Anne Makinda anunua nyumba kwa Tsh. Milioni 900, Dar

Mawazo Ya Umasikini ndio haya angekua Mhindi ana hizo mil 900 usingeshangaa...Huyu Mama Mm simjui Lakini Tangu awr kiongozi since 1974 mpaka leo akikosa mil 900 hata mm namuona ni zoba..Acheni Wivu kwanza ungemshauri ajenge kiwanda aajiri watu wengi....Kuliko kijicho chako.
 
Hatupo hapa duniani ili kufurahisha watu wengine bali Mungu.
 
Umbea. Ujumbe wake wa bodi mbalimbali unaweza kumpatia hizo hela. Na ukimbuke huyo ni
Mfanyakazi wa siku nyingi unaweza alikuwa ana save au kakopa.
wapi marekani au?🙄
 
Mama Makinda ana mtoto (Binti wa Kumzaa mmoja ) na pia anakaa na watoto wa dada na wadogo zake.Binti ake Jina lake linaanzia na J
Ni kweli. Huyu binti yake Ndugai alimsimulia mwaka huu alipokuwa akifafanua sakata la kumfukuza yule mbunge wa kike aliyeingia na suruali ya kubana makalio.

Ndugai alieleza kwamba "amewahi kuzuiwa binti wa mhe. Anna Makinda kuingia bungeni kama mgeni kwasabb ya mavazi yasiyo na staha huku mama yake (Anna Makinda ) akiwa spika.
 
Hongera kwa kuwa mfuatiliaji wa maisha ya watu. Jitahidi sasa na wewe tukupost.

#Mama 2025.
 
Wanasemaga mtanzania mpe picha tu maelezo atatoa yeye
 
Umesema mwenyewe ndiyo kamaliza kujenga ukumbi watu wametafuta fursa,yeye pia katafuta fursa biashara ni watu na watu haohao wanaweza kuua biashara yako kwakuto nunua bidhaa zako ama huduma
 
Weka ya 200x
 
Wakati mnaendelea kumjadili huyu mama nawakumbusha tu, yeye ndio mwenyekiti wa bodi ya NHIF na pia amepewa ulaji kwenye sensa ya watu na makazi.

Nitawaona vijana mnatumia akili zenu vizuri huyu mama kama hana mume mnamliaje mingo ya kumpa starehe za kimwili ili na nyinyi awapunguzie huu ukwasi mkubwa alionao, mkumbuke baada ya vumbi la Congo sasa kuna Vicks kutoka Congo ni hatari, waweza tunukiwa hili ghorofa.
 
Mkuu naomba please mawasiliano ya mama yangu Makinda
 
Mama MAKINDA NI Shujaa na anajiamini.
Hata Bunge lake lilikua sikivu.

Amelitumikia taifa hili kwa Muda Mrefu.

Tatizo la watawala wa nchi za kiafrika ni kujenga nchi zenye unyang'anyi.
Yaani mwenye nguvu Mpishe.
Vita zilizopo kwenye nchi nyingi barani Afrika zimesaidia sana vyama vikongwe kudumu Madarakani.

Mfano Makomando wanapigwa na Makada wa vyama na hakuna wa kuwasemea watu waliofuzu medani za kivita kwa level za juu kabisa kimataifa. Yaani komando anachomwa bisibisi na Mtanzania Mwenzake kwa sababu tu ya kujikomba kwa wanasiasa RAIA ili kudhibiti fursa za wanasiasa kikatiba.
Badala ya kumtumia Komando kulinda amani na kutoa taarifa toka kwenye vyama wao wanawaua matokeo yake watatafuta majitu yasiyo na kiapo kujilinda na kulitia taifa kwenye vurugu.




Mama Makinda aijitahidi kuishauri serikali vizuri na kuwasikiliza pia wapinzani.


Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
Watu wanajenga kwa mkopo, muhimu uwe na colateral
 
Mfanya biashara huyo

Ana mahoteli muda tu

Chapa kazi acha uchawi
 
Laana ni kitu kibaya sana,na ukiwa Rais ni lazima upate Trilioni? Kwa akli hizi ni halali kabisa Africa kuwa maskini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…