Angekuwepo Hayati Rais Magufuli Kamwe Asingekubali Haya Yatokee

Angekuwepo Hayati Rais Magufuli Kamwe Asingekubali Haya Yatokee

Jerlamarel

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2021
Posts
843
Reaction score
2,525
1. Kamwe asingekubali Mita za LUKU kutumika kukata kodi za majengo. Hapa waathirika wengi ni wapangaji ambao wengi wao ni masikini na sio wamiliki wa hayo majengo/nyumba.

2. Kamwe asingekubali Tozo za miamala ya simu. Hili asingelikubali abadani asilani. Maana miamala tayari ilikuwa na VAT, sasa kuongeza tozo ni kama unamminya mwananchi mpaka aishiwe kabisa. Tena tozo zenyewe zinakatwa kwenye kutuma na kutoa😪.

IMG_20220804_035557.jpg


3. Kamwe asingekubali Gharama za maisha kupanda kiholela. Ndio hatukatai kuna mfumuko wa bei ila siyo katika kiwango hiki. Kuna bidhaa ambazo hazina scarcity lakini kwa sababu ya poor market control basi watu wameamua kujipandishia kiholela kwa visingizio visivyo na mashiko.
4. Kamwe asingekubali Watumishi kudanganywa kuhusu maslahi yao. Ijapokuwa yeye mwenyewe hakuwaongezea watumishi chochote kwa kipindi kirefu, lakini angalau alikuwa mkweli na ndio maana watumishi walimvumilia kwa kipindi kirefu.
5. Kamwe asingekubali Bei ya mafuta kuzidi kupanda wakati kwenye soko la dunia yameshuka. Hapa naamini kwa spirit aliyokuwa nayo ya kutetea wananchi basi angefanya lobbying yoyote ile ili kupunguza ukali wa bei ya mafuta. Nchi imezungukwa na bahari hii, tungeweza kuagiza mafuta hata Urusi kama angekuwepo mzee wetu maana hakuwa muoga kufanya chochote as long as ni for the benefit of his country.
Angalia hii chart hapa chini, utaona ni mwezi wa 3 sasa mafuta yanashuka bei wakati huku kwetu yanazidi kupaa bei. Hizo bar 3 nyekundu kwenye kibox zinaonesha mafuta yapo downtrend ila cha kushangaza sisi huku tupo uptrend.
IMG_20220804_044009.jpg


IMG_20220804_044226.jpg


6. Kamwe asingekubali bei za vifurushi vya simu viwe vinabadilika kiholela. Katika dunia ya sasa ambayo inaenda na sayansi na teknolojia, huduma ya internet ni moja ya basic need. Sasa unapowaminya watu wasiweze kupata internet unawaweka kwenye njaa ambayo ni sawa na njaa zingine. Bahati mbaya Waziri anayejusika na yeye anaonekana kama amebariki maana kwa mdomo wake amesema kabisa "Gharama zitaendelea kupanda".
IMG-20220803-WA0054.jpg


7. Asingekubali kamwe wamasai kuhamishwa kwa lazima kutoka kwenye ardhi yao. Japokuwa inawezekana kulikuwa na nia njema kwenye hili, lakini naamini mzee angelishughulikia vizuri zaidi kuliko ambavyo imefanyika sasa. Ukiona wamasai walikuwa wanagoma kuhama ujue kuna kitu hakikuwa sawa.
IMG_20220804_040619.jpg


8. Kamwe asingekubali Bei za pembejeo za kilimo kupanda kiholela. Moja ya eneo ambalo mzee alikuwa hapendi kabisa lichezewe basi ni kilimo. Kwenye utawala wake bei za vyakula zilikuwa nafuu sana na ndio maana raia hatukupata shida sana pamoja na hali mbaya ya uchumi iliyokuwepo. Lakini kwa sasa bei za pembejeo zimepaa, kitu ambacho kinapelekea hata bei za vyakula ziwe juu pia.
IMG_20220804_041327.jpg



 
Jiwe alikua jeshi la mtu moja akisema wote wanaufyata na alikua anahoji vitu kwa logic. saiv mama yuko busy kuwafunda wakinachalamila ili wakue na kuwaambia mawaziri kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake. Unamchaguaje mtu kuwa kiongozi ili hali ajakua? Rubbish leader ever happen in Tanzania. MUNGU AKUWA MJINGA KUMUUMBA MWANAMKE KUWA MSAIDIZI PALE KWENYE BUSTANI YA EDEN.
 
Cha muhimu ni kua KAFA

Yule muuaji na mbaguzi aliyeharibu uchumi wa Tanzania, kupora wafanyabishara fedha, kupora wakulima mazao, kujaza bungeni vilaza, kukopa mikopo mikubwa kwa pupa, uanzishwaji wa miradi mfululizo mingine isiyo na faida
Mbaguzi, laghai, roho mbaya iliyojawa na kiburi...ataketee milele

Hata mafuta yakifika 5000 ni afadhali kuliko kutawaliwa na yule mpuuzi aliyekuwa akiteua majambazi, na yeye angekuwepo maisha ndio yangekuwa balaa maana angelazimisha jeshi kuingilia biashara ya mafuta kama alivyofanya kwenye korosho na fedha za kigeni alivyo na akili fupi
 
Magufuli ndo alipandisha bei na ada za huduma maradufu ya alizoacha kikwete.

Magufuli ndo alikuja na kikokotoo cha kinyonyaji kwa wafanyakazi...

Ni magufuli aliyeleta 15% ya makato kutoka 8% aloacha kikwete

Ni Magufuli aliyeta kizaazaa NHIF...

Yule mshamba ameiharibu sana nchi.
 
Magufuli ndo alipandisha bei na ada za huduma maradufu ya alizoacha kikwete.

Magufuli ndo alikuja na kikokotoo cha kinyonyaji kwa wafanyakazi...

Ni magufuli aliyeleta 15% ya makato kutoka 8% aloacha kikwete

Ni Magufuli aliyeta kizaazaa NHIF...

Yule mshamba ameiharibu sana nchi.
Endelea kupambana punde tu utaacha
 
Kila mtu na nyakati zake, JPM hizi nyakati ngumu ndio saizi yake. Haogopi kutetea wananchi maskini kwa gharama yoyote. Najua bado mapema kugundua mengi lakini panapo uzima yapo mengi tutajua kwanini alifanya maamuzi magumu, mengine tayari tumepata majibu ikiwemo Covid 19!

Imagine tungeingia lock down tungekuwa na hali gani leo? Covid 19 imejifia kihuni tu, nyakati ngumu zinahitaji watu wagumu.
 
... kamwe asingekubali masikini wa nchi hii like Rostam, GSM, Mo, etc. walipishwe vitambulisho vya 20,000 kufanya biashara zao pembezoni na katikati ya barabara kwani wanajitafutia mlo wao na familia zao.
 
Ni kweli mkuu maana angegawa mafuta bure,vyuma vilivyokaza angeleta greese,machinga aliokuwa anawalipisha 20,000 angeacha na salary angeongeza na mikopo angeacha Kukopa maana Nchi hii nintajiri na tunajenga kwa pesa zetu.
 
5. Kamwe asingekubali Bei ya mafuta kuzidi kupanda wakati kwenye soko la dunia yameshuka. Hapa naamini kwa spirit aliyokuwa nayo ya kutetea wananchi basi angefanya lobbying yoyote ile ili kupunguza ukali wa bei ya mafuta. Nchi imezungukwa na bahari hii, tungeweza kuagiza mafuta hata Urusi kama angekuwepo mzee wetu maana hakuwa muoga kufanya chochote as long as ni for the benefit of his country.
Angalia hii chart hapa chini, utaona ni mwezi wa 3 sasa mafuta yanashuka bei wakati huku kwetu yanazidi kupaa bei. Hizo bar 3 nyekundu kwenye kibox zinaonesha mafuta yapo downtrend ila cha kushangaza sisi huku tupo uptrend.
Jiulize wanaofanya biashara ya mafuta nchini ni nani utajua kwanini amekaa kimyaaaa
 
Cha muhimu ni kua kafa

Naam, Mungu alikuwa na kusudi kubwa kumleta Magufuli na kumchukua kwa wakati aliyomchkua. Pamoja na kuwa Mungu alituamulia huo ugomvi, huo miradi yake mingi ya kifahari aliyoanzisha kwa wakati mmoja bila kujali uwezo wa nchi ndiyo iliyomfanya asimamishe maendeleo mengine mengi ikiwa ni pamoja na maslahi ya watumishi na kuelekeza sehemu kubwa ya mapato ya nchi kwenye miradi ya utukufu wake.

Ni hiyo miradi ya utukufu ndiyo inayoendelea kuitesa serikali ya SSH na kuifanya kuchagua fedheha iliyo nafuu: kati ya kuendelea kuwaumiza watumishi wote na kuwatuliza angalau wale wa kipato cha chini kabisa.

Hii ni kwa sababu ni ukatili mkubwa sana kuwaacha watumishi wa umma kwa miaka saba bila kuwarekebishia maslahi yao.

Uongozi unaojinasibu kuwa umechaguliwa na watu kamwe hauwezi kufanya hivyo. Magu hakuwa kiongozi wa kuchaguliwa bali ni mtu aliyewekwa na mfumo uliojimilikisha nchi yetu. Magufuli alithamini mapato ya serikali zaidi kuliko ustawi wa raia mmoja mmoja.

Hii ni kwa sababu alihitaji fedha za kutekeleza miradi yake ya kifahari kwa utukufu wake binafsi. Kwa hali hiyo tozo zote za sasa zingekuwepo tu na pengine zingekuwa nyingi, kubwa na mbaya zaidi. Mipango ya kuwapora Wamasai ardhi iliandaliwa wakati wake na bila shaka yoyote JWTZ ndiyo wangetekeleza kama ilivyokuwa kwenye korosho.

Watu makini wa nchi watakuwa wamebaini kuwa mpango wa kuhamisha Wamasai wa Ngorongoro kama ulivyobuniwa na Magu ulilenga kuwaondoa wote kwa nguvu badala ya hiari.

Ingawa haya ni maamuzi yaliyokwishafanyika Serikali ya sasa imeendelea nayo huku ikifanya marekebisho kila ilipobidi. Magu alitaka kuigeuza Ngorongoro kuwa Hifadhi ya Taifa ili aweze kuhodhi mapato yake yote.
 
Naomba CHADEMA itulie wala isiwapiganie watanzania. Wengi ni Wajinga na hawajielewi.
Tuka muliwe weeeee. Ili akili zitukae sawa.

Ajira za Boda na Bajaji zitakufa soon..nani apande boda shs 2000 umbali wa nauli ya 1000
 
6. Kamwe asingekubali bei za vifurushi vya simu viwe vinabadilika kiholela. Katika dunia ya sasa ambayo inaenda na sayansi na teknolojia, huduma ya internet ni moja ya basic need. Sasa unapowaminya watu wasiweze kupata internet unawaweka kwenye njaa ambayo ni sawa na njaa zingine. Bahati mbaya Waziri anayejusika na yeye anaonekana kama amebariki maana kwa mdomo wake amesema kabisa "Gharama zitaendelea kupanda".
Hiki Kiwaziri kimesahau kilikwenda kupiga magoti kwa mtu huku kikitoka jasho
 
Back
Top Bottom