku?”

“Kulala itakuwa shilingi ngapi?”

“Utaongezea mara mbili ya ile tuliyokubaliana.”

“Haina shida.”

Bwana yule wa kichina akakwapua simu yake na kusimama, “Ningojee hapa.”

Akaenda zake sebuleni. Glady akatulia pale kitandani kwa muda kidogo kisha akasimama na kwenda mlangoni kutega sikio. Kulikuwa kimya. Ila baada ya muda kidogo akasikia sauti ikianza kuteta na simu.

Kuna wazo likamjia kichwani. Haraka akaendea simu yake na kutafuta jina la Lee. Akajaribu kubipu. Alipoona haiiti, akazama upande wa ujumbe, ila akatoka tena na kwenda kwenye mtandao wa whatsapp, huko akamsaka Lee na kumtumia ujumbe.


**

“Kuna ulinzi, ila tutafanikisha,” alisema bwana mmoja mshirika na yule bwana wetu wa kichina. Aliposema hayo akaweka simu mfukoni kisha akatazama kando, kulikuwa na jamaa yake mwingine. Walikuwa wameazimia kufanya kazi hii watu wawili tu kuepusha msongamano ambao ungelipeleka kushtukiwa.

Akampatia ishara ya kichwa, na huyo mwenzake, kwa haraka, akaenda nyuma ya jengo. Jengo hili ni lile ambalo amelazwa bwana Sheng kwa matibabu zaidi. Na halipo pweke, bali limezingirwa na walinzi kadhaa.

Basi huyu bwana baada ya kutia simu yake mfukoni, akaanza kujongea, punde akamfikia mlinzi na kusalimiana naye, akaumulizia hali ya mgonjwa.

“Anaendelea vema,” akajibu mlinzi, na kisha kama mtu asiye na habari au shaka, akatazama zake kando kuendelea na kazhi yake.

“Naweza kumwona?” bwana yule akanena. Mlinzi akamtazama kwa kukunja ndita.

“Saa hii?”

“Kwani kuna shida?”

“Huoni kama kuna shida? Mgonjwa anatazamwaje saa hii. Daktari amesema anahitaji ma …” upesi akadakwa shingo, kak! Akavunjwa. Akadondoka chini kama mzigo.

Basi bwana yule haraka akasonga ndani asionekane na mlinzi mwingine yeyote. Akadaka korido na kusonga kwa hatua kadhaa kubwa kabla hajakutana na nesi.

“Nikusaidie nini, mlinzi?”

Alikuwa ni nesi wa kichina. Mfupi na mdogo kwa umbo. Sura yake ilikuwa thabiti na macho yenye mkazo. Basi bwana huyu akatabasamu na kusema, “Samahani, ni usiku mkubwa. Nimekuja kumtazama mkuu, kuna machache ya kusema naye.”

“Siwezi nikakuruhusu kwa sasa. Njoo kesho asubuhi.”

“It’s urgent, please. In fact nimeagizwa na mkuu. Hatonielewa kama nikimwambia sijafanikiwa.”

Nesi akashusha pumzi na kuminya lips zake nyembamba. “Ok, ni muda mfupi nakupa.”

Hakujua amempatia kibali muuaji. Bwana yule akatabasamu na kwenda zake upesi akakamilishe kazi. Ila bahati isiwe kwake, hakuwa anajua wapi alipolazwa mlengwa wake. Hivyo ikamlazimu kupoteza kama dakika mbili kabla hajawa mbele ya mtu anayetakiwa kumuua.

Kabla hajafanya hilo, simu yake ikanguruma mfukoni. Akaitoa na kutazama, alikuwa ni mtu aliyemuagiza akafanye tukio. Akapokea na kumwambia kwa kunong’oneza, “I am in, wait.” kisha akakata simu.

Sasa ikawa imebakia kumaliza tu kazi, bwana Sheng akawe historia ya kale inayotisha.

Alikuwa amelala kitandani hajielewi hata linaloendelea. Dripu ilikuwa ipo kwa juu ikidondosha matone, na usoni alikuwa ana ‘nyago’ ya kumpatia hewa ya oksijeni. Mwili wake wote ulikuwa umefunikwa n shuka isipokuwa shemu yake ya kichwa na mikono tu.

Kando kando yake kulikulikuwa na vifaa kadhaa vinavyobeba uhai wake kwa ncha ya kidole. Na pia kulikuwa na kifaa kioo kionyesha maendelea ya mapigo yake ya moyo. Ama kwa hakika yalikuwa hafifu.

Bwana yule akaweka mikono yake shingoni mwa Sheng. Hajaminya, mara akasikia kipyenga cha ‘hafla, Prrrrriiiiiii!!!! prrrrrrrriiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii! Prrrrriiiiiiiiiii! Akatoa macho. Huko nje akasikia vishindo vya watu vikitesa ardhi!

Kwa muda kidogo akawa ametekwa na buwazo. Akimbie? Au amalize kazi yake? Alihisi kutetemeka. Kama angeendelea kumnyonga bwana Sheng, wazi ingelimchukua muda kidogo na yeye huo muda hakuwa nao. Basi afanye nini cha haraka kunusuru roho yake na huku atimize wajibu?

Akanyofoa waya za mashine zimsaidiazo mgonjwa, kisha upesi akatoka nje akikimbia. Kufika nje, akakutana na watu taribani kumi kwa idadi ya haraka. Wote wakiwa wamemnyooshea bunduki, akaamriwa anyanyue kwapa. Akatii.

Kule ndani nesi akawahi chumba cha mgonjwa. Huko akakuta ‘alarm’ zalia kwa fujo na mgonjwa akiishilia uhai. Haraka akarejesha mashine katika hali ya kawaida, na akaokoa maisha ya mkuu wake kwa ncha ya sindano. Mashine ya mapigo ya moyo ikaanza kusoma upya. Akatip! … akatip! … akatip! … akatip!

Mgonjwa akihema kwanguvu ndani ya kinyago.


***

Ngo! Ngo! Ngo! Bwana wa kichina alisikia hodi hiyo, ila akasita kwanza. Macho yalikuwa yamemtoka. Jasho jembamba lilikuwa lamchuruza. Na moyo wake ulikuwa unakita kwanguvu kubisha hodi mbavu.

Hodi ikarudiwa tena. Na hakuwa na namna ya ziada sasa zaidi ya kwenda kuiitikia. Akiwa na kibukta chake, na mwili unamtetemia, akajonga na kutengua kitasa. Nje akawaona wanaume wawili anaowatambua wakiwa wamepigishwa magoti, na wanaume wengine takribani kumi wakiwa wamewasimamia na bunduki.

“Walitaka kumuua mkuu Sheng!” shtaka likatolewa kwa sauti kuu. “Wamevamia hospitali na kuua walinzi wanne katika jaribio hilo!”

“Inawezekanaje jambo kama hilo?” akashangaa bwana huyu wa kichina, kisha akawatazama walengwa na kuwauliza kwa sauti ya ukali kidogo,

“Ni kweli yanayozungumzwa?”

Wale watu wawili wakamtazama. Na kwa soni, akaepusha macho yake kutazama kando.

“Mkuu, wanastahili kuuawa mara moja!” akasema mmoja wa wale mabwana waliowaleta wale mateka. Akaungwa mkono na wenzake wote. Ndio! Wanastahili kuuawa. Na hiyo ndiyo ilikuwa sheria. Hamna anayebakiziwa uhai akidiriki kufanya jaribio la kummaliza mkuu. Na adhabu yake yafanyika mbele ya umati.

Hata bwana huyu hakuweza kulikataa hili kwani litazua mjadala mkubwa na hata kumweka rehani. Basi akakbidhiwa bunduki kutimiza agizo. Bunduki ilikuwa na risasi kumi na nane.

Wakati hayo yote yanaendelea, Glady alikuwa anashuhudia kwa kupitia dirisha. Mambo haya yalikuwa yanamtisha mno. Ametoa macho na kinywa chake kipo wazi.

Risasi zikavuma mara mbili! Wale watu wakadondoka wafu. Wakabebwa na kwenda kuzika kana kwamba mizoga, na huku nyuma wakimwacha bwana yule wa kichina majuto na maumivu makubwa sana kifuani.

Aliingia ndani akamtaka Glady aondoke zake upesi. Na baada ya punde akakutana na jamaa wake mmoja mpangoni aliyebaki. Akiwa amekabwa na donge la uchungu kooni, akasema, “Mpango wetu ulikuwa wa kipumbavu na wenye papara. Sasa tumeshawapoteza wawili.”

Yule bwana akamuuliza, “Una mpango mwingine?”

“Pengine ninao,” akasema bwana huyu wa kichina. “Na sasa nitaufanikisha mwenyesha jua likiwa linawaka.”

Basi hawakuongea sana, jamaa yule akaendaze. Watakutana baadae.


***

Saa tatu asubuhi …


“Do we need to hold on more?” aliuliza Wales akimtazama Denmark. Wote walikuwa wameketi sebuleni, vichwani wa earphones zilizokuwa zinawaletea taarifa toka kwenye kifaa maalum kidogo walichomfungia Sheng. Na mpaka sasa kifaa hicho kiilikuwa kimeshawatanabahisha makazi aliyopo Sheng na hata sauti ya yale yanayozungumwa ndani ya duara la robo kilomita toka kila pande ya dunia ya mahali alipo Sheng. Tena kwa usikivu mzuri.

“No,” akajibu Denmark. “Perhaps we should wait a bit. It seems the are more and more to discover.”


***
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 58*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

“Do we need to hold on more?” aliuliza Wales akimtazama Denmark. Wote walikuwa wameketi sebuleni, vichwani wa earphones zilizokuwa zinawaletea taarifa toka kwenye kifaa maalum kidogo walichomfungia Sheng. Na mpaka sasa kifaa hicho kiilikuwa kimeshawatanabahisha makazi aliyopo Sheng na hata sauti ya yale yanayozungumwa ndani ya duara la robo kilomita toka kila pande ya dunia ya mahali alipo Sheng. Tena kwa usikivu mzuri.

“No,” akajibu Denmark. “Perhaps we should wait a bit. It seems the are more and more to discover.”

ENDELEA

Saa nane mchana.

Japo ilikuwa ni katikati ya siku, yaani mchana, jua halikuwa linaonekana na hali ya hewa ilikuwa ya abridi kana kwamba kuna mvua yaja muda si mrefu. Upepo ulikuwa unapuliza na angani hakukuwa kweupe ama kweusi sana, wastani.

Muda huu, ndani ya jengo ambalo ndilo makao makuu ya familia ya Wu kulikuwa ni kutulivu haswa. Si kwamba watu hawakuwa wanapita, lah! Watu walikuwa huku na kule, wanakatiza kutoka kushoto na kwenda kulia wakiwa wamevalia mavazi yao ya majoho rangi ya karoti,

Hata zaidi wakiteta, lakini kwa ukimya kiasi kwamba ni ngumu kujua kama hapa pana watu kama umefumba macho.

Katika utulivu huu, mara mtu mmoja anakuja kwa kasi akikimbia. Anasimama malangoni na kufungua, kisha anazama ndani upesi. Anaenda moja kwa moja kuonana na ‘master’ na kumweleza kuwa kuna jambo nje anapaswa kwenda kuliona.

Basi pasi na ajizi, master, tumtambue kwa jina hilo, anatoka akiongozana na kijana huyo mpaka nje. Huko wakitembea umbali mfupi, wanakutana na vijana wengine watatu wakiwa wamembelea mwanaume asiyejiweza.

Ni Lee. Master anamtambua. Kabla hajauliza nini kilichotokea, vijana wale wanasema wamemkuta akiwa njiani, amejilaza, hajiwezi. Mgongoni ana matundu mawili ya risasi na mwili wake umejawa majeraha.

Lee anapelekwa kwenye chumba fulani kidogo chenye uhaba wa mwanga, analazwa chini na kisha vijana wale wanaondoka wakimwacha master peke yake. Anawasha mishumaa, na kisha anaanza kuandaa madawa.

Anatwanga hiki. Anamiminia kile. Anachuma hiki. Anaweka pale. Anachanganya hili na lile na mara anapata uji mzito wa rangi ya kahawia. Anampakaa Lee shingoni, kisha anachukua pini kali ndefu, anamchanja na kutoa risasi mwilini.

Kwenye majeraha anatia majani fulani aliyoyaponda na kuyachanganya na unga alioutoa kwenye kibakuli fulani cha udongo juu ya shelfu. Baada ya hapo, anawasha moto kwenye vijiti viwili vyembamba na kisha anaviwacha ndani vikiwa vinafuka moshi mzito.

Anarejea mahali pake pa kazi na anaketi akitafakari kilichomsibu kijana yule, yaani Lee. Akatengeneza mawazo mengi sana kichwani ila akaona ni bora avute subira, alimradi amerejea salama, atapata tu kujua kilichotokea kwa kupitia kinywa cha mlengwa.


***


Saa kumi jioni, Hongkong …


Mlango wa kioo unafunguliwa na anazama ndani jibaba jeusi la miraba minne. Jibaba hili ndilo lile lililopewa kazi ya kumtafuta na kummaliza bwana Lee tangu kipindi kile alichoingia anga za wenyewe.

Anaketi kitini, kiti kinabonyea kidogo. Anasafisha koo lake na kumtazama mwanamke mrembo wa kizungu aliyekuwa mbele yake akitafuna ‘bubblegum’ kwa pozi za kike. Macho ya mwanamke huyu, ndani ya miwani kubwa nyeupe, yalimwangazia huyu mgeni na kumuuliza kwa sauti ya chini ila sikivu,

“Cany I help you, Rob?”

“Surely, you can. You know why I am here.”

Mwanamke huyu akapuliza puto na kulipasua, kiisha akaendelea kutafuna na sasa macho yake yakiangazia tarakilishi yake ya mezani.

“I don’t see any appointment here. Are you sure you’re supposed to be here at this time?”

“Yikes!” jibaba likalaumu. “Please can you do something? You know it gat to be serious issue for me to be here, ayt?”

Mwanamke yule akanyanyua simu yake na kupiga. Akaleza kuna mgeni papo. Basi alipoweka simu mezani akamtazama mgeni wake na kumpatia ishara ya kichwa. Jibaba akanyanyuka na kwenda zake ndani kukutana na bosi.

Bosi huyu alikuwa amevalia suruali ya kitambaa rangi ya bluu na kiatu cheusi safi. Hakuonekana kwa juu na hivyo basi tutamtambua kwa sauti yake nzito kwa sasa.

“I am done,” akasema yule jibaba.

“Sure?” bosi akauliza kwa sauti yake ya kukoroma.

“Sure. Now the document is within our hands and the man is down.”

“Perfect. One step at a time.”

“So what’s next?”

“Future is so exciting, Rob. Full of bloodshed. But now I can confidently declare the death of Wu family. Confidently. It’s just a matter of time.”

Rob akacheka.

“Let me see what I can do today,” akasema bosi na mara Rob akanyanyuka na kwenda zake.


***

Saa kumi na mbili jioni, nchini, kambi ya wachina.


Bwana yule wa kichina alirejeshea mlango wa maabara na kutengenezea suti yake vema. Akapiga hatua kubwa na dhahiri mgongoni akiwa amewekelea kitu fulani ambacho hakutaka kionekane.

Punde akawa ameshafika kwenye makazi yake na baada ya dakika kama kumi hivi, akatoka na kuelekea kule hospitali ya kambi kwenda kukutana na Sheng. Ulinzi ulikuwa umeimarishwa maradufu tofauti na hapo awali. Idadi ya walinzi ilikuwa imeongezeka, takribani kama watu kumi wakiongezwa lindoni.

Akakutana na daktari na kupewa ripoti ya maendeleo ya mgonjwa. Na baadae akapewa ruhusa ya kwenda kumwona mgonjwa. Fursa adhimu aliyokuwa anaitaka. Daktari alimsindikiza ila hakukaa ndani, akamwacha mgeni mwenyewe na mgonjwa.

Bado Sheng alikuwa kwenye hali ya kutojielewa. Ni mashine tu ndizo ambazo zilikuwa zimeshikilia uhai wake. Macho yake hayakuwa yamefumba vema, na alikuwa anahema kwanguvu.

Bwana yule wa kichina akatulia humo kwa kama dakika tano hivi kisha akachomoa sindano ndogo ndani ya mfuniko yenye kimiminika rangi ya manjano. Akatazama usalama. Akasogelea dripu, na kisha akadungia sindano ile ndani ya mfuko na kutikisa fuko hilo la dripu mpaka pale ambapo hali ya kimiminika ilirejea kwenye mazingiira yake ya awali.

Alafu akamwita daktari na kumwambia amemaliza haja yake.

“Anatia matumaini. Amenishika mkono japo hajasema jambo,” alisema bwana yule wa kichina akitabasamu. Hakukaa sana akaenda zake.

Usije dhani bwana huyu ni mjinga kujiweka rehani kiasi cha ‘kifala’. alikuwa anajua anachokifanya na anakijua fika.

Alipofika nyumbani, muda si mrefu akaja yule jamaa wake mmoja aliyebaki, akamweleza, “Nimeshakamilisha kazi. Sasa itachukua juma moja kwa Sheng kufa. Kuanzia sasa atakuwa anakufa taratibu taratibu.”

Yule jamaa mwingine akatabasamu na basi akampatia mwenzake mkono wa pongezi.


**

Saa tatu usiku …


“They have poisoned him,” alisema Scotland. Tayari wanaume hawa wa kizungu wakawa wameshalijua hilo kwa kupitia kifaa chao ambacho wamekipandikiza kwenye mwili wa Sheng.

Katika namna ya kitaalamu, baada ya mabadiliko kadhaa kutokea mwilini mwa mhusika, kifaa hicho kilitoa taarifa kwa waliokiweka.

“But why they did this?” akauliza Wales. “Why do they want to kill their master?”

“There’s something behind here,” akasema Denmark akikuna kidevu. Kwa sekunde kama mbili hivi wakatazamana. Ila punde wakasikia kitu nje. Wakapata shaka.

Walipokuja kutoka, wakagundua kulikuwa kuna mtu ndani ya eneo lao. Kwenye perving, kulikuwa kuna nyayo mbichi za viatu.



***
 
Back
Top Bottom