SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #3,561
*ANGA LA WASHENZI II --- 64*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Jona, akiwa amefinyanga macho yake, akamtazama Sheng. “Siwezi kumwacha huyu hai. Hana sababu yoyote ya mimi kumbakizia pumzi.”
Akamnyooshea bunduki, lakini Miranda akaishika bunduki hiyo na kusema, “Ngoja kwanza …”
ENDELEA
“Pengine kabla ya kumuua, tuntamhitaji,” akavuma mwanamke huyo. Watu wote wakamtazama lakini Jona ndiye akamuuliza, “Tutamhitaji kwa kitu gani na ilhali yupo huyu mwingine?”
Miranda akamnong’oneza Jona sikioni, na basi mwanaume huyo akaridhia kumbakiziauhai bwana Sheng, ambaye bado kiuhalisi hakuwa anaonekana kama mwenye matarijio ya kupona. Hata hapa wakati watu wanajadili juu ya uhai wake, yeye hakuwa anafahamu lolote lile.
Tendo pekee la uhai alilokuwa analifanya ni kuhema tu.
Basi Lee na Sheng wakakusanywa na kuingizwa ndani, Lee akahifadhiwa kwenye chumba cha peke yake, kwakuwa bado hakuwa anaaminika. Na Sheng akawekwa pia kwenye chumba chake. Bado usimamizi ukionyeshwa kwa kufungiwa mlango.
Sasa hapo vikawa vimebaki vyumba viwili tu ambavyo viliwapa mawazo wenyeji juu ya namna gani watalala kwa sasa.
Asubuhi ya saa tatu …
“Kinoo, inabidi uende town kuchukua double decker,”alisema Miranda. “Lakini pitia kwanza kwa Kilonzo, chukua pesa hapo. Usijali, ntamtaarifu akupatie.”
Kinoo akapokea maagizo hayo na kwenda zake. Angalau hivyo ndivyo namna walivyokuwa wanaendesha familia yao. Kwakuwa mirija yote ilikuwa imezibwa na hakukuwa na yeyote miongoni mwao ajihusishaye na shughuli rasmi, Miranda alikuwa akichakarika kufufua na kuendeleza vibiashara vyake vya hapa na pale.
Jambo hili lilikuwa linamkwaza sana Jona. Alitamani kusaidia lakini Miranda hakutaka kabisa hilo maana Jona bado hakuwa amesahaulika kwenye taswira za watu, tena kama muuaji wa kamanda wa polisi, na lile tukio lake la kutoroshwa toka kituoni.
Ilikuwa ni hatari kwake kwenda huko nje na kuzurura. Lakini mbali na yote hayo, bado Jona aliona anapaswa kuwa na cha kufanya kumsaidia mzigo wote ulioangukia kwenye mabega ya mwanamke huyu, japo kitu chenyewe hakuwa anakifahamu. Hakuwa anajua ajihusishe na nini awe salama na atoe mchango.
“Hey,” Miranda aliita kumng’oa Jona mawazoni. “Are you ok?”
“Yes, I am,” Jona akajibu akimtazama Miranda kwa tabasamu ambalo halikuwa laendana na macho yake.
“Sure?” Mirand akauliza.
“Yeah! No problem,” Jona akasema akitikisa kichwa. Walikuwa wenyewe sebuleni maana Kinoo aliongozana na Marwa kwenda huko kwa mtu ajulikanaye kama Kilonzo.
“You think about Sheng? … listen, its going to be alright. We need him at this time. Unahitaji antidote kumbuka. Na zaidi we can use him kama frontline wetu kukamilisha kazi. Don’t you think about that?”
Wakati Miranda anasema hivyo, alishika mikono ya Jona na kuiminyaminya. Alikuwa anamtazama Jona kwa macho yanayoongea, kwa macho yanayomaanisha akitamkacho.
“Naelewa,” Jona akajibu. “You don’t have to repeat that, Miranda. Thanks. I appreciate kila unachokifanya for me. Unajitolea sana. Nina deni kubwa sana kwako.”
“No no no. Hauna deni lolote kwangu. Jona, mpaka sasa tupo hapa ni kwasababu yako wewe. Umetupa tumaini na kitu cha kukipigania. Umetufanya tuwe tayari kufa lakini kwa heshima tukiacha historia kuwa tulipambania upande ulio mwema. We thank you for that.”
Basi wakakaa hapo na kuteta kwa kama nusu saa. Kinoo akapiga simu akiwa eneo la kununua kitanda, akamweleza Miranda kuwa kwa pesa waliyoipata kwa Kilonzo, basi aina ya kitanda wanachoweza kukipata si kile alichokuwa anatamania.
Hapo ikawa hamna namna, Miranda akamwambia achukue kilichopo, atajua nini cha kufanya. Alipokata simu, akamwambia Jona, “Inabidi niende.”
Akanyanyuka na kwenda chumbani. Baada ya muda kidogo, akatoka akiwa ameshajiandaa. Amevalia gauni lake matata likabalo kiuno na viatu vyake vya visigino virefu. Mkononi amebebelea pochi ndogo.
“Natoka kidogo. Nitarejea muda si mrefu sana.”
Jona akaitikia kwa kichwa, Miranda akaenda zake akimsindikiza kwa macho.
**
Saa tano asubuhi …
“Miranda, Miranda, ulikuwa wapi siku zote hizo? … ulinikimbia si ndio?”
“Hapana, mpenzi. Sikukumbia. Kwanini nifanye hivyo?” Miranda alijitetea kidhaifu akimtazama Boka usoni. Boka alikuwa ofisini kwake, ameketi kwenye kiti chake kikubwa akizunguka zunguka huku na kule. Amejaa.
“Hivi unajua hata kesi iliendaje, iliishaje?” Boka akamuuliza Miranda.
“Hapana, sijui. Lakini Boka, hatuna haja ya kuongelea yaliyopita tena mpenzi. Yashapita, right? Let’s focus kwa yajayo. Here I am.”
Boka akatabasamu. Akagongagonga kalamu yake mezani mulipojaa mafaili kadha kwa kadha na kusema, “Baba yako mzungu alikutorosha nchini?”
Miranda akatazama chini kwa sekunde tano pasipo kusema jambo. Aliporejesha uso wake juu, macho yalikuwa mekundu na punde yakaanza kumwaga chozi.
“Amefariki,” akasema kwa sauti ya chini. Boka akashikwa na huruma. Akakunja ndita zake kumtazama Miranda kwa pole.
“Amefariki lini na mbona hukunambia, Miranda?”
Basi hapo Miranda akapata upenyo wa kupenyesha ulaghai wake. Akamwambia Boka kuwa hata ukimya wake ulisababishwa na msiba huo. Ilimpasa aende Uingereza kinyume na masharti aliyopewa. Na hata aliporejea hakuwa sawa kabisa. Imemchukua muda kurejea halini.
“Pole sana, mpenzi. Sikuwa nafahamu yote hayo,” Boka alijinasibu. “Ila usijali. Mambo yako sawa sasa. Baada ya yule Kamanda aliyepita kufariki, huyu wa sasa ni rafiki yangu sana. Na hata ndiye yeye aliyefanya jitihada mimi kuwa huru. Kwahiyo hakuna tena haja ya kuhofia.”
Baada ya maongezi haya machache, Boka akafunga ofisi kwa muda na kutoka na Miranda kwenda mahali patakapowa- ‘refresh’. mahali tulivu watakapoweza kuongea kwa uhuru. Huko wakaongea sana, na mwishowe Boka akampatia Miranda pesa taslimu.
“Bado nia yangu ya kukuoa ipo palepale. Tafadhali utakapojihsi poa, tuonane.”
Miranda akaenda zake.
***
Saa kumi jioni …
“We are still looking for …” simu ikakata. “Shit!” Denmark akalalama. Akaweka simu chini na kuwatazama wenzake. “Boss is so mad!” akasema kwa ufupi kisha kukawa kimya kwa sekunde kadhaa. Ni wazi walikuwa katika hali ngumu. Lazima wampate na kummaliza Sheng ili kazi yao isemekane kumalizika.
Denmark akamtazama Wales na kumuuliza, “Anything?”
Wales alikuwa ni mtu ahusikaye na mitandao na mambo ya teknolojia. Ndiye yeye hata aliyehusika na kumpandikiza Sheng chip ndani ya mwili wake. Na kwa kutwa nzima, alikuwa bado anahangaika na tarakilishi yake kuona kama anaweza kupata namna ya kumpata Sheng.
“No,” akasema akitikisa kichwa. “Not yet. I think we should wait more.”
“No, Wales!” akafoka Denmark. “We have no time to waste more. We have limited days here, remember! You have to do something.”
“I do!” Wales akajibu. “I do it everytime. When I tell you to wait just wait because I am on to something. Can’t you see? I don’t just sit and do nothing.”
Basi maongezi haya y kutupiana mipira, yakaendelea mpaka pale majira ya saa moja usiku, ambapo Wales alikuja kutoa taarifa kuwa kuna jambo amelipata kwa kutumia ‘satellite’. Wenzake wote wakajongea na kumskiza.
“I think I’ve found him,” akasema kwa kujiamini.
“Sure?” Ireland akauliza akitoa macho.
“Yes, sure.”
Lakini kabla hajasema jambo hilo, simu ya Denmark ikaita. Kupokea akaambiwa sentensi moja,
“Kill the president before the next night.”
Na kisha simu ikakata. Kabla hajawaambia wenzake jambo, akapiga simu na kuuliza, “What about the chinese man?”
“Kill both of them. The president has already signed many Chinese huge contracts that we cant allow any of them to operate. It is very dangerous. So kill him.”
Simu ikakata tena. Denmark akafikisha taarifa hizo kwa wenzake. Bado wakiwa katika joto hilo, wakasikia sauti ya honi getini.
***
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Jona, akiwa amefinyanga macho yake, akamtazama Sheng. “Siwezi kumwacha huyu hai. Hana sababu yoyote ya mimi kumbakizia pumzi.”
Akamnyooshea bunduki, lakini Miranda akaishika bunduki hiyo na kusema, “Ngoja kwanza …”
ENDELEA
“Pengine kabla ya kumuua, tuntamhitaji,” akavuma mwanamke huyo. Watu wote wakamtazama lakini Jona ndiye akamuuliza, “Tutamhitaji kwa kitu gani na ilhali yupo huyu mwingine?”
Miranda akamnong’oneza Jona sikioni, na basi mwanaume huyo akaridhia kumbakiziauhai bwana Sheng, ambaye bado kiuhalisi hakuwa anaonekana kama mwenye matarijio ya kupona. Hata hapa wakati watu wanajadili juu ya uhai wake, yeye hakuwa anafahamu lolote lile.
Tendo pekee la uhai alilokuwa analifanya ni kuhema tu.
Basi Lee na Sheng wakakusanywa na kuingizwa ndani, Lee akahifadhiwa kwenye chumba cha peke yake, kwakuwa bado hakuwa anaaminika. Na Sheng akawekwa pia kwenye chumba chake. Bado usimamizi ukionyeshwa kwa kufungiwa mlango.
Sasa hapo vikawa vimebaki vyumba viwili tu ambavyo viliwapa mawazo wenyeji juu ya namna gani watalala kwa sasa.
Asubuhi ya saa tatu …
“Kinoo, inabidi uende town kuchukua double decker,”alisema Miranda. “Lakini pitia kwanza kwa Kilonzo, chukua pesa hapo. Usijali, ntamtaarifu akupatie.”
Kinoo akapokea maagizo hayo na kwenda zake. Angalau hivyo ndivyo namna walivyokuwa wanaendesha familia yao. Kwakuwa mirija yote ilikuwa imezibwa na hakukuwa na yeyote miongoni mwao ajihusishaye na shughuli rasmi, Miranda alikuwa akichakarika kufufua na kuendeleza vibiashara vyake vya hapa na pale.
Jambo hili lilikuwa linamkwaza sana Jona. Alitamani kusaidia lakini Miranda hakutaka kabisa hilo maana Jona bado hakuwa amesahaulika kwenye taswira za watu, tena kama muuaji wa kamanda wa polisi, na lile tukio lake la kutoroshwa toka kituoni.
Ilikuwa ni hatari kwake kwenda huko nje na kuzurura. Lakini mbali na yote hayo, bado Jona aliona anapaswa kuwa na cha kufanya kumsaidia mzigo wote ulioangukia kwenye mabega ya mwanamke huyu, japo kitu chenyewe hakuwa anakifahamu. Hakuwa anajua ajihusishe na nini awe salama na atoe mchango.
“Hey,” Miranda aliita kumng’oa Jona mawazoni. “Are you ok?”
“Yes, I am,” Jona akajibu akimtazama Miranda kwa tabasamu ambalo halikuwa laendana na macho yake.
“Sure?” Mirand akauliza.
“Yeah! No problem,” Jona akasema akitikisa kichwa. Walikuwa wenyewe sebuleni maana Kinoo aliongozana na Marwa kwenda huko kwa mtu ajulikanaye kama Kilonzo.
“You think about Sheng? … listen, its going to be alright. We need him at this time. Unahitaji antidote kumbuka. Na zaidi we can use him kama frontline wetu kukamilisha kazi. Don’t you think about that?”
Wakati Miranda anasema hivyo, alishika mikono ya Jona na kuiminyaminya. Alikuwa anamtazama Jona kwa macho yanayoongea, kwa macho yanayomaanisha akitamkacho.
“Naelewa,” Jona akajibu. “You don’t have to repeat that, Miranda. Thanks. I appreciate kila unachokifanya for me. Unajitolea sana. Nina deni kubwa sana kwako.”
“No no no. Hauna deni lolote kwangu. Jona, mpaka sasa tupo hapa ni kwasababu yako wewe. Umetupa tumaini na kitu cha kukipigania. Umetufanya tuwe tayari kufa lakini kwa heshima tukiacha historia kuwa tulipambania upande ulio mwema. We thank you for that.”
Basi wakakaa hapo na kuteta kwa kama nusu saa. Kinoo akapiga simu akiwa eneo la kununua kitanda, akamweleza Miranda kuwa kwa pesa waliyoipata kwa Kilonzo, basi aina ya kitanda wanachoweza kukipata si kile alichokuwa anatamania.
Hapo ikawa hamna namna, Miranda akamwambia achukue kilichopo, atajua nini cha kufanya. Alipokata simu, akamwambia Jona, “Inabidi niende.”
Akanyanyuka na kwenda chumbani. Baada ya muda kidogo, akatoka akiwa ameshajiandaa. Amevalia gauni lake matata likabalo kiuno na viatu vyake vya visigino virefu. Mkononi amebebelea pochi ndogo.
“Natoka kidogo. Nitarejea muda si mrefu sana.”
Jona akaitikia kwa kichwa, Miranda akaenda zake akimsindikiza kwa macho.
**
Saa tano asubuhi …
“Miranda, Miranda, ulikuwa wapi siku zote hizo? … ulinikimbia si ndio?”
“Hapana, mpenzi. Sikukumbia. Kwanini nifanye hivyo?” Miranda alijitetea kidhaifu akimtazama Boka usoni. Boka alikuwa ofisini kwake, ameketi kwenye kiti chake kikubwa akizunguka zunguka huku na kule. Amejaa.
“Hivi unajua hata kesi iliendaje, iliishaje?” Boka akamuuliza Miranda.
“Hapana, sijui. Lakini Boka, hatuna haja ya kuongelea yaliyopita tena mpenzi. Yashapita, right? Let’s focus kwa yajayo. Here I am.”
Boka akatabasamu. Akagongagonga kalamu yake mezani mulipojaa mafaili kadha kwa kadha na kusema, “Baba yako mzungu alikutorosha nchini?”
Miranda akatazama chini kwa sekunde tano pasipo kusema jambo. Aliporejesha uso wake juu, macho yalikuwa mekundu na punde yakaanza kumwaga chozi.
“Amefariki,” akasema kwa sauti ya chini. Boka akashikwa na huruma. Akakunja ndita zake kumtazama Miranda kwa pole.
“Amefariki lini na mbona hukunambia, Miranda?”
Basi hapo Miranda akapata upenyo wa kupenyesha ulaghai wake. Akamwambia Boka kuwa hata ukimya wake ulisababishwa na msiba huo. Ilimpasa aende Uingereza kinyume na masharti aliyopewa. Na hata aliporejea hakuwa sawa kabisa. Imemchukua muda kurejea halini.
“Pole sana, mpenzi. Sikuwa nafahamu yote hayo,” Boka alijinasibu. “Ila usijali. Mambo yako sawa sasa. Baada ya yule Kamanda aliyepita kufariki, huyu wa sasa ni rafiki yangu sana. Na hata ndiye yeye aliyefanya jitihada mimi kuwa huru. Kwahiyo hakuna tena haja ya kuhofia.”
Baada ya maongezi haya machache, Boka akafunga ofisi kwa muda na kutoka na Miranda kwenda mahali patakapowa- ‘refresh’. mahali tulivu watakapoweza kuongea kwa uhuru. Huko wakaongea sana, na mwishowe Boka akampatia Miranda pesa taslimu.
“Bado nia yangu ya kukuoa ipo palepale. Tafadhali utakapojihsi poa, tuonane.”
Miranda akaenda zake.
***
Saa kumi jioni …
“We are still looking for …” simu ikakata. “Shit!” Denmark akalalama. Akaweka simu chini na kuwatazama wenzake. “Boss is so mad!” akasema kwa ufupi kisha kukawa kimya kwa sekunde kadhaa. Ni wazi walikuwa katika hali ngumu. Lazima wampate na kummaliza Sheng ili kazi yao isemekane kumalizika.
Denmark akamtazama Wales na kumuuliza, “Anything?”
Wales alikuwa ni mtu ahusikaye na mitandao na mambo ya teknolojia. Ndiye yeye hata aliyehusika na kumpandikiza Sheng chip ndani ya mwili wake. Na kwa kutwa nzima, alikuwa bado anahangaika na tarakilishi yake kuona kama anaweza kupata namna ya kumpata Sheng.
“No,” akasema akitikisa kichwa. “Not yet. I think we should wait more.”
“No, Wales!” akafoka Denmark. “We have no time to waste more. We have limited days here, remember! You have to do something.”
“I do!” Wales akajibu. “I do it everytime. When I tell you to wait just wait because I am on to something. Can’t you see? I don’t just sit and do nothing.”
Basi maongezi haya y kutupiana mipira, yakaendelea mpaka pale majira ya saa moja usiku, ambapo Wales alikuja kutoa taarifa kuwa kuna jambo amelipata kwa kutumia ‘satellite’. Wenzake wote wakajongea na kumskiza.
“I think I’ve found him,” akasema kwa kujiamini.
“Sure?” Ireland akauliza akitoa macho.
“Yes, sure.”
Lakini kabla hajasema jambo hilo, simu ya Denmark ikaita. Kupokea akaambiwa sentensi moja,
“Kill the president before the next night.”
Na kisha simu ikakata. Kabla hajawaambia wenzake jambo, akapiga simu na kuuliza, “What about the chinese man?”
“Kill both of them. The president has already signed many Chinese huge contracts that we cant allow any of them to operate. It is very dangerous. So kill him.”
Simu ikakata tena. Denmark akafikisha taarifa hizo kwa wenzake. Bado wakiwa katika joto hilo, wakasikia sauti ya honi getini.
***