Angalizo: Vyeo vya WHO siyo vya Urithi

Angalizo: Vyeo vya WHO siyo vya Urithi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kwanza Kabisa nachukua nafasi hii kutoa pole kwa Msiba wa Dkt Faustine Ndugulile, Lakini pole hii naitoa kwa familia yake tu, Sitoi Pole kwa Bunge wala kwa mwingine yeyote yule.

Baada ya Utangulizi huo naomba niingie moja kwa moja kwenye hoja yangu fupi sana, Ni hivi, Vyeo vya Kimataifa, kama vya WHO au UNICEF si vyeo vya kurithishana kama vyeo vya Tanzania, hivi ni vyeo vinavyogombewa baada ya Usaili mzito kutoka kwa Watu wenye akili nyingi, anayesailiwa ni mtu binafsi, Mtu huyo huchunguzwa mwenendo wake tangu huko kwao alikotoka kama yeye binafsi anao weledi.

Ndugulile alifukuzwa Uwaziri baada ya kumpinga Rais wa Tanzania, John Magufuli kuhusu namna ya kupambana na Korona, Magufuli aliamini katika Ushirikina wa Kupiga nyungu, Jambo ambalo Dr Faustine alilipinga, na likamgharimu Cheo chake na mambo mengine ambayo sitayataja, jambo hili ni miongoni mwa yaliyomfanya apigiwe kura na Watu wengi, Alichaguliwa Dr Ndugulile, haikuchaguliwa Tanzania

Vyeo vya WHO si kama Ubunge wa ccm, kwamba kwa vile Selina Kombani kafa basi Ubunge wake tumpe Mwanaye, mwanaye ambaye kazi yake kubwa bungeni ilikuwa kuorodhesha dawa za kuongeza nguvu za kiume likiwemo vumbi la Congo, Nani aliyesahau hili?

Hoja yangu ni kwamba Kifo cha Dr Faustine hakitaifanya Tanzania ionewe huruma ili Hata wakipeleka mgombea Duni basi achaguliwe tu.
 
Hiyo ilikuwa kampeni na inaruhusiwa, na moja ya kampeni aliyofanya JK ilikuwa kuwaeleza wajumbe kwamba huyu alipinga nyungu, na kupinga kwake kulifanya atimuliwe
Na Dr Mollel ataelezewa hivyo hivyo kwsmba aliunga Juhudi na kutwaa nafasi ya Ndugulile na kurejesha chanjo

Ikumbukwe Dr Mollel ndiye aliwashauri Wabunge wa Chadema waende lockdown 😂😂😂😂
 
Kwanza Kabisa nachukua nafasi hii kutoa pole kwa Msiba wa Dkt Faustine Ndugulile, Lakini pole hii naitoa kwa familia yake tu, Sitoi Pole kwa Bunge wala kwa mwingine yeyote yule.

Baada ya Utangulizi huo naomba niingie moja kwa moja kwenye hoja yangu fupi sana, Ni hivi, Vyeo vya Kimataifa, kama vya WHO au UNICEF si vyeo vya kurithishana kama vyeo vya Tanzania, hivi ni vyeo vinavyogombewa baada ya Usaili mzito kutoka kwa Watu wenye akili nyingi, anayesailiwa ni mtu binafsi, Mtu huyo huchunguzwa mwenendo wake tangu huko kwao alikotoka kama yeye binafsi anao weledi.

Ndugulile alifukuzwa Uwaziri baada ya kumpinga Rais wa Tanzania, John Magufuli kuhusu namna ya kupambana na Korona, Magufuli aliamini katika Ushirikina wa Kupiga nyungu, Jambo ambalo Dr Faustine alilipinga, na likamgharimu Cheo chake na mambo mengine ambayo sitayataja, jambo hili ni miongoni mwa yaliyomfanya apigiwe kura na Watu wengi, Alichaguliwa Dr Ndugulile, haikuchaguliwa Tanzania

Vyeo vya WHO si kama Ubunge wa ccm, kwamba kwa vile Selina Kombani kafa basi Ubunge wake tumpe Mwanaye, mwanaye ambaye kazi yake kubwa bungeni ilikuwa kuorodhesha dawa za kuongeza nguvu za kiume likiwemo vumbi la Congo, Nani aliyesahau hili?

Hoja yangu ni kwamba Kifo cha Dr Faustine hakitaifanya Tanzania ionewe huruma ili Hata wakipeleka mgombea Duni basi achaguliwe tu.
CHADEMA mbona mnalithishana; HATA hivyo tumesema tunagombea tena nafasi itakapotangazwa hatukusema tunaomba tupewe fursa ya kuziba nafasi ya mteule aliyefariki- UPO HAPO MSEMAJI WA CHADEMA JF
 
CHADEMA mbona mnalithishana; HATA hivyo tumesema tunagombea tena nafasi itakapotangazwa hatukusema tunaomba tupewe fursa ya kuziba nafasi ya mteule aliyefariki- UPO HAPO MSEMAJI WA CHADEMA JF
Masahihisho: Mimi si msemaji wa Chadema, Ni mwandishi tu hapa JF kama ulivyo wewe
 
Binafsi nitagombea na nitashinda sitaki chawa wala nini ,mwenye kujua taratibu kuanzia tuma maombi atusaidie
 
Masahihisho: Mimi si msemaji wa Chadema, Ni mwandishi tu hapa JF kama ulivyo wewe
Mkuu usituone sisi wote humu ni wajinga na usinizuie kutoa maoni yangu- maoni yangu ni kuwa wewe ni MSEMAJI WA CHADEMA HUMU JF
 
Back
Top Bottom