Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II --- 64*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Jona, akiwa amefinyanga macho yake, akamtazama Sheng. “Siwezi kumwacha huyu hai. Hana sababu yoyote ya mimi kumbakizia pumzi.”


Akamnyooshea bunduki, lakini Miranda akaishika bunduki hiyo na kusema, “Ngoja kwanza …”


ENDELEA


“Pengine kabla ya kumuua, tuntamhitaji,” akavuma mwanamke huyo. Watu wote wakamtazama lakini Jona ndiye akamuuliza, “Tutamhitaji kwa kitu gani na ilhali yupo huyu mwingine?”


Miranda akamnong’oneza Jona sikioni, na basi mwanaume huyo akaridhia kumbakiziauhai bwana Sheng, ambaye bado kiuhalisi hakuwa anaonekana kama mwenye matarijio ya kupona. Hata hapa wakati watu wanajadili juu ya uhai wake, yeye hakuwa anafahamu lolote lile.


Tendo pekee la uhai alilokuwa analifanya ni kuhema tu.


Basi Lee na Sheng wakakusanywa na kuingizwa ndani, Lee akahifadhiwa kwenye chumba cha peke yake, kwakuwa bado hakuwa anaaminika. Na Sheng akawekwa pia kwenye chumba chake. Bado usimamizi ukionyeshwa kwa kufungiwa mlango.


Sasa hapo vikawa vimebaki vyumba viwili tu ambavyo viliwapa mawazo wenyeji juu ya namna gani watalala kwa sasa.


Asubuhi ya saa tatu …


“Kinoo, inabidi uende town kuchukua double decker,”alisema Miranda. “Lakini pitia kwanza kwa Kilonzo, chukua pesa hapo. Usijali, ntamtaarifu akupatie.”


Kinoo akapokea maagizo hayo na kwenda zake. Angalau hivyo ndivyo namna walivyokuwa wanaendesha familia yao. Kwakuwa mirija yote ilikuwa imezibwa na hakukuwa na yeyote miongoni mwao ajihusishaye na shughuli rasmi, Miranda alikuwa akichakarika kufufua na kuendeleza vibiashara vyake vya hapa na pale.


Jambo hili lilikuwa linamkwaza sana Jona. Alitamani kusaidia lakini Miranda hakutaka kabisa hilo maana Jona bado hakuwa amesahaulika kwenye taswira za watu, tena kama muuaji wa kamanda wa polisi, na lile tukio lake la kutoroshwa toka kituoni.


Ilikuwa ni hatari kwake kwenda huko nje na kuzurura. Lakini mbali na yote hayo, bado Jona aliona anapaswa kuwa na cha kufanya kumsaidia mzigo wote ulioangukia kwenye mabega ya mwanamke huyu, japo kitu chenyewe hakuwa anakifahamu. Hakuwa anajua ajihusishe na nini awe salama na atoe mchango.


“Hey,” Miranda aliita kumng’oa Jona mawazoni. “Are you ok?”


“Yes, I am,” Jona akajibu akimtazama Miranda kwa tabasamu ambalo halikuwa laendana na macho yake.


“Sure?” Mirand akauliza.


“Yeah! No problem,” Jona akasema akitikisa kichwa. Walikuwa wenyewe sebuleni maana Kinoo aliongozana na Marwa kwenda huko kwa mtu ajulikanaye kama Kilonzo.


“You think about Sheng? … listen, its going to be alright. We need him at this time. Unahitaji antidote kumbuka. Na zaidi we can use him kama frontline wetu kukamilisha kazi. Don’t you think about that?”


Wakati Miranda anasema hivyo, alishika mikono ya Jona na kuiminyaminya. Alikuwa anamtazama Jona kwa macho yanayoongea, kwa macho yanayomaanisha akitamkacho.


“Naelewa,” Jona akajibu. “You don’t have to repeat that, Miranda. Thanks. I appreciate kila unachokifanya for me. Unajitolea sana. Nina deni kubwa sana kwako.”


“No no no. Hauna deni lolote kwangu. Jona, mpaka sasa tupo hapa ni kwasababu yako wewe. Umetupa tumaini na kitu cha kukipigania. Umetufanya tuwe tayari kufa lakini kwa heshima tukiacha historia kuwa tulipambania upande ulio mwema. We thank you for that.”


Basi wakakaa hapo na kuteta kwa kama nusu saa. Kinoo akapiga simu akiwa eneo la kununua kitanda, akamweleza Miranda kuwa kwa pesa waliyoipata kwa Kilonzo, basi aina ya kitanda wanachoweza kukipata si kile alichokuwa anatamania.


Hapo ikawa hamna namna, Miranda akamwambia achukue kilichopo, atajua nini cha kufanya. Alipokata simu, akamwambia Jona, “Inabidi niende.”


Akanyanyuka na kwenda chumbani. Baada ya muda kidogo, akatoka akiwa ameshajiandaa. Amevalia gauni lake matata likabalo kiuno na viatu vyake vya visigino virefu. Mkononi amebebelea pochi ndogo.


“Natoka kidogo. Nitarejea muda si mrefu sana.”


Jona akaitikia kwa kichwa, Miranda akaenda zake akimsindikiza kwa macho.



**


Saa tano asubuhi …



“Miranda, Miranda, ulikuwa wapi siku zote hizo? … ulinikimbia si ndio?”


“Hapana, mpenzi. Sikukumbia. Kwanini nifanye hivyo?” Miranda alijitetea kidhaifu akimtazama Boka usoni. Boka alikuwa ofisini kwake, ameketi kwenye kiti chake kikubwa akizunguka zunguka huku na kule. Amejaa.


“Hivi unajua hata kesi iliendaje, iliishaje?” Boka akamuuliza Miranda.


“Hapana, sijui. Lakini Boka, hatuna haja ya kuongelea yaliyopita tena mpenzi. Yashapita, right? Let’s focus kwa yajayo. Here I am.”


Boka akatabasamu. Akagongagonga kalamu yake mezani mulipojaa mafaili kadha kwa kadha na kusema, “Baba yako mzungu alikutorosha nchini?”


Miranda akatazama chini kwa sekunde tano pasipo kusema jambo. Aliporejesha uso wake juu, macho yalikuwa mekundu na punde yakaanza kumwaga chozi.


“Amefariki,” akasema kwa sauti ya chini. Boka akashikwa na huruma. Akakunja ndita zake kumtazama Miranda kwa pole.


“Amefariki lini na mbona hukunambia, Miranda?”


Basi hapo Miranda akapata upenyo wa kupenyesha ulaghai wake. Akamwambia Boka kuwa hata ukimya wake ulisababishwa na msiba huo. Ilimpasa aende Uingereza kinyume na masharti aliyopewa. Na hata aliporejea hakuwa sawa kabisa. Imemchukua muda kurejea halini.


“Pole sana, mpenzi. Sikuwa nafahamu yote hayo,” Boka alijinasibu. “Ila usijali. Mambo yako sawa sasa. Baada ya yule Kamanda aliyepita kufariki, huyu wa sasa ni rafiki yangu sana. Na hata ndiye yeye aliyefanya jitihada mimi kuwa huru. Kwahiyo hakuna tena haja ya kuhofia.”


Baada ya maongezi haya machache, Boka akafunga ofisi kwa muda na kutoka na Miranda kwenda mahali patakapowa- ‘refresh’. mahali tulivu watakapoweza kuongea kwa uhuru. Huko wakaongea sana, na mwishowe Boka akampatia Miranda pesa taslimu.


“Bado nia yangu ya kukuoa ipo palepale. Tafadhali utakapojihsi poa, tuonane.”


Miranda akaenda zake.



***


Saa kumi jioni …



“We are still looking for …” simu ikakata. “Shit!” Denmark akalalama. Akaweka simu chini na kuwatazama wenzake. “Boss is so mad!” akasema kwa ufupi kisha kukawa kimya kwa sekunde kadhaa. Ni wazi walikuwa katika hali ngumu. Lazima wampate na kummaliza Sheng ili kazi yao isemekane kumalizika.


Denmark akamtazama Wales na kumuuliza, “Anything?”


Wales alikuwa ni mtu ahusikaye na mitandao na mambo ya teknolojia. Ndiye yeye hata aliyehusika na kumpandikiza Sheng chip ndani ya mwili wake. Na kwa kutwa nzima, alikuwa bado anahangaika na tarakilishi yake kuona kama anaweza kupata namna ya kumpata Sheng.


“No,” akasema akitikisa kichwa. “Not yet. I think we should wait more.”


“No, Wales!” akafoka Denmark. “We have no time to waste more. We have limited days here, remember! You have to do something.”


“I do!” Wales akajibu. “I do it everytime. When I tell you to wait just wait because I am on to something. Can’t you see? I don’t just sit and do nothing.”


Basi maongezi haya y kutupiana mipira, yakaendelea mpaka pale majira ya saa moja usiku, ambapo Wales alikuja kutoa taarifa kuwa kuna jambo amelipata kwa kutumia ‘satellite’. Wenzake wote wakajongea na kumskiza.


“I think I’ve found him,” akasema kwa kujiamini.


“Sure?” Ireland akauliza akitoa macho.


“Yes, sure.”


Lakini kabla hajasema jambo hilo, simu ya Denmark ikaita. Kupokea akaambiwa sentensi moja,


“Kill the president before the next night.”


Na kisha simu ikakata. Kabla hajawaambia wenzake jambo, akapiga simu na kuuliza, “What about the chinese man?”


“Kill both of them. The president has already signed many Chinese huge contracts that we cant allow any of them to operate. It is very dangerous. So kill him.”


Simu ikakata tena. Denmark akafikisha taarifa hizo kwa wenzake. Bado wakiwa katika joto hilo, wakasikia sauti ya honi getini.



***
 
Shunie, njoo huku uondoe stress za ban, story ndio kwanza iko nusu.....
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 65*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Na kisha simu ikakata. Kabla hajawaambia wenzake jambo, akapiga simu na kuuliza, “What about the chinese man?”


“Kill both of them. The president has already signed many Chinese huge contracts that we cant allow any of them to operate. It is very dangerous. So kill him.”


Simu ikakata tena. Denmark akafikisha taarifa hizo kwa wenzake. Bado wakiwa katika joto hilo, wakasikia sauti ya honi getini.


ENDELEA


Basi kwa tahadhari kabla hawajakwenda huko getini, wakatazama taarifa za kamera kadhaa walizokuwa wamezipachika kwenye makazi yao. Na walipotazama wakapata kujua kuwa wageni waliopo getini ni polisi.


Wamekuja kufanyaje hapo? Ina maana walijua makazi yao? Hawakuwa na muda mrefu wakujipanga. Denmark akatoka ndani akiwa hajabebelea silaha yoyote. Wenzake wakabaki ndani kwa miadi ya kutazama kinachoendelea na kuchukua hatua pale watakapoona panastahili.


Geti likafunguliwa.


“You are under arrest!” akafoka polisi mmoja akimnyooshea Denmark bunduki. Akamwamuru mwanaume huyo aweke mikono yake kichwani na aongoze kwenda ndani kuwatoa wenzake.


Jumla ya polisi walikuwa sita. Wanne wamevalia sare zao na wawili wakiwa ndani ya mavazi ya kiraia. Basi wakaongozana na Denmark na kuzama naye mpaka ndani. Lakini kabla hawajafanya ukaguzi wao, Denmark akataka kwanza kujua nini kinaendelea kama moja ya haki ya mtuhumiwa.


“You are the suspect of murder of two policemen,” polisi mmoja akaeleza.


“Me?” Denmark akatahamaki. “Ok, may I contact my lawyer, please?”


“After issue us your all valid documents of being here and bring us all of your mates here,” polisi akatoa sharti. Denmark akamtazama pasipo kusema jambo, kisha akaomba ruhusa ya kwenda ndani kuleta vitu vinavyohitajika.


Hapo akakabidhiwa polisi wawili wa kumsindikiza. Sebuleni wakabakia polisi wawili, na kule nje wakiwa wawili wengine. Baada ya muda, Denmark akarudi akiwa amebebelea nyaraka zake, ila wenzake hawakuwapo hapo.


“Where are your mates?” akauliza polisi.


“They are out,” akajibu Denmark. Basi polisi huyo amuulizaye maswali, akawaamuru polisi wale waliomsindikiza bwana Denmark kwa mara ya kwanza, wafanye upekuzi wa nyumba nzima. Agizo likaanza kutekelezeka.


Wakazama vyumbani na kupekuapekuwa huku na kule. Chini na juu. Mikononi mwao wakiwa wamebebelea silaha za moto.


Baada ya muda mdogo, polisi mmoja aliyekuwa anafanya upekuzi akagundua jambo lililomshtua. Alipotazama dirishani kule nje, aliona miili miwili ikiwa imelala chini. Akatahamaki.


Kutazama vema akagundua miili hiyo ilikuwa ni ya wenzao wawili ambao walikuwa wamekaa nje. Akahisi kusisimka. Vinyweleo vikasimama na macho yakamtoka. Wameuawa!


Basi kugeuka aende kutoa taarifa, akakutana uso kwa uso na Ireland. Kabla hajavuta pumzi, akawa ameshambuliwa na kulazwa chini mfu. Ireland akakwapua silaha yake.


Yule polisi mwingine wa pili, akiwa huko chumba kingine, akiwa hana hili wala lile, hajui liendealo. Akaendelea kupekua na kupekua. Kuja kutahamaki amezibwa mdomo. Akafurukuta. Mara akakitwa na kitu kichwani, akadondoka kama mzigo.


Sasa polisi wanne wakawa wapo chini. Walibakia polisi wawili tu ambao wapo sebuleni.


Kwakuwa muda ulikuwa umeenda na wale walioagizwa hawakurejesha taarifa, basi yule polisi, ambaye alionekana ni mkubwa kuliko wenzake kwa cheo, akamtazama polisi aliyekuwa naye hapo sebuleni na kumpatia ishara ya kichwa kuelekea chumbani.


Yule mwenzake pasipo kusita akaenda huko asijue aenda kujitoa uhai. Alipopotelea huko, akapotelea kweli. Sasa Denmark akabaki na yule mmoja pale sebuleni. Muda ukaenda. Akaanza kutabasamu.


Polisi yule akatia shaka. Na muda si mrefu akapewa sababu ya kuhofia zaidi baada ya washirika wote wa Denmark kutoka chumbani, yaani Ireland, Sweden na Wales.


“Would you mind putting your gun down, officer?” akasema Denmark. Polisi akagoma kutii hilo agizo. Akiwa aliyeshikwa na woga, akasonga nyuma mpaka dirishani. Akafungua dirisha na kuchungulia upesi. Akaona wenzake wakiwa chini. Wamekufa!


Mikono yake ikaanza kutetemeka. Na mate yakawa magumu kumezeka. Alikuwa hana ujanja tena, alikuwa hana cha kufanya. Risasi zake kadhaa ndani ya bunduki zisingeweza kumwokoa dhidi ya wadhalimu wale.



***



Usiku wa saa mbili …


“Wameondoka,” alisema Marwa akimtazama Jona. Mwanaume huyo alikuwa ametoka kutazamia kwenye tarakilishi yake kufuatia vifaa walivyoviweka kule kwa wale wazungu.


“Na wale polisi je?” Jona akauliza.


“Sijajua nini kimewakumba,” akasema Marwa. “Gari lao halijatoka. Limebakia ndani.”


Ndani ya nusu saa, Jona na Kinoo wakawa wamefika kwenye eneo husika. Jona akamwambia Kinoo atulie nje kusoma ramani, yeye atazama ndani. Basi akaingia na kupembua. Akakuta maiti za wale polisi, nje, sebuleni na vyumbani. Akapiga picha za maiti hizo na kisha akamtumia Marwa kwa kupitia mtandao, alafu akamtumia ujumbe kumuuliza,


“Watakuwa wameenda wapi?”


Akiwa anangoja majibu, akatoka ndani ya nyumba hiyo na kwendaze mbali pamoja na Kinoo. Muda kidogo ujumbe ukaingia toka kwa Marwa, “Wapo karibu na sisi!”


“Karibu na wakina nani?” Jona akauliza. Punde ujumbe ukaingia toka kwa Marwa ukisema, “Naona kama wanajongea kuja kwenye makazi yetu!”


“Serious, Marwa?”


“Yes. I think they are coming!”


Yote aliyokuwa anayaongea Marwa hayakuwa ya kutilia shaka kwani gari walitumialo wazungu wale lilikuwa limepachikwa kifaa tambuzi cha GPS hivyo wakijua mwenendo wake. Zoezi la upachikaji wa kifaa hicho lilifanywa na Jona kipindi kile almanusura kukamatwa.


Sasa hapa kwenye kioo cha tarakilishi ya Marwa, ‘GPS tracker’ ilikuwa inaonyesha gari hilo likisonga kuja walipo. Na kasi yake ilikuwa kubwa ajabu!


“Kinoo, we have to go! Haraka!” Jona akabwatuka kisha upesi wakaanza kukimbia kufuata chombo chao cha usafiri. Walipokwea, wakatimka upesi, Jona akikamata usukani.


Alikimbiza gari kwa kasi mno. Macho yake yalituama barabarani, mikono yake ilikamatia usukani kwanguvu na miguu yake ikikanyagia mafuta na breki kwa zamu.


“Call Miranda!” Jona akamwagiza Kinoo. Kinoo akafanya hilo jambo upesi. Simu ikaita mara moja na mara ikapokelewa, ikawekwa ‘loudspeaker’.


“Miranda!” Jona akaita. “Ondokeni hapo nyumbani upesi!”


“Hatuwezi!” Miranda akajibu. “Hatuwezi kuondoka kwa sasa, it’s too late! Wameshawasili. Yatupasa kupambana nao.”


“Hamuwezi kupambana mkiwa wawili, hamtaweza kuwamudu. Just escape!” Jona akazidi kusisitiza akitamani gari igeuke kuwa ndege ya kivita.


“No, Jona. Hatuna namna! Huwezi jua huko nje ni hatari kuliko humu ndani. Vipi kama wata ….” simu ikakata.


“Miranda! Miranda!” Jona akaita. “Piga tena!” akamwamuru Kinoo. Simu ikaita tena, haikupokelewa. Walipopiga kwa mara nyingine, ikawa haipatikani. Jona akazidi kuchanganyikiwa. Aliamini Miranda na Marwa wasingeweza kuwazuia watu wale, tena wanne na waliokubuhu kwenye sekta ya mauaji.


Kwake ikawa mtihani mkubwa. Na hata akajuta kwanini alitoka kwenda kule kwenye makazi ya wale wazungu. Ubaya zaidi ni kwamba hakuweza kutoa taarifa hizo polisi. Katika vita hii walikuwa wenyewe tu.



***



“Let’s spread!” akasema Denmark, kisha akamalizia, “Show them no mercy!”


Basi wanaume watatu, Ireland, Wales na Sweden wakagawanyika kuizingira nyumba ya wakina Miranda. Wakati huo wakiwa tayari wameshajivika nguo zao za kazi.


Punde kidogo, umeme ukakatika katika nyumba hiyo na kuwa kiza totoro isijulikane mlango na dirisha lipo wapi. Hapa sasa wale ‘the intellectual instinct’ wakawa wanaona kana kwamba mchana mkavu wa saa nane.


Hakuna huruma. Hakuna mtu yeyote kutoka na uhai.



***


WAZUNGU HAWA WALIJUAJE MAKAZI YA WAKINA JONA?


NINI KITAJIRI HAPA?
 
Sijui Miranda na Jonah wata-----sema hiii story unaweza shangaa demu wa Jonaa anatokea season 5 hukooo haitabiriki kabisa,,, well Dan Mr Steve
 
Back
Top Bottom