Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II --- 68*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


“Kuna jambo unatakiwa kuona. Upesi!” Marwa akasisitiza na kisha wakaongozana mpaka sebuleni. Jona akakalia kiti na kutazama tarakilishi. Lakini kabla hajaona kitu, Marwa akasema:


“Wapo karibu na Ikulu. Nadhani ….”


“Watakuwa wameenda kumuua Raisi?” Jona akakatiza kwa tahamaki.


ENDELEA


Saa moja na robo usiku, Ikulu.



Walinzi lukuki walikuwa wamesimama kwa nje na hata kutembea ndani. Wengi wao walikuwa wamevalia kaunda suti na kuna baadhi wamevalia sare za jeshi. Watu hao walikuwa na silaha mikononi, japo si wote. Na wale waliovalia kaunda suti walikuwa wana vifaa vya mawasiliano vimepachikwa masikioni.


Mbali na walinzi hao kulikuwa na kamera za ulinzi hapa na pale. Kulionekana kunalindwa haswa. Sidhani kama kunahaja ya kueleza sana namna mahali akaapo Raisi panavyolindwa.


Kulikuwa kumetulia haswa. Na pengine unaweza kusema kuwa mahali hapa ndipo salama kuliko mahali pengine popote nchini. Huenda ikawa kweli, lakini pia yaweza kuwa sio sahihi. Kuna muda yule asiyelindwa ndiye yupo salama zaidi kuliko yule alindwaye. Masikini hulala milango wazi na wakati wale walio juu wakilindwa na binadamu na teknolojia za hali ya juu!


Basi, huwezi amini katika rundo hili la walinzi, watu huthubutu kuja kupavamia. Tena wakiwa wanne tu! Ilikuwa ni ajabu na kweli. Na watu hao wasiwe wajinga kubeba hatari kama hiyo, walikuwa wamejikamilisha ipasavyo.


Masaa kabla ya tukio hili walikuwa wameshatumiwa taarifa zote wanazotakiwa kuzijua kuhusu eneo hili kwa kukusanya taarifa toka kwenye mfumo wa satelaiti. Pili, watu kadhaa washawahi kuja kutembelea eneo hili la Ikulu, si kila mtu ni mwema.


Hukusanya taarifa kidogo kidogo, pengine zinaweza zikawa kidogo, lakini nini hutokea pale kidogo na kidogo huungana? Na tatu, watu hawa kabla hawajavamia hapa, waliitumia vema pwani ipakanayo na jengo vamiwa kutimiza haja zao.


Lakini mbali na yote hayo, kuna kosa moja tu walikuwa wamelifanya. Lipi hilo?


Taratibu taratibu walinzi wakawa wanapunguzwa. Wanadondoshwa chini na kufichwa. Ni kama vile mchezo wa kuigiza uonavyo kwenye televisheni. Wavamizi hawa walikuwa wanafanya mambo yao kwa ustadi wa hali ya juu na pasipo kupoteza muda kwa aina yoyote ile.


Kila kitu kwenye mahesabu. Hata hatua wapigazo. Walitakiwa kuwa humo eneoni pasipo kuzidi dakika arobaini na tano! Na katika hizo, nusu saa pasipo kufahamika kama wapo humo.


Walifanikiwa sana kutimiza hilo. Mpaka dakika ya kumi na mbili hakuna aliyekuwa anafahamu kama nyumba ya Raisi ipo chini ya uvamizi. Na pale ilipogundulikana ikawa hivi …


Mwanaume mmoja, afisa usalama, mweusi mwenye mwili mrefu kakamavu, alisikia sauti za ajabu za wanyama waliomo ndani ya eneo. Akapata hamu kutazama kama moja ya jukumu lake. Aliposonga, akafanikiwa kuona mguu wa mtu ukiwa chini.


Basi haraka akapaza sauti yake kwenye kifaa kutoa taarifa ya tahadhari. Alipofanya hivyo hakungoja majibu, akasonga kuufuata ule mguu, akagundua kuna mwili wa mwenzake umelala hapo pasi na fahamu!


Alikuwa tayari amesachomoa bunduki yake. Akakimbia ila hakufika mbali akakutana na mvamizi aliyevalia barakoa. Mvamizi huyo hakuwa na kitu mkononi isipokuwa glovu zake nyeusi. Macho yake alikuwa ameyafunika na miwani yenye mshikio wa mpira na mgongoni ana begi.


“Weka mikono juu!” afisa akamwamuru kisha akateta na kifaa chake cha mawasiliano, “Nimemkamata mmoja wao! … nimemkamata mmoja wao!”


Alipomalizia kauli hiyo, akastaajabu kukitwa na kitu kichwani. Akadondoka hoi hajiwezi hata ukucha. Lakini je vipi kuhusu taarifa yake aliyoitoa kwa wenzake?


Habari mbaya ni kuwa, hakuna taarifa yoyote ile iliyokuwa inaenda wala kufika kwa yeyote yule! Kabla ya wavamizi hawa kufanya kazi yao, walishahakisha hilo jambo la mawasiliano ya walinzi linapatiwa ufumbuzi. Walipachika vifaa vinne vyeusi, ukubwa wa tofali la kuchoma, kwenye pande nne za dunia zizungukazo Ikulu.


Wakazipanga vema kwa kuzificha alafu wakaziwasha wakiwa tayari wameingia eneoni. Vifaa hivyo vilikuwa vinazalisha nishati kali sana mithili ya ‘radioactive’ ambayo ilikuwa na uwezo wa kupumbazisha ama kuchelewesha jitahada za mwasiliano ndani ya eneo husika.


Na kutokana na kuzalisha nishati hiyo kali, haikuweza kudumu kwa muda mrefu. Hukaa kwa nusu saa tu kabla ya kuzima na kufanya mawasiliano kurudi kwenye hali yake ya awali baada ya dakika tano.


Basi dakika zikaendelea kuyoyoma na kuyoyoma. Na sasa zikiwa zimebakia dakika mbili tu kwa vile vifaa vya mawasiliano kuzima lakini bado haja ya tukio ikiwa bado haijamalizika.


“We have a few minutes!” alitoa tahadhari mmoja wao. Walikuwa wameshashika korido wakielekea chumba walichoamini watamkuta mlengwa wao.


Mara ghafla mbele wakatokea wanaume wawili walinzi, afisa wa usalama. Katika hali hiyo hiyo ya ghafla, mmoja wa wavamizi akachojoa visu vitatu nyuma ya mgongo wake na akavitupa kwa utaalamu wa hali ya juu, vikawakita wale walinzi na kuwadondosha chini.


Haraka wakajongea chumba wakihisicho ndicho chenyewe, kufungua hawakukuta mtu!


Ti ti ti ti ti ti! ‘Alarm’ ikalia kutaarifu vifaa vya kuminya taarifa vimezima! Hivyo basi wakawa na dakika tano tu za kutoka na kutokomea hapo kabla ujumbe wa uvamizi haujawafikia wahusika, aidha kwa mfumo sauti au mfumo picha wa kamera za CCTV.


“We have to go!” mmoja akasisitizia.


“No! We aren’t going anywhere till we finish this!” sauti nyingine ikasema ikiwa na mamlaka ndani yake. Ilikuwa ni sauti ya Denmark.


“He is not here!” sauti nyingine ikatahadharisha. “Just let’s go!”


“He must be here,” Denmark akafoka. “Its whether we get him or we die in here! Let’s search!”


Kiongozi alishasema, hakukuwa na kupinga. Agizo likabebwa na utekelezaji ukaanza mara moja. Wanaume hao wakaanza kupekua huku na kule.


Na hilo ndilo lilikuwa kosa lao kubwa, hawakuwa wanajua haswa Raisi yupo wapi. Taarifa ya kuwa yupo Dar es salaam haikutosha kudhihirisha kuwa atakuwa Ikulu.


Dakika tano zikapita. Mawasiliano yakaanza kurejea. Maafisa wa usalama waliomo ndani ya jengo wakaanza kupata taarifa kadha wa kadha. Japo zilikuja kwa kasi, walitambua kuwa hali si shwari. Na wale wanaohusika na kuendesha mitambo ya CCTV wakaanza kuona taswira mbalimbali viooni.


Sasa taarifa rasmi ikawa wazi kuwa ngome ipo chini ya uvamizi!


Katikati ya taharuki hiyo, king’ora kikasikika kikilia. King’ora hicho kilifika kwenye sikio la kila mtu aliyekuwapo mule ndani ya jengo. Na hali isiwe tenge, king’ora hicho ndiyo kikazidi kuwatia watu vimuhemuhe kupita kiasi kwani kilimaanisha Raisi alikuwa anarejea jengoni.


Kwenye jengo ambalo lilikuwa na wavamizi!


Basi taarifa zikazuka, na Afisa aliyekuwa anahusika na Ulinzi jumla wa Ikulu, bwana Kulanga Hassan, akawapasha wale maafisa wanaokuja na Raisi ya kuwa wasitishe zoezi lao haraka mno na Raisi apewe ulinzi maradufu maana wapo chini ya uvamizi.


Na wakati wao wakifanya maamuzi hayo, wale mabwana wavamizi, wakaona sasa hiyo ndiyo ilikuwa nafasi adhimu ya wao kumaliza kazi. Ilikuwa ni lazima Raisi auawe! Sasa wameshapata uhakika kuwa yupo ndani ya eneo la karibu.


“Mwingize Raisi ndani … narudia, mwingize Raisi ndani. Huko nje si salama. Fanya hivyo haraka iwezekanavyo!” amri ilisikika kwenye masikio ya maafisa waliomo msafarani.


Na punde baada yake, afisa aliyeitoa amri hiyo akavunjwa shingo na wavamizi baada ya kazi yake kuisha. Basi mara punde, gari limbebealo Raisi likiwa limeongozana na magari mengine, likazama ndani.


“Niliwaambia msimwingize ndani!” bwana Kulanga akafoka. “Ndani tumevamiwa, narudia ndani tumevamiwa!”


Ilikuwa ‘too late’ wanasema wazungu. Raisi alikuwa ameshazama eneoni. Kitendo tu cha bwana Kulanga kumaliza kuongea, umeme ukakatika! Eneo lote likawa giza kana kwamba ni chini ya handaki.


Hapa sasa wale wavamizi wakawa mithili ya majini!




****
 
A away a as easyaààààsaaaasasysa seasaAa@a££aaaaaàasya££Ππàsyyysyaasaaπ£a£ÀASaaaaaπ£3@6@@Sousa'saA aasaaa wswsww wws wwwaww s statwsawe a a was ßsa££@@6@@6@6@@@6@a@9opk,ydjkklwaszààaywwasw saesesaaaaàay6syßy s@Saaa@ayá@a@a art sww aày6way s a awaAYsh aylll ßayaysyasaaaaaaa
Utamu umekatikia pabaya
 
Back
Top Bottom