Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

samahani hili swali langu au la Steve??? Maana mi nilikoment kule kama kuna MTU au watu wanaweza kui endeleza wajitokeze kama kuna memba anamawasiliano Na familia tushauriane humu tufanye Jambo jema kumuenzi ibra
La kwako......
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 75*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Lakini pia kwa wakati huohuo, kuitikia wito wa Wales, Underground office kule Uingereza ilikuwa imeshatuma watu wake kadhaa kwa ajili ya kwenda kumsaidiza Wales kumaliza kazi. Hivyo lilikuwa ni swala la muda tu kwa watu hawa kukutana na kuonyeshana ubabe.


Kisiwa hiki kilikuwa kinaenda kumezwa na damu.


ENDELEA


Basi kufikia usiku kukawa bado kimya kisiwani. Hakukuwa na tabu wala shaka sana, Wales hakuwa amekutana wala kuonana na wakina Jona, na hii ilikuwa ni kwasababu hawakutafutana. Baada ya kupungukiwa na mtu, Wales aliona afanye stara kungoja, na kwa wakati huohuo wakina Jona wakiwa wamejihifadhi ndani ya giza.


Usiku ukakomaa zaidi na zaidi. Kwenye majira ya saa saba hivi usiku, makomandoo wa kitanzania wakawa wa kwanza kuwasili karibu na eneo la tukio. Wanaume hao walitua ndani ya maji na kisha kupiga mbizi mpaka kwenye kisiwa.


Kulikuwa ni baridi sana na upepo ulikuwa unapuliza sana. Ila kwa makomandoo hawa halikuwa shida hata kdogo. Walikuwa ni watu walofundwa kuishi mahali mbalimbali na kukabiliana na hali mbalimbali. Kuitwa jina la komando halikuwa jambo la lelemama. Ni kuzoeza mwili na patashika na kila shurba za dunia.


Wanaume hao ‘walipotimba’ hapo kisiwani wakatulia na kujadili kwa muda kidogo. Hawakuwa wanafahamu kama hapa palikuwa pana watu, dhumuni kubwa haswa ni kuangazia upande upi wa dunia ambapo ndege hiyo ilikuwa imeangukia ama kupotelea.


Basi baada ya muda wakawasiliana na makaoni na kuwataarifu wapo juu ya ardhi kavu ndani ya bahari iliyosolemba. Kule makaoni walipozama kwenye ramani ya dunia iliyopo kwenye vifaa vya elektroniki, wakabaini eneo walilopo. Na hata walipo ‘trace’ ile ndege, wakabaini kuwa ukanda ule ndiyo ambapo ndege ilikuwa imepotelea kwenye rada.


Kwa taarifa hizo, makomando wakaona ni vema basi vifaa viwahishwe ili wapate kuwandawanda kwenye bahari kuangaza. Vifaa hivyo vikahaidiwa kufika haraka iwezekanavyo.


Mawasiliano yalipokata, wanaume hao wakaona wasipoteze muda, kwa wakati huo ambapo hawawezi kutanga baharini, basi wahakikishe pia na pale kisiwani ni mahali salama. Kwakuwa ndiyo ardhi pekee ipatikanayo karibu na ukanda wa kupotea kwa ndege, huenda ikawa na watu ambao wanawatafuta ama wanahitaji msaada.


Huenda.


Basi wakaanza kuzama ndani, mikononi mwao wakiwa wamebebelea silaha na macho yao yakiangaza dhidi ya msitu. Giza lilikuwa kubwa. Waliwasha kurunzi nzao na kuendelea na kazi. Wakatembea kwa umbali mrefu, kisiwa kilikuwa kipana. Wakiwa wanatembea, mtu wa kwanza kuwatia machoni akawa ni Wales.


Mwanaume huyo aliyekuwa amejibana nyuma ya mti, aliwatazama vema kuwang’amua kuwa wale hawakuwa watu wake, yaani wale ambao alikuwa amewaomba waje kumsaidia. Akapata mawazo, ina maana maadui zao, yaani wakina Jona, na wao watakuwa wamewatuma watu wa kuja kuwasaidia?


Basi akaona ni vema kama akiwatia watu wale machoni muda wote ili ajue nini watakuwa wanapanga na vilevile iwe rahisi endapo watu wake wakifika awapashe habari eneo ambapo walengwa wake wanapatikana.


Sasa akawa anawafuatilia, taratibu akihama toka kwenye mti mmoja kwenda mti mwingine. Kwa hali ya utulivu kabisa na kwa tahadhari. Basi wakaenda kwa kama dakika tano, ila ikafikia muda mmoja wa wale makomandoo akahisi kuna kitu.


Alisikia kitu kikitembea na si mara moja, zaidi ya mara tatu. Basi akiwa hajawaambia wenzake, akaanza kutilia maanani yale alokuwa anayasikia. Muda si mrefu, akagundua kuna mtu.


Hakutaka kuwashtua wenzake na pia hakutaka kuanza kumwaga risasi kwanza kabla hajajiridhisha. Akapaza sauti, “wewe nani? Jitokeze!”


Ila mtu yule, ambaye alikuwa ni Wales, akanyuti nyuma ya mti akiwa ametulia. Na sasa kutokana na sauti ile ya maulizo, makomandoo wengine wote wakawa nao wameelekezea nyuso na hata silaha zao huko.


“Kuna mtu,” akasema yule komando aliyemwona Wales. Macho yao yaliganda eneo la tukio na wakiwa tayari kwa ajili ya lolote lile litakalojiri, aidha mtu huyo awe rafiki ama adui.


Kwa wakati huo Wales akawa anawaza namna ya kufanya. Kama akikimbia, basi risasi zitatupwa kwa wingi kumfuata. Lakini pia kama akiendelea kukaa hapo, ni wazi wale watu watajongea kumfuata.


Kichwa chake kikawa kimetingwa. Macho yake yakawa yanaangaza huku na kule kukimbizana na muda apate fursa ya kuokoa maisha yake. Hali ilikuwa tete.


Baada ya sekunde kadhaa za ukimya, Wales akiwa bado hajafanya maamuzi, makomandoo wakaanza kujongea kuufuata mti alipojifichia. Kurunzi zao zilimulika hapo kuhakikisha hawapitwi na kitu. Miguu yao iliyovekwa buti kubwa ikawa inajongea ikipiga hatua kubwa na kwa upole.


Bado Wales akawa amekwama hajui la kufanya. Alihema kwa sauti ya chini ila upesi upesi. Akashikilia bunduki yake vema na kuamua kupigania maisha yake kwa kupambana na maadui uso kwa uso. Hakukuwa na namna sasa.


Basi ikiwa imebakia hatua kama sita tu kufikiwa, mara sauti kubwa ikasikika tokea baharini. Ilikuwa ni sauti ya boti lililokuwa linaendeshwa kwa kasi. Makomandoo wale wakasita na kutazamana kwa namna ya maswali.


Kama haitoshi wakasikia na sauti kadhaa za watu wakizungumza. Usiku ulikuwa mtulivu hivyo basi sauti ilikuwa inavuma katika namna ya kusikika pasipo tabu, ukijumuisha na upepo wa bahari.


Sauti hizo zilizokuwa zinavuma zilikuwa si za kiswahili bali za kiingereza hivyo basi zikazalisha shaka kwa wale makomandoo kwamba huenda hao watu wakawa ni miongoni mwa maadui walioshiriki na mpango wa kummaliza Raisi.


Basi kitendo hicho cha kuzubaa, kikampatia mwanya bwana Wales. Akachoropoka upesi baada ya kujitupia kwa samasoti mbugani, na kwa upesi akaanza kukimbia akikakatiza mitini.


“Ni mzungu!” akasema Komandoo mmoja aliyekuwa amebebelea kurunzi, kisha akaongezea, “Amevalia nguo za rubani!”


Basi hapa wakawa na uhakika kuwa bwana huyu ni mmoja wa maadui wanaowatafuta, wakaanza kumrushia risasi pasi na kifani na hata kumkimbiza kwa kasi.


Bwana Wales akakimbia mno akikatiza hapa na pale. Nyuma yake vyuma vya risasi vilikuwa vinapiga na kutoboa ama kuchana miti. Aliinamishia chini kichwa chake na kunyoosha mapaja haswa.


Akaruka kuvuka matawi, majani na hata visiki. Muda mwngine kurunzi ya wanaomkimbiza ilikuwa inamsaidia juu ya wapi apite na kukanyaga. Akakimbia kwa kama dakika moja kabla hajachomoa chombo chake cha mawasiliano na kuanza kuwaelekeza watu waliokuja kumsaidia wafuate milio ya bunduki.


Akiwa anatoa maelekezo hayo, akastaajabu kadunguliwa bega lake la kushoto. Akalalama kwa maumivu makali, ila hakusimama. Akaendelea kukimbia kwa kasi, akivuka, akipambana, akikumbatiana na miti na matawi yake.


Mara akadondoka chini! Kama kheri alipodondokea palikuwa na korongo la wanda wa majani, akabiringita kama tairi na kwenda kujikuta chini akiangukia bega lililoumia. Akasaga meno kwa maumivu makali mno. Kabla hakanyanyuka, akasikia, “Yule kule chini!”


Mara risasi tena zikaanza kumwagwa. Mojawapo ikamtoboa mguu wake wa kulia, hivyo hata alipoamka, akajikuta hawezi kukimbia tena kama awali! Makomandoo wakaserereka kwenye kile kikorongo na kuendelea kumkimbiza.


Lakini kama kuna kosa walilofanya mabwana hawa basi ni kumkimbiza bwana huyu kwa wingi, takribani makomando wanne walikuwa wanalifanya hilo zoezi wakimkimbiza pasipo kujua ama kujali kwamba wanajiweka bayana kwa ajili ya shambulizi la kushtukiza.


Kama inegeliwezekana, kwakuwa watu hawa walikuwa na mawasiliano, wangejigawa, na watu wawili tu wangetimiza hiyo kazi, kiasi kwamba hata wakishambuliwa na kuuawa, ‘gape of number’ isiwe kubwa.


Basi hatua ya kwanza, ya pili, tatu … saba na nane, mara makomandoo wakawa wamempoteza bwana Wales. Hawakumwona wapi ameelekea. Alikuwa amjificha lakini bado sauti yake ya kuugumia maumivu ilikuwa inasikika kwa mbali.


Makomandoo wakatembeza kurunzi yao huku na kule. Hili pia ikiwa ni mojawapo ya kosa kwenye vita za msituni kwani hukuweka wazi upo eneo gani hata pale adui anapokuwa mbali. Walipoyumbisha kurunzi juu mitini,, wakawaona watu nane kwa ghafla. Watu hao walikuwa wamevalia barakoa na macho yao yamezibwa na miwani.


Bwana we, kabla hata hawajasema suuh! Wakamiminiwa risasi kana kwamba mvua ya vuli. Zikawatoboa vichwa na kupasua miili. Zikavujisha damu na kuwageuza bucha ndani ya kasi ya kufumba na kufumbua! Hakuna aliyeibuka salama! Wote wakalala chini wakiwa wamefunikwa na damu nzito.


Wauaji wakatua chini na wawili miongoni mwao wakaelekea upande wao wa kushoto ambapo huko walimkuta Wales akiwa amelala chini. Upesi wakamfanyia huduma ya kwanza kwa kuziba majeraha yake, begani na mguuni, kisha wakambeba na kumpeleka kwenye boti waliyokuja nayo, huko tena kulikuwa na watu wawili, wanaume wa kizungu.



***



“Siwapati!” akasema Komandoo mmoja akitikisa kichwa punde baada ya kushusha radio call yake toka sikioni. Alikuwa ametoka kuwatafuta wenzao wanne walioenda kumfukuzia Wales.


“Jaribu tena,” mmoja akashauri. Komandoo yule mwenye radio call akaruda tena hilo zoezi, majibu yakawa yaleyale. Hawakuwa wanawapata walengwa wao. Basi hapa wakapata shaka kuwa huenda milio ile ya risasi waliyokuwa wanaisikia iliwamaliza wenzao.


Wakiwa bado hawajaamua la kufanya, mara wakasikia sauti toka kwenye radio call. “Your friends are dead. Would you want the same service?”


“Yes, you bitch!” akafoka komandoo mwenye radio call. Uso wake mweusi ulijawa na ndita na kona za mdomo wake zilishuka chini. “If you are a man, show yourself up!” akatema mate kwa kufoka.


“Then come down where you heard shots. I will be waiting!” sauti ikamjibu.



****



Je, wataenda? Na wakina Jona wapo wapi wakifanya nini? Mchezo huu utakomea upande wa nani?
 
ningependa kuiendeleza ikiwezekana.
Mmh! Ila itakuwa kwa mtizamo wako sio wa ibra maana nafikia kusema tungejua tungemuuliza ibra na mapema ...mwisho itakuwaje japo kiufupi!
Lakini nakuaminia mkuu....unaweza..twende kazi!
 
Back
Top Bottom