Anna Mghwira: Tuendeleze mjadala wa Mikopo ya Elimu ya Juu na tuchukue hatua

Kimsingi elimu ni kwa walewenye uwezo mdogo. Wenye uwezo mkubwa wanaweza kujisadia. Tulenge wenye uwezo mdogo, wasio na watu wa kuwalipia, nk...maan ahata wao wana mchango kwa pato la taifa, wakiwa na kitu cha kuzalisha.
 
Hapana Kididimo. Kwanza hili ni wazo langu. Ninajua madini na bidhaa zingine zipo lakini bado mikopo hakuna. Mimi sikusomakwa mkonge nk lakini hiyo iliwezesha vijana wengi kupata elimu kwa urahisi na umahiri mkubwa. Kulikuwa na hatua zake. Ninaendkeza hizi maana kodi ya madini nk hatujui inafanya kazi zipi, taarifa zetu si wazi wakati wote.

Kama tunachangia harusi nk, uchangie elimu pia kisha tuidai serikali kutuoa mrejesho wa mapato mengine. Matuizi ni mengi na hata micango hii haitamaliza changamoto zote.
 
Mama, upo sahihi sana ila jaribu kutumia njia nyingine yakuwa na MTU asiye na taswira ya kisiasa.kwako itagomewa na wengi wakiamini utajenga chama chako.ila pia wakati unabdilisha mtizamo,unaweza ibiwa idea
 
Wazo zuri lakini litazuiwa ili uwekwe utaratibu mzuri wa kuchangia na CCM ndio watakuwa wasimamizi wa ugawaji wa hizo fedha .
 
Mi sitachanga maana niliowachangia maafa hazijafika hadi leo
 
Maisha ni magumu, kodi tunalipa lakini viongozi hawana priorities. Unanunuaje ndege huna dawa. Unajengaje airport chato huna hela za mikopo ya elimu ya juu. Ishu kubwa ni prioritie na wananchi tukiona serikali iko kinyume na sisi nani atasaidia? Nchi jirani wanapambana na baa la njaa sisi bei hazishikiki na haturuhusiwi kusema kitu. Unadhani mtu mwenye machungu moyoni kiasi hicho atachanga?
 
Asante mama, sasa nimekuelewa vizuri
 
Transcend,
Asante kwa wazo lako. Nitarudi na mrejesho!
 
Unajua kama sisi tuliopo hapa tu tungechanga elfu moja tu kwa watu laki 4 tungepata milioni 400,000, 000.00 kamii za kuanzia. Hizi zingekopesha wanafunzi zaidi ya wanafunzi 200+ wangeweza kupatamopo wa m2 kila moja moja. mfuko ukianza, utartibu utakuwa tofauti na ninaamini watu zaidi, tasisi nk, zitaweza kuchangia zaidi. Niko safari nikirudi tutawasiliana. Asante sana
 
Alright! This sounds positive!

Then, naamini tayari una watu ambao wanafanya analysis na kuweka mipango ya mawazo ambayo unayapata hapa...

Weka mpango kazi mezani ili ukishaanza utekelezaji inakuwa ni rahisi kuwaeleza watu ambao humu hawapo lakini tunaamini watakuwa na moyo wa kuinua Elima kama wewe.

Uwe na safari njema.

You have our support...!
 
Ni kweli na ukizingatia teknolojia ya mambo ya kifedha imekua,Aliye Njombe au Kyerwa anaweza kushiriki. Mama,nashauri angalia zaidi mnaoendana kimawazo,ndo uwashirikishe kimkakati kwenye Menejiment ya usimamizi. Ukitaka tuwapendekeze, tuko tayari,tunawajua. Otherwise,nakutakia kila la heri.
 
Maskini nchi yangu....
Natamani sana siku moja mama Anna mghirwa ushike nchi hii qwa roho na Huruma uliyonayo watoto wa maskini watapata ahueni ktk kusoma...coz umeelezea tatizo kma vile tuko wote pale chuoni jamani Kama kuna viongozi wanawake humu Jf embu unganneni na mama Anna mfanikishe hili hakika mtakumbukwa na kuzidishiwa thawabu na Mungu wa mbinguni...
Life la chuo bila mkopo asikwambie mtu haliendi jaman maybe uwe na watu wa karibu yako watakao guswa na hali uliyonayo wawe wanakupiga tafu mdogomdogo jamani.... Coz mahitaji ni mengi sana ya kitaaluma na kiafya namaanisha chakula mpaka inafikia hatua mtu unaona aibu kuomba hela nyumbani coz unahisi utaonekana tapeli..
 
Mama yangu naomba hili wazo lako lisiishie humu JF kama umekusudia qweli kufanya hivyo naomba amka hata wasipo kusuport wanasiasa kuna wasanii , wanamitindo niseme tasnia ya michezo qwa ujumla watatoa support ya nguvu qwako ktk hili na hakika utakua umeokoa vizazi vilivyopo na hata vijavyo coz first year Waleo ndio taifa lijalo ..
Mama amka uanzishe project hii plz hata qwa mitatu utapata support na nchi nzima itaenea hii a idea yako na itasaidia sons and daughters of poor peasants
 
Kimsi

Kimsingi elimu ni kwa walewenye uwezo mdogo. Wenye uwezo mkubwa wanaweza kujisadia. Tulenge wenye uwezo mdogo, wasio na watu wa kuwalipia, nk...maan ahata wao wana mchango kwa pato la taifa, wakiwa na kitu cha kuzalisha.

Shida ya hiyo approach mama, ni changamoto ya namna bora na effective ya kuweza kuestablish uwezo mdogo wa kiuchumi. Ni namna gani tuta define uwezo mdogo wa kiuchumi na tuta evaluate vipi. Changamoto hii wameendelea kukumbana nayo HESLB na kutokana na subjectivity ktk kuamua, watumishi wasio waaminifu wametumia kama namna ya kujipatia pesa kwa kupitia rushwa. Lakini, ikiwekwa kigezo cha ufaulu, basi awe mtoto wa masikini, awe mtoto wa tajiri, basi ajitahidi ili aweze kumeet kigezo cha kupata huo mkopo/ufadhili.
 
POINT! Kuna contradictions nyingi ambazo ufumbuzi wake utahitaji mawazo sahii ya wananchi na wadau kama Mama yetu mleta post. Issue,wataongelea wapi? Nani ataratibu? Na kwa ruhusa ya nani? Ninaona Mawaziri ndo wameachiwa na system kuamua kila kitu. Mfano, unasema Versity waende Div 1 na 2. Hao wote wametokana zaidi na shule za private ambao kwa vigezo hawatapewa mikopo. Ni watoto wa matajiri! Mama kaja JF,tumwunge mkono. Na naomba aunganishe wenye maono kama yeye Ulimwenguni kote,waunge mkono hoja yake.
Kuna wengi hapa Kenya jirani zetu,walisoma kwa michango" Harambee funds",na wakamaliza masomo,sasa wanajenga Taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…