Angalia umri wa afisa mpya wa mawasiliano/habari wa ikulu ya Marekani (White House) pamoja na elimu yake! Njoo bongo!

Ili aende na wakati mnajua tena vijana ni rahisi kufuatilia vitu kuliko wazee
Sisi mpaka augue au afie madarakani

Dunia inaenda kasi sana inahitaji wanaoendana nayo
Wazee wa Africa simu zao wanajua ku download uchafu tu
Mpaka kwenye baraza hili la sasa, Mkuchika bado ni waziri!!
 
Nyerere aliteua mabalozi hata waliokuwa kwenye early twenties na mid twenties, fanya utafiti.
Mkuu, Nyerere alipata urais mwaka 1962 akiwa na miaka 40, bado kijana. Enzi hizo za mkoloni, wasomi walikuwa ni wachache na wengi walikuwa vijana, sasa ungetegemea awateue wazee kutoka wapi tena?? Hivyo aliteua vijana wenzake

Au unapomzungumzia Nyerere akilini mwako unamuweka yule mzee wa miaka 70, ndio unaona kuwa aliteua vijana wa miaka 20 ilhali yeye akiwa ni mzee hivyohivyo??
 
Kwani nyie si mmeshapewa nafasi ya uchawa? Au hii haiwatoshi🀣🀣🀣🀣🀣
 
27 nipo nilikuwa fomfour🀣nagombania Chai πŸ€”
 
Hapa wanawaza wakikupa maisha katika umri mdogo utajipanga na kutoboa kimaisha ........yaani wanaona utawapita wakati wao wako kwenye serikali miaka 40 kazini .........wameiba na kurundika mali balaa.........ila tu kukupa ka ajira ka milioni 3 kwa mwezi kwao nongwa .............. wanataka mpaka uzeeke na tena huwe wa kwao sio kutoka sehemu nyingine................
 
kwani wa saa100 ni yupi mbona hamjamuweka ili watu waweze kufanya comparison vizuri? nchi ambayo inategemea dini ama ukanda wa mtu ama chama ndio apewe position regardless of what. ni balaa sana Mungu atusaidie sana.
 
Sisi huku tuna akina George Huruma Mkuchika na tunatamba nao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…