TANZIA Anne Rwigara afariki dunia. Ni dada wa Diane aliyejaribu kugombea Urais dhidi ya Kagame. Mama asema kifo hicho ni fumbo

TANZIA Anne Rwigara afariki dunia. Ni dada wa Diane aliyejaribu kugombea Urais dhidi ya Kagame. Mama asema kifo hicho ni fumbo

Mkuu soma btween lines bas 😂😂
Hawana cha kujifunza hapa kwa mambumbumbu. ungefahamu historia ya wakomunisti wa uchina hapa Afrika ndio ungeelewa kwa nini hao wakomunisti wana mahusiano na tu vyama fulani huku kusini mwa jangwa la Sahara.

CCM haina chochote kile cha kuwaoffer hao wakomunisti kwanza CCM ni moja ya wanafunzi wa hao wakomunisti wa China Afrika.
 
IMG-20231229-WA0002.jpg
Anne Rwigara (41), aliyekuwa mkosoaji wa Serikali ya Rwanda na mtoto wa mfanyabiashara maarufu wa zamani nchini Rwanda, Assinapol Rwigara amefariki dunia nchini Marekani saa chache baada ya kueleza kupatwa na maumivu makali ya tumbo.

Rwigara alifahamika zaidi baada ya kukamatwa yeye na familia yake na kukaa gerezani kwa siku kadhaa mwaka 2017 baada ya uchaguzi wa urais wakituhumiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo ukwepaji kodi na kupelekea mali za familia, kikiwemo kiwanda cha tumbaku na akaunti za benki kushikiliwa.
 
Huwa najiuliza kivipi mtu mmoja anakua na nguvu, wapi madikteta kama Kagame wanapata nguvu zao?

Nikagundua idadi kubwa ya watu huwa wana focus na familia zao, watu wao wa karibu na mahitaji yao ya kila siku kama maji, dawa na chakula

Siasi sio kipaumbele kikubwa cha waafrika wengi, kwa maneno mengine wanyarwanda ndio wanaoruhusu Kagame afanye anachojisikia

Watu wakichafukwa na kuamua, huyo Kagame anaweza fia sehemu ambayo hata panya hatamani afie hapo

Madikteta wanapewa nguvu na watu wasiojali
Tumelaaniwa
 
Ni kweli amefia Marekani but sio sahihi kuhusisha kifo chake na mambo ya kisiasa kama anavyo taka kushawishi mtoa mada.

Kifo cha huyo Dada, hakiwezi kutenganishwa na mambo ya siasa!!!
Kagame anaachaje kuhusishwa hata kama kifo cha kawaida kwa namna huyo dada alivyokuwa treated na serikali yake??
 
Mdada mzuri kama huyu kuwa mwanaharakati ni kujitakia balaa. The same nawaambia kina Maria Sarungi na Acheni mambo ya kujifanya wanaharakati wakati hao mnaowapigania wenyewe hawajui kujipigania.
Huyo dada ameteseka sana yeye na familia yake yeye na mama yake wamekaa ndani muda mrefu lakini pale Rwanda hakuna mwananchi aliyepaza sauti kuwatetea.
Hawa kina Mwabukusi pia nawaasa nchi hii unapoteza muda kujifanya unatetea sijui haki sijui nini wewe pambania familia yako na ndugu zako tena wa karibu. Mambo ya kufanya unatetea haki za wanyonge kwa hizi nchi za kusini mwa jangwa la sahara bado sana utaumia utakufa unaacha familia yako iliyokuwa inakutegemea.
Lissu na Mbowe wameanza kugundua hili, siku hizi wanafanya siasa kwa afya sio kujitesa.
Liverpool huwa tuna watu smart we sijui wa wapi.. puuzi kabisa
 
Kagame amechukua roho za wengi sana, naona ameshazoea kuua, kuanzia Tanzania mpaka SA leo hii amefika USA!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Ile sura yake tu inatisha sana,roho za aliowaua huwa zinamlilia.

Naamini huwa akikaa peke yake pia huwa ana mahangaiko makubwa ya nafsi yake na huenda ndiye mtu anaekiogopa zaidi kifo chake.
 
Mkuu anayajua kweli ya Idd Amin Dadah? Babu yangu Mimi mzaa Mama aliondoka na maaskari wake anaitwa kituoni mwaka 1976 hajawahi kurudi hadi leo. Unamaanisha bado anahojiwa?
Yapo yaliyotokea ambayo Amin mwenyewe alikiri hakuhusika nayo. Kwenye mahojiano fulani na BBC nadhani mwaka 2003 aliwahi kuulizwa kuhusu watu kuuawa na kupotea. Alijibu kuwa inawezekana baadhi ya matukio kufanywa na askari pasina idhini ya moja kwa moja kutoka kwake.

La muhimu tambua kuwa kulikuwa na upinzani na njama nyingi dhidi ya Amin na katika mazingira ya kujihami kesi kadhaa za ukiukwaji wa haki za binadamu zinaweza kutokea.

Hakuna mtu aliyekamilika kila mmoja ana mapungufu yake lakini Amin hakuwa kama ambavyo watu wanavyomzungumza kwa ubaya.
 
Hawana cha kujifunza hapa kwa mambumbumbu. ungefahamu historia ya wakomunisti wa uchina hapa Afrika ndio ungeelewa kwa nini hao wakomunisti wana mahusiano na tu vyama fulani huku kusini mwa jangwa la Sahara.

CCM haina chochote kile cha kuwaoffer hao wakomunisti kwanza CCM ni moja ya wanafunzi wa hao wakomunisti wa China Afrika.
I know that..ccm haina cha maana hata cha kutupa sisi wananchi itakua na kipi cha ku offer kwa watu wenye akil kama ccp?
 
Back
Top Bottom