Pre GE2025 Anna Tibaijuka: Kimfumo uwezekano wa kutangazwa mshindi ukitokea upinzani haupo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tilipu hii watake wasitake watamtangaza MH LISU
 
Wamepanga sana nani awe mrithi. Ila kila zama hakuna liyefanikiwa kutinga ikulu. Mwinyi aliingia ndivyo sivyo, akaletwa Mkapa kwa Mbeleko ya Nyerere, Sumaye hakuamini JK alivyoingia, Magufuli kikawa kama kifurushi kutoka juu, Samia wakajiuliza kumbe katiba ina tobo kubwa kiasi hiki? Tujiandae!
 
Anna Tibaijuka ameandika katika ukurasa wa X kuwa alimwambia Edward Lowassa abaki CCM baada ya kukatwa jina lake kwenye majina ya wagombea Urais ila Lowassa alokataa kubaki akodai hataki kuonewa.

Anna Tibaijuka ameandika alimwambia uwezekano wa kutangazwa mshindi ukitokea upinza haupo kutokana na mfumo na Lowassa alojibu kiwa anajua.

Je, kauli hii yaTibaijuka kwenda kwa Lowassa inakupa picha gani wakati ambapo tunaelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu hapo Mwakani?

"Familia Lowassa poleni. Taifa twaomboleza kifo cha Kiongozi STATESMAN. Nilishuhudia ukiweka maslahi ya nchi mbele ya yako. Jina lilipokatwa nilikushauri ubaki CCM kimfumo uwezekano kutangazwa mshindi ukitokea upinzani HAUPO Ukanijibu "UNAJUA
ila hutaki MANYANYASO kuendelea. RIP"

 
Katumbua jipu, hapo vyama vya upinzani ndipo mjue mnapuyanga tu kuonesha watoa misaada kuna mageuzi but ndani huko ni uongo mtupu!.
Unadhani hawajui wanajua ila kuna ruzuku ndio target kubwa kwa vyama vya upinzani kwa sasa they are not serious..
Viongozi wa vyama vya upinzani wanatambua sintofahamu hiyo, lakini ni wananchi ndiyo wanaoweza kuwapa nguvu ili haki za mpiga kura ziheshimiwe.

Watanzania kila kitu tunataka tufanyiwe. Mengine nasi tuonyeshe misimamo kama wananchi.
 
Wapinzani hawahawa waliopo kwenye payroll ya CCM! Tutasubiri sana
Payroll ipi?. Msipende kuongea kisa mpo nyuma ya keyboard. Nenda kwenye ground Kama huwezi Kaa kimya. CHADEMA wakiitisha maandamano mnakaa Kama wanafiki kuangalia yasifanikiwe, halafu Leo unaongea ujinga eti pay roll, unaijua pay roll au unaropoka.
 
Tibaijuka is so wrong for distracting the conversation from mourning to an overly controversial topic, complete with Lowassa's words, when Lowassa is not even here to clarify his side.

I am noticing a lack of social graces amongst Tanzanians, regardless of status.

From the common hustler on the streets to our so called esteemed leaders and people of eminent stature.

How does one go from "poleni familia" to that raggedy in less than 60 seconds?

There is a time and place for everything.

Where is your savoir faire Dr. Tibaijuka?
 
huo ndio ukweli.... za lowassa akapewa jiwe za jiwe akapewa lowassa, na huwez enda mahakama yoyote itayotengua uchaguzi wa raisi.. bila katiba mpya ccm itatawala milele hata ichukiwe na dunia nzima.
Weeewee! Lowasa asingeliweza kipambana na jiwe!
 
Anaongea nn? Ni CCM wale wale kashazeeka anapoteza maslahi basi kelele kila siku.
 
Duh 🙄 !
Yaani anajiamini kabisa kuusema ukweli hadharani kwamba Uwezekano wa kutangazwa upinzani umeshinda haupo 😅😅
Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya firauni !!
😂😂😂
 
Bibi anajitahidi kweli katika kuwasahaulisha nyumbu 'hela ya mboga'.
 
Katika salamu zake za pole kwenye msiba wa hayati Edward Lowassa, Anna Tibaijuka anasema, “
Familia Lowassa poleni. Taifa twaomboleza kifo cha Kiongozi STATESMAN. Nilishuhudia ukiweka maslahi ya nchi mbele ya yako. Jina lilipokatwa nilikushauri ubaki CCM kimfumo uwezekano kutangazwa mshindi ukitokea upinzani HAUPO Ukanijibu "UNAJUA
ila hutaki MANYANYASO kuendelea. RIP

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…