Angelina Jolie aanza kusumbuliwa na Mama wa mtoto aliyemuasili

Angelina Jolie aanza kusumbuliwa na Mama wa mtoto aliyemuasili

Mkuu kwa wabongo tunafanya au tuliwahi fanya hiyo mambo lakini kwakweli wabongo ni tatizo.
Mimi niliwahi kuasili watoto 3 wawili walikuwa ndugu na mmoja ni wa familia nyingine
Tatizo lilikuja pale wale wawili walipo fika chuo kikuu wana boom akijitokeza mtu kuwa ni mzazi wao na mambo kibaaao!
Nilipata usumbufu wa kila aina ikabidi niache watoto waamue kwasababu tayari ni wakubwa.

Akabaki 1 ambae sasa yupo kidato 4 huyu nae mlezi wake akaanza longolongo kwakuwa sipendi vyesi nikamburuza Ustawi wa jamii kwasababu sikumchukua mtoto kienyeji. Akasalim amri amuache mtoto asome Mtoto ataamua pa kwenda akifikisha miaka 18.

Kuasili watoto wa watu wasiojielewa ni mtihani.
Ukitaka kuasili nenda kaasili kutoka vituo vya watoto yatima tofauti na hapo fanya shughuli nyingine za kusaidia wasiojiweza. Lakini usiali mtoto mwenye wazazi hatakama hajiwezi kupindukia.
Mimi mwenyewe nina mpango wa kuasili yatima kabisa. Ninaishi na watoto wa ndugu zangu na wengine wako chuo ila wana baba zao na mama zao, wakishafika malengo yao wanarudi kwa wazazi.
 
Mama yake wa kumzaa ana haki bado... maisha yanampiga kila mtu kikumbo ndo maana watu tunaamua ku escape kwa namna ile.

Japo naunga mkono mtoto aendelee kuwa mama mlezi ila kwa kweli afanye namna hata amsaidiea mama yake
Screenshot_20231107-140404_Chrome.jpg
Screenshot_20231107-140404_Chrome.jpg
 
Nikujibu ndugu mtoa thread. Yupo professor alikua udsm enzi hizo. Bwana mkubwa na mke wake waliaadapt mtoto akapataga ajali yule. Na wimbi la na professor wengi walifanya adoption enzi zile. Baaadae yule professor alikuja kumzalisha mtoto wa mama mdogo wa mkewe.
Adoption mbona zinafanyika sana bongo haswa miaka ya karibuni.
Waliosoma wanamfahamu yule mzee wetu wa ununio.
 
Angelina Jolie aliadopt mtoto wa kwanza wa kiume nchini Cambodia, akaja kuadopt mwengine wa kiume nchini Vietnam, akaja kuadopt mtoto mwengine wa kike nchini Ethiopia, hakua peke yake kwenye safari hiyo alikua na aliyekua mumewe Brad Pitt waliadopt wote,

Kwa mtoto wa Ethiopia jina lake Zahara, Angelina alimkuta kituo cha kulea watoto yatima akiwa ana miezi 7 tu, wahusika wa kituo wakamwambia mtoto yule ni yatima wazazi wake walifariki kwa virusi vya Ukimwi, huruma ilimjaa Jolie na kuamua kumchukua kwa taratibu zote stahiki,

Ukweli ukaja kujulikana miaka mitatu baadae, mama mzazi wa Zahara alikua hai, ni binti aliyepata ujauzito kwa kubakwa, huku akiishi na bibi yake na mjomba wake wakiwa katika maisha ya ufukara, baada ya kumzaa Zahara hali ilizidi kua mbaya, Mama Zahara akatoroka nyumbani na kumuachia mtoto bibi yake, bibi nae kwa hofu ya kumkosa mtoto kutokana na lishe duni akampeleka kituo cha kulea watoto yatima na kuomba msaada wampokee mtoto, atakufa kwa njaa,

Mama mtoto alichokiomba ni kuongea na mwanae hata kwa njia ya simu, kumjulisha kua ana familia Ethiopia na mama yake hajafa pia anampenda sana.

Wala hakutaka kumchukua ampeleke wapi na umaskini bado umemtawala.
kweli inasikitisha kama alibakwa ila hapaswi kumshobokea mwanae sababu alimkimbia!
wakina mama wana nguvu kubwa sana ya kuwarubuni watoto, Jolie akilogwa tu akamruhusu Zahara aongee na ***** kwa simu IMEKULA!
 
Mtoto kama ana maokoto amsaidie tu mama yake japo kuna uongo ulifanywa na kituo kilichokuwa kinamlea kwa angelina, na sidhani kama angelina atamkataza mtoto kumsaidia biological mother wake au kuwasiliana naye, japo kiukweli mtoto kwa sasa ni wa angelina.

Angalizo, huyo mama asije tu akaanza zile tamaa za kiafrica kumtaka mtoto kisa kaona anaweza kuponeapo


Ila mtoto kawa pisi aisee
mkuu huo uongo hata hapa kwetu unafanywa sana, mtoto ana wazazi wote wawili ila anapelekwa kituo cha watoto yatima.
hii tabia ya kuona watoto kama mtaji wa kutokea kimaisha ni mbaya sana. Usishangae hata baba aliyebaka akajitokeza kudai mwanae
 
kweli inasikitisha kama alibakwa ila hapaswi kumshobokea mwanae sababu alimkimbia!
wakina mama wana nguvu kubwa sana ya kuwarubuni watoto, Jolie akilogwa tu akamruhusu Zahara aongee na ***** kwa simu IMEKULA!
Waongee ni watu wa dunia 2 tofauti
 
mkuu huo uongo hata hapa kwetu unafanywa sana, mtoto ana wazazi wote wawili ila anapelekwa kituo cha watoto yatima.
hii tabia ya kuona watoto kama mtaji wa kutokea kimaisha ni mbaya sana. Usishangae hata baba aliyebaka akajitokeza kudai mwanae
mkuu upo sahihi kabisa kuna mchungaji mmoja wa haya makanisa ya kiroho aliwadanganya wafadhili kuhusu watoto waliokuwa wanataka msaada, badala ya kupeleka wenye uhitaji akapeleka watoto wake, watoto wakawa wanasomeshwa english medium za hela ndefu, wanoko wakaenda kutibua mchezo, watoto wakasitishiwa ufadhili, ikabdi mchungaji awarudishe st kayumba.
 
Back
Top Bottom