Angalia mkataba wa Sweden na UAE ulivyotoa haki na wajibu kwa pande zote mbili. Ulinganishe na wa kwetu

asante sana. HGA ndizo tanesco atasign kwa utekelezaji wa miradi ndani ya IGA! na huyo investor from abroad lazima katika mkataba Tanzania will feature as authorizing to Tanesco to sign the contract on its behalf! I stand to be corrected


Hapa chini nakuwekea kifungu 123 cha Katiba ya UAE ambacho Mahakama yenyewe imesema imetia shakha kama Dubai anauwezo wa kuingia mkataba wa kimataifa.

 
Uko sahihi watasema hivyo. wanashau kuwa Issue hapa ni protection ya interest za Tanzania, not location of the contracting parties
Wazee wa bahasha za buku teni za DP world biashara ya protection ya interest za Tanzania hawajali!! Kikubwa ni matumbo yao yashibe vzr.
 
Serikali yenu kwani ina wanasheria? Mnanilaumu bure tu.
 
Hawa waarbu kama wamemwaga mpunga wamemwaga mwingi mno, ndomaana hata ukomo hauna labda maji yakauke! Matusi makubwa haya,sijui hata Mababu wa Mababu zetu wange kubaliana ujinga huu
 
Kwani ccm inategemea sanduku la Kura? Polisi siwapo?
Vyama pinzani huwa hawajipangi vizuri kusimamia masanduku ya kura. Huwa aidha hawana mawakala au wanakuwa na mawakala waliohongwa na ccm.

Zamu hii chadema wanajipanga vizuri na tayari walishaanza kampeni miaka miaka 2 na nusu kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025. Tena ni kampeni ya nguvu. Yaani ruhusa ya mikutano ya hadhara chadema waliichukulia kama filimbi ya kuanza kampeni ya uchaguzi mkuu wa 2025.

ACT wazalendo nao hawako nyuma. Bila shaka watamchukua Dr Slaa kama mgombea wao wa ngazi ya urais. Hapo vumbi litatimuka, upande wa chadema mgombea uraisi akiwa Mr Tundu. Hivyo Mama atapata kazi kweli kweli kupambana na mijitu ya namna hiyo na hasa kama hataachana na hii IGA ya DP World.
 
Kuna tofauti kati ya taifa na nchi kavu. Tanzania ni nchi kavu.
 
Kuna mahali nilipata hii vdeo fupi - jamaa akacomment -TZ tunavyojifunga na mikataba mibovu!
 

Attachments

  • VID-20230805-WA0001.mp4
    4.6 MB
Ujue kuwa mkataba uliopita bungeni ni wa kimataifa na unakwenda kwa mujibu wa masharti ya kimataifa haiwezekani pande mbili zenye kugombana zipate usuluhishi katika nchi mmojawapo ya hizo mbili.

Ndio sababu wanakwenda afrika ya kusini, huwezi kuuchukulia mkataba wa kimataifa kwa tafsiri za sheria zetu za ndani, huu uelewa ndio ule ule wa Mwabukusi na wanasheria wenzake waliopata aibu kule Mbeya.
 
Mnazidi kulishana matango pori, nani kakwambia kwamba bandari ni rasilimali ya nchi?. Kipi pale kinakuwa rasilimali, makontena au Meli?.

Usidanganywe na ile post inayotembea whatsapp ikiongelea rasilimali, hakuna kitu kama hicho.
 
Ile ni IGA ambayo ni summary tu ya mambo mengi yanayotakiwa kuandikwa kwenye project contracts.

Katika hii mikataba mipya ya Consession na Lease ndio sisi watanzania tuandike mahitaji yetu yote ya kibiashara.

Mnaleta ujuaji mpaka mnaishia kujichanganya tu.
 


Halafu ni UAE sio Dubai!
 
Ujomba na njaa ni shida sana.
Tanganyika nayo in general haijielewi.
 
Hawa waarbu kama wamemwaga mpunga wamemwaga mwingi mno, ndomaana hata ukomo hauna labda maji yakauke! Matusi makubwa haya,sijui hata Mababu wa Mababu zetu wange kubaliana ujinga huu
Ukomo unakuwa kwenye mikataba ya kibiashara huwezi kukuta ukomo kwenye IGA, haya ndio aliyosema Profesa Assad kwamba kila mtu anajifanya kukosoa hili suala wakati uelewa wetu wengi ni zero kabisa.
 
Imenibidi nicheke kwa andiko lako hili.

Ninapata shida sana kutumia "lugha ngumu"kwa mtu kama wewe, hata kama nikiwa na shaka juu ya lengo halisi la kujifanya kuwa na ujuha wa kiwango fulani katika maandishi yako.

Hiyo IGA umeisoma ukayakuta hayo unayoyaeleza juu ya "kuelewana na kurekebisha"?
Hukuona popote Tanzania ilipopewa masharti ya kuomba ruhusa kama inaona jambo halifai, na huyo mwenye kutoa ruhusa akikataa ni nini kinachofuata?

Wewe siyo pekee unayejitoa akili na kujaribu kupotosha na wengine wakose akili.
Wewe unafanya haya si kwa uelewa wako kuwa mambo yapo hivyo, bali ni kwa kazi maalum ya kupotosha watu.
Nirudie tena.
Hopeless Kabisa.
 
Inarekebishika lini ?!.
Ujomba na uswahili tabu kidogo nchi hii.
 
Everybody knows that, lakini hiyo ni discretion yenu! Mnaweza kuamua iwe ndani ya host country, SI SHURUTI MUENDE NJE. Usichanganye mambo! Umesoma mkataba niliouweka hapo ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…